New Action Movies 2017 | New Adventure movies 2017 English Subtitles
Tanzania\'s leading online News Edition (The National Newspaper). Get access to the most current and latest authoritative news on local issues, politics, events, celebrations, editorial, columnists, features, people and business.
Tuesday, 12 December 2017
Master Thief 2017 NEWEST ADVENTURE Movies Crime ACTION Full Length Movies
Master Thief 2017 NEWEST ADVENTURE Movies Crime ACTION Full Length Movies
Kwanini Jumuiya ya Wazazi Bungeni aingie 1, hii nitaifuta, tutaenda pasupasu - JPM
Kwanini Jumuiya ya Wazazi Bungeni aingie 1, hii nitaifuta, tutaenda pasupasu - JPM
Takukuru yaendelea na uchunguzi dhidi ya Manyara

Dar es Salaam. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru), imesema inaendelea na uchunguzi wa tuhuma dhidi ya mkuu wa mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti.
Mkurugenzi mkuu wa Takukuru, Valentino Mlowola aliliambia gazeti hili jana kuwa uchunguzi unaendelea baada ya kukamilika hatua nyingine zitafuata.
Mnyeti ambaye kabla ya kutuhumiwa kutoa rushwa alikuwa ni mkuu wa wilaya ya Arumeru, anadaiwa kunaswa katika mkanda wa video na sauti kupitia mtandao wa kiuchunguzi uliokuwa umetegwa na mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari.
Oktoba mosi, Nassari na Godbless Lema (mbunge wa Arusha Mjini) walipeleka ushahidi ambao unawatuhumu madiwani 10, kuhama katika chama hicho kwa kupewa rushwa huku wakiomba Rais John Magufuli kuchukua hatua ili kukomesha vitendo hivyo.
Nassari alisema katika ushahidi wao, ambao wameuonyesha kwa wanahabari wakidai madiwani waliojizulu wamepokea rushwa ya fedha, ajira, posho za vikao vyote vilivyobaki na kiinua mgongo cha udiwani miaka mitano na kulipiwa mkopo wa benki.
Kuhusu matumaini ya kukamilika kwa uchunguzi huo, Mlowola alisema: “Muda wa sheria kwa uchunguzi unaendelea tukikamilisha hatua nyingine zitafuata.”
Hata hivyo, kwa nyakati tofauti viongozi hao walikana tuhuma hizo, katibu tawala wa wilaya ya
Arumeru, Timoth Mzava ambaye alionekaa katika video hiyo, alisema ameufuatilia ushahidi unaozungumzwa na wabunge hao na kubaini kuwa ni wa kuungaunga na hauna ukweli wowote.
Arumeru, Timoth Mzava ambaye alionekaa katika video hiyo, alisema ameufuatilia ushahidi unaozungumzwa na wabunge hao na kubaini kuwa ni wa kuungaunga na hauna ukweli wowote.
Huyu ndie mshindi wa tuzo ya mchezaji bora Afrika

Mohamed Salah wa Misri amechaguliwa kuwa mshindi wa Tuzo ya BBC kwa Mwanakandanda Bora wa Afrika Mwaka 2017.
Nyota huyu wa Liverpool alipata kura nyingi zaidi ya Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon, Naby Keïta wa Guinea, Sadio Mané wa Senegal na mchezaji wa Nigeria Victor Moses.
"Nimefurahi sana kupata tuzo hii," mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 aliiambia BBC Sport.
"Huwa ni hisia ya kipekee unaposhinda kitu. Unahisi ulikuwa na mwaka mzuri sana. Kwa hivyo nina furaha sana. Ningependa kushinda tena mwaka ujao!"
Salah, aliyefunga mabao mengi zaidi ligi kuu England, akiwa na mabao 13, amekuwa na mwaka wenye mafanikio.
Mapema 2017 alikuwa nyota wa Misri walipochukua nafasi ya pili katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika.
