Friday, 20 October 2017

Chris Brown kurudiana na Rihanna?

Mkali wa Muziki wa Pop, Christopher Maurice ‘Chris Brown’ akiwa na Rihanna.
TAARIFA kutoka chini ya kapeti zinaeleza kuwa, miezi michache baada ya kutengeneza filamu fupi ya maisha yake, mkali wa Muziki wa Pop, Christopher Maurice ‘Chris Brown’ huenda akarudiana na aliyewahi kuwa mpenzi wake, Rihanna.
Kwa mujibu wa chanzo cha karibu na Chris, baada ya filamu hiyo kutoka inayoitwa Welcome To My Life, Chris anaamini kwa asilimia kubwa Rihanna ameiona yote na atakuwa tayari kurudiana naye. “Chris anaamini Rihanna ameshamsamehe baada ya kuangalia filamu.
Chris alishawahi kumwambia rafiki yake anataka kuwa anamchukua Rihanna na kwenda naye kwenye filamu,” kilisema chanzo.

Moto wateketeza Hoteli ya Kifahari

Moto mkubwa imeteketeza hoteli kubwa ya kifahari katika mji wa Yangon nchini Myanmar na kumuua mtu mmoja.
Watu wengine walijeruhiwa kwenye moto huo ambao ulianza mwendo wa saa 20:30 GMT siku ya Jumatano katika hoteli ya Kandawgyi Palace.
Iliwachukua mamia ya wazima moto saa kadha kuuzima moto huo. Zaidi ya wageni 140 waliondolewa.
Haijuliana moto huo ulinza kwa njia gani huku ripoti za kukanganya zikisema kuwa kulikuwa na mlipuko wa mtungi wa gesi au hutilafu ya umeme.
"Hakukuwa na king'ora na vurugu zilikuwa ni kama kulikuwa na walevi hotelini," mtalii mmoja alisema, akiongeza kuwa ni mfanyakazi mmoja ambaye alimuelekzea eneo salama.
Wageni wamehamishwa kweda kwa hoteli zingine mjiji Yangon.
Hoteli hiyo ili kando ya ziwa Kandawgyi, ilijengwa miaka ya 1990 lakini huenda uwepo wake uliazia miaka ya 1930 wakati eneo hilo lilikuwa likitumia kama klabu ya wanajeshi wa Uingereza.
Hoteli ya kifahari kabla ya kuteket

AUDIO | Timmy Tdat Ft Dela _ We'll Be Ok | Download

AUDIO | Timmy Tdat Ft Dela – We’ll Be OK | Mp3 Download

https://my.notjustok.com/track/download/id/282765/by/DM19joF3B~

VIDEO : Harmonize _ Nishachoka | Download

https://cloudup.com/files/iuRG9ODfNAv/download

Thursday, 19 October 2017

Nyalandu Akomalia katiba

Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM) amefunguka na kusema katika kikao cha Tisa cha Bunge kinachotarajiwa kuanza Novemba 7, 2017 Dodoma anakusudia kuwasilisha azma yake ya kupeleka muswada binafsi utakao weka sharti la kurejea mjadala wa Katiba Mpya.
Nyalandu amesema hayo leo kupitia mitandao yake ya kijamii na kusema amekusudia kufikisha jambo hilo mbele ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai.
"Nakusudia kuwasilisha kwa spika wa Bunge Mh. Job Ndugai. Azma yangu ya kuleta muswada binafsi wa sheria katika kikao kijacho cha Bunge itakayoweka sharti la kurejea upya mjadala wa Katiba Mpya ya Tanzania, kwa kuzingatia rasimu ya Katiba kama ilivyowasilishwa na Tume ya Jaji Warioba" alisema Lazaro Nyalandu
Suala la Katiba Mpya licha ya kuwa siyo kipaumbele cha Rais John Pombe Magufuli lakini wadau mbalimbali wamekuwa wakilizungumzia wakisema kuna haja kubwa ya mchakato huo wa Katiba mpya kuendelea sasa wakidai kuwa huu ni wakati sahihi zaidi mchakato wa Katiba Mpya kuendele

