Saturday, 20 January 2018

Sheria kali yaandaliwa kulinda misitu nchini

SERIKALI kwa kushirikiana na wadau wa uhifadhi wa misitu na bayoanui, inakamilisha taratibu za kutungwa sheria mpya pamoja na kanuni zake ili kudhibiti uharibifu wa misitu nchini.

Hatua hiyo inakuja kutokana na sheria zilizokuwepo kupitwa na wakati na kuchangia kuharibika kwa misitu kila mwaka.

Maamuzi ya kuanzisha sheria hiyo mpya yamekuja kutoka na sekta ya misitu na nyuki hapa nchini kuwa katika hatari ya kutoweka hali inayochangiwa kwa asilimia kubwa na vitendo vya uchomaji wa mkaa pamoja na ukataji kuni.

Akizindua mchakato wa kuhakiki rasimu ya taifa ya misitu, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga, alisema maamuzi ya kutunga sheria mpya yanatokana na ile iliyopo ya mwaka 1998 kutokuendana na mabadiliko ya jamii ya sasa ambayo yanatishia kwa kasi uhai wa sekta hiyo ya misitu.

Naibu Waziri alisema sekta ya misitu na nyuki ni mtambuka kwani inashirikisha wizara mbalimbali kama Nishati, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),Afya, Viwanda na Biashara hivyo kulingana na sheria mpya kazi ya kulinda misitu itakuwa ikifanywa kwa pamoja.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS),Profesa Dos Santos Silayo, alisema kuanzishwa kwa sheria hiyo mpya itakuwa mkombozi wa misitu nchini kwa kuwa iliyopo ilitoa mwanya kwa baadhi ya watu kufanya uharibifu.

Alisema kuwa rasilimali za misitu zipo za kutosha kulingana na ikolojia mbalimbali za kila eneo kama kuweka sheria kali za kuhifadhi kuna hatari ya vizazi vijavyo vikashindwa kuzitumia rasilimali hizo.

Mtalaam wa misitu, Dk. Felician Kilahama,alisema kuwa sekta ya misitu inakabiliwa na changamoto kubwa ya usimamizi,ukataji wa miti ambapo katika kipindi cha miaka mitatu iliopita hekta 582 zilifanyiwa uharibifu kwa ajili ya shughuli za uchomaji wa mikaa na ukataji wa kuni.

Alisema kuwa kuanzishwa kwa sheria hiyo mpya ya misitu na kusimamiwa kwa pamoja , serikali pamoja na wadau kutawezesha kurudisha misitu ya asili kwa haraka ambayo imeanza kutoweka kutokana na uharibifu mkubwa wa mazingira.

Agizo la Waziri Mwigulu kwa Polisi kuhusu kukamata wazururaji

January 20, 2018 Waziri wa Mambo ya Ndani, Dr. Mwigulu Nchemba amelitaka Jeshi la Polisi nchini kutafuta namna ya kupunguza wahalifu wanaokamatwa kwa makosa kama uzururaji ili kupunguza mrundikano kwenye mahabusu.

Ameeleza kuwa suala hili pia litaepusha watuhumiwa wanaopelekwa mahabusu kwa makosa ya uzururaji kupata nafasi ya kuzungumzia masuala ya uhalifu na watuhumiwa waliozoea.

Kwa upande mwingine Dr. Mwigulu ameagiza wananchi kushirikiana na serikali katika ujenzi wa vituo vya polisi kwa kuwa suala la ulinzi ni ajenda ya kila Mtanzania na linapaswa kupewa kipaumbele.

Akizungumza na wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Dr. Mwigulu amesema kuwa mkakati wa Halmashauri hiyo kujenga kituo cha kisasa cha polisi ni kitendo cha kupongezwa kwani wanalenga kukomesha uhalifu wa aina zote.

VIDEO: Le Mutuz, Awataka watumia mitandao waitumie kwa manufaa

Mtoto wa aliekuwa waziri mkuu mstaafu, William malecela 'Le Mutuz' amewataka watumia mitandao ya kijamii kuitumia vizuri kwa manufaa ili kujitengenezea kipato, ameyasema hayo leo akiwa katika chuo cha T I A kilichopo uhasibu ambapo alialikwa kama mgeni na kikundi cha Victorious Women Empowerment Ili kuelezana machache juu ya namna ya kumkomboa mwanamke.

vile vile amesisitiza na kuwataka kusoma kwa bidii wanafunzi ambao bado wako mashuleni wanasoma na kusema kuwa elimu ndio mafanikio yao na itawafanya kufikia leo, vile vile akawaeleza baadhi ya changamoto alizopitia hadi alipofikia hapo alipo kuwa alianza kulala stendi ya magari na kuchoma kuku KFC na hakujali kama baba yake alikuwa waziri mkuu.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA...... USISAHAU KUSUBSCRIBE.....

