Tanzania\'s leading online News Edition (The National Newspaper). Get access to the most current and latest authoritative news on local issues, politics, events, celebrations, editorial, columnists, features, people and business.
Wednesday, 6 December 2017
Kutokwa Na Majimaji Kwenye Matiti (Galactorrhea)

Tatizo hili husimama lenyewe kama ugonjwa ingawa pia inaweza kuwa ni dalili kama mwanamke ni mjamzito, ananyonyesha au ametoa mimba au ameharibikiwa na mimba.Kusimama kwake kama ugonjwa ni pale yanapotoka wakati mwanamke hana historia ya dalili hizo hapo juu.
Tatizo hili huwapata wanawake wengi na kwa mujibu wa takwimu huathiri asilimia tano hadi 32 ya wanawake walio katika umri wa kuzaa.Pamoja na kuwapata zaidi wanawake, hali ya kutokwa na majimaji katika matiti pia huweza kuwatokea wanaume watu wazima, vijana walio katika umri wa balehe, wa kike na wa kiume, watoto wachanga wa kike na wa kiume.
Chanzo cha tatizo
Matiti yanaweza kutoa majimaji endapo chuchu zitachezewa au kunyonywa mara kwa mara na kusababisha kuvuruga baadhi ya homoni mwilini.
Homoni zinazohusika zaidi na tatizo hili ni homoni ya ‘prolactine’. Vilevile katika hali hii ya kutokwa na majimaji asilimia 50 ya matatizo chanzo chake bado hakijulikani.
Mama anayenyonyesha homoni zinazochangizwa na kusababisha matiti yatoe maziwa ni ‘Prolactin’, Estrogen’ na Progesterone.
Dawa nyingine zinazoweza kumfanya mtu atokwe na majimaji katika matiti ni dawa kama Methyldopa, madawa ya kulevya na dawa za magonjwa ya akili.
Pamoja na matatizo katika mfumo wa homoni, hali ya kusuguasugua kifua mara kwa mara, hali ya kuwa na hofu na wasiwasi au shauku f’lani, mfano ya kuhitaji kupata ujauzito husababisha kuamsha homoni za uzalishaji wa maziwa au hayo majimaji.
Vyanzo vingine ni matatizo kichwani kwenye tezi ya ‘pituitary au pituitary adenoma’.
Dawa nyingine zinazoamsha tatizo hili ni kama vile ‘Cimetidine’ ambazo hutibu vidonda vya tumbo.
Pia zipo dawa nyingine za asili ambazo hazijafanyiwa utafiti wa kutosha zinazoweza kusababisha tatizo hili.
Dalili za tatizo
Mwanamke mwenye tatizo hili la kutokwa na maziwa kwenye matiti wakati si mjamzito na wala hana historia ya kuwa na mimba, huwa hapati ujauzito.
Mwanaume mwenye tatizo hili hupungukiwa na nguvu za kiume, uzalishaji wa mbegu za kiume huwa mdogo.
Kwa ujumla tatizo hili husababisha ugumba.
Kwa vijana na watoto wa kiume au wa kike ni vema uchunguzi wa kina ufanyike.
Maziwa yanaweza kutoka tu yenyewe au kwa kuminyaminya matiti au chuchu.
Uchunguzi
Hufanyika hospitalini kwa madaktari wa masuala ya uzazi. Vipimo vya damu kuangalia homoni, matatizo katika matiti, na ikibidi CT-Scan vitafanyika kuangalia matatizo katika tezi ya Pituitary.
Ushauri Wahi hospitali kwani athari ya tatizo hili ni kupoteza uwezo wa kuzaa.
Epuka kuchezea chuchu ziwe zako mwenyewe au za mpenzi wako au za mtoto kwani unaamsha homoni ambazo katika wakati huo hazitakiwi.
Saratani Ya Shingo Ya Kizazi, Inasababishwa Na Ngono Na Mambo Mengine Ya Fahamu Hapa

UTAFITI mpya wa kitabibu umebaini kuwa saratani ya shingo ya kizazi, inasababishwa pamoja na mambo mengine na ngono kama ilivyo kwa ugonjwa wa Ukimwi, madaktari bingwa wa magonjwa ya maradhi hayo wamesema.

wametaja mambo mengine yanayoweza kusababisha saratani ya shingo ya kizazi kuwa ni kujiingiza kwenye mapenzi katika umri mdogo, kuolewa mara nyingi, kuwa na wapenzi wengi, kusafisha sehemu za siri kwa bidhaa zenye kemikali na kuzaa mara nyingi.