Chadema yajilipua kuhusu lowassa

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar), Salum Mwalimu amefunguka na kusema kwamba wanawaruhusu Chama cha Mapinduzi watumie nafasi ya Lowassa kuwepo Chadema kuwaita wao mafisadi kama jinsi wao walivyofanya kwa miaka mingi.
Salumu amesema kwamba kuwataja watu ambao waliwaita vinara wa ufisadi na leo wapo nao kwenye chama chao ulikuwa ni wajibu wao kama chama cha upinzani kutumia upenyo wa udhaidfu wa chama cha mapinduzi kuonyesha wananchi madhaifu ya serikali.
"Lazima ukubali kwamba ni wajibu wetu kuonyesha madhaifu ya serikali, Kama tulikuwa tunampinga Lowassa kwamba ni fisadi ulikuwa ni wajibu wetu Chadema. Sasa kama leo hii Lowassa yupo kwetu ni wajibu wao CCM kuwaambia watanzania kuwa Chadema kina mafisadi. Kwa sababu Lowassa amekuja Chadema ni yule yule wala hajawa malaika kama jinsi ambavyo kelele zinavyopigwa," Mwalimu amefunguka
Akizungumzia kuhusu chama kupwaya na kumtegemea mtu mmoja kuwa mkosoaji wa serikali iliyopo Madarakani, Mwalimu amesema kupanga ni kuchagua hivyo wao kama Chadema wanauwezo mkubwa wa kukosoa lakini huamua kuchagua nani atoe hoja kwa wakati gani na siyo kwamba wameishiwa.
"Hata kwenye timu ya mpira wapo mastaa wengi wanaofanya vizuri lakini huangaliwa ni nani wa kuibeba timu, ndivyo hata Chadema ilivyo, mnaweza kuwa wengi lakini kupanga ni kuchagua, Tundu ni Mwanasheria Mkuu wa chama hivyo chama kinaanda ajenda lakini atachaguliiwa mmoja wa kuifikisha ajenda hiyo huku wengine tukitoa sapoti, inategemea ajenda hiyo pia inatolewa wakati gani, mbona hapa katikati mengine yametokea kwani tumemuinua Lissu kitandani atusaidie kusema. si tulisema wenyewe. ? hivyo hakuna mtu mmoja anayeibeba Chadema bali tunashirikiana pamoja", Mwalimu ameoneza.
Huu ni utaratibu wetu hata kipindi cha kina Mh. Zitto Kabwe pamoja na Dkt. Slaa wote agenda zilikuwa ikitengenezwa na watu ndani ya chama na wanaozipeleka mbele huwa ni wachache siyo kwamba eti chama kimepwaya.
Katika hatua nyingine Mwalimu amesema lengo la chama cha upinzani ni kushika dola na siyo kusikiliza jinsi ambavyo watu wengine wanavyokosoa na kusisitiza kwamba Chama chao kilianzishwa kwa malengo ya kuja kushika dola.

Wema Sepetu na wasanii wengine wamfaliji Lulu

Dar es Salaam . Msanii wa fani ya uigizaji filamu nchini, Wema Sepetu ni miongoni mwa watu waliomfariji Elizabeth Michael ‘Lulu’ anayekabiliwa na kesi ya kuua bila kukusudia iliyoanza kusikilizwa leo katika Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.
Wasanii wametumia mtandao wa Instagram kumfariji mwigizaji Lulu ambaye ni mshindi wa tuzo za filamu za AMVCA.
Jackline Wopler, Katarina Karatu, Nisha, Aunt Ezekiel na wengine wametuma picha za mwigizaji huyo zikiambatana na maneno ya kumfariji wakimweleza kuwa atavuka salama katika mtihani huo.
Kupitia ukura wake wa Instagram, Wema ameweka picha ya Lulu na kuandika, “This Too Shall Pass Baby… God is Great u know… so have faith… ur in my prayers,” akiwa na maana hata hili litapita, Mungu ni mkubwa hivyo anatakiwa kuwa na imani na atamwombea.
Lulu anadaiwa Aprili 7,2012 alimuua bila ya kukusudia mwigizaji mwenzake Steven Kanumba, eneo la Sinza Vatican jijini Dar es Salaam. Kesi inasikilizwa na Jaji Sam Rumanyika.

