Tuesday, 21 November 2017

Sophia Simba arudi CCM



Dar es Salaam. Aliyekuwa Mwenyekiti wa Wanawake CCM (UWT), Sophia Simba aomba radhi na kuomba kurejea CCM baada ya kufukuzwa uanachama.

Mwenyekiti wa CCM Rais John Magufuli amesoma barua ya Sophia kuomba radhi mbele ya Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na kuwahoji wajumbe kama wanakubali kumsamehe jambo lililokubaliwa.

"MwanaCCM aliyefukuzwa uanachama amekuwa akiandika barua nyingi za kuomba radhi lakini tumekuwa tukinyamaza,  kikao hiki ndiyo kilimfukuza," amesema Rais Magufuli katika kikao hicho kinachofanyika leo Jumanne.

Baada ya kuwahoji wajumbe na kukubaliwa Rais Magufuli aliandika kwenye barua hiyo kuwa amekubaliwa kurudi CCM.

Ruge kukutana na Makonda Kuhusu Tamasha la Fiesta



Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, Jumatatu hii amefunguka kuzungumzia tetezi ya kwamba Tamasha la Muziki la Fiesta litaishia 6 usiku tofauti na miaka iliyopita kutokana na hali ya usalama.

Hatua hiyo imekuja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda hivi karibuni akiwa katika kituo cha redio cha EFM kuzungumza juu ya matukio ya burudani kutotakiwa kufanyika zaidi ya saa sita usiku kwenye maeneo ya wazi Dar es salaam.

Tamasha la FIESTA 2017 linatarajiwa kufanyika Leaders Club Jumamosi hii November 25 huku ticket tayari zikiwa zimeshazagaa mitaani.

Ruge ambaye ni Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group amesema “Tunafanya juhudi za kujaribu kuona kama tunaweza tukampata Mkuu wa Mkoa”

Zelothe azungumza kimasai wakati akiomba kura




    Arumeru. Vituko na vioja vimezidi kutawala kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani Kata ya Musa mkoani hapa baada ya mgombea udiwani kupitia CCM, Flora Zelothe kuamua kuongea kimasai kwa lengo la kuwashawishi wananchi wampe kura.

Zelothe, aliamua kutumia lugha hiyo juzi wilayani Arumeru kama njia mojawapo ya kuwashawishi wapigakura wa eneo hilo ambao kwa asilimia kubwa ni makabila ya Wameru na Wamasai.

Akizungumza katika mkutano huo, Zelothe alisema wananchi wakimchagua atatekeleza mradi wa maji uliokuwa unagharamiwa na Benki ya Dunia eneo la Makutian ambao umesimama baada ya kuvurugwa na baadhi ya wanasiasa.

Akinadi sera zake kwa kimasai huku akiwa na mtafsiri wake pembeni aliwaambia wapigakura amejipanga kujenga shule ya sekondari.

Alisema kwa miaka mitano akiwa diwani wa viti maalumu alifanikiwa kuchonga barabara zote za vitongoji ndani ya Kata ya Musa kwa kiwango cha changarawe.

“Tutaboresha Shule ya Sekondari ya Kata ya Musa na kuleta walimu wa masomo ya sayansi na sanaa,” alisema Zelothe huku akishangiliwa.

Awali akimkaribisha jukwaani mwenyekiti wa CCM mkoani Arusha, Lekule Laiser alisema mgombea huyo ni mwanamke lakini ni jasiri na anajenga hoja.

Laiser alisema Zelothe aliwahi kwenda kupinga matokeo ya uchaguzi wa udiwani wa kata hiyo mwaka 2015 mahakamani na kusimamia kesi bila kuyumba na hilo linaonyesha dhahiri anafaa kuwa kiongozi.   

Breaking News: Clouds Media Group inawaka moto



Sehemu ya jengo la kituo cha Chouds Media Group linaungua moto muda huu. Juhudi za kuuzima moto huo bado zinaendelea.

MAGAZETI YA LEO 21/11/2017

MAGAZETI YA LEO 21/11/2017























Rais Magufuli hajatengua uteuzi wa Dkt. Laurian Ndumbaro


Taarifa zinazoenezwa kupitia mitandao ya kijamii kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt. Laurian Ndumbaro sio za kweli na zipuuzwe.