Waziri arudi CCM atwae jimbo 2020

Mwanasiasa  wa upinzani na aliyekuwa Naibu Waziri katika serikali ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete, Goodluck Ole Medeye, ametangaza kurejea Chama Cha Mapinduzi huku akidai kuwa ameamua kufanya hivyo kwa kuwa vitendo vya rushwa,-Hususan nyakati za uchaguzi, vimemalizwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Dk. John Magufuli.

 Ole Medeye juzi alisema kilichomkimbiza CCM mwaka 2015 na kujiunga na Chadema ni vitendo vya rushwa katika mchakato wa kupata wagombea wa chama hicho tawala.

Alisema anafurahi kuona sasa vitendo hivyo havipo ndani ya CCM baada ya kudhibitiwa na Rais Magufuli.Ole Medeye alikuwa mmoja wa wabunge watano wa CCM waliojiunga na Chadema Agosti 12, 2015 wakiongozwa na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa (Monduli).

Ole Medeye aliteuliwa na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kuwania nafasi ya Uspika wa Bunge baada ya Uchaguzi Mkuu.

Wengine waliohama pamoja na Lowassa ni Makongoro Mahanga (Segerea), James Lembeli (Kahama) na mbunge wa viti maalum, Esther Bulaya ambaye sasa ni mwakilishi wa wananchi wa Bunda Mjini (Chadema).

Hata hivyo, Ole Medeye alihama Chadema kabla ya mwaka kumalizika na kujiunga na UDP kinachoongozwa na John Cheyo Juni 12, 2016.

Medeye alisema alihamia UDP kwa kuwa inasimamia haki na demokrasia na kwamba yeye alikuwa akitaka demokrasia ya kweli na jukwaa la haki katika kuleta haki na maendeleo kwa Watanzania.

Alisema  kuwa alikaa chama hicho cha 'Bwana Mapesa' kwa miezi mitatu tu hata hivyo, kwa kuwa "nilikwenda kufanya kazi maalum."

Na sasa, Ole Medeye amesema ameamua kurejea CCM kwa kuwa kila mwanachama anayo fursa kushiriki uchaguzi, ikiwamo kugombea nafasi yoyote bila kutoa rushwa na akashinda.

"Mimi sijawahi kuwahonga watu ili wanichague," alisema Ole Mideye na "wakati huo CCM kulikuwa na rushwa sana; ndiyo maana nikaamua kukimbia.

"Lakini kwa sasa hakuna tena kitu kama hicho, hivyo nimeamua kurejea CCM."

Ole Medeye alisema katika Uchaguzi Mkuu ujao, mwaka 2020, anataka kurudi na kuwatumikia wananchi kupitia nafasi ya ubunge.

Maseneta wakwamisha serikali ya Trump

Bunge la Seneti nchini Marekani limeshindwa kuidhinisha mswada ambao ungeongeza ufadhili wa serikali ya kitaifa kwa mwezi mmoja.

Kufuatia hatua hiyo huduma nyingi za serikali zitakwama, hata hivyo athari kamili itaanza kuonekana siku ya Jumatatu, wakati wafanyakazi wa serikali watarejea kazini.

Mara ya mwisho shughuli za serikali zilikwama nchini Marekani ni mwaka wa elfu mbili na kumi na tatu, na ilidumu kwa muda wa siku kumi na sita wakati ambapo wafanyakazi wengi wa serikali walishurutishwa kwenda likizo ya lazima.

Ni mara ya kwanza kwa huduma za serikali kukwama huku chama cha Republican kudhibiti mabunge yote na ikulu ya White house.

Ikulu ya whitehouse imewalaumu wabunge wa Democrats kwa kuweka siasa juu ya maswala ya kiusalama , familia za wanajeshi, watoto walio katika mazingira magumu, na uwezo wa taifa hilo kuwahudumia raia wa Marekani.

Lakini kiongozi wa wabunge wa Democrats Chuch Schumer, alisema kuwa rais Trump alikataa makubaliano yasiopendelea upande wowote na hakukishinikza chama chake katika bunge la Congress.