Harmonize afurahia support anayopata toka kwa Wolper

Msanii wa Bongo Flava kutoka label ya WCB, Harmonize amefunguka mambo kadhaa kuhusu aliyekuwa mpenzi wake, Jacqueline Wolper.
Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Shulala’ ameiambia XXL ya Clouds Fm kuwa anafurahi kuona anapata support ya Wolper katika muziki wake.
“Nadhani mwanzo ilikuwa hasira tu, nashukuru kuona support ya Wolper, namchukulia kama shabiki yangu tu” amesema Harmonize.
Hiyo juzi katika mtandao wa Instagram Jacqueline Wolper aliposti video mbili zikimuonyesha akifurahia kusikiliza ngoma hiyo ambayo Harmonize amemshirikisha Korede Bello.

Waziri kigwangalla atoa siku 7

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Hamisi Kigwangalla amefunguka na kuwapa siku saba wavamizi ambao wapo kwenye pori tengefu la Loliondo kuondoka mara moja ndani ya siku hizo kwani wasipofanya hivyo baada ya hapo mali zao zitataifishwa na serikali.
Kigwangalla amesema uwepo wa wavamizi hao ambao wana ng'ombe zaidi ya 6,000 na matrekta zaidi ya 200 kutoka nchi ya jirani imekuwa sababu kubwa ya chanzo cha mgogoro wa ardhi baina ya vijiji na hifadhi hiyo.
"Kuna taarifa kwenye eneo lenye mgogoro la Pori Tengefu la Loliondo, kuna ng'ombe zaidi ya 6,000 na trekta zaidi ya 200 toka nchi jirani, yote kinyume cha sheria! Uwepo wao siyo tu unahatarisha uhai wa mfumo wa ikolojia ya Serengeti-Mara, bali pia unapunguza eneo la kuchungia kwa wenyeji wa Loliondo. Hivyo kuleta kiu ya wananchi wa Loliondo kuingia ndani zaidi ya eneo la hifadhi kutafuta malisho na hatma yake kuhatarisha uhai wa Serengeti. Uvamizi huu wa wenzetu kutoka nchi jirani ni moja ya sababu kubwa (zilizojificha) za mgogoro wa ardhi baina ya vijijj na hifadhi kukolea moto" alisema Waziri Kigwangalla
Aidha Waziri huyo amesema wakati wanaendelea kutafuta ufumbuzi wa kudumu wamewataka wavamizi hao kuondoka katika maeneo hayo
"Wakati tukiendelea kutafuta suluhisho la kudumu, tutaondoa makando kando kama haya haraka. Leo tumetoa siku saba kwa wavamizi wote toka nchi jirani waliopo eneo la Loliondo bila kufuata taratibu za kisheria waondoke na mali zao la sivyo tutazitaifisha" alisisitiza Kigwangalla.