Wananchi endeleeni kupokea taarifa rasmi kutoka kwenye mamlaka na vyombo rasmi vya Serikali, na pia watumiaji wa mitandao ya kijamii mnakumbushwa kuwa kueneza taarifa za uongo ni makosa kisheria.

Serikali itawafuatilia wote waliozusha taarifa hizi na kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam


Baada ya Polisi kushikilia simu yake, Zitto ajipanga kuwashitaki




Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Kabwe, amesema anajipanga kulifungulia kesi ya kikatiba jeshi la polisi nchini kutokana na kushikilia simu yake.

Zitto ameeleza kuwa simu yake inashikiliwa tangu Novemba 7 mwaka huu alipokamatwa kwa tuhuma za kuvunja sheria ya takwimu  na sheria ya makosa ya mtandao.

“Walisema watahitaji simu hiyo kwa siku mbili tu, nilikwenda polisi KAMATA siku tatu baadaye nikaelezwa kuwa bado wanaendelea na uchunguzi. Nimerudi leo tarehe 20, Polisi wanasema bado wanahitaji simu yangu hiyo”, amesema Zitto.

==>Aliyoyasema Zitto kupitia akaunti yake ya Facebook:

Ndugu, Jamaa na Marafiki, mtakumbuka kuwa mnamo tarehe 7/11/2017 Jeshi la Polisi walichukua Simu yangu kwa ajili ya uchunguzi wao kuhusu tuhuma dhidi yangu kwa mujibu wa sheria ya takwimu na sheria ya makosa ya mtandao. Walisema watahitaji simu hiyo kwa siku 2 tu.

Nilikwenda polisi KAMATA siku 3 baadaye nikaelezwa kuwa bado wanaendelea na uchunguzi. Nimerudi leo tarehe 20/11/2017, Polisi wanasema bado wanahitaji simu yangu hiyo.

1) Nawakumbusha kuwa msitumie simu ile 0767777797 kwani bado imeshikiliwa na Polisi

2) Katiba ya Nchi yetu kifungu cha 16(1) na (2) imeweka msingi wa nguvu sana haki ya FARAGHA kwa raia na kwamba hata sheria ikitaka haipaswi kuingilia mawasiliano binafsi ya Raia.

Nina mashaka kuwa Jeshi la Polisi linakaa na Simu yangu muda wote huu kwa sababu za zaidi ya uchunguzi wao wa makosa wanayonituhumu nayo. Nimeamua kuwaachia Simu mpaka hapo watakapotosheka lakini wajiandae na kesi ya kikatiba ambayo pia italinda haki za wananchi wengi wanaothirika na matumizi mabaya ya sheria ya Mtandao ( cybercrime act ).
Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Kabwe, amesema anajipanga kulifungulia kesi ya kikatiba jeshi la polisi nchini kutokana na kushikilia simu yake.

Zitto ameeleza kuwa simu yake inashikiliwa tangu Novemba 7 mwaka huu alipokamatwa kwa tuhuma za kuvunja sheria ya takwimu  na sheria ya makosa ya mtandao.

“Walisema watahitaji simu hiyo kwa siku mbili tu, nilikwenda polisi KAMATA siku tatu baadaye nikaelezwa kuwa bado wanaendelea na uchunguzi. Nimerudi leo tarehe 20, Polisi wanasema bado wanahitaji simu yangu hiyo”, amesema Zitto.

==>Aliyoyasema Zitto kupitia akaunti yake ya Facebook:

Ndugu, Jamaa na Marafiki, mtakumbuka kuwa mnamo tarehe 7/11/2017 Jeshi la Polisi walichukua Simu yangu kwa ajili ya uchunguzi wao kuhusu tuhuma dhidi yangu kwa mujibu wa sheria ya takwimu na sheria ya makosa ya mtandao. Walisema watahitaji simu hiyo kwa siku 2 tu.

Nilikwenda polisi KAMATA siku 3 baadaye nikaelezwa kuwa bado wanaendelea na uchunguzi. Nimerudi leo tarehe 20/11/2017, Polisi wanasema bado wanahitaji simu yangu hiyo.

1) Nawakumbusha kuwa msitumie simu ile 0767777797 kwani bado imeshikiliwa na Polisi

2) Katiba ya Nchi yetu kifungu cha 16(1) na (2) imeweka msingi wa nguvu sana haki ya FARAGHA kwa raia na kwamba hata sheria ikitaka haipaswi kuingilia mawasiliano binafsi ya Raia.

