Wednesday, 24 January 2018

CCM, Chadema kuzindua kampeni siku moja


Vyama vya CCM na Chadema vinatarajia kuzindua kampeni za ubunge jimbo la Kinondoni Jumamosi Januari 27,2018.

Wakati CCM ikisema itazindua kampeni katika viwanja vya Biafra; Chadema haijaweka wazi eneo la uzinduzi.

Uchaguzi katika jimbo hilo unafanyika baada ya aliyekuwa mbunge kwa tiketi ya CUF, Maulid Mtulia kujivua uanachama wa chama hicho akisema anamuunga mkono Rais John Magufuli na baadaye alijiunga na CCM.

Mtulia amepitishwa na CCM kuwania tena ubunge jimboni humo ambako atachuana na Salum Mwalimu wa Chadema ambaye pia ni naibu katibu mkuu wa chama hicho Zanzibar.

CCM imeanza kwa kumtambulisha Mtulia katika vikao vya ndani na kwenye kata mbalimbali.

Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Simon Mwakifamba amesema kampeni zitaanza saa sita  mchana.

Amewaomba wakazi wa jimbo hilo kujitokeza kwa wingi katika mkutano huo wa hadhara.

Naye Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Itifaki wa Chadema, John Mrema amesema watazindua kampeni Kinondoni Jumamosi, ikiwa ni siku moja baada ya uzinduzi kufanyika katika jimbo la Siha.

“Jimbo la Siha kampeni zitafanyika uwanja wa Ngarenairobi na Kinondoni bado hatujajua ni wapi ila tutawaeleza. Kampeni hizi zitahudhuriwa na viongozi wakuu na ndiyo maana tumetofautisha siku ya uzinduzi,” amesema.

Uchaguzi katika jimbo la Siha unafanyika baada ya aliyekuwa mbunge kwa tiketi ya Chadema, Dk Godwin Mollel kujivua uanachama na kujiunga na CCM ambayo imempitisha kuwania tena nafasi hiyo.

Mwanakwaya afariki Dunia baada ya kutoa sadaka


Mwanakwaya wa kwaya ya Mtakatifu Secilia, Kigango cha Muze Parokia ya Zimba, Jimbo Katoliki Sumbawanga, Flora Nandi (25) ameanguka na kufariki dunia muda mfupi baada ya kutoa sadaka ya shukrani akiwa kanisani.

Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita saa nne za asubuhi wakati wa ibada ya kwanza wakati kwaya ya Mtakatifu Secilia ilipokuwa ikimsifu Mungu katika ibada hiyo.

Akizungumzia tukio hilo, mwalimu wa kanisa aliyekuwa akiongoza ibada hiyo, Katekista Philipo Lupadasi alisema wanakwaya wakiwa wanaimba na marehemu akiwa ametoka kutoa sadaka ya shukrani alirejea katika sehemu yake kwenye kwaya na kuendelea kuimba lakini ghafla alianguka chini hali iliyozua mshtuko na kusababisha ibada kusimama kwa muda.

Alisema wanakwaya wenzake walimnyanyua na kumtoa nje ya kanisa ili apate hewa wakiamini kuwa amepoteza fahamu. Katekista huyo alisema baada ya kumpepea kwa muda, waliona hapati fahamu hali iliyowalazimu kumpeleka Zahanati ya Kijiji cha Muze kwa ajili ya matibabu.

Alisema baada ya kufikishwa katika zahanati hiyo alipokewa na wahudumu wa afya ambao baada ya kumfanyia uchunguzi walibaini kuwa alikuwa ameshafariki dunia.

Baada ya kupewa taarifa za kifo hicho, wanakwaya hao waliangua kilio na hawakuweza kurudi tena kanisani kuimba katika ibada ya pili na badala yake waliuchukua mwili wa marehemu na kuupeleka nyumbani kwake kwa taratibu za mazishi.