Baadaye mwakani, mshambuliaji huyu aliye na kasi alichangia katika magoli yote yaliyowasaidia Mafirauni kufuzu kushiriki michuano ya Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza tangu 1990 - aliwasaidia wenzake kufunga mabao mawili, naye akafunga mabao matano, moja ikiwa penalti kati yao na Congo iliyowawezesha kufuzu kwa fainali hizo za Urusi.
"Ninataka kuwa mwanakandanda bora zaidi wa Misri kwa hivyo mimi hutia bidii," anasema kijana huyu ambaye amekuwa raia wa tatu wa Misri kupata tuzo hii tangu 2008.
"Mimi hufuata njia yangu na ninataka watu wote Misri kufuata njia yangu"
Mchezo wake kwenye klabu yake umekuwa mzuri sana, sawa na ule wa nchi yake.
Nchini Italia, alifunga mabao 15 na kusaidia ufungaji wa mengine 11 na kuisaidia Roma kumaliza katika nafasi ya pili kwenye Serie A, nafasi yao bora zaidi kwenye ligi katika miaka saba, kabla ya kujiunga na Liverpool na kufunga bao mara 13 katika mechi zao 16 za kwanza kwenye ligi.
"Ningependa kuwashukuru wenzangu wa timu ya Liverpool na pia nilikuwa na msimu mzuri na Roma, kwa hivyo lazima niwashukuru wenzangu huko na wale pia wa timu ya taifa," alisema Salah.
"Tangu nije hapa, nilitaka kujia bidii sana na kuonyesha kila mtu uchezaji wangu. Nilitaka kurudi Ligi ya Premia tangu nilipoondoka, kwa hivyo nina furaha sana."
Salah amerejea Ligi ya Premia kwa kishindi msimu huu, tofauti sana na alipokuwa kwenye ligi hiyo mara ya kwanza akiwa na Chelsea kati ya 2014-15.
"Anastahiki," anasema meneja wa Liverpool Jurgen Klopp, aliyemkabidhi mchezaji huyo tuzo yenyewe katika uwanja wa mazoezi wa klabu hiyo wa Melwood.
"Kwa kweli mimi ni mtu mwenye bahati sana. Nilikuwa na fursa ya kufanya kazi na wachezaji wachache wa kipekee, wazuri, na nina furaha kwamba sasa nina Mo.
"Jambo zuri ni kwamba yeye bado mdogo wa umri, anaweza kuimarika sana, ana uwezo mwingi ambao bado tunaweza kuufanyia kazi, na hivyo ndivyo inafaa kuwa. Ni furaha sana kwangu, kusema kweli, kufanya kazi naye."
Salah sasa ameongeza jina lake kwenye orodha ya wachezaji hodari kutoka Afrika, kama vile Abedi Pele, George Weah, Jay-Jay Okocha na Didier Drogba, ambao wamewahi kushinda Tuzo ya BBC kwa Mwanakandanda Bora wa Afrika wa mwaka.
"Nina furaha isiyo na kifani kuwa kama wao katika kushinda tuzo hii," amesema raia huyo wa Misri, ambaye amewafuata raia wenzake Mohamed Barakat (2005) na Aboutreika (2008) katika kushinda taji hilo.
Washindi wa awali wa Tuzo ya BBC kwa Mwanakandanda Bora wa Afrika wa Mwaka:
2016: Riyad Mahrez (Leicester City & Algeria)
2015: Yaya Toure (Manchester City & Ivory Coast)
2014: Yacine Brahimi (Porto & Algeria)
2013: Yaya Toure (Manchester City & Ivory Coast)
2012: Chris Katongo (Henan Construction & Zambia)
2011: Andre Ayew (Marseille & Ghana)
2010: Asamoah Gyan (Sunderland & Ghana)
2009: Didier Drogba (Chelsea & Ivory Coast)
2008: Mohamed Aboutrika (Al Ahly & Misri)
2007: Emmanuel Adebayor (Arsenal & Togo)
2006: Michael Essien (Chelsea & Ghana)
2005: Mohamed Barakat (Al Ahly & Misri)
2004: Jay-Jay Okocha (Bolton & Nigeria)
2003: Jay-Jay Okocha (Bolton & Nigeria)
2002: El Hadji Diouf (Liverpool & Senegal)
2001: Sammy Kuffour (Bayern Munich & Ghana)
2000: Patrick Mboma (Parma & Cameroon)
Atiwa mbaroni kwa kubaka watoto wanne

JESHI la Polisi Mkoa wa Kusini Unguja, linamshikilia kijana wa miaka 30 kwa tuhuma za kuwabaka watoto wanne, wawili wa familia moja.