Nina mashaka kuwa Jeshi la Polisi linakaa na Simu yangu muda wote huu kwa sababu za zaidi ya uchunguzi wao wa makosa wanayonituhumu nayo. Nimeamua kuwaachia Simu mpaka hapo watakapotosheka lakini wajiandae na kesi ya kikatiba ambayo pia italinda haki za wananchi wengi wanaothirika na matumizi mabaya ya sheria ya Mtandao ( cybercrime act ).



Kinga ya VVU kutolewa mwakani

Serikali inatarajia mwakani, kuanza kutoa dawa za kujikinga na maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU), ikiwa ni mkakati za kuwazuia watu kutopata maradhi hayo



Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Faustine Ndugulile

Dawa hiyo ni Truvada na utaratibu huo utakuwa wa majaribio na utahusisha watu 12,000 wanaojidunga dawa za kulevya, machangudoa na wanaofanya mapenzi ya jinsia moja.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Gazeti la Serikali la Habari Leo, imeeleza kuwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Faustine Ndugulile alisema: “Hii ni tiba kama kinga na tutawapima kwanza wote 12,000 na wale wasiokuwa na maambukizi ya VVU ndiyo tutawapa dawa ambao tunajua wanaendelea na ngono zembe, kisha tutafuatilia mienendo yao kwa mwaka mmoja na ikibidi kuongeza iwe miaka miwili.”

Watu hao watakaofanyiwa utafiti huo wa majaribio ni kutoka mikoa ya Njombe, Kagera, Iringa, Mwanza, Mbeya na Dar es Salaam. Dk Ndugulile alisema kutakuwa na timu ya wataalamu ya kufuatilia mienendo yao na afya zao wote watakaokuwa kwenye majaribio hayo. Alisema timu hizo zitagawanywa katika kanda tatu ikiwemo Kanda ya Ziwa.

Alisema dawa hizo watakuwa wakipewa kila mwezi. Vidonge hivyo serikali haijanunua, bali imepata taasisi za Presidents Emergency Plan for Aids Relief (PEPFAR) na Global Fund. “Hizi dawa ni katika mkakati wa kidunia wa kuzuia maambukizi mapya na sisi tumepewa na taasisi hiyo ya Marekani ya PEPFAR na Global Fund,” alieleza Dk Ndugulile.

Dk Ndugulile alisema wanakamilisha taratibu za kuanza kwa majaribio hayo ikiwemo kupata vibali, hivyo hawajajua rasmi lini wataanza kazi hiyo isipokuwa itakuwa mwakani. Sasa hivi nchi nyingi zinatumia Truvada kama kinga dhidi ya maambukizi mapya ya Virusi Vya Ukimwi na miongoni mwao ni pamoja na Kenya, Uganda, Peru na Marekani.

Kwa mujibu wa mtandao wa Truvada.com, utumiaji wa dawa hizo ambao umeidhinishwa na Shirika la Afya Duniani(WHO) una mafanikio makubwa, unaweza kuleta madhara kama ya matatizo ya figo, kuwepo asidi ya lactic nyingi, maumivu ya tumbo, maumivu ya misuli.

Athari nyingine ni kuhema kwa kasi au kasi ya kuhema kuwa chini, kutapika, mapigo ya moyo kuwa katika hali isiyo ya kawaida, tatizo la ini, kichwa kuuma na kupungua uzito. Dawa hiyo ya Truvada imeingizwa nchini mwaka 2013 na imekuwa ikitumika kwenye tiba kama sehemu ya dawa za kufubaza Virusi Vya Ukimwi (ARVs). Inakadiriwa watu milioni 1.4 wanaishi na VVU nchini na maambukizi mapya yameonekana kupungua kila mwaka.

Takwimu zilizotolewa na Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) zinaonesha mwaka 2013 maambukizi hayo mapya yalikuwa kwa watu 72,000, mwaka uliofuata yalikuwa watu 69,603 na mwaka 2015 yameshuka na kuwa watu 48,000. Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Tacaids, Dk Jerome Kamwela amesema katika semina ya wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ukimwi kadiri dawa za kufubaza virusi vya Ukimwi (ARVs) zinavyoongezeka, vifo vitokanavyo na Ukimwi vinapungua.