Wahamiaji Haramu 21 kutoka DRC wamekamatwa

JESHI la Polisi Mkoani Tabora linawashikilia wahamiaji haramu 21 raia wa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kwa tuhuma za kuingia nchini bila kufuata utaratibu. Taarifa hiyo imetolewa leo na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora (RPC) Wilbrod Mutafungwa wakati wa mkutano na waandishi wa habari Ofisini kwake.
Alisema kuwa watuhumiwa hao wa uhamiaji haramu walikamatwa tarehe 17 mwezi huu wilayani Urambo baada ya Polisi kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema. Kamanda huyo wa Mkoa alisema kuwa baada ya wasamaria wema kutoa taarifa kwa Polisi ndipo waliweka mtego na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao ambao ni wa familia tano tofauti za kutoka DRC.
Alisema kuwa katika orodha hiyo wapo wanaume wawili, wanawake watano na watoto 14 ambao walikamatiwa Urambo baada ya kushuka katika gari la abiria la Saratoga linalofanya safari zake kutoka Kigoma hadi Tabora. Kamanda Mutafungwa aliongeza kuwa watuhumiwa hao walikuwa wakitatafuta usafiri wa kwenda Tabora mjini kutoka Urambo na ndipo Jeshi la Polisi lilifanikiwa kuwakamata.
Alisema kuwa Jeshi la Polisi linaendelea kushirikiana na Uhamiaji na vyombo vingine kuwahoji sababu ya kuja nchini bila kufuata taratibu inagwa wao wanadai kuwa walikuja kutafuta Kambi ya Wakimbizi kufuatia machafuko yanayoendelea nchini mwao. Kamanda Mutafungwa alisema watuhumiwa kutoka familia ya kwanza ni Dieudonne Buloze (32), Kigwasa Mariya(20), Medianne Buloze(3) na Alber Buloze(1). Wengine ni Byamungu Mateus(38), Mulasi Nabunane(33), Busime Mateusi(13), Faida Mateusi(8), Mbamba Mateusi(6), Hadija Mateusi(3) ,Bereke Mateusi(2) na Lebinde Omary(60).
Aliwataja wengine walikamatwa kuwa ni Betie Kasongo(24) , Yoshuwa Ekombe(3) , Yosia Ekombe(miezi 10), Aline Chekanabo (28), Francoise Heva (9), Jistin Faiba (7) , Amida Faiba (6), Kikombe Sumaili(4) na Gulenne(miezi 10). Mmoja wa wahamiaji haramu hao Dieudonne Buloze alikiri kuwa walikimbia DRC kukimbia mapigano yanayoendelea , wakiwa wanatokea Kivu ambapo wavuka mpaka kupitia ziwa Tanganyika na kujikuta wako upande wa Tanzania.
Alisema wamekuja Tanzania kutafuta hifadhi ili kuokoa maisha yao kutokana na mapigano yanayoendelea baina ya vikosi vya Serikali na Waaasi. Katika hatua nyingine Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora alisema kuwa watoto wawili wa shule ya Ncheli katika Kata ya Sungwizi wilayani Simbo wamefariki dunia baada ya kutumbukia katika kisima kilikuwa hakina uzito.
Alisema kuwa chanzo cha vifo hivyo ni wakati mtoto wa kwanza Mwashi Yohana alipoteleza na kuanguka kisimani wakati akijaribu kutaka kunywa maji na ndipo wa pili ajulikanaye kama Wande Shija alifariki baada ya kutumbukia katika kisima wakati akijaribu kumwokoa mwezie.
Kufuatia vifo hivyo Kamanda Mutafungwa alitoa wito kwa wakazi wote Mkoani hapa kuweka uzio katika visima vyote walivyovichimba wakati wa kiangazi na kuhakikisha wazazi wanawasindikiza watoto wao wakati wa kwenda na kutoka shule hasa kwa wale wa shule za awali.

TANGAZO: FAMOUS FURNITURE, WASAMBAZAJI WA MAGODORO YA SEALY POSTURPEDIC NA MASOFA YA LA-Z-BOY WAFUNGUA DUKA DAR ES SALAAM

