Wednesday, 29 November 2017

Wakulima Kilombero wametakiwa kutumia Viwanda kuongeza thamani ya Mazao


Wakazi wa Wilaya ya Kilombero wametakiwa kutumia viwanda vilivyopo kuongeza thamani mazao wanayozalisha na kuyauza.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero, Denis Londo alitoa rai hiyo jana wakati akizindua kiwanda cha kati cha kukoboa, kupanga madaraja na kuuza mchele (Jatu) katika Kijiji cha Igima.

Alisema ujio wa kiwanda hicho ambacho kipo karibu na mashamba ya wakulima wa mpunga ni neema kwa kuwa malighafi zinapatikana kwa urahisi na kutawezesha kunufaika kwa kuuza ziada ya chakula.

Kwa mwaka jana pekee wilaya hiyo ilipata wastani wa mazao mchanganyiko tani 572,000 wakati mahitaji yalikuwa ni tani 138,0000 hivyo kuvuka lengo.

Londo alisema kuanzishwa kwa kiwanda hicho cha kati ni juhudi za Serikali za kutaka kila Mkoa kuhakikisha inafikisha viwanda 100, agizo lililotolewa hivi karibuni na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Selemani Jaffo.

Mkurugenzi wa kiwanda hicho, Petter Isare alisema baada ya kuhitimu masomo ya sheria ya elimu ya juu, waliamua kuanzisha asasi iliyolenga kutoa msaada wa kisheria na katika majukumu yao, wakagundua sehemu kubwa ya waliohitaji ni kutoka kundi la watu maskini wa kipato.

Isare alisema ndipo wakaamua kuangalia namna ya kusaidia kundi kubwa hilo kiuchumi na kiafya kwa wakati mmoja kwa kupitia fursa ya mazao mchanganyiko ndipo wakaanzisha kiwanda hicho.

Mwenyekiti wa kijiji cha Igima Timothy Mwakitalu alisema licha ya kusogea kwa kiwanda hicho kitakachosaidia pia kuhifadhi bure mazao kwenye ghala, kuna changamoto ya barabara.


Atupwa jela miaka 10 kwa kukutwa na bastola




MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemhukumu mfanyabiashara Gairo Mtozoma (43) kwenda kutumikia kifungo cha miaka 10 jela baada ya kukutwa na hatia ya mashtaka mawili, likiwamo la kupatikana na bastola kinyume cha sheria.

Pia Mtozoma alipatikana na hatia ya kukutwa na risasi kinyume cha sheria.

Mtozoma ambaye ni, mkazi wa Magomeni Kagera, jijini Dar es Salaam, alihukumiwa jana na Hakimu Mkazi, Godfrey Mwambapa.

Akisoma hukumu hiyo, hakimu Mwambapa alisema baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na pande zote mbili, amejiridhisha kuwa bila kuacha shaka upande wa Jamhuri umethibitisha makosa dhidi ya mshtakiwa.Alisema kutokana na ushahidi huo, mahakama yake inamtia mshtakiwa hatiani.

"Mahakama hii baada ya kupitia ushahidi wa mashahidi watano wa Jamhuri, imemwona mshtakiwa ana hatia na inamhukumu kwenda jela miaka 10," alisema hakimu Mwambapa. "Kosa la kwanza atatumikia miaka mitano na la pili, atatumikia mitano mingine."

Mapema mahakamani hapo upande wa Jamhuri ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga uliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshtakiwa iwe fundisho kwa wengine.

Katika kesi ya msingi, ilidaiwa kuwa Agosti 11, mwaka jana katika eneo la Magomeni Kagera wilayani Kinondoni, jijini Dar es Salaam, Mtozoma alikutwa na bastola moja aina ya Browing yenye kumbukumbu  namba 90002 iliyosajiliwa kwa namba TZCAR-A222683 bila kuwa na leseni.

Pia ilidaiwa kuwa Agosti 11,2016 katika maeneo ya Magomeni Kagera wilayani Kinondoni alikutwa na risasi sita bila kuwa na leseni.

Bibi afungua kesi ya kuomba talaka mahakamani



MWANAMKE ambaye yupo kwenye ndoa kwa miaka 55, amefungua kesi mahakamani kuomba mumewe ampe talaka kwa madai kuwa hamjali, na anamthamini zaidi mke mdogo.

Mwalimu huyo mstaafu, Marcella Mukami Kinyugo (73), anaiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kangema, isitishe ndoa yake na Peter Kinyugo (76) iliyofungwa Septemba 16, 1962 katika Kanisa Katoliki Kiriaini.

Bibi huyo mkazi wa mjini Kiria-ini, Mathioya, kwenye kaunti ya Murang’a, pia aliomba apewe nusu ya mali za familia yao na pia mumewe alazimishwe kulipa gharama za kesi. Katika kesi hiyo bibi huyo aliwakilishwa na Margret Nyangati kutoka kampuni ya mawakili ya Muchoki Kang’ata.

Aliieleza Mahakama kuwa, waliishi maisha ya furaha ya mume na mke tangu walipofunga ndoa, lakini miaka sita iliyopita hali ilibadilika wakati mumewe alipoacha kutimiza majukumu yake kama mume.