Alisema hali ya maambukizi kwa Tanzania ni asilimia 5.3 huku Manyara na Tanga kwa Tanzania Bara, kiwango cha maambukizi kikiwa chini zaidi na Zanzibar, Pemba kipo chini. Makundi yaliyo hatarini zaidi kwa maambukizi na asilimia yao kwa wastani wa kitaifa yakiwa kwenye mabano ni makahaba (26), wanaume wanaofanya mapenzi ya jinsia moja (22.2) na wanaojidunga dawa za kulevya (15). Mengine yaliyo hatarini ni madereva wa malori ya masafa marefu, wafungwa na wafanyakazi wanaohama kufuata ajira.

Waliokwapua fedha Saudi Arabia watakiwa kurejesha



Mamlaka za Saudi Arabia zimewataka watoto wa kiume wa familia za kifalme na baadhi ya wafanyabiashara wanaoshikiliwa kurudisha mali walizojipatia kwa njia isiyo halali ili waweze kuachiwa huru, vyombo vya habari vimeripoti.

Shirika la habari la Bloomberg limesema watu 201 wakiwemo wafanyabiashara, mawaziri na wana wa ufalme miongoni mwao mwana mfalme Alwaleed bin Talal anayemiliki jengo refu la ghorofa katika mji mkuu, Riyadh wanashikiliwa na mamlaka za Saudi Arabia katika kampeni yake ya kukabiliana na rushwa. Pia, mamlaka zimefunga akaunti zao za benki.

Taarifa za vyombo vya habari zinasema kuwa mamlaka nchini Saudi Arabia zimewataka wanaoshikiliwa kurudisha mali walizopata kwa njia ya rushwa ikiwa wanataka kuachiwa huru na wasifunguliwe mashitaka. Inakadiria kuwa kati ya dola za Marekani 50 bilioni na 100 bilioni zitahamishwa kwenda hazina ya taifa.

Mapambano dhidi ya mafisadi yanaongozwa na mwana mfalme Mohammed bin Salman anayejaribu kuimarisha nguvu yake ya kimamlaka kabla ya kuapishwa rasmi kuwa mrithi wa ufalme.

Wachambuzi wa masuala ya siasa wanaamini kuwa anataka kukusanya fedha anazohitaji kwa ajili ya kufanya mageuzi ya kiuchumi nchini.

Rose Ndauka awafungukia watoa mimba


Rose Ndauka.

MSANII wa Filamu Bongo, Rose Ndauka amewarushia dongo wasichana wa kizazi kipya ambao wengi wao wakipata mimba wanakimbilia kutoa badala ya kujifungua.

Ndauka ameiambia Full Shangwe, kuwa wanawake wengi wakipata ujauzito hutoa bila kujua kuwa mtoto ni faraja ya mwanamke na uhusiano kwa ujumla. “Nawashangaa wasichana wengi ambao wakipata mimba wanakimbilia kutoa.

I wish kama wangejua furaha, faraja na thamani ya mwanamke ni mtoto, wasingefanya hivyo,” alisema. Aliongeza: “Huwezi amini furaha ya kuwa na mtoto kwa mzazi ni zaidi ya changamoto.”

Jaji Warioba, Serukamba waumizwa kichwa na Mfumo wa elimu

Jaji Warioba, Serukamba waumizwa kichwa na Mfumo wa elimu



   Dar es Salaam. Waziri mkuu mstaafu, Joseph Warioba na mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo na Huduma za Jamii, Peter Serukamba wamesema mfumo wa elimu unaotolewa sasa una kosoro hivyo unahitaji kufumuliwa na kuundwa upya.

Mbali ya Jaji Warioba na Serukamba, wadau wengine wamesema Tanzania ya viwanda haitafanikiwa ikiwa elimu itolewayo haiwaandai wahitimu kujitegemea badala yake wanakuwa tegemezi.

Hayo waliyasema jana katika kongamano litakalomalizika leo ambalo limeandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Taasisi ya HakiElimu linalojadili kuelekea Tanzania ya viwanda na Sera ya Ujamaa na Kujitegemea.

Jaji Warioba ambaye ni mwenyekiti wa kongamano hilo, alisema elimu inayotolewa inapaswa kuendana na mazingira ya wakati huu na kujibu mahitaji ya wahitimu.

Alisema licha ya mafanikio yanayofanywa na Serikali, kuna changamoto kubwa hususan ubora wa elimu inayotolewa kutowaandaa wahitimu kujitegemea kama ilivyokuwa awali.

