Saturday, 20 January 2018

JINSI MWANAMKE ANAVYOWEZA KUPATA SARATANI YA MATITI-2


WIKI iliyopita nilianza kuzungumzia namna mwanamke anavyoweza kupata saratani ya matiti. Wiki hii nitaimalizia mada hii ili nianze mada nyingine. Iko hivi, saratani ya matiti pia inarithiwa. Endapo katika familia yenu au ndugu mwingine wa karibu sana alipatwa na saratani ya matiti, basi upo uwezekano wa wewe kupata saratani hii. Vinasaba vya saratani vinavyozunguka katika ukoo wenu ambavyo husababisha watu wa kwenu wapate saratani ya matiti, vinasaba vya saratani ya matiti vinaitwa BRCA 1 na BRCA 2.

Hali ya maisha pia huchangia mwanamke kupata saratani ya matiti. Wanawake walio katika hali bora ya maisha mfano wale wasomi wenye kipato kizuri au wafanyabiashara na wengine ambao wapo vizuri kiuchumi wapo hatarini kupatwa na tatizo hili. Wengine ni wanawake ambao wanazaa halafu hawanyonyeshi watoto au wanawanyonyesha kwa kipindi kifupi kutokana na sababu Jinsi

mbalimbali pia wapo hatarini kupata saratani hii. Mionzi iwe ya Xray au ya viwandani ikielekezwa mara kwa mara kwenye kifua cha mwanamke mwenye umri wa chini ya miaka thelathini basi anaweza kuja kupata saratani ya matiti miaka ijayo. Ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi mfano nyama choma, kitimoto, unywaji wa pombe na hata uvutaji wa sigara kwa mwanamke vinaweza kuleta madhara baadaye na kujikuta unapata tatizo hili.

Wengine wanaoathirika na tatizo hili ni wanawake wanene sana. Unene uliopitiliza utaujua kwa kupima uzito kwa kiwango cha BMI au Body Mass Index. Mwanamke mnene ana kiwango kikubwa cha homoni ya Estrojen inayoweza kumletea saratani ya matiti. Mwanamke ambaye tayari alishawahi kutibiwa saratani ya titi moja naye yupo hatarini kuathirika titi la pili. Matumizi holela ya vidonge vya uzazi wa mpango bila ya ushauri wa kitaalamu unaweza kuchochea kutokea kwa tatizo hili la saratani ya matiti.

Tatizo hili huanza kuwatokea wanawake kuanzia umri wa miaka ishirini hadi arobaini, hawa ndiyo kundi kubwa na likitokea katika umri wa zaidi ya miaka arobaini hali huwa mbaya zaidi. Kuna baadhi ya tafiti zinaonyesha kwamba, makundi mengine ya wanawake walio hatarini kupatwa na saratani ya matiti ni wale wanaofanya kazi za usiku, endapo watakaa karibu na taa za umeme zenye mwanga mkali kwa kipimo cha 50-60Hz, kutokana na miale yake ya magnetic kuzuia hali ya kawaida ya utoaji wa vichocheo vya melatonin ambavyo hasa hutoka wakati wa usiku mwilini mwa kila mwanamke, vikiwa na kazi maalumu ya kudhibiti utolewaji holela wa vichocheo vya Estrojeni ambavyo vikizidi ndipo saratani hii inatokea.

Makundi mengine ni wanawake wasagaji kutokana na tabia yao ya kutozaa au kuja kuzaa katika umri mkubwa wapo hatarini kupatwa na tatizo hili la saratani ya matiti, wafanyakazi wa kwenye ndege, hawa hupata saratani ya matiti.

NINI CHA KUFANYA? Saratani ya matiti ni rahisi kuidhibiti. Kuwepo na utaratibu wa mwanamke mmoja mmoja au kwa vikundi kumwona daktari au wataalamu wa afya kwa uchunguzi. Uwepo utaratibu wa maeneo ya kazi kuwafanyia upimaji wakinamama. Saratani ya matiti ikichelewa unaweza kupoteza uhai.