Mume wa bibi huyo ni mwalimu mstaafu na Chifu. Mukami alidai mahakamani kuwa matatizo yalianza baada ya Kinyugo kukaa kwa mke mdogo kwa wiki kadhaa bila kwenda kwake, na kwamba, yeye na mke mwenzake wanaishi kwenye eneo moja. Kwa mujibu wa bibi huyo, wakati mumewe anafanya hivyo, hawakuwa na ugomvi.
Chanzo; Habari Leo

Zari ampa makavu mzazi mwenzie




Zarinah Hassan ‘Zari The BossyLady’

Mipasho! Mwanamitindo mjasiriamali, Zarinah Hassan ‘Zari The BossyLady’ ambaye aliingia katika mtafaruku wa maisha yake ya kimapenzi, kwa mara nyingine juzikati alionyesha kuwepo kwa kutoelewana kwao baada ya kuliamsha dude kwa kutoa maneno ya kumnanga mzazi mwenzake.

Awali, vyanzo vyetu vilivyo karibu na mrembo huyo mwenye watoto watano, alisema kwa sasa hana uhusiano mzuri na baba wa watoto wake wawili, kwa kile kinachosemwa kuwa ni kitendo cha mwenzake huyo kuendekeza mapenzi na wanawake wengine.

“Ni kama mchezo unaelekea mwishoni hivi sasa, maana maneno na ugomvi kati yao hauishi, jamaa anafanya kazi kubwa kuficha kuhusu huu uhusiano wake kuwa juu ya mawe, lakini ukweli ni kwamba hakuna dalili za wawili hawa kukaa tena imara kama zamani,” kilisema chanzo hicho.

Katika tukio la hivi karibuni, mwanamama huyo aliandika katika mtandao wake maneno yenye kumlenga mzazi mwenzake, akisema anaendekeza wanawake na watoto wengi na kwamba badala ya kuona anauza kazi zake nyingi za muziki, yeye amekuwa hodari wa eneo ambalo hahusiki.

Katika kumnanga huko, Zari alisema endapo mtu anatafuta ubalozi wa kondom, ambacho ni kifaa cha kinga dhidi ya magonjwa ya kuambukizwa kupitia ufanyaji mapenzi, basi hana haja ya kuhangaika kumpata, kwa kuwa tayari mtu.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro apata ajali



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Steven Kebwe 

Morogoro. Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Steven Kebwe amepata ajali katikati ya Hifadhi ya Taifa ya Mikumi iliyopo wilayani Kilosa mkoani hapa.

Ajali hiyo ilitokea saa saba usiku wa kuamkia leo Jumatano ambapo inadaiwa gari la mkuu huyo wa mkoa lilimgonga mnyama aina ya Nyati na gari hilo kuharibika vibaya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Urlich Matei amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza kuwa taarifa kamili ataitoa mara baada ya kukamilika.

Inadaiwa kuwa ndani ya gari hilo mbali na kuwepo mkuu wa mkoa pia aliambatana na mlinzi wake ambao wote kwa pamoja walitoka salama.

Mwandishi wa Mwananchi alifanya juhudi za kumtafuta mkuu wa mkoa kwa njia ya simu ili kuzungumza naye juu ya ajali hiyo lakini simu yake iliita bila kupokelewa

Dogo Janja alipoulizwa kwanini hakumsindikiza Uwoya Rwanda?


Kitu Yanga wamesema baada ya kuona Ngoma anacheza Zimbabwe



Kitu Yanga wamesema baada ya kuona Ngoma anacheza Zimbabwe



MA- EX WA DIAMOND PLATNUMZ



MA- EX WA DIAMOND PLATNUMZ



Audio | Mafikizolo Ft Harmonize – Don’t Go | Mp3 Download

Audio | Mafikizolo Ft Harmonize – Don’t Go | Mp3 Download

Mafikizolo Ft Harmonize - Don’t Go

Audio | Mafikizolo Ft Harmonize – Don’t Go | Mp3 Download



                                                       DOWNLOAD HERE

Video | Coyo Ft Honeya – Noma | mp4 Download

Video | Coyo Ft Honeya – Noma | mp4 Download

Coyo Ft Honeya - Noma

Video | Coyo Ft Honeya – Noma | mp4 Download




                                                DOWNLOAD HERE

Audio | Coyo Ft Honeya – Noma | Mp3 Download

Audio | Coyo Ft Honeya – Noma | Mp3 Download


Audio | Coyo Ft Honeya – Noma | Mp3 Download



                                           DOWNLOAD HERE

Video | David Wonder – Mtindo | Mp4 Download

Video | Davidonder – Mtindo | Mp4 Download


Video | David Wonder – Mtindo | Mp4 Download





                                                            

Gospel Audio | David Wonder – Mtindo | Mp3 Download

Gospel Audio | David Wonder – Mtindo | Mp3 Download

Gospel Audio | David Wonder – Mtindo | Mp3 Download


                                            DOWNLOAD HERE