Tukio hilo limeripotiwa Desemba 8, mwaka huu, huko Muyuni A, Mkoa wa kusini Unguja na mtuhumiwa huyo anadiwa kuwabaka na kuwalawiti watoto hao ambao ni chini ya umri wa miaka 18.
Kamanda wa Polisi mkoa huo, Makarani Khamis, alisema hapo awali mtuhumiwa huyo alidaiwa kuwabaka watoto saba, lakini baada ya uchunguzi wa daktari ulibainika kuwa ni watoto wanne ndio walioharibiwa na watatu wakiwa salama.
Alisema mtuhumiwa huyo ambaye ni fundi seremala alidaiwa kuwafanyia matukio hayo watoto hao kwa siku na nyakati tofauti.
Alisema mtuhumiwa yupo ndani kwa hatua za kiupelelezi na zitapokamilika atafikishwa katika vyombo vingine vya kisheria kwa hatua zaidi.
Aliitaka jamii isiwe mbali na watoto wao kutokana na matukio ya udhalilishaji wanaofanyiwa watoto siku hadi siku.
Aidha, aliwashauri wazazi na walezi kufuatilia nyendo za watoto wao na kuhakikisha wanawaogesha badala ya kuwaacha waoge wenyewe ili kama ana majeraha aweze kugundua mapema.
Watoto hao walitambuliwa kuwa wanafanyiwa vitendo hivyo baada ya mmoja ya wazazi wa watoto hao kumgundua mwanawe akiwa anaharufu mbaya na alipomuhoji ndipo alipomtaja mtuhumiwa huyo.
Baada ya kumuhoji mtoto wake alimtaja mtuhumiwa huyo na kuwataja watoto wenzake ambao wamekuwa wakifanywa na mtuhumiwa huyo na kuwapa Sh. 5,000.
Sheha wa Shehia ya Muyuni ‘A’ Maulid Hassan Zidi, alisema baada ya kutokea tukio hilo kuna wananchi wengine zaidi ya saba wanalalamika watoto wao wameharibiwa na mtu huyo, lakini hakuna aliye kwenda kuripoti.
Aliitaka jamii kuripoti matukio hayo yanapotokea badala ya kulalamika mitaani kwani kufanya hivyo kunachangia watendaji wa makosa hayo kuendelea kuyafanya.Sheha huyo alisema katika shehia yake hilo ni tukio la kwanza kutokea ndani ya mwaka huu, lakini huko nyuma kuna matukio kama hayo yalitokea na watuhumiwa wapo mitaani ndio kinachowafanya wananchi kushindwa kuripoti matukio hayo.
Mbowe ameitaka Serikali kutoa tamko kuhusu Azory

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ameitaka Serikali kutoa tamko kuhusu aliko mwandishi wa habari wa kujitegemea wa kampuni ya Mwananchi Communications Ltd, Azory Gwanda.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam kwa niaba ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Mbowe alisema kitendo cha Serikali kukaa kimya kinaleta wasiwasi kwa ndugu na jamii ya wanahabari.
“Sasa ni wiki ya tatu tangu Azory ametoweka nyumbani kwake, lakini Serikali haijatoa tamko lolote, hatuelewi nini kimemtokea,” alisema.
Azory (42), anayefanya kazi za uandishi wa habari Kibiti na Rufiji mkoani Pwani ametimiza siku 22 tangu atoweke kwa kuchukuliwa na watu wasiojulikana Novemba 21.