Katika kiwango cha kimataifa, wastani wa mwanamke kuzaa bila kuwa katika hatari ya kupata ugonjwa wa saratani, ni watoto wanne.
Madaktari hao walisema saratani ya shingo ya kizazi inatokana na aina 40 ya virusi, aina mbili ikiwa ni virusi vinavyosambaa kwa njia ya ngono “Human papilloma virus (HPV) Squamos cell carcinoma kirusi namba 16 na Adenocarcinoma namba 18, ni kati ya virusi 40 vinavyosababisha saratani ya kizazi na vyenyewe vinachangia tatizo hilo kwa asilimia 70.” Wanasema saratani ya uzazi ndiyo inayoongoza ikilinganishwa na nyingine nchini na asilimia 80 ya wagonjwa, wameambukizwa kwa ngono. “Saratani hiyo husambaa kwa ngono kutoka mwanamke mmoja kwenda kwa mwingine.
Mwanamke mwenye saratani ya kizazi akifanya ngono, mwanamume huchukua virusi na kumwambukiza mwingine atakayefanya naye ngono,” alisema na kuongeza:
“Wagonjwa wengi na wale ambao tayari wana maambukizi, wamekuwa wakikutwa na virusi hawa wa aina mbili ambao wamekuwa wakienezwa zaidi kwa njia ya zinaa. Inawezekana mwanamume akawa ametoa kirusi kwa mwanamke mmoja kwenda kwa mwingine.”
“Hata hivyo, kuna wanaume ambao tayari wameshakuwa na maambukizi ya HPV wanatembea na virusi, hawa tunawaita (high risk sexual male patner) wanaume hawa utakuta kila akioa mke anakufa kwa saratani ya shingo ya uzazi, lakini kamwe virusi hao hawawezi kumwathiri yeye.”
Kuanza ngono mapema nako kunachangia kwa kiasi kikubwa maambukizi ya saratani hiyo, kwani binti anakuwa katika hatari zaidi ya kupata maambukizi mapema na hivyo kuweza kumwathiri mapema zaidi, tofauti na yule aliyeanza baadaye.
“Idadi kubwa ya wanawake wamekutwa na saratani mapema sana, ukilinganisha na umri wao, lakini wengi wao wamekuwa wakikutwa na ugonjwa huu kuanzia umri wa miaka 35 kwenda juu. Hii inamaanisha kuwa walipata maambukizi hayo walipokuwa na miaka 20-25.”
Licha ya hivyo mgonjwa anaweza asitambue tatizo hilo mpaka miaka 10 hadi 15 baadaye ambapo
tatizo linajitokeza hadharani. “Unapopata maambukizi ya HPV inakuchukua muda mpaka kujulikana, kwa kawaida mwanamke anaishi miaka 10 hadi 15 na baadaye anagundulika na tatizo hili, lakini itategemea na kushuka kwa kinga zake.
Kama ikitokea hapo katikati ukajitokeza ugonjwa mwingine kama HIV basi saratani nayo itajitokeza.” Utafiti walioufanywa Septemba 2011 kuhusu tatizo la HIV na saratani ya shingo ya uzazi unaonyesha kuwa idadi kubwa ya wanawake waliokuwa na maambukizi ya HIV na CD4 ziliposhuka tu, saratani ya kizazi nayo iliibuka, hiyo inamaanisha kuwa tatizo hilo ni kubwa tofauti na linavyodhaniwa. Kwa upande wake virusi vya HPV huambukizwa kwa mwanamke moja hadi mwingine, pale mwanamume anapofanya tendo hilo na mwanamke mwenye maambukizi na kwenda kufanya tendo hilo na mwanamke mwingine. Kinga Madaktari hao wameeleza kinga ya maradhi hayo kuwa ni pamoja na matumizi ya kondomu na uaminifu wa wapenzi katika uhusiano wao.
Ninatoa wito kwa Watanzania na jamii kiujumla kujijengea tabia ya kupima mara kwa mara ili kubaini maambukizi mapema. Ongezeko la watu wanaougua saratani ya shingo ya uzazi imetokana na ongezeko kubwa la watu, ikiwa ni pamoja na tabia ya kuchangia ngono kwa wapenzi.
Alisema chanjo ya saratani ya shingo ya uzazi inayotarajiwa kuanza kutolewa kwa mabinti wa miaka tisa mpaka 12 baadaye, Ni moja ya juhudi ya Serikali katika kupambana na ugonjwa huo.
Kula Blueberry Kunaongeza Uwezo Wa Ubongo