Ni vema uwahi hospitali kwa uchunguzi wa kina na tiba. Endapo itathibitika kuna tatizo kwenye titi lako, basi vipimo vya awali ni ultrasound, mamography, X-ray ya kifua na majimaji au kinyama kwenye titi ni muhimu. Endapo utahisi titi linauma, linatoa majimaji wakati hunyonyeshi au ukikamua linatoa damu, basi muone haraka daktari wako. Dalili nyingine ni kuhisi titi gumu au kuna uvimbe kwapani au ndani ya titi, chuchu zimezama ndani au ngozi ya titi inakuwa na makunyanzi kama ganda la chungwa.
DK. CHALE SIMU: +255713350084

TAHADHARI KUHUSU HOMA YA CHIKUNGUNYA, HAKUNA TIBA MAHUSI WALA KINGA

Serikali kupitia Wizara ya Afya imeutahadharisha umma kuhusu ugonjwa wa Homa ya Chikungunya ambao huambukizwa na mbu aina ya aedes na hauna tiba mahsusi wala kinga. Isome taarifa hii kuelewa zaidi kuhusu ugonjwa huo.








MAJALIWA ‘AMTUPA’ KIGOGO MIKONONI MWA TAKUKURU


BREAKING NEWS: WAZIRI AMTUMBUA MKURUGENZI WA MAJI MUSOMA



Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isaack Kamwelwe , ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira wa Mji wa Musoma, Gantala Said (pichani kushoto) ambaye anachunguzwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha kwenye Mradi wa Maji Bunda na akizivunja Bodi za Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira za Mikoa ya Arusha na Mara (Musoma) baada ya kujiridhisha kuwa utendaji wao siyo mzuri.

Kamwele amefikia uamuzi huo leo baada kubaini kuwa kumekuwepo na uzembe wa utekelezaji wa miradi ya serikali ya maji kwa baadhi ya watendaji katika idara hizo.

“Kufuatia ziara ya Waziri Mkuu, Kassim Majliwa mkoani Mara, imebainika kuwa kumekuwepo na matatizo ya huyo Mkurugenzi Gantala ambaye Waziri Mkuu ameagiza Mkurugenzi huyu watendaji wengine wachunguzwe na TAKUKURU.

“Hivyo kuanzia leo Januari 20, 2017 ninatengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira wa Mji wa Musoma, Gantala Said na nafasi yake itakaimiwa na Eng. Robert Petro Mponya wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUASA), ninamuagiza aisaidie Musoma ili waweze kufanya kazi inayotakiwa,” alisema Kamwele.
VIDEO: FUATILIA TUKIO HILO HAPA

Audio | Isha Mashauzi – Nibembeleze | Mp3 Download

Audio | Isha Mashauzi – Nibembeleze | Mp3 Download

Audio | Isha Mashauzi – Nibembeleze | Mp3 Download

DOWNLOAD MP3

New AUDIO & VIDEO: Chombaa – Baby Sumaya

New AUDIO & VIDEO: Chombaa – Baby Sumaya

New AUDIO & VIDEO: Chombaa – Baby Sumaya
DOWNLOAD VIDEO

DOWNLOAD MP3

Audio | Mr Blue – Mbwa Koko | Mp3 Download

Audio | Mr Blue – Mbwa Koko | Mp3 Download
 
Audio | Mr Blue – Mbwa Koko | Mp3 Download

DOWNLOAD Mp3

Wadaiwa kubakwa baada ya kujifungua hospitalini Kenya



Waziri wa afya nchini Kenya Dkt Cleopha Mailu ameamrisha uchunguzi kufanywa katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta baada ya wanawake waliojifungua kudai kwamba wanadhalilishwa kingono.

Taarifa zilizoenezwa kwenye mitandao zinadai kina mama waliojifungua wamekuwa wanashambuliwa na baadhi ya wafanyikazi wakati wakienda kwenye chumba cha watoto wachanga kuwanyonyesha watoto wao.

Chumba hicho cha watoto huwa ghorofa tofauti na wadi za wanawake waliojifungua.

Wasimamizi wa hospitali hiyo wamesema hawajapokea malalamiko yoyote.

Yote yalianza baada ya ujumbe kuandikwa aktika ukurasa wa Facebook kwa jina Buyer Beware ambao mara nyingi hutumiwa kuwatahadharisha wateja na wanunuzi wa bidhaa na huduma.

Ujumbe uliwatahadharisha kina mama wanaojifungulia katika hospitali hiyo kwamba wamo hatarini ya kudhalilishwa kingono na baadhi ya wafanyakazi wa hospitali hiyo.

