Msanii wa miondoko ya singeli Man Fongo amesema hawezi kukaa na kumzungumzia Sholo Mwamba kwa madai yeye ni mfa maji ndiyo maana haishi kutapa tapa kila uchao kumtaja.
Man Fongo ameeleza hayo baada ya masaa machache kupita tokea kuonekana kwa 'video' ya Sholo iliyorushwa na EATV katika kipindi cha 'FRIDAY NIGHT LIVE' (FNL) usiku wa kuamkia leo, ikiwa imemuonyesha akimlaumu msanii mwenzake kuwa hana kipaji cha kuendelea kufanya muziki mzuri ndani ya mwaka 2018 huku akimtaka arejee katika fani yake ya awali ya 'DJ'.
"Mimi kwa sasa siwezi kumzungumzia mtu yeyote kwa maana naangalia muziki wangu kwa sababu ndiyo unaonifanya nieleweke kwa wadau wangu, pia unasababisha familia yangu ipate kula. Kwa hiyo mtu akitaka kutoka kwa kutumia kiki na kupitia mgongo wangu nakuwa bado simuelewi. Hivyo siwezi kumtumikia Sholo Mwamba 'eti aniambie mimi nirudi katika fani yangu ya 'DJ' wakati yeye hayupo katika 'manegement' yangu na yeye ni msanii kama mimi", alisema Man Fongo wakati alipofanyiwa mahojiano maalum.
Pamoja na hayo, Man Fongo ameendelea kwa kusema "ninachopenda kumshauri Sholo Mwamba ni kwamba atoe ngoma mpya ili aweze kusikilizwa na raia anachokifanya, apambanie muziki wake aweze kufika mbali na asiangalie muziki wangu mimi", alisisitiza Man Fongo.
Kwa upande mwingine Man Fongo amesema mwaka 2018 amejiandaa vizuri katika ufanyaji kazi wake na wala haiwezi kuwa kama alivyosema mpinzani wake huyo ambae kwa muda mrefu wamekuwa wakitoleana mapovu katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.
"Kazi mpya nimeangusha juzi tu na mpaka sasa ninapo kwambia inafanya vizuri hivyo Sholo Mwamba ni mfa maji tu kama mtu ambae anatapa tapa yaani mfa maji haishi kutapa tapa. Kwa hiyo ameona bora apate kiki kwa mgongo wangu ili aweze kutoka", alisema Man Fongo.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amewataka viongozi wa chama hicho Manispaa ya Moshi, kuacha kutembea na watu mifukoni na kutengeneza kofia za ubaguzi ndani ya chama kwa kuwa hali hiyo imekuwa ikikigharimu chama wakati wa uchaguzi.

Msanii wa filamu bongo ambaye sasa amegeukia ujasiriamli, Jackline Wolper, amewapa somo mabinti na kuwafunda juu ya kujishughulisha ili kujipatia kipato chao, na hatimaye waweze kuheshimika.
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watumishi wa Halmashauri na Mji wa Bunda pamoja na Madiwani washirikiane katika utekelezaji wa ujenzi wa miradi ya maendeleo.
SERIKALI kwa kushirikiana na wadau wa uhifadhi wa misitu na bayoanui, inakamilisha taratibu za kutungwa sheria mpya pamoja na kanuni zake ili kudhibiti uharibifu wa misitu nchini.
January 20, 2018 Waziri wa Mambo ya Ndani, Dr. Mwigulu Nchemba amelitaka Jeshi la Polisi nchini kutafuta namna ya kupunguza wahalifu wanaokamatwa kwa makosa kama uzururaji ili kupunguza mrundikano kwenye mahabusu.
Mwanasiasa wa upinzani na aliyekuwa Naibu Waziri katika serikali ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete, Goodluck Ole Medeye, ametangaza kurejea Chama Cha Mapinduzi huku akidai kuwa ameamua kufanya hivyo kwa kuwa vitendo vya rushwa,-Hususan nyakati za uchaguzi, vimemalizwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Dk. John Magufuli.
Bunge la Seneti nchini Marekani limeshindwa kuidhinisha mswada ambao ungeongeza ufadhili wa serikali ya kitaifa kwa mwezi mmoja.
Waziri wa elimu,sayansi,na teknolojia na ufundi Profesa Joyce Ndalichako amewapa wiki moja Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kuonyesha maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa, hostel na ofisi kwa ajili ya chuo kikuu cha Muhimbili Kampasi ya Mloganzil