“Uwiano wa wanafunzi wanaomaliza shule na wanaoendelea sekondari ni mdogo, wanaomaliza sekondari na kwenda chuo mdogo zaidi. Zamani mtu akimaliza darasa la nne anajua kusoma, kuandika na kuhesabu lakini sasa mtu anamaliza darasa la saba hajui kusoma, kuandika na kuhesabu,” alisema Warioba ambaye ni Jaji mstaafu na kuongeza: “Kuna matatizo makubwa ya miundombinu katika shule na vyuo kama madarasa na nyumba za walimu. Vitendea kazi na idadi ya walimu katika ngazi zao na maslahi ya walimu ni tatizo, haya yote yanatakiwa kupata majibu.”

Jaji Warioba aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba alisema: “Siku hizi watu wanamaliza lakini hawana la kufanya, lazima tujiulize elimu yetu ni bora kwa mazingira ya baadaye?

Naye Serukamba ambaye ni mbunge wa Kigoma Kaskazini (CCM) akichangia mada alisema: “Wote tunakubali tatizo lipo ila hatujui lini tunalimaliza. Umefika wakati tukae tuangalie mfumo, tuangazie elimu ya awali hadi vyuo vikuu.”

Alitaja maeneo yanayohitaji kuangaliwa kuwa ni ubora wa elimu inayotolewa, ufundishaji, uongozi, muda wa kusoma na maudhui kuanzia chini hadi juu.

“Tukifikia hapo tutaweza kujibu challenges (changamoto). Tunapaswa kuufumua mfumo wetu tuunde tume ya elimu ambayo itakuja na majibu ya wapi tuboreshe... leo wanaokwenda kusoma ualimu si waliofaulu vizuri, ukiangalia Finland anayekwenda kusoma kafaulu vizuri na mtumishi anayelipwa vizuri ni mwalimu,” alisema Serukamba.

Makamu mkuu wa UDSM, Profesa Rwekaza Mukandala alisema elimu bora ni ile inayomfanya mtu aweze kutumia maarifa na ujuzi alioupata kupambana na mazingira yake.

“Elimu sahihi ni ile inayoondoa pengo kati ya maarifa ya kinadharia yanayotolewa darasani na yale ya vitendo yanayopatikana katika jamii. Elimu mwafaka ni elimu ya kujitegemea,” alisema.

Akizungumza kwenye kongamano hilo, mkuruenzi mtendaji wa HakiElimu, John Kalage alisema: “Tunahitaji kuuangalia mfumo, je unajibu mahitaji ya sasa, je mfumo gani tuutumie sasa, kwani uliopo umeshindwa kuwaandaa wahitimu watakaokwenda kujitegemea na si kuwa tegemezi?”

Akifungua kongamano hilo kwa niaba ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Waziri wa Nchi (Tamisemi), Suleiman Jafo alisema Serikali itayachukua mapendekezo yote watakayofikia na kuyafanyia kazi.

“Tupo pamoja, Rais John Magufuli amefurahishwa na ninyi wasomi kukutana kujadili ikiwamo suala la uchumi wa viwanda na yeye amesema atakuwa tayari kupokea mapendekezo mtakayoyafikia na kuyafanyia kazi,” alisema Jafo.

“Taifa hili litajengwa na sisi wenyewe, tutumie kongamano hili kujadili kwa kina bila woga kwani tusipojenga msingi mzuri wa elimu yetu katika ushirikiano huu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, tutakuwa wasindikizaji,” alisema.

Naye Waziri wa viwanda, Charles Mwijage alisema: “Hakuna hofu mtu kujitathmini wapi ametoka, yupo wapi na anakwenda wapi.”

Mwigage alisema tayari ameagiza uongozi wa Chuo cha Biashara (CBE) kutoa kozi kwa kila mwanafunzi ya ujasiriamali ili kuwawezesha wanapohitimu waweze kuwa wajasiriamali. 



Dk Kaunda kwenda kumshawishi Mugabe ajiuzulu


Harare, Zimbabwe. Chama tawala cha Zanu-PF kimewaita wabunge wake ili kuwapanga waanzishe mchakato wa kumshtaki bungeni Rais Robert Mugabe huku kukiwa na taarifa kwamba rais wa zamani wa Zaimbia, Kenneth Kaunda anakwenda kumshawishi mpigania uhuru mwenzake ajiuzulu.