Famous Furniture, wasambazaji wa magodoro ya Sealy Posturpedic na masofa ya La-Z-Boy wafungua duka Dar es salaam, Tanzania.
Oktoba 18, 2017 Dar es salaam, Famous Furniture wamefungua duka lao Mlimani City, Dar es salaam , Tanzania kwa ajili ya wanaopenda kuishi maisha yasiyo na karaha. Famous Furniture watakuwa ni wasambazaji rasmi magodoro na vitanda vya Sealy Posturepedic pamoja na sofa na viti vya La-Z-Boy nchini.
Magodoro ya Sealy Posturepedic
Sealy ina uzoefu wa utengenezaji wa magodoro na vitanda kwa zaidi ya miaka 100, na kwa sasa ndiyo chapa inayoongoza kwa kutengeneza vitanda na magodoro bora kabisa duniani kote. Vitanda vya Sealy vimetengenezwa na wabobeaji wa afya ya mfupa ili kukupatia starehe, mfumo bora wa egemezi yote haya yakiwa kuhakikisha unapata usingizi mzuri na wenye afya.
Sealy wana vitanda na magodoro ya aina mbalimbali yanayokidhi mahitaji ya kiafya na starehe na yanayodumu kwa muda mrefu.
Zaidi ya watu milioni 40 duniani wanapata usingizi mzuri na kuamka wenye afya kwa sababu ya kutumia bidhaa za Sealy. Tunahakikisha usiku wako unakuwa wenye pumziko na amani. Usingizi mzuri hupoza mwili, unakupa nguvu, unahakikisha unakua vyema na afya nzuri huku akili yako ikizidi kujijenga vizuri. Kumbuka, unatumia theluthi ya maisha yako yote kwenye usingizi.
Leo hii, kuna bidhaa mbalimbali za Sealy unazoweza kuchagua lakini lengo letu ni moja; kuhakikisha tunakuwa sababu ya wewe kuwa na maisha yenye starehe.
Masofa na viti vya La-Z-Boy
Fenicha za La-Z-Boy zinatengenezwa na kusambazwa kwa leseni katika nchi nyingi duniani. La-Z-Boy ina haki miliki za US na kimataifa kwenye miundo zaidi ya 200. Dizaini ya kwanza ilitengenezwa mwaka 1928 na tangia hapo, wamekuwa ni mabalozi “maisha ya starehe” wanaoongoza duniani.
Kupumzika ni starehe
Binadamu hutumia muda mwingi wakiwa wamekaa chini, hii ndio ya sababu ya wabunifu, watafiti na wataalamu wa afya kuumiza vichwa kutoa bidhaa zitakazoleta starehe katika mikao. Unahitaji kukaa kwenye viti bora na vizuri vinavyokujenga kiafya. Ryan Beattie kutoka Bravo Group, wasambazaji wa La-Z-Boy kutoka Famous Furniture anasema “Starehe ya mkao sio katika muonekano t
u – baliile inayokupa starehe ya mwili na mfumo bora wa egemezi, hasa kama unakaa kwa muda mrefu”.
Kuhusu Famous Furniture Ltd
Famous Furniture Limited (iliyosajiliwa na namba 135127) iliona umuhimu wa kutambulisha bidhaa bora za nyumbani ili kukidhi soko linalokuwa la Tanzania. Bidhaa bora za La-Z-Boy zitaboresha mwonekano wa nyumba yako na starehe yako ya mkao wakati magodoro ya Sealy posturepedic yatahakikisha usingizi wenye afya. Na sasa vyote hivi vinapatikana katika duka namba 47, Mlimani City. Wataalamu wetu wapo tayari kusikia mahitaji yako na kuyafanyia kazi. Famous Furniture inatarajia kufungua maduka mengine matano (5) nchini kote kabla ya mwisho wa mwaka 2018.
Famous Furniture ni kampuni iliyo chini ya Bravo Group Manufacturing (Pty) Ltd yenye viwanda 7 Afrika Kusini na inayoongeza kwa kuwa na bidhaa bora za chumbani na sebuleni.
UKWELI
Anuani: Mlimani City Mall, duka namba 47, Barabara ya Sam Nujoma, Dar es salaam, Tanzania
Simu: Nabeel Dharsee - +255713722911
Kwa maelezo na msaada zaidi, wasiliana na:
Nabeel A Dharsee, Meneja Mkuu
+255713722911
nabeel@bravogroup.co.za