Mwalimu wa kwaya hiyo, Aloyce Mwandanje alisema kuwa kifo cha mwanakwaya mwenzao ambaye alikuwa na ujauzito wa miezi mitano, kimewaachia majonzi makubwa lakini hawana la kufanya kwa kuwa ni mapenzi ya Mungu.

Alisema mwili wa marehemu Nandi ulizikwa Jumatatu katika makaburi ya Kijiji cha Muze.

Wanafunzi 229 wanasoma chini ya miti kutokana na uhaba wa Madarasa


Picha ya mtandao

Mtwara. Wanafunzi 229 wa Shule ya Msingi Mitambo wilayani Mtwara wanasoma wakiwa chini ya miti kutokana na uhaba wa madarasa matano.

Wanafunzi wanaosoma wakiwa chini ya miti ni wa darasa la tatu, nne, tano na sita.

Akizungumza na MCL Digital, mwalimu mkuu wa shule hiyo, Rashidi Chalilo amesema wanafunzi hao ni kati ya 436 wa shule hiyo.

Chalilo amesema wanafunzi wa darasa la kwanza na la pili kutokana na kuhitaji uangalizi zaidi wanasoma darasani pamoja na wa darasa la saba wanaojiandaa kwa mitihani.

Amesema shule hiyo ilianzishwa mwaka 2009 ikiwa na wanafunzi 99 na sasa wapo 436 ikiwa na madarasa matatu pekee.

Mwalimu mkuu huyo amesema wazazi walijenga madarasa ya muda kwa kutumia miti na udongo na kuyaezeka kwa nyasi lakini baadaye yalibomolewa kwa maelekezo ya Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara ili kupisha ujenzi wa madarasa ya kudumu.

Akizungumzia suala hilo, kaimu ofisa mtendaji wa Kijiji cha Mitambo, Ally Mselemu amesema wanasubiri kupelekewa saruji na vifaa vingine vya ujenzi.

“Wananchi tuko tayari kujitolea nguvu kazi kuboresha shule yetu, hivyo tunaiomba Serikali ituletee vifaa,” amesema Mselemu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, Omari Kipanga amesema wameshatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa matatu pamoja na nyumba ya mwalimu.

Amesema Sh156 milioni zimetengwa kutoka katika mfuko wa elimu ambazo zinatokana na mapato ya korosho.

Kipanga amesema mfuko wa P4R pia umeidhinisha Sh326 milioni kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu katika halmashauri hiyo.

Shahidi afunguka alivyomrekodi Sugu


Mvutano wa kisheria katika kesi inayowakabili mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga umeibuka kwa mawakili wa pande mbili kuhusiana na ushahidi wa sauti iliyorekodiwa kwa kinasa sauti ambao upande wa Jamhuri uliiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi-Mbeya kuusikiliza na upande wa utetezi kuupinga.

Mvutano huo umeibuka baada ya shahidi wa tano upande wa Jamhuri, Inspekta Joram Magova akiongozwa na wakili wa Serikali mkuu, Joseph Pande kudai kwamba ndiye aliyefanya kazi ya kurekodi sauti za Sugu na Masonga kwenye mkutano wao wa Desemba 30 mwaka jana hivyo kuiomba Mahakama kupokea kifaa kilichotumika kurekodia kama kielelezo cha pili kilichowasilishwa na shahidi wa wanne, askari Daniel Masanja katika ushahidi unaondelea kutolewa mahakamani hapo.

Upande wa utetezi ukiongozwa na mawakili Boniface Mwabukusi na Hekima Mwasipu waliupinga ushahidi huo wakiiomba Mahakama kutoupokea wala kusikiliza wakidai shahidi aliyetoa kifaa hicho ana masilahi na kesi hiyo hivyo wanaona ushahidi huo haujakidhi matakwa kisheria.

Hata hivyo, mawakili wa Serikali, Pande na Baraka Mgaya kwa nyakati tofauti, waliinuka na kupinga hoja zilizotolewa na mawakili wa utetezi kwa hoja kwamba walichoiomba mahakama hiyo ni kusikiliza maudhui yaliyomo kwenye kifaa hicho ambacho kimewasilishwa kama kielelezo na kimepokewa.