Mkwamo wa huduma za serikali nchini Marekani ulifanyika mara ya mwisho 2013 na ukachukua muda wa siku 16.

Republicans waliutaja muswada huo kwa jina la ''Schumer Shutdown' na hawakukosea.

Chuck Schumer na wabunge wenzake wa Democrats kupitia usaidizi wa wabunge wachache wa Republican walizuia muswada ambao ungesaidia serikali kuendelea na shughuli zake, hata ijapokuwa kwa muda.

Hatahivyo kuchukua jukumu na kutoa lawama ni vitu viwili tofauti.

Democrats watasema kuwa walikuwa wamekubaliana na rais kupitisha muswada usiopendelea upande wowote kuhusu mabadiliko ya sheria ya uhamiaji, kabla ya kukiuka makubaliano hayo wakati wa mkutano katika afisi ya Oval wiki iliopita.

Swala la kurushiana lawama lilianza saa sita usiku na mshindi bado hajatangazwa.

Hatahivyo atakayeshindwa katika mkwamo huu ni chama kitakachoingia katika vita na idadi ndogo ya wabunge ikiwa ni habari mbaya kwa rais Trump na chama cha Republicans.

Habari njema ni kwamba , pande zote mbili na ngome zao za kisiasa zitafurahishwa kwa kufanya mambo kuwa magumu.

Kwa nini pande hizo mbili zisikubaliane?

Swala linalogombaniwa ni lile la Democrats kutaka zaidi ya wahamiaji wasio na vibali walioingia nchini Marekani kutofurushwa.

Wahamiaji hao walipatiwa vibali vya kuwa nchini humo kwa muda chini ya mradi ulioanzishwa na rais wa zamani Barrack Obama.

Mnamo mwezi Septemba, bwana Trump alitangaza alikuwa anasitisha mpango huo huku akilipatia bunge la Congress hadi mwezi Machi kuwa na mpango mbadala.

Waziri Ndalichako awapa wiki moja TBA

Waziri wa elimu,sayansi,na teknolojia na ufundi Profesa Joyce Ndalichako amewapa wiki moja Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kuonyesha maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa, hostel na ofisi kwa ajili ya chuo kikuu cha Muhimbili Kampasi ya Mloganzil

Waziri Ndalichako ametoa agizo hilo leo alipokuwa kwenye ziara ya kutembelea mradi huo na kutoridhishwa nao, baada ya kukuta hauna maendeleo yoyote huku serikali ikiwa imeshalipa gharama za ujenzi.

“Ninawapa wiki moja, nataka hapa nione vifaa vyote vya ujenzi viwe vimemwagwa vywa kutosha, nataka nione mafundi wa kutosha, haiwezekani site kubwa kama hii mafundi hawafiki hata 40, kweli kazi itaenda!? Niliwaambia muongeze mafundi mwezi wa 11 lakini kwa sababu mlizozijua wenyewe hamjaongeza, sasa ndani ya wiki moja wasipoongeza mafundi, hatuwezi kuwa na mkandarasi ambaye haendani na matakwa ya mteja, nimekwisha wapatia bilioni 3 na milioni 900,  nikiangalia fedha nimezitoa tangu mwezi wa 8 sioni kazi ambayo inafanana na kiwango cha fedha ambayo nimewapatia, ndani ya wiki moja wasipotimiza angalieni namna ya kuvunja huo mkataba.”, amesema Waziri Ndalichako.

Waziri Ndalichako ameendelea kwa kulalamika kuwa wakandarasi hao wamekuwa wakiaminiwa na serikali na kuwapa miradi mingi, lakini wamekuwa wakisua kukamilisha miradi kwa muda.

New VIDEO: Mr. Blue – Mbwa Koko

New VIDEO: Mr. Blue – Mbwa Koko

New VIDEO: Mr. Blue – Mbwa Koko

DOWNLOAD VIDEO

Nafasi za kazi leo Jan 20

Kocha Mpya wa Simba apagawishwa na Okwi

KIKOSI cha Simba,  Alhamisi kilijitanua kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Singida United katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo ambao Simba ilikuwa ikihitaji zaidi matokeo ya ushindi ili ijihakikishie nafasi yake ya kukaa kileleni, ilifanikiwa kupata bao la mapema dakika ya tatu lililofungwa na Shiza Kichuya. Beki wa kati wa timu hiyo,

Asante Kwasi, aliongeza bao la pili dakika ya 24 baada ya kukwepa mtego wa kuotea aliowekewa na mabeki wa Singida United.