Taarifa kutoka Lusaka, Zambia zinasema Rais Edgar Lungu amemtuma Dk Kaunda kwenda Harare kujaribu kumshawishi Rais Mugabe “ajiuzulu kwa heshima” baada ya jeshi kutwaa madaraka wiki iliyopita.

"Dk Kaunda alisafiri kwa ndege ya rais na ametua Harare," ofisa mwandamizi wa serikali ya Zambia aliliambia jana shirika la habari la Reuters. Kaunda ana umri wa miaka 93 sawa na Mugabe.

Hazijapatikana habari zaidi juu ya safari hiyo. Lakini ndani ya makao makuu ya Zanu PF, gazeti la NewsDay la Zimbabwe limripoti kwamba mbunge mmoja aliyezungumza kwa sharti la kutoandikwa jina alisema kikao cha wabunge wa chama tawala kiliitishwa kujadili hatua ya kumshtaki mwanampinduzi huyo ambaye taifa linamtaka astaafu.

"Tumeitwa na tumeambiwa tufike kwenye makao makuu ya chama kabla au ifikapo saa 8:30 mchana leo (jana)” alisema. Mnadhimu mkuu wa Zanu-PF Lovemore Matuke alithibitisha habari hizo na kwamba kikao kilitarajiwa kuanza saa 10:00 jioni.

Chama cha Zanu PF, ambacho Mugabe alikiasisi na kukiongoza kwa miongo kadhaa Jumapili kilitoa tamko la kumfuta uongozi wa chama na kikamtaka awe amejiuzulu urais kufikia saa 6:00 mchana jana vinginevyo asubiri kushtakiwa na kuondolewa bungeni.

Mugabe alipuuza hali ambayo Rais Lungu ameamua kumtumza Dk Kaunda ili mkongwe huyo aliyetawala kwa miaka 37 tangu Zimbabwe ilipopata uhuru asiondolewe katika namna itakayomwondolea heshima.



Muda wa mwisho

Muda wa mwisho wa kujiuzulu kwa hiari ambao Rais Mugabe alikuwa amepewa na chama chake cha Zanu PF ulipita bila kutolewa taarifa rasmi huku uvumi ukienea kuhusu hatima yake

Japokuwa haijatolewa taarifa yoyote chanzo kilichokaribu na timu ya majadiliano upande mmoja wakiwemo majenerali waliotwaa madaraka wiki iliyopita kimeliambia shirika la utangazaji la CNN kwamba Rais Mugabe amekubali kung’atuka na kwamba ameshaandaa barua ya kujiuzulu.

Chanzo hicho kilidokeza kwamba majenerali wameridhia matakwa mengi ya Mugabe ikiwa ni pamoja na kupewa kinga ya kutoshtakiwa yeye na mkewe Grace, na abaki na mali zake.

CNN limeambiwa kwamba chini ya makubaliano hayo, Mugabe na Grace hawatashtakiwa. Pia, viongozi wawili waandamizi wa serikali ya Mugabe waliliambia shirika la habari la Reuters Jumapili kwamba Mugabe alikuwa amekubali kujiuzulu lakini hawakuwa wanajua yaliyomo katika mkataba wa kuondoka kwake.

Ili ionekane amejiuzulu rasmi, utaratibu ni kwamba barua lazima iandikwe kwenda kwa Spika wa Bunge, chanzo kingine kimeongeza.

Mugabe ambaye anakabiliwa na shinikizo la kujiuzulu kutoka kila kona aliwashangaza watu Jumapili alipokataa kufanya hivyo alipolihutubia taifa kwa njia ya televisheni akiwa ikulu.

Chama chake cha Zanu PF kimempa Mugabe, ambaye amekuwa katika kizuizi cha nyumbani na jeshi lililotwaa madaraka kimempa hadi mchana leo kuondoka vinginevyo atashtakiwa bungeni.

Jumamosi, maelfu ya Wazimbabwe walijimwaga mitaani kupaza sauti zao wakimtaka mzee huyo mwenye umri wa miaka 93, ajiuzulu.

Agoma

Jumapili mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 93 aliwashtua watu alipokataa wito wa kujiuzulu na hivyo kuitumbukiza Zimbabwe katika wiki ya pili ya mgogoro wa kisiasa huku juhudi za kuhitimisha utawala wake wa miaka 37 mfululizo zikikwama.

Chama cha Zanu PF alichoasisi na kukiongoza kwa miongo kadhaa kilitangaza kumwondoa kama kiongozi na kilimpa muda hadi Jumatatu mchana kuachia urais vinginevyo atashtakiwa bungeni.

