Monday, 11 December 2017

Msanii Gilad amesema Cinderella ya Ali Kiba ilimfunza kuimba Kiswahili



Msanii wa muziki toka nchini Kenya mwenye asili ya Israel, Gilad amesema wimbo wa Alikiba Cinderella ndio uliomfunza kuimba Kiswahili.

Muimbaji huyo ameiambia FNL ya EATV kuwa ngoma hiyo ndio ya kwanza kuimba kwa lugha ya Kiswahili ndipo na nyingine zikafuata.

“Cinderella ni wimbo wa kwanza kujifunza kuimba, ni wimbo wa kwanza kuinba kwa Kiswahili. Nilikuwa naimba na bendi jukwaani, kwa hiyo ni wimbo wa kwanza kuimba kwa Kiswahili na nilikuwa natumbuiza kila wiki, nikaja nikaimba Kidumu ‘Haturudi Nyuma’, pia Juliana ‘Tawala’ amesema.

Miongoni mwa ngoma alizoimba kwa Kiswahili Gilad ni pamoja na Nakuhaidi, Sema Milele, Unajua na Mapenzi. Pia mwaka huu ameweza kushinda tuzo mbili za Afrima.

Gilad kwa sasa anasikika Bongo kupitia ngoma mpya ya rapper Azma ‘Shubiliga’.

No comments:

Post a Comment