Mbowe alisema kumekuwa na matukio ya kutisha kama watu kupotea na maiti kuokotwa zikiwa zimefungwa kwenye mifuko hali ambayo inawatia wasiwasi wananchi.
“Tunaomba vyombo vya dola kuhakikisha uchunguzi wa kina unafanyika ili kufahamu aliko mwandishi huyo,” alisema.
Mbali ya wito huo, mwenyekiti wa Baraza Kuu la CUF, Julius Mtatiro alisema kufungia vyombo vya habari kwa sababu vimekosea kuandika takwimu si halali.
Alisema makosa ya takwimu yanatakiwa kusahihishwa lakini si kukifungia chombo cha habari kwa kuwa madhara yake ni watu kukosa ajira hata ambao hawakuhusika moja kwa moja na makosa yaliyofanywa.
Dully Sykse atokwa povu kisa Bombardier

Mkongwe wa Bongo Fleva nchini, Dully Sykse.
ETI kisa Bombardier! Mkongwe wa Bongo Fleva nchini, Dully Sykse ametoa povu ikiwemo kutangaza vita na wasanii wa kizazi kipya kwa sababu ya kushindwa kumsapoti kwenye wimbo wake mpya.
Dully Sykes ambaye ameachia wimbo mpya wa Bombardier, alisema wasanii wa sasa ambao wengi ni wapya wana roho mbaya na yeye yuko tayari kupambana nao.
“Wasanii wa sasa wana roho mbaya, hawasapotiani kama wasanii wa zamani, ndiyo maana Bombadier yangu hawajanisaidia kuitangaz, hiyo inaonesha muziki ni vita na mimi niko tayari kupambana nao,” alisema Dully
Ben Kinyaiya anatarajia kusogeza jiko

MTANGAZAJI maarufu Bongo, Ben Kinyaiya amefunguka kuwa anatarajia rasmi kuvuta jiko.
Kinyaiya aliiambia Full Shangwe kuwa, Mungu akijalia hivi karibuni atauaga ukapera rasmi kwa kufunga ndoa na mwenza wake ambaye hakutaka kumuanika wazi.
“Unajua ndoa ni mapenzi ya Mungu, kama mwanadamu sina mamlaka kihivyo, ila Mungu akijalia ‘soon’ ninafunga ndoa na mwandani wangu,”alisema Kinyaiya.
Mzee aliepata msamaha wa Rais Magufuli atoa ya moyoni

Mzee Mganga Matonya (kulia) akisalimiana na ndugu na jamaa zake walipomtembelea nyumbani kwake baada ya kutoka gerezani
Dar es Salaam. Rais John Magufuli alishangaza wengi alipotaja jina la mfungwa aitwaye Mganga Matonya, mwenye umri wa miaka 85, wakati akitangaza msamaha kwa watu 61 waliohukumiwa kunyongwa na mmoja aliyekuwa na kifungo cha maisha.
Haikuwa kitu cha kawaida kwa mkuu wa nchi kutaja jina la mfungwa, lakini ni mwendelezo wa maajabu yaliyowahi kumkuta Matonya katika maisha yake ya gerezani. Mara ya kwanza alifutiwa adhabu ya kunyongwa hadi kufa na Rais wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere.
“Namshukuru sana Rais Magufuli,” alisema Matonya alipoongea na mwandishi wetu jana akiwa kijijini kwake Wiliko mkoani Dodoma.
“Sikutegemea kama nitatoka gerezani. Naomba salamu zimfikie kwani sijui namna ya kuonana naye. Ningebahatika kuonana naye siku ile nilipotoka gerezani, ningemkumbatia kwa furaha.”
Matonya alipata taarifa za msamaha akiwa gereza la Kingolwira mkoani Morogoro, lakini awali alikuwa Gereza la Isanga mkoani Dodoma akiwa mahabusu baada ya kufanya kosa akiwa na umri wa miaka 39. Aliishi Isanga hadi Mei 10, 1980 wakati alipohukumiwa.