Wanawake wengine walichangia na kudai wamewahi kudhalilishwa au jaribio kufanywa, au jamaa na marafiki zao wakadhalilishwa.

Wengi wanadai kina mama waliojifungua waliviziwa wakiwa njiani kuelekea chumba hicho cha kunyonyeshea watoto au wakirudi chumba chao baada ya kunyonyesha.

Baadhi ya wanaodaiwa kunyanyaswa kingono, ujumbe unasema, walitendewa kitendo hicho siku chache baada yao kujifungua kupitia upasuaji.

Waziri Mailu ameagiza uchunguzi wa dharura kufanyika na ripoti kamili kuwasilishwa kwake kufikia Jumatatu.

Afisa mkuu mtendaji wa hospitali hiyo Lily Koros amesema hakuna mwanamke hata mmoja aliyewahi kulalamika kwamba alidhalilishwa kingono hospitalini humo.

Amesema hospitali hiyo huwa chini ya uangalizi wa kamera za usalama (CCTV) wakati wowote na hakuna kisa hata kimoja kilichogunduliwa.

Amewataka walio na habari kupiga ripoti kwa maafisa wa hospitali au polisi.

Hospitali ya taifa ya Kenyatta, Nairobi huwahudumia kina mama takriban 100 wanaojifungua kila siku.

Watoto waliozaliwa huwekwa chumbani ghorofa ya kwanza nao wanawake kwenye wodi za kujifungulia kwenye ghorofa ya chini.

Maswali sasa yameanza kuulizwa kuhusu muundo na mpangilio wa vyumba katika hospitali hiyo ambao huwalazimu kina mama waliojifungua kupanda ngazi au lifti kwenda kuwanyonyesha watoto wao, ikizingatiwa kwamba baadhi hujifungua kupitia upasuaji.

Diwani afariki dunia Kwimba



Diwani wa Kata ya Lyoma katika Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza, Julius Samamba (CUF), amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Taarifa kwa umma iliyotelewa leo Ijumaa (jana) na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Pendo Malebeja imeeleza kuwa diwani huyo alifariki dunia Januari 16 akiwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza alikolazwa kwa matibabu.

“Mazishi ya marehemu yanatarajiwa kufanyika leo Januari 19 katika kijiji cha Kimiza kata ya Lyoma,” anasema taarifa hiyo.

Pamoja na kutoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki, madiwani na watumishi wa halmashauri hiyo, Malebeja amesema kifo cha diwani huyo kuwa pigo kwa halmashauri kutokana na umahiri na uwezo aliokuwa nao katika kujenga na kusimamia hoja kwenye mijadala ya masuala ya maendeleo.

Source: Mwananchi

Povu la kocha wa Simba kwa Mavugo


Laudit Mavugo.

KOCHA Msaidizi wa Simba, Masoud Djuma amesema kuwa ushindi ambao timu yake iliyoupata juzi Alhamisi katika mchezo dhidi ya Singida United ulichangiwa kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya wachezaji wake huku akimtolea ‘povu’ straika wale Laudit Mavugo.

Simba ilipata ushindi wa mabao 4-0 katika mchezo wa Ligi kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa dhidi ya wababe hao wa Singida ambapo mabao yake yalifungwa na Shiza Kichuya, Asante Kwasi na Emmanuel Okwi aliyefunga mawili. Akizungumza mara baada ya mchezo huo, Djuma alisema nafasi ya Okwi kucheza ilitakiwa ichukuliwe na Mavugo lakini kwa kuwa

Mavugo hakuonyesha kiwango kizuri mazoezini ilimbidi afanye mabadiliko hayo. “Okwi amefanya mazoezi na sisi siku mbili tu kama mnavyojua hakuwepo kambini, nilipanga kumtumia Mavugo lakini nimemwambia kuwa hakuonyesha uwezo mzuri, ndiyo maana nikaamua kumpa nafasi Okwi na kweli ameitumia vizuri. “Nimeshamueleza Mavugo kuwa yeye ni ndugu yangu lakini katika hili suala la kazi anatakiwa kuonyesha uwezo na kufanya kweli, siwezi kumpa nafasi kama haonyeshi uwezo,” alisema kocha huyo.