Utafiti mpya umegundua kuwa, kunywa vikombe viwili na nusu vya juisi ya blueberry kwa siku ( mie naziita kunazi za bluu) kunaongeza uwezo wa ubongo wa kufahamu, na kuondoa matatizo ya usahaulifu yanayotokana na utu uzima. Wataalamu wanasema kuwa
kunywa kila siku juisi hiyo kunamzuia mtu uwezekano wa kupatwa na ugonjwa wa kupoteza akili uzeeni au wendawazimu. Blueberry kwa kuwa na kiwango kikubwa cha phytochemical, tunda hilo lina limejaa anti oksidanti na lina uwezo wa kuzuia uvimbe. Vilevile kunazi za
bluu kwa kuwa na mada iitwayo Anthocyanin, huweza kusaidia kuongeza kumbukumbu katika ubongo. Pia tunda hilo husaidia kupunguza kasi ya kitendo cha kupungua kumbukumbu katika ubongo kwa kuondoa gulukosi zinazopatikana kwenye ubongo.
Uchunguzi huo umebaini kwamba, kula blueberry kupitia vidonge maalum vya kusaidia afya au supplements kunaweza kumpatia mtu faida kubwa katika ubongo. Hata hivyo wataalamu hao wameshauri kuwa ni bora tunda hilo liliwe katika hali ya kawaida.
Huko nyuma pia wataaamu walieleza kuwa, Blueberry husaidia kupunguza usongo wa mawazo pamoja na kiwango cha juu cha gulukosi katika damu.
Haya tena wadau…usichelewa kula tunda hili, najua katika nchi zetu za Afrika tunda hili
halipatikana na ndio sababu hata jina lake katika kamusi yetu haliko, lakini usife moyo unaweza kupata tunda hilo madukani na katika supermarkets ambapo huhifadhiwa katika makopo au kama juisi. Kwa wale walioko ughaibuni basi hakuna tabu hiyo na usikose kula tunda hilo tamu wakati wa msimu wake na wakati miwngine wowote.
Daima tuzilinde afya zetu!
Samsung yafanya majaribio ya teknolojia ya 5G

Katika intaneti yenye kasi hivi sasa katika nchi zetu za Afrika ni teknolojia ya 4G na hiki ndio kizazi kinachoonekana kuwa chenye kasi ya intaneti lakini hali ni tofauti kwa Samsung ambao wanafikiria kuhusu kizazi cha 5 cha intaneti.
Tangu mwaka 2015 Samsung imeunganisha nguvu na kampuni nyingine ya mawasiliano ya Japani inayofahamika kama KDDI katika kufanikisha teknolojia ya intaneti ya 5G inatumika kwenye bidhaa/huduma kati ya makampuni hayo mawili.
Samsung kwa kushirikiana na KDDI ilifanya majaribio ya kasi ya intaneti ya 5G kwenye treni ya mwendokasi na kasi ya intaneti hiyo ikiwa ni 1.7Gbps.
Kilichofanyika kwenye majaribio ya intaneti ya 5G.
Kwenye majaribio hayo ambayo yalifanyika kwenye treni iliyokuwa ikisafiri kwa kasi ya zaidi ya Km 100/saa ilihusisha kifaa cha kisasa zaidi cha kuongeza kasi ya intaneti kama ikiwa ndogo (5G router), 5G Virtualised Radio Access Unit (vRAN) na Virtualised core.
Treni hiyo ambayo ilikuwa kwenye kasi huku umbali kati ya vituo viwili ukiwa karibu Km 1.5; ilishuhudiwa katika majaribio hayo video ya kiwango cha 8K kupakuliwa pamoja na video ya kiwango cha 4K iliyokuwa inachukuliwa ndani ya treni kutoka kwenye kamera iliyokuwa eneo la mbele ndani ya treni kuweza kuwekwa (uploaded).
Usalama wa teknolojia hiyo umearifiwa kuwa ni wa kuaminika kwa maana ya uduukuzi (udukuzi wa WI-FI, wizi wa taarifa za abiria, n.k) na kuwa yenye kasi zaidi itakayowafurahisha abiria/watumiaji wa teknolojia hiyo.
Tangu mwaka 2015 Samsung na KDDI wamekuwa wakifanyia majaribio teknojia ya 5G. KDDI wenyewe wanatarajia kuanza kutumia teknolojia ya intaneti ya 5G mwaka 2020.
Matumizi ya teknolojia ya 5G yanatarajia kufungua milango kwa aina mbalimbali za biashara kufikiria kutoa huduma hiyo huku KDDI wakiahidi kuendelea kufanyia majaribio teknolojia hiyo katika sekta mbalimbali.
Tuesday, 5 December 2017
Video | Rudeboy (P – Square) – Fire Fire | Mp4 Download
Video | Rudeboy (P – Square) – Fire Fire | Mp4 Download