“Hakimu aliamuru ninyongwe mpaka kufa. Wakati nasubiri utekelezaji wa hatua hiyo mwaka 1984, rais wa wakati huo, Julius Nyerere alinibadilishia adhabu kutoka kunyongwa hadi kifungo cha maisha,” alisema Matonya.
Baada ya kuhukumiwa kunyongwa, Matonya na mwenzake walisubiri kifo kwa miaka mitano, lakini mabadiliko ya tabia waliyoonyesha wakiwa gerezani yalishawishi wasimamizi wao wapendekeze majina yao ili wabadilishiwe adhabu.
Baada ya Rais Nyerere kuwapunguzia adhabu hiyo, wawili hao walihamishwa kutoka Gereza la Isanga mkoani Dodoma na kwenda Kingolwira mkoani Morogoro.
Anasema hakuwahi kufikiria kuwa kuna siku angetoka gerezani, zaidi ya kujipa matumani na kumuomba Mwenyezi Mungu amnusuru na adhabu ya kufia ndani ya kuta za majengo hayo.
Jana ilikuwa siku ya furaha kwa Matonya, familia yake, ndugu na wanakijiji wa Wiliko, kijiji ambacho kiko takriban kilomita 85 kutoka Dodoma Mjini.
Akizungumza na Mwananchi jana, Matonya alionyesha furaha, mwenye kutafuta maneno asijue la kusema zaidi ya shukrani nyingi kwa Rais Magufuli kwa uamuzi wake wa kumsamehe adhabu ambayo ni nadra kunusurika isipokuwa kwa kushindana kisheria.
“Natamani kuonana na Rais Magufuli na kuongea naye mambo mbalimbali, lakini sina uwezo,” alisema Matonya.
“Lakini kupitia gazeti hili naamini ujumbe utamfikia. Kwa kweli, namshukuru sana kwa hili.”
Pamoja na Rais kumtaja jina, Matonya anasena hakuwa anafahamu lolote kuhusu msamaha huo.
“Taarifa zilinifikia ghafla,” alisema.
“Siku hiyo nilikuwa nimepumzika gerezani na wenzangu walikuwa wanaangalia televisheni. Mara nikasikia wenzangu wakiniita. ‘Mzee Matonya, Mzee Matonya. Njoo uone huku jina lako limetajwa na Rais Magufuli kuwa umeachiwa huru’.
“Sikuamini na sikula chakula kwa furaha niliyokuwa nayo.”
Kosa mpaka kufungwa
Matonya na mwenzake anayeitwa Myeya Nyagalo walikamatwa Oktoba 1974 wakati walipoenda kuuza ng’ombe wa wizi kwenye mnada katika Kijiji cha Nyang’oro kilichopo kati ya Iringa na Dodoma. Walikuwa wamemuua mwenye mifugo hiyo kwa mkuki wakati wakiiba na hivyo walikuwa wanasakwa hadi walipoibuka mnadani.
Matonya na Nyagalo walikuwa miongoni mwa watu 12 walioorodheshwa kuwa walihusika katika mauaji hayo.
Akikumbuka tukio hilo, Matonya alisema wakati huo alikuwa kijana na mwenye tabia ya wizi wa mifugo.
Anasema siku alipofanya kosa hilo, alikuwa na Nyagalo na vijana wengine wawili wa kabila la Kimasai walioshirikiana kuiba ng’ombe hao.
“Tuliandaa mpango wa kujiongezea mifugo. Baada ya kujiridhisha wapi tunaenda kuiba mifugo hiyo, tuliamua kwenda,” alisema Matonya.
“Haikuwa mara yetu ya kwanza. tulishafanya matukio kama hayo maeneo mengine. Lakini, kwa hili, arobaini za mwizi zilikuwa zimefika. Tulipata upinzani mkubwa uliosababisha mapigano na kifo cha mwenye mali.
“Mimi na mwenzangu Nyagalo hatukufahamu kama mtu yule amefariki. Tulijua tumemjeruhi tu.”
Alisema wenzao walifahamu kwamba mwenye mali hangepona. Alisema tofauti na matukio ya awali, wenzao walitaka wagawane mifugo waliyoiba na kila mmoja ashike njia zake.
