
WAKAZI wa Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro, wameiomba serikali kupitia Wakala wa Barabara nchini (Tanroads), kuweka matuta katika barabara ya Sanya Juu- Bomang’ombe, ili kuzuia ajali ambazo zimekuwa zikitokea na kusababisha watu kupoteza maisha.
WAKAZI wa Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro, wameiomba serikali kupitia Wakala wa Barabara nchini (Tanroads), kuweka matuta katika barabara ya Sanya Juu- Bomang’ombe, ili kuzuia ajali ambazo zimekuwa zikitokea na kusababisha watu kupoteza maisha.
Wakazi hao wamesema barabara hiyo kwa muda mrefu imekuwa na ajali nyingi za watu kugongwa na magari na kupoteza maisha papo hapo na hakuna jitihada zozote ambazo zimekuwa zikichukuliwa na serikali kuzuia ajali hizo.
Mmoja wa wakazi wa Majengo Sanya Juu, Idrisa Mndeme, alisema serikali kupitia Tanroads inapaswa kuwawekea matuta katika barabara hiyo kwenye maeneo ya kuanzia Standi Kuu ya Sanya hadi Fuka, kwa kuwa madereva wa magari wamekuwa wakiendesha kwa mwendo kasi bila kujali watembea kwa miguu.
“Ndani ya mwezi huu kuna ajali mbili zimetokea. Mtu mmoja aligongwa na gari na kupoteza maisha na mwingine ambaye ni mwendesha pikipiki aligongwa na gari na kufariki papo hapo,”alisema.
Yassin Kimaro kwa upande wake aliwatupia lawama madereva wenye magari makubwa kwa kuendesha kwa mwendokasi na mara nyingine hudharau alama za pundamilia kwa kupitisha magari bila kujali watu wanaovuka.
“Madereva wa magari huendesha magari kwa kasi mno, hali ambayo imekuwa ikichangia sana ajali ambazo zinaweza kuepukika iwapo matuta yangekuwa yamewekwa,”alisema.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Siha, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Onesmo Busweru, alikiri kuwapo kwa baadhi ya madereva ambao wamekuwa wakiendesha kwa kasi, hivyo kusababisha ajali ambazo zingeweza kuepukika
Kutokana na hali hiyo aliagiza Jeshi la Polisi kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani kuweka kidhibiti mwendo (tochi) katika maeneo hayo ili kuwadhibiti madereva ambao wamekuwa akiendesha kwa kasi.
Mwanaharakati na mwanamke shujaa nchini Tanzania, Joyce Kiria ameweka hadharani kuwa mahusiano yake kwa sasa na mumewe Henry Kileo ambaye alishawahi kushika nyadhifa mbalimbali CHADEMA.
Kocha msaidizi wa vinara wa ligi kuu soka Tanzania Bara Simba SC Masoud Djuma, ameweka wazi kuwa pamoja na kumpatia nafasi ya kucheza hivi sasa nyota wa timu hiyo kutoka Ghana Nicholas Gyan, lakini aliwahi kumwambia hajui kucheza.




Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima leo Januari 21, 2018 amepata pigo kwa kuondokewa na mama yake mzazi Ruth Basondole Gwajima ambaye amefariki asubuhi ya leo.





Chama cha ACT Wazalendo kupitia kwa Naibu Katibu Mkuu wake Bara Msafiri Mtemelwa kimetangaza kutoshiriki Uchaguzi mdogo wa marudio katika Majimbo ya Kinondoni na Siha.