Kifo Cha kanumba : Ushahidi Wa kwanza umetolewa Leo 19 October

Leo Oktoba 19, 2017 mahakama kuu chini ya Jaji Sam Rumanyika imeanza kuisikiliza shauri la kesi ya jinai namba 125 ya mwaka 2012, Inayomkabili Msanii Elizabethi Michael ya kumua msanii mwenzie Steven Kanumba bila kukusudia mbapo leo upande wa jamhuri ulikuwa na Mashahidi 2 na shahidi namba moja alikuwa ni Mdogo wake Steven Kanumba Aliyejimabulisha kama Seth Bosco, lakini shahidi wa pili aliomba udhuru wa kutofika leo.
Katika maelezo ya Shahidi Seth Bosco akiongozwa na wakili wa Jamhuri Faraja George ameieleza mahakama kuwa Kanumba ndiye aliye mfungulia mlango Lulu, na alipofika ndani baada ya muda kidogo yeye akiwa chumbani kwake alianza kusikia mvutano wa sauti ya Kanumba ikimwambia Lulu
"kwanini Unaongea na 'Boyfriend' wako mbele yangu?" Mabishano yalianzia kwenye korido, na baada ya kuingia chumbani zilianza kusikika kelele
Baada ya muda mfupi Lulu aliinita na kuniambia Kanumba ameanguka najaribu kumwagia maji naona haamki, nilipoingia chumbani nikweli nilikuta yuko chini akiwa ameegemea ukuta, nikamchukua nikamlaza chali na ndipo nilipoanza kumtafuta Daktari wake anayeitwa Paplas Kageiya, daktari alipofika alimfanyia 'Chek up' akasema ameshafariki, akashauri tumpeleke Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, niliendesha gari mpaka muhimbili, tulipofika muhimbili kwenye kitengo cha dharura walituambia tukatafute utaratibu wa kipolisi, wakati wao wanaandaa vibali vya kuruhusiwa apelekwe mochwari, Baada ya mahojiano ya Polisi katika kituo cha urafiki Ubungo, niliondoka na Askari kurudi nyumbani kwaajili ya uchunguzi, baada ya polisi kufika pale wakiwa chumbani wanaendelea na uchunguzi walikuta Panga chini ya kitanda" Alisema shahidi Seth Bosco
Baada ya ushahidi huo, mahakama imeahirisha shauri hilo hadi kesho Oktoba 20, 2017 kwaajili ya kuendelea kusikiliza mashidi wengine Wanne kutoka upande wa Jamhuri.
Upande wa mstakiwa unaongozwa na Wakili Msomi Peter Kibatala.
Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa kwa siku tatu mfulilizo, ingawa Jaji Rumanyika ameelekeza upande wa mstakiwa na Jamhuri kuona kama wnaweza kutumia hata siku mbili kuisikiliza na siku ya tatu ikatumika kuandika hukumu.

Mke Wa Mugabe Amshtaki Mfanyabiashara kwa kutomuuzia Pete ya $1.35m

Zimbabwe na mkewe Grace MUgabe
Mke wa rais nchini Zimbabwe Grace Mugabe amemshtaki mfanyibiashara mmoja kwa kushindwa kumpatia pete ya almasi yenye thamani ya $1.35m kulingana na chmbo cha habari cha Herald.
Jamal Ahmed alidaiwa kumpatia pete yenye thamni ya $30,000 badala ya ile aliyoagiza.
Ni mgogoro wa hivi karibuni kuhusu pete hiyo yenye Carat 100 iliotarajiwa kuwa zawadi ya rais Mugabe kwa mkewe wakati wa maadhimisho ya miaka 20 ndoa yao.
Mwaka uliopita, bwana Ahmed aliwashtaki Bi Grace Mugabe na mwanawe wa ndoa yake ya kwanza mahakamani baada ya kuchukua mali zake katika mgogoro wa pete hiyo.
Alisema katika nakala za mahakamani kwamba bi Mugabe alitaka kurudishiwa fedha zake baada ya pete hiyo ya almasi ilionunuliwa Dubai kukabidhiwa yeye baada ya kusafishwa na mtu mwengine.
Wakati aliposhindwa kulipa fedha hizo kwa akaunti moja huko Dubai, licha ya kusema kuwa fedha hizo zilitumwa kupitia benki moja ya Zimbabwe mke huyo wa rais alichukua kwa lazima nyumba zake.
Bwana Ahmed alisema kuwa alinyanyaswa, kutukanwa na kutishiwa na kuambia hawezi kuchukua hatua yoyote kwa kuwa walioshtakiwa ndio 'Zimbabwe'.
Disemba iliopita jaji mmoja alimuagiza bi Mugabe kurudisha mali hiyo.
Na sasa anamshtaki bwana Ahmed , ambaye ana kibali cha kuishi nchini Zimbabwe na biashara katika taifa hilo kwa $1.23m ili kulipa deni hilo.