“Tulishangaa, lakini mwisho wa siku tuligawana, tukaachana,” alisema.
Alisema baada ya muda hawakuwa na njia nyingine zaidi ya kupeleka mifugo mnadani kuiuza bila kujali kama Jeshi la Polisi lilikuwa linawatafuta. Ndio maana walikamatwa kirahisi.
Familia ya Matonya
Leo hii, Matonya amerejea mtaani ambako ana watoto sita, wajukuu 33 na vitukuu ambao idadi yake haikuweza kupatikana mara moja. Lakini alimuacha mkewe akiwa na watoto wawili na ujauzito wa miezi nane, hivyo watoto waliozaliwa wakati akiwa jela wanahesabika kuwa wake.
Kama ilivyokuwa kwa Nguza Mbangu Vicking na mwanae Papii Kocha waliotoka gerezani saa chache baada ya kutangaziwa msamaha, ndivyo ilivyokuwa kwa Matonya na mwenzake waliotoka gerezani juzi.
Mzee Matonya alisema anaangalia uwezekano wa kujikita kwenye kilimo, shughuli aliyokuwa akiifanya kabla ya kuhukumiwa, lakini anasema umri ushaenda.
Baada ya kuishi gerezani mwezi mmoja, alizaliwa mtoto ambaye mkewe alimuita Aron (45) ambaye akiwa shule ya msingi, alikuwa akipokea barua za baba yake kutoka kwa wafungwa waliokuwa wanamaliza kutumikia adhabu zao au mahabusu walioshinda kesi.
Aron ambaye kwa sasa ni baba wa watoto wanne na wajukuu, alisema alijisikia furaha baada ya kupata taarifa za kuachiwa kwa baba yake kwa kuwa hakuamini kama angekuwa huru tena.
“Tulikataa tamaa kama Mzee angetoka gerezani,” alisema Aron.
“Niliwahi kwenda kumuona mara nne na mwisho ilikuwa ni mwaka 2014. Ninapozungumza naye. Najisikia furaha iliyopitiliza. Kila mtu hapa kijijini haamini kilichotokea,” alisema Aron.
Baada ya kuongezeka kwa mzee wao, Aron anasema watu hawakauki nyumbani kwao kwa kuwa kila mtu anataka kumuona na kumshika mkono. Hapo nyumbani, anasema watu hawalali, wanashangilia huku wengine wakifanya maombi ya kumshukuru Mungu na Rais Magufuli aliyempa msahama.
Source: Mwananchi
Waziri Jafo ampa wiki sita Mkandarasi wa mradi wa maji Muheza

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mh. Selemani Jafo amempa wiki sita Mkandarasi wa mradi wa maji wa Kivindo Wilayani Muheza mkoani Tanga, kuhakikisha anakamilisha mradi huo na uanze kutoa huduma.
Waziri Jafo ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo wilayani Muheza, ambapo alikagua miradi katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri hiyo ukiwemo mradi huo wa maji.
“Sitegemei kusikia sababu zozote zitakazofanya mradi huu usikamilike ndani ya wiki sita, ni mategemeo yangu wananchi wataanza kufaidi matunda ya mradi huu baada ya muda mfupi tu kuanzia sasa, Mkandarasi fanya kazi yako” amesema Jafo.
Aidha Waziri Jafo alimtaka Mkandarasi wa Mradi huo ambao umefikia asilimia 90 ya utekelezaji wake kuwaahidi wananchi kuwa ataukamilisha ndani ya muda wa wiki sita ambao amepewa na waziri.
Mbali na mradi huo wa maji wa Kivindo pia Waziri Jafo amefanikiwa kutembelea Miradi ya afya na
elimu katika kituo cha afya Mkuzi na Ubwari pamoja na kutembelea ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Msingi Kilulu.
elimu katika kituo cha afya Mkuzi na Ubwari pamoja na kutembelea ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Msingi Kilulu.
Subscribe to:
Comments (Atom)
 
 