Video | Rudeboy (P – Square) – Fire Fire | Mp4 Download
DOWNLOAD NOW

Video | Rudeboy (P – Square) – Fire Fire | Mp4 Download
DOWNLOAD NOW
TANGAZA BIASHARA YAKO NA WINOKEMEDIA360

Tangaza Biashara yako nasi ili uweze kufikia malengo uliyo jiwekea katika Biashara yako, WINOKEMEDIA360 inauwezo mkubwa sana wa kuitangaza Biashara yako yoyote ile.
Kama vile
Maduka / Bidhaa
Makampuni na Mashirika
Shule / Vyuo
Viwanja / Mashamba
Nyumba / Apartment
Hotel / Restaurant
Mikutano / Sherehe
Bei zetu ni nafuu sana mawasiliano nasi 0675762540 Au 0688108760 Kwa Namba Ya Whatsapp.
Tanga: Kifaa cha kujifunzia Kingereza chasambazwa

Wadau mbalimbali wa elimu kwa kushirikiana na Serikali wamesambaza vifaa maalum vya kufundishia somo la Kingereza mashuleni ili kusaidia kumaliza changamoto na kuongeza uelewa kwa wanafunzi wa sekondari mkoani tanga.
Kifaa hicho kijulikanacho kwa jina la E.rider kitaanza kutumika rasmi kwa mwaka 2018,huku mtaalamu kutoka shirika la CAMFED ambao ndio wametoa vifaa hivyo anasema kifaa hicho kina uwezo wa kuhifadhi jumla ya vitabu elfu moja na mia nne kwa wakati mmoja.
Kwa upande wa Mwakilishi wa Afisa Elimu mkoa wa Tanga ametoa wito kwa walimu waliokuwa wakipewa mafunzo ya kutumia kifaa hicho huku kamera ya ITV ikushuhudia mwitiko huo wa waakimu.
Wadau hao wamefanya kitendo hicho baada ya kuonekana kuwa lugha ya kingereza imekuwa ni kikwazo kwa wanafunzi wanaofaulu shule za msingi kwenda sekondari hasa mkoani Tanga.
Mtanzania azidiwa na dawa za kulevya na kufariki ndani ya ndege

Dar es Salaam. Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Rogers Sianga amethibitisha kupokea taarifa ya Mtanzania kufariki dunia akisafirisha dawa za kulevya.
Amesema alikuwa akisafiri kuelekea nchini China kwa ndege ya Shirika la Ethiopia na alizidiwa kutokana na dawa alizokuwa amemeza.
“Ni kweli kuna Mtanzania amekutwa amekufa kwenye ndege ya Shirika la Ethiopia akiwa amemeza dawa za kulevya. Tunaendelea kufuatilia kujua jina lake na amezitoa wapi hizo dawa,” amesema.
Sianga akizungumza na MCL Digital leo Desemba 5,2017 amesema taarifa hizo walizipata jana na kwamba wanaendelea kufuatilia.
Amesema hivi sasa Watanzania wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya wengi wanatumika kupokea mizigo na kuisafirisha kunakohitajika.
Waziri Lukuvi awaonya wenye nyumba wanaotoza kodi ya mwaka