“Shahidi anapaswa kuwa yule aliyeona, kushuhudia na aliyefanya na kusikia. Sasa hawa wenzetu wanataka kutuaminisha kwamba shahidi siyo yule aliyeona, aliyesikia na kufanya na kushuhudia, kitu ambacho sicho. Kama kielelezo kimepokewa na Mahakama hivyo hoja kwamba kisisikilizwe kilichomo ndani yake, itakuwa imepokea ya nini wakati hatujui kilichomo? Hivyo mheshimiwa hakimu naomba hoja hii itupiliwe mbali.”

Kifaa hicho kilitolewa na shahidi wa wanne Masanja ambaye alidai ndiye aliyekipokea na kukihifadhi katika chumba cha kuhifadhia vielelezo vyote vinavyotakiwa kutolewa ushahidi mahakamani katika Ofisi ya Upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO).

Shahidi huyo aliongozwa na wakili wa Mgaya na mahojiano yalikuwa:

Wakili: Shahidi hebu tueleze wewe ni nani na unafanya kazi ofisi gani.

Shahidi: Ni askari polisi nafanyia Ofisi ya Upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO) lakini vilevile ni mtunza vielelezo katika ofisi hiyo.

Wakili: Tangu lini unafanya kazi hiyo?

Shahidi: Tangu mwaka 2004.

Wakili: Vielelezo gani unavyotunza?

Shahidi: Vielelezo vya kesi inayopelelezwa na kuna aina mbili, kwanza vielelezo ambavyo vimeshafunguliwa kesi na pili vielelezo ambavyo kesi yake inakuwa haijafunguliwa mahakamani.

Wakili: Ieleze Mahakama Desemba 30 mwaka jana ulikuwa wapi na ulikuwa unafanya nini?

Shahidi: Siku hiyo majira ya saa 12 jioni nilikuwa nyumbani lakini nikapigiwa simu na Inspekta Joram akinihitaji ofisini niweze kupokea vielelezo.

Wakili: Ulifanyeje baada ya hapo?

Shahidi: Ilinibidi niende na baada ya kufika ofisini nilimkuta Inspekta Joram akanieleza kuna vielelezo vya kuhifadhi, ametoka kwenye mkutano.

Wakili: Mkutano gani?

Shahidi: Mkutano wa Chadema.

Wakili: Ulifanyika wapi?

Shahidi: Ulifanyika maeneo ya Ruanda Nzovwe.

Wakili: Kielelezo gani ulichopokea?

Shahidi: Ni tape recorder.

Wakili: Baada ya kukueleza hivyo ulifanya nini?

Shahidi: Baada ya kuelezwa hivyo, nikavihifadhi kwa kuvifungia kwenye kasiki ofisini.

Wakili: Hebu ieleze Mahakama, Januari 2 mwaka huu ulikuwa wapi na kufanya nini?

Shahidi: Nilikuwa ofisini kwangu nikiendelea na majukumu yangu na akaja Inspekta Joram akihitaji tape recorder ile kwa ajili ya kwenda kuwasikilizishia viongozi wa Chadema akiwamo mbunge (Sugu).

Wakili: Baada ya hapo nini kiliendelea?

Shahidi: Inspekta Joram aliendelea na mahojiano na viongozi hao hadi saa nane mchana akanirudishia kifaa hicho nami nikakihifadhi kwenye kasiki.

Wakili: Tokea siku hiyo ulipokabidhiwa hadi leo (jana) hii nini kiliendelea?

Shahidi: Niliendelea kuhifadhi hadi leo (jana) nilioambiwa vinahitajika mahakamani.

Wakili: Ukiviona unaweza kuvitambua?

Shahidi: Ndiyo.

Wakili: Unahitaji Mahakama ifanyie nini vielelezo hivi?

Shahidi: Naomba Mahakama ivipokee kama vielelezo vya ushahidi katika kesi hii.

