SERIKALI kwa kushirikiana na wadau wa uhifadhi wa misitu na bayoanui, inakamilisha taratibu za kutungwa sheria mpya pamoja na kanuni zake ili kudhibiti uharibifu wa misitu nchini.
Hatua hiyo inakuja kutokana na sheria zilizokuwepo kupitwa na wakati na kuchangia kuharibika kwa misitu kila mwaka.
Maamuzi ya kuanzisha sheria hiyo mpya yamekuja kutoka na sekta ya misitu na nyuki hapa nchini kuwa katika hatari ya kutoweka hali inayochangiwa kwa asilimia kubwa na vitendo vya uchomaji wa mkaa pamoja na ukataji kuni.
Akizindua mchakato wa kuhakiki rasimu ya taifa ya misitu, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga, alisema maamuzi ya kutunga sheria mpya yanatokana na ile iliyopo ya mwaka 1998 kutokuendana na mabadiliko ya jamii ya sasa ambayo yanatishia kwa kasi uhai wa sekta hiyo ya misitu.
Naibu Waziri alisema sekta ya misitu na nyuki ni mtambuka kwani inashirikisha wizara mbalimbali kama Nishati, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),Afya, Viwanda na Biashara hivyo kulingana na sheria mpya kazi ya kulinda misitu itakuwa ikifanywa kwa pamoja.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS),Profesa Dos Santos Silayo, alisema kuanzishwa kwa sheria hiyo mpya itakuwa mkombozi wa misitu nchini kwa kuwa iliyopo ilitoa mwanya kwa baadhi ya watu kufanya uharibifu.
Alisema kuwa rasilimali za misitu zipo za kutosha kulingana na ikolojia mbalimbali za kila eneo kama kuweka sheria kali za kuhifadhi kuna hatari ya vizazi vijavyo vikashindwa kuzitumia rasilimali hizo.
Mtalaam wa misitu, Dk. Felician Kilahama,alisema kuwa sekta ya misitu inakabiliwa na changamoto kubwa ya usimamizi,ukataji wa miti ambapo katika kipindi cha miaka mitatu iliopita hekta 582 zilifanyiwa uharibifu kwa ajili ya shughuli za uchomaji wa mikaa na ukataji wa kuni.
Alisema kuwa kuanzishwa kwa sheria hiyo mpya ya misitu na kusimamiwa kwa pamoja , serikali pamoja na wadau kutawezesha kurudisha misitu ya asili kwa haraka ambayo imeanza kutoweka kutokana na uharibifu mkubwa wa mazingira.
January 20, 2018 Waziri wa Mambo ya Ndani, Dr. Mwigulu Nchemba amelitaka Jeshi la Polisi nchini kutafuta namna ya kupunguza wahalifu wanaokamatwa kwa makosa kama uzururaji ili kupunguza mrundikano kwenye mahabusu.
Mwanasiasa wa upinzani na aliyekuwa Naibu Waziri katika serikali ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete, Goodluck Ole Medeye, ametangaza kurejea Chama Cha Mapinduzi huku akidai kuwa ameamua kufanya hivyo kwa kuwa vitendo vya rushwa,-Hususan nyakati za uchaguzi, vimemalizwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Dk. John Magufuli.
Bunge la Seneti nchini Marekani limeshindwa kuidhinisha mswada ambao ungeongeza ufadhili wa serikali ya kitaifa kwa mwezi mmoja.
Waziri wa elimu,sayansi,na teknolojia na ufundi Profesa Joyce Ndalichako amewapa wiki moja Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kuonyesha maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa, hostel na ofisi kwa ajili ya chuo kikuu cha Muhimbili Kampasi ya Mloganzil

KIKOSI cha Simba, Alhamisi kilijitanua kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Singida United katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Waziri wa fedha na mipango, Dk Philip Mpango
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Engine ambaye hivi karibuni kulikuwa na tetesi za kumng'oa Jackline Wolper na kumuweka ndani, ameweka wazi sababu za kuamua kumtumia msanii huyo kwenye kazi yake.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameamuru Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Mara kumkamata na kumuhoji Mkurugenzi Mtendani wa Mamlaka ya Maji Musoma (MUWASA) Mhandisi Gantala Said.