Kabla ya kumwondoa Mugabe katika nafasi ya uongozi, Zanu PF ilitangaza kumrejesha katika chama makamu wa rais aliyefukuzwa Emmerson Mnangagwa kisha kikamteua kuwa kiongozi wake mpya. Mugabe alimfukuza Mnangawa Novemba 6 kwa madai ya usaliti hali iliyochochea mgogoro wa kisiasa.


Maneno ya Mama Lulu baada ya mwanae kwenda jela

Maneno ya Mama Lulu baada ya mwanae kwenda jela





Elizabeth Michael ‘Lulu’.

SIKU tano baada ya mwanaye ambaye ni staa wa Bongo Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’ mama yake mzazi, Lucresia Karugila, kwa mara ya kwanza amefunguka baada ya mtoto wake huyo kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili jela kwa kosa la kumuua bila kukusudia staa mwenzake, Steven Kanumba aliyekuwa pia mwandani wake.

Awali, kulienea lawama nyingi mitandaoni baada ya Lulu kuhukumiwa kuwa huenda kuna mahali wazazi walikosea malezi ndiyo sababu ya mtoto wao huyo kujihusisha na masuala ya kimapenzi akiwa na umri wa chini ya miaka 18 ambao hakubaliki.

Kufuatia hali hiyo, Ijumaa Wikienda lilimtafuta mama Lulu ili kujua mtazamo wake juu ya mwanaye kwenda jela na madai ya mitandaoni ndipo akafunguka mazito. Mama Lulu aliliambia gazeti hili kuwa, kwa sasa hapendi kuzungumza hovyo na watu na anahitaji muda mwingi wa kupumzika kwa kuwa hayuko vizuri. “Nafikiri kwa kipindi hiki nahitaji zaidi kupumzika kwa muda mwingi na sipendi kuzungumza hovyohovyo, siko vizuri kabisa,” alisema mama Lulu kwa sauti ya unyonge.

Lulu akiwa na mama yake Lucresia Karugila.
Akiendelea kuzungumza, mama huyo alisema kuwa, tangu apate majanga ya mtoto wake huyo hadi kwenda jela hayupo vizuri na wala hapendi kuongea kwa sababu hajisikii kufanya hivyo kwani anahisi anaiona dunia chungu. “Najua watu watanishangaa sana, lakini ndiyo nimeamua kuwa hivyo, siko sawa na sijisikii vizuri kabisa. “Sidhani kama kuna mzazi yeyote anaweza kupata usingizi wakati mwanaye yupo kwenye mateso kama ilivyokuwa zamani, kiukweli ninaumia sana,” alisema mama Lulu.

DAKTARI NAYE ANENA!

Naye daktari wa magonjwa ya binadamu, Dk Godfrey Chale, akizungumzia hali ya Lulu baada ya hukumu hiyo alisema kuwa, kuna magonjwa ambayo huweza kumpata mtu mwenye matatizo ya kimaisha ikiwemo kufungwa jela ikiwa ni pamoja na kuwa kichaa kutokana na msongo.

Dk Chale alisema mara nyingi watu ambao hupatwa na majanga makubwa kama la Lulu, huwa kwenye uwezekano mkubwa wa kukumbwa na msongo ambao husababisha mpangilio mbovu wa homoni kiutendaji na mhusika kuchanganyikiwa endapo atashindwa kukubaliana na mazingira ya tatizo.
Alisema kuchanganyikiwa kwa watu wenye matatizo kama ya Lulu, hutokana na kuzidiwa na huzuni na mgandamizo wa hisia (depression) hivyo kushindwa kabisa kuzuia mfumo wa kufikiri na kutafakari na ndiyo maana unakuta mtu anaongea peke yake au kufanya vitendo vya ajabu kama kuokota vitu mbalimbali kama sehemu ya kujifariji na hapo ndipo tatizo la kuchanganyikiwa huanzia.

Tatizo kubwa jingine ambalo linaweza kumpata Lulu ni kupoteza popularity momentum (nguvu ya umaarufu) na kushuka kwa uchumi atakapomaliza kifungo kwani kwa kipindi ambacho yuko jela atapoteza mikataba yake ya kikazi kama matangazo na uigizaji, vitega uchumi ambavyo vilikuwa vikimuingizia kipato cha kuyaendesha maisha yake