Wakili: Mheshimiwa Hakimu, shahidi wetu anaomba vidhibiti hivi vyote vipokewe na Mahakama yako kama vielelezo katika kesi hii.

Baada ya wakili kumuongoza shahidi huyo, Wakili Mwabukusi wa utetezi alisimama na kuweka pingamizi juu ya kielelezo hicho akipinga kisipokewe kwa madai kwamba hakijakidhi matakwa ya kisheria na hakina ubora unaotakiwa.

“Kifaa kinachotaka kuwa kielelezo mahakamani hapa ni kifaa ambacho kinasemekana kina maelezo yaliyorekodiwa na mtu mwingine na huyu aliyerekodi hatujaambiwa alirekodi kwa maudhui gani,” Mahakama haijaelezwa kwa namna gani ‘data massage’ zilizomo katika kifaa hiki hazijawa ‘tempered’ na haziwezi kuwa ‘tempered’ kwa namna gani. Tunapinga kifaa hiki kisipokewe kwa vile hakijakidhi matakwa na hakina ubora unaotakiwa kisheria.

Baada ya hoja hizo za Wakili Mwabukusi, Wakili wa Jamhuri, Pande aliinuka na kusema msingi wa hoja hizo unapinga kutolewa kwa kifaa hicho kama ushahidi kwa madai kwamba shahidi aliyewasilisha si aliyerekodi kwamba hawana pingamizi ikiwa kitatolewa na shahidi anayefuata ambaye kimsingi atakitambua.

Hata hivyo, mawakili wa utetezi walipinga hoja za wakili huyo na kutaka visipokewe vyote

Mabishano hayo yalidumu kwa takriban nusu saa kabla ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Michael Mteite kuahirisha kesi hiyo kwa nusu saa ndipo atoe uamuzi juu ya kinachobishaniwa.

Baada ya kurejea, Hakimu Mteite alisema Mahakama imejiridhisha kwamba vielelezo hivyo vinaonekana katika muonekano wake halisi, hivyo inavipokea kama vidhibiti na itatoa ufafanuzi wa kwa nini iliamua kuvipokea siku ya hukumu ya kesi yenyewe. Kesi hiyo inaendelea leo.

New AUDIO: AKA ft Stogie T – Star Signs

New AUDIO: AKA ft Stogie T – Star Signs

New AUDIO: AKA ft Stogie T – Star Signs

AKA kickstarts 2018 with a fat tune tagged Star Signs a collaboration with rap veteran Stogie T. The rapper has been speaking on his 2018 album Touch My Blood since las year. Stogie T in his way brags on the joint. Most of his lines are very memorable, with “when a nigga ego matches his balance sheets“, the one we felt the most one time.

AKA even took a vacation to make music such is how he is deep right now. Star Signs is AKA reminiscing where he is coming from, where he is now and the future. Sticking to the usage of autotune although this is not singing, this is pure rap. Produced by Gemini Major

                                      DOWNLOAD Mp3

Tuesday, 23 January 2018

Audio | Enock Bella – Window |Mp3 Download

Audio | Enock Bella – Window |Mp3 Download

Audio | Enock Bella – Window |Mp3 Download

DOWNLOAD Mp3

Audio | Enock Bella – Nikaribie | Mp3 Download

Audio | Enock Bella – Nikaribie | Mp3 Download

Audio | Enock Bella – Nikaribie | Mp3 Download

DOWNLOAD Mp3

AUDIO Audio | Aslay & Nandy – Subalkheri Mpenzi | Mp3 Download

AUDIO
Audio | Aslay & Nandy – Subalkheri Mpenzi | Mp3 Download

AUDIO
Audio | Aslay & Nandy – Subalkheri Mpenzi | Mp3 Download

DOWNLOAD Mp3

Aslay X Nandy - Subalkheri Mpenzi (Official video)

Aslay X Nandy - Subalkheri Mpenzi (Official video)

Aslay X Nandy - Subalkheri Mpenzi (Official video)