Mara baada ya Kwasi kufunga bao hilo, kocha mpya wa Simba, Pierre Lechantre raia wa Ufaransa, alinyanyuka kwenye kiti chake akiwa jukwaani na kuanza kushangilia pamoja na ofisa habari wa timu hiyo, Haji Manara huku akiwapungia mkono mashabiki wa timu hiyo.

Dakika ya 65 wakati Emmanuel Okwi wa Simba anajiandaa kuingia kuchukua nafasi Mzamiru Yasin, mashabiki wa timu hiyo walikuwa wakimshangilia kwa nguvu jambo ambalo lilimhamasisha straika huyo na kuipatia Simba bao la tatu dakika ya 75.

Okwi aliongeza bao la nne dakika ya 82 ambapo kwa mara nyingine, Mfaransa, Lechantre aliinuka kwenye kiti na kushangilia kwa nguvu. Katika mchezo huo, Simba ilifanya mabadiliko ya wachezaji wawili ambapo ilianza kumtoa Mwinyi Kazimoto dakika ya 22 na nafasi yake kuchukuliwa na Said Ndemla kabla ya dakika ya 65 kutoka Mzamiru na kuingia Okwi.

Kwa upande wa Singida United, dakika ya 59 ilimtoa Kiggy Makasi na nafasi yake kuchukuliwa na Salum Chuku. Kwa matokeo hayo, Simba inaendelea kukaa kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 29 ikifuatiwa na Azam yenye pointi 27. Mtibwa Sugar ni ya tatu ina pointi 24, Singida inakamata nafasi ya nne na pointi 23, huku Yanga ikiwa ya tano na pointi 22.

Wafanyabiashara waifungukia Serikali

Waziri wa fedha na mipango, Dk Philip Mpango

Wafanyabiashara nchini wameiomba Serikali kuacha kufanyakazi kwa kukurupuka ikiwamo kuwaadhibu kwa makosa ya wengine badala yake iwe kitu kimoja na sekta binafsi ambayo ina mchango mkubwa kwa Taifa.

Wito huo ulitolewa jana na makamu mwenyekiti wa Mfuko wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Salum Shamte kwenye mkutano baina yao na Serikali ulifanyika katika ukumbi wa Hazina mjini hapa na kuhudhuriwa na wabunge na baadhi ya mawaziri.

Shamte alisema katika baadhi ya maeneo, Serikali imekuwa ikifanya mambo kwa kukurupuka na kujikuta ikiwaumiza wafanyabiashara ikiwamo masuala ya kodi.

Makamu mwenyekiti huyo alisema sekta binafsi inaumizwa kwa kiasi kikubwa na uamuzi wa kukurupuka hasa wa kuwaadhibu watu wasiohusika kwa kosa la mtu mmoja.

“Wakati mwingine watu wanaumizwa sana kwa ajili ya maamuzi haya, kodi na kufunga biashara za watu ilhali kosa linakuwa la mtu mmoja. Kwa nini hamuondoi kasoro hiyo?” alihoji Shamte wazo ambalo liliungwa mkono na mkurugenzi mtendaji wake, Godfrey Simbeye.

Akijibu hoja hiyo, waziri wa fedha na mipango, Dk Philip Mpango alikiri kuwapo kwa uamuzi wa kushtukiza serikalini na kusema wakati mwingine inalazimika kufanya hivyo.

Dk Mpango alisema wakati mwingine kuna madhara kwa watu kukurupuka na kufanya vitu visivyokuwepo na kusema ndani ya Serikali, kuna baadhi ya watumishi wasiokuwa waaminifu ambao wanafanya vitu ama kwa kukurupuka au kutokujua.

“Nakiri kweli ndani ya Serikali kuna watu ambao wanafanya mambo ya ovyo na kuisababishia Serikali hasara kubwa, lakini kuna wakati tunafanya hivyo kwa sababu inabidi tufanye hivyo kwa masilahi ya nchi,” alisema Dk Mpango.

Hata hivyo, aliwatupia lawama baadhi ya wafanyabiashara akisema wamekuwa na tabia ya kukwepa kodi jambo ambalo ni kinyume na Serikali.

Sababu ya Engine kumchukua Wolper

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Engine ambaye hivi karibuni kulikuwa na tetesi za kumng'oa Jackline Wolper na kumuweka ndani, ameweka wazi sababu za kuamua kumtumia msanii huyo kwenye kazi yake.