Dar es Salaam. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amewaonya wamiliki wa nyumba wanaopangisha na kudai kodi ya mwaka mzima.
Akizungumza leo Jumanne Desemba 5,2017 akifungua jengo la makao makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) jijini Dar es Salaam na sanamu ya Mwalimu Julius Nyerere, amesema kodi ya nyumba inatakiwa kutozwa kila mwezi.
"Mpangaji anatakiwa kulipa kodi kila mwezi labda atake mwenyewe kulipa kwa miezi zaidi ya mmoja," amesema.
Lukuvi amesema hata NHC inatoza kodi kwa wateja wake kwa mwezi. "Acheni tamaa wenye nyumba chukueni kodi kila mwezi," amesema.
Amesema kuna vijana wanaoajiriwa wanashindwa kukaa jirani na mjini kutokana na kutozwa kodi ya nyumba kwa mwaka.
Mbali ya kauli hiyo, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula Novemba 17,2017 akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Halima Bulembo bungeni alisema Serikali iko katika mchakato wa maandalizi ya muswada wa sheria ambayo itasimamia sekta ya nyumba, hivyo kuondoa changamoto ya wamiliki kudai kodi ya pango ya zaidi ya mwezi mmoja.
Halima katika swali lake alisema vijana ambao ni kati ya asilimia 56 na 60 nchini, wanashindwa kutimiza ndoto zao kutokana na gharama kubwa ya kodi ambayo hutakiwa kulipa kwa kipindi cha mwaka mmoja au miezi sita.
Akijibu swali hilo, Mabula alisema Serikali imeliona tatizo hilo na ipo katika mchakato wa kuandaa muswada wa sheria utakaosimamia sekta hiyo.
Mabula alisema baada ya kukamilika kwa sheria ambayo itaunda chombo cha kusimamia sekta hiyo, wapangaji hawatalipa kodi ya mwaka wala miezi sita tena bali watalipa kwa mwezi na kuweka amana ya miezi mitatu.
Zanzibar Heroes yaifumua Rwanda 3-1 CECAFA

Timu ya taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Rwanda kwenye mchezo wake wa kwanza Kundi A michuano ya CECAFA Challenge inayoendelea nchini Kenya.
Zanzibar ambayo imecheza soka safi na kujiamini ilifanikiwa kuandika bao la kuongoza dakika ya 35 kipindi cha kwanza kupitia kwa Abdu-Aziz Makame ambaye alimalizia kwa kichwa krosi nzuri ya Mudathir Yahya. Bao hilo lilidumu hadi mapumziko.
Kipindi cha pili Rwanda ilianza kwa kasi na kufanikiwa kusawazisha bao hilo dakika ya 47 kupitia kwa kijana Hakizimana Niyonzima ambaye ni mdogo wake na nyota wa Simba Haruna Niyonzima.
Bao la pili la Zanzibar limefungwa na Mohammed Juma dakika ya 52 huku bao la tatu likifungwa na Kassim Khamis dakika ya 86. Matokeo hayo sasa yanaiwezesha Zanzibar kushika nafasi ya pili katika kundi A nyuma ya Kenya.
Zanzibar Heroes itacheza mchezo wake wa pili na ndugu zao wa Kilimanjaro Stars siku ya Alhamis Desemba 7. Kilimanjaro ilitoka sare ya bila kufungana na timu ya taifa ya Libya kwenye mchezo wa kwanza.
Ethiopia: Mtalii kutoka Ujerumani auawa kwa kupigwa risasi

Mtalii mmoja kutoka Ujerumani amepigwa risasi na kuuawa kaskazini mashariki mwa Ethiopia.
Dereva wake pia alijeruhiwa wakati wa tukio hilo, ambalo lilifanyika katika jimbo la Afar, karibu na mpaka wa Eritrea.
Ripoti zanasema raia huyo wa Ujerumani alikuwa miongoni mwa kundi la watalii ambao walikuwa kwenye ziara ya volkano ya Erta Ale - kivutio kikubwa kwa watalii wanaozuru Ethiopia.
Mwandishi wa BBC Emmanuel Igunza anasema hadi kufikia sasa haijabainika ni nani hasaa aliyetekeleza shambulio hilo lakini serikali ya Ethiopia inasema inachunguza mauaji hayo.
Serikali pia inasema vikosi vya usalama vimetumwa kuimarisha usalama huko.
Eneo hilo la mpakani linatumika sana na kundi la waasi linalotaka kujitenga na Ethiopia.
Mnamo mwaka 2012, watalii watano waliuawa na wengine wanne kutekwa nyara baada ya wapiganaji kuwashambulia katika eneo hilo.
Kundi lililojihami la Afar Revolutionary Front lilidai kuhusika kwenye shambulio hilo.
Subscribe to:
Comments (Atom)
