VIDEO: Sakata la Nyoso Latua TFF


Sakata la Mchezaji wa Kagera Suger Juma Nyoso la kumpiga mshabiki na kuzimia leo limeibuka kwenye mkutano wa waandishi wa Shirikisho la Soka Nchini TFF na Kulitolea ufafanuzi.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI .......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Kiwanja Cha Kujenga Nyumba Kinauzwa Eneo la Mapinga Karibu na Bunju B


Kiwanja cha Kujenga Nyumba Kinauzwa , Kina Size ya 20 Kwa 20 Mita, Kipo Eneo la Mapinga Karibu na Bunju B, Kipo Karibu na Barabara ya Lami
Shilingi Mil 8. Maongezi yapo Kidogo

Piga simu 0714604974 Kwa Mawasiliano zaidi


Jeshi la Polisi lasema Nabii Tito anamatatizo ya akili


JESHI la Polisi mkoani Dodoma,  baada ya kumkamata na kumfanyia mahojiano Onesmo Machija (44) anayejiita ‘nabii’ Tito, kutokana na mahubiri ya kidini anayoyafanya, limesema mtu huyo ana  matatizo ya akili.

Akizungumza na wanahabari mjini Dodoma leo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Gillesi Muroto, amesema mnamo Juni 23, 2014, mtu huyo aliwahi kulazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu ya akili chini ya daktari aliyejulikana kwa jina moja la William ambapo aliporuhusiwa alitakiwa kurejea hospitalini hapo Julai 9 mwaka huohuo lakini hakurejea.

Kamanda Muroto aliendelea kusema kwamba baada ya hapo, Machija ambaye kanisa lake halijasajiliwa popote,  aliibukia mkoani Dodoma katika kijiji cha Nong’ona kilicho karibu na Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) akifanya  mahubiri ya kidini yaliyodaiwa kuwa hayakuwa na maadili ya kidini.

Kwa msingi huo, alisema jeshi la polisi limempeleka Hospitali ya Rufaa ya Mirembe iliyoko mkoani Dodoma  kwa ajili ya kumpima tena matatizo hayo ya akili na baada ya majibu kutolewa,  Dkt. Dixon Philipo aliyemshughulikia alithibitisha kwamba bado ana matatizo hayo.

Pamoja na hayo, Muroto alisema jeshi la polisi mkoani humo  bado linaendelea kumshikilia kutokana na matendo yake aliyoyafanya ili kufanya uchunguzi zaidi.

Source:Global Publishers

Wenger kumsajili Aubameyang




Meneja wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amethibitisha kuendelea kwa mazungumzo ya kumsajili mshambuliaji wa timu ya Borussia Dortmund, Pierre-Emerick Aubameyang.

Aubameyang mshambuliaji huyo wa kimataifa wsa Gabon amehusishwa kujiunga na the Gunners na Wenger amesema kila kitu kinaendelea.
Alipoulizwa na waandishi wa habari kama anauhakika wa kunasa saini ya Aubameyang, Wenger amesema “Kuwe na uhakika kusiwe na uhakika, mi sijui.”

Wenger ameongea “Huwezi jua ni kwa jinsi gani dirisha la usajili litakavyo kamilika.”

“Hivi ni vitu ambavyo uwezekano wa kukamili upo lakini pia tuna mambo mengine tunayofikiria mbali na usajili huo na nafasi tunayo na muda bado haujakwisha.”

“Kwa kipindi hiki bado hatujakamilisha dili lolote kuhusu Aubameyang au mtu mwingine yeyote.”

 Alipoulizwa kama mchezaji wake, Olivier Giroud atakuwa sehemu ya dili la kumnasa Aubameyang kwa yeye kuelekea Dortmund, Wenger amesema kuwa mazungumzo hayajafikia katika hatua hiyo.

Timu hiyo imekamilisha mpango wa Alexis Sanchez kutua Manchester United huku Arsenal ikinufaika kwa kumnasa Henrikh Mkhitaryan.