Akizungumza kwenye Friday Night Live Engine amesema Wolper ni miongoni mwa wanawake wachache Tanzania wanaojitambua, na ndio sababu iliyomfanya asifikirie mara mbili kumfuata.

“Wolper ni mwanamke jasiri, mwanamke anayejitambua , anajituma yuko fit kila idara, na ndio maana nikamfuata”, amesema Engine.

Msanii huyo ambaye ameachia kazi yake mpya, amewaomba watanzania kufuatilia kazi zake kwani alishafanya kazi nyingi siku za nyuma lakini hazikuwahi kufanya vizuri.

Waziri Mkuu aagiza kiongozi huyu akamatwe

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameamuru Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Mara kumkamata na kumuhoji Mkurugenzi Mtendani wa Mamlaka ya Maji Musoma (MUWASA) Mhandisi Gantala Said.

Agizo la Waziri Mkuu limekuja kufuatia tuhuma za ubadhirifu wa fedha za mradi wa maji Wilayani Bunda mkoani Mara zinazomkabili Mkuregenzi huyo. Waziri Mkuu yupo Mkoani humo kwa ziara ya kikazi.

Mhandisi Gantala Said ameshindwa kueleza sababu zilizosababisha mradi wa maji mjini Bunda kutokamilika pamoja na Serikali kutoa fedha nyingi kwaajili ya kutekeleza Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani.

Majaliwa amesema Mkurugenzi huyo amekuwa akimlipa mkandarasi fedha kabla ya kufanya kazi ambapo hadi sasa tayari mkandarasi wa mradi huo ameshalipwa zaidi ya Sh. bilioni saba na mradi haujakamilika huku wananchi wakiendelea kutumia maji ambayo siyo salama.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara Bw. Adam Malima ameagiza kufungwa kwa ofisi za MUWASA na kuwataka wafanyakazi wa mamlaka hiyo kutoruhusiwa kuingia ofisini hadi hapo uchungi utakapokamilika.

Wastara: "Sitozikwa na wasanii pekee"



Msanii Wastara Juma

Msanii wa filamu nchini Wastara Juma amesema hatokuja kumladhimisha mtu yeyote katika tasnia ya 'bongo movie' kuwa yeye hana pesa ya kujitibia ugonjwa wake unaomsumbua kwa madai hata siku ikitokea akifa hawezi kuzikwa na hao pekee yao.

Wastara ametoa kauli hiyo kwenye kipindi cha 'FRIDAY NIGHT LIVE' (FNL) kinachorushwa na EATV tinga namba moja kwa vijana, baaada ya kuwepo kwa baadhi ya watu kutomuamini kwa kile kinachomsumbua huku wengine wakidiriki hata kujaribu kumwambia anatafuta kiki kupitia tatizo hilo linalomsumbua la mguu wake.

"Yani hapa mtu anaweza akaniumiza kwa maneno au vitendo kwa sababu yeye anaamini kwa mawazo yake na kichwa chake kwamba, mimi nimekaa kitandani siumwi au pengine nimejiona nimepotea katika ulimwengu hivyo natafuta kiki yaani nijifunue nguo niupige picha mguu wangu uliyochanika kisha niuweke kwenye gazeti ama kwenye runinga (Tv) ?", alihoji Wastara.

Hata hivyo Wastara amesema hawezi kubadilisha fikra za watu wanavyofikilia kwa kuwa hayo ndiyo maisha yao ya kutoamini jambo lolote lile.

"Na kama kuna wasanii ambao wanaamini mimi siumwi siwezi kumladhimisha hata siku moja na ambaye atasema hatokuja kumtembelea Wastara kwa sababu haumwi au hana shida pesa, mimi siwezi kumfanya aniamini kwamba sina pesa. Sitoweza kufanya hicho kitu kwa sababu maelezo ninayoyaeleza katika runinga ndiyo yaleyale hayotokuja kubadilika. Kwa hiyo ninachoongea hapa ni ukweli hautokuja kubadilika miaka yote hata nikifa", alisisitiza Wastara.

Pamoja na hayo Wastara aliendelea kwa kusema "wapo watu wa kweli wanaoamini na wengine wasioamini ambao huwezi kuwafanya waniamini. Watanzania wanaoniamini mimi wanatosha kwa sababu mwisho wa siku sitokuja kujizika mwenyewe au kuzikwa na wasanii pekee yake", alisema Wastara.