KUHUSU KOCHA MPYA

Kuhusu kocha mpya wa Simba, Pierre Lechantre raia wa Ufaransa aliyekuwepo jukwaani akifuatilia mchezo huo, Djuma alisema yeye hana tatizo na ujio wa kocha huyo, anamkaribisha na yupo tayari ku- fanya naye kazi. “Nipo tayari wala sina tatizo, namkaribisha na tutakuwa pamoja, kuhusu mfumo na maendeleo mengine nitampatia ripoti kisha yeye ndiye atakayeamua juu ya kutumia au la,” alisema. Upande wa Kocha wa Singida United, Hans van Pluijm alisema matokeo ya mchezo huo yametokana na walinzi wake kufanya makosa na Simba wakayatumia vizuri.

Mapenzi yamtesa Kajala kisa mwanaye



STAA wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja amefunguka kuwa hivi sasa anaumizwa na mapenzi ya kufichaficha kwa sababu ya kulinda heshima yake kwa mtoto wake wa kike, Paula kwa kuwa sasa amekuwa msichana mkubwa.

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Kajala alisema amekuwa kwenye wakati mgumu sana wa kuwa na uhusiano wa kificho lengo likiwa ni kutomharibu mwanaye huyo ambaye ana uelewa mkubwa na anatambua kila kitu.

“Sipendi Paula anijue kiundani kuhusiana na mahusiano kwa sababu kwa umri aliofikia na darasa alilopo (Kidato cha nne) kama sitakuwa na usiri ataelewa kila kitu, sio Kajala yule tena wa zamani wa kuweka mpenzi wazi ingawa inaniumiza kwani sikuzoea, na mapenzi ya siri yanaumiza asikwambie mtu,” alisema Kajala.



Chuchu Hans afunguka kuachana na Ray


MSANII wa filamu za Kibongo, Chuchu Hans ameibuka na kusema kuwa tetesi zilizozagaa akidaiwa kuachana na mzazi mwenziye Vincent Kigosi ‘Ray’ na kwamba ndiyo sababu ya kubadili jina lake kwenye ukurasa wake wa Instagram siyo za kweli.

Awali kwenye ukurasa wa Insta Chuchu alikuwa akijiita Chuchu Hans the Great na sasa anajiita Chuhans Kichuna, jambo lililowafanya wengi waamini safari ya mapenzi yao imefika mwisho.

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Chuchu alisema kuwa yeye ameamua tu kubadili jina na wala hajaachana na Ray na kama wapo wanaosubiri penzi livunjike, watasubiri sana.

“Waniache jamani kila siku nimeachana na Ray… nimeachana na Ray…, nina sababu zangu za kubadilisha jina, haina maana kwamba tumeachana, hata hivyo sitaki kuongelea sana suala hilo kama tumeachana au la, majibu mtayapata subirini tu,”alisema Chuchu.

Serikali Yakataza Kulima Pamba kwa Mkataba


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imekataza kilimo cha pamba cha mkataba kwa sababu kinawanyonya wakulima.

Ameyasema hayo jana (Ijumaa, Januari 19, 2018) wakati akizungumza na wananchi baada ya kukagua zahanati ya Hunyari wilayani Bunda, akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Mara.

“Ni marufuku kwa wanunuzi wa pamba kulima pamoja na wakulima kwa sababu wakulima wanakosa uamuzi wa kupanga bei. Kuanzia sasa zao hilo litauzwa kwa njia ya mnada.”

Alisema Serikali imeweka mkakati wa kuimarisha mazao makuu ya biashara ambayo uzalishaji wake umeanza kupungua likiwemo na zao la pamba.

Waziri Mkuu alisema Serikali imeamua kushiriki kikamilifu katika usimamizi wa kilimo cha zao la pamba kuanzia hatua za maandalizi ya shamba, pembejeo hadi masoko.

Pia Waziri Mkuu amewaagiza Maofisa Kilimo katika wilaya hiyo wawafuate wakulima vijijini kwa ajili ya kutoa elimu itakayowawezesha wakulima kulima kwa kufuata njia bora za kisasa.Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka wafugaji kuhakikisha wanakuwa na idadi ya mifugo kulingana na uwezo wa eneo lao.“Marufuku kulisha mifugo katika mashamba ya watu.”

Amesema Serikali itachukua hatua kali za kisheria kwa mfugaji yeyote atakayelisha mifugo yake katika mashamba ya wakulima kwani tabia hiyo huchangia migogo baina yao.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU