Thursday, 18 January 2018

Makonda: Dar Kujengwa Kiwanda Kikubwa Zaidi Barani Afrika


Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda leo amekutana wawekezaji kutoka China kujadiliana kuhusu mambo ya uwekezaji nchini Tanzania.

Mhe Makonda akizungumza katika mkutano huo Mhe. Makonda amesema kuwa  kutokana na malengo yaliyo wekwa na Wizara ya TAMISEMI maelekezo kutoka kwa Rais John Pombe Magufuli kuwa kila Mkoa uhakikishe unajenga viwanda 100 hivyo wawekezaji hawa wanakwenda kuwekeza Tanga na kunduchi jijini Dar es Salaam na wana wekeza miradi yenye  thamani ya Dola  bilioni 3dola.

Aidha amewataka wanachi wa mkoa huo kuchangamkia fursa za uwekezaji
"sisi kazi yetu  kama serikali ni kuweka mazingira ya uwekezaji na hawandugu zetu wametoka jimbo la  nilizungumza nao nilipotembelea huko kwao mwakajana"Amesema Makonda.

Pamoja na hayo Makonda  amesema kuwa kuna clip ina zungunguka mtandaoni ikieleza kuwa Ethiopia wana kiwanda kikubwa zaidi kuliko nchi zote barani Afrika na kusema kuwa wananchi wasihofu kwani Dar es Salaam itajenga kiwanda kikubwa zaidi ya mara tatu ya hicho chenye  mita za mraba Milion Tano na uwekezaji huu utafanyika wilayani Kigamboni.

"Kuna mwekezaji mwingi ameonyesha nia ya kuwekeza kiwanda cha sukari nawaomba wafanyabiashara wetu mchangamkie fursa hizo za kibiashara   na vijana pia mchangamkie fursa za ajira" Amesema Makonda.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa jimbo la Gwangzou , Xie zhenghy kutoka China amesema wao wako tayari kwa uwekezaji na katika nchi ambazo zitaendana kiutamaduni kama ilivyo kwa Tanzania.
Hata hivyo amesema kuwa China imekuwa na nafasi kubwa ya kuwekeza barani Afrika ambapo imekuwa na uwekezaji mkubwa nchini Misri.

Akizungumzia uwekezaji hapanchini amesema kuwa uwekezaji watakaofanya ni ule unaendana na kaulimbiu ya Rais John Pombe Magufuli.

Bunduki ya kivita yenye skafu ya Chadema yakamatwa Shinyanga


Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule akionesha silaha aina ya AK-47 yenye namba 18116428 na mafuta ya kulainishia silaha yaliyotupwa na majambazi waliotaka kuvamia kiwanda cha Jielong

 Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limefanikiwa kukamata silaha ya kivita aina ya AK-47 iliyotupwa na watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi waliokuwa wanataka kuvamia kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Jielong Holdings (Tanzania) Ltd kilichopo Nhelegani katika kata ya Kizumbi manispaa ya Shinyanga.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Alhamis Januari 18,2018 Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Simon Haule amesema walikamata silaha hiyo usiku wa kuamkia leo majira ya saa tano eneo la Tinde wakati majambazi hao wanafuatiliwa na polisi ndipo wakaamua kutupa bunduki hiyo.

“Silaha hii aina ya AK-47 yenye namba 18116428 ilikuwa imefungwa kwenye skafu yenye rangi ya nembo ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ikiwa na risasi 25 ndani ya magazine yake na risasi zingine 8,zikiwa kwenye mfuko mdogo wa nailoni”,alieleza Kamanda Haule.

“Majambazi wawili pia walitelekeza pikipiki aina ya SANLG yenye namba za usajili MC 856 BPF,mafuta ya cherehani ya kulainishia silaha,tochi mbili na koti zito”,aliongeza.

Alisema jeshi la polisi lilipata taarifa za majambazi hao kutaka kuvamia kiwanda hicho kinachomilikiwa na raia wa China tangu tarehe 6.01.2018 kisha kuanza kuwafuatilia na kubaini kuwa baadhi yao ni wakazi wa Kahama na Ushirombo ambapo amewataka kujisalimisha polisi.

Magari zaidi ya 200 yakiwepo ya Watalii yakwama Monduli




Arusha. Magari zaidi 200 yakiwepo ya watalii yaliyokuwa yanaelekea Karatu kwenda Hifadhi ya Ngorongoro na Serengeti yamekwama katika eneo la Makuyuni baada ya daraja kusombwa na maji.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi, Kamanda ya Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amesema jitihada za kutengenezwa njia ya muda zinaendelea.

Amesema daraja hilo limesombwa na maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha Wilaya ya Monduli.

"Hadi sasa hakuna vifo ambavyo vimetokea ila ni kusombwa kwa daraja ambalo lilikuwa linaendelea kujengwa," amesema.

Baadhi ya madereva waliokwama Ismail Kessy na John Michael wamesema tangu saa 12 alfajiri wamekwama katika eneo hilo.

"Hii si mara ya kwanza daraja hili kusombwa na mafuriko tunaomba Serikali kuingilia kati kwani tuna watalii ambao walipaswa kuwa Serengeti lakini wamechelewa," amesema.

Mwenyekiti wa Chama cha Waongoza Watalii (TTGA), Khalifa Msangi ameomba daraja hilo kujengwa kwa ubora unaostahili ili kuondoa adha ya kuharibiwa na mafuriko mara kwa mara.

RC Iringa atoa agizo kwa Wakuu wa Shule

Iringa. Siku moja baada ya Rais John Magufuli kupigilia msumari wa mwisho suala la michango kwa wanafunzi mashuleni, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza amewataka walimu wakuu wa shule zote mkoani kwake kuandika barua kueleza aina ya michango iliyopo shuleni kwao na sababu za uwepo wake.

Masenza ameonya mwalimu ambaye atatoa taarifa za uongo katika barua yake hatua zitachukuliwa dhidi yake ikiwamo ya kuondolewa katika nafasi yake.

"Kwenye waraka ambao kila mtu anao unazungumzia elimu bila malipo, tayari Serikali ilishaelekeza namna ya kuendesha elimu bila malipo, waraka namba 3 wa 2016 unaozungumzia elimu bila malipo na waraka wa elimu namba 8 wa 2011 kuhusu michango mbalimbali wanayopaswa kutoa wazazi kupitia kamati na bodi za shule," amesema Masenza na kuongeza;

"Mimi ninajua katika kamati na  bodi za shule ninyi ni makatibu, ikifika katika jambo hili, tafadhali kila mwalimu aone hahusiki na jambo lolote linalozungumzia michango katika shule za msingi na sekondari na kama kuna hitaji lolote libainishwe na jamii," amesema.

Amesema shule ni za jamii na jamii ikibainisha yenyewe nje ya utaratibu wa mwalimu mkuu juu ya nini wanataka kufanya na kusimamia wao wenyewe hilo linaruhusiwa.

"Sasa nimewaita ili nijiridhishe, nitamtaka kila mwalimu mkuu wa shule kwa mkono wake mwenyewe aandika barua ya kueleza kama shule yake ina mchango ama la na barua sote ziandikwe kwa mkuu wa mkoa," amesema Masenza.

Masenza amesema barua hizo zitapitiwa na ofisi yake na kisha ukaguzi utafanyika katika kila shule  zikihojiwa kamati na bodi za shule kubaini michango kama ipo sababu za uwepo na namna amehusika kuwepo kwa michango hiyo.

Katika hatua nyingine mkuu huyo amewaagiza wakuu wa shule kuwapokea wanafunzi wote wanaotarajia kujiunga na kidato cha kwanza bila kujali wana sare za shule ama la.

Katika hatua nyingine mkuu huyo wa mkoa amewataka wakuu wa shule zote za binafsi mkoani humo kuwarejesha wanafunzi waliowaondoa shuleni mwao kutokana na kutofikia wastani wa ufaulu wanaoutaka la sivyo shule zao zitafungwa.

Simba SC yamtangaza rasmi Kocha mpya


Pierre Lechantre

Klabu ya Simba leo imemtangaza rasmi Mfaransa Pierre Lechantre, kuwa Kocha mpya atakayekinoa kikosi hicho ambacho kilikuwa hakina mwalimu baada ya kumfukuza aliyekuwa kocha wake, Joseph Omog mwishoni mwa mwaka jana.

Taarifa hiyo iliyotolewa na Msemaji Mkuu wa Klabu hiyo, Haji Manara imeeleza kuwa kocha huyo ataanza kazi mara moja na atasaidiwa na kocha msaidizi wa sasa Masoud Djuma ambae alikuwa akikaimu nafasi hiyo na Mfaransa huyo atashuhudia mchezo wa Simba SC dhidi ya Singida United leo Januari 18, 2018 katika Uwanja wa Taifa.

Mfaransa huyo alishawahi kukinoa kikosi cha timu ya taifa ya Cameroun kilichoshinda ubingwa wa Afrika mwaka 2000 na ameshawahi kushinda tuzo ya kocha bora wa bara la Afrika 2001.

Soma zaidi taarifa hiyo kutoka Simba SC;

                                          TAARIFA KWA UMMA

Klabu ya Simba inayo furaha kubwa kuwajulisha Wanachama na washabiki wake kwamba imempata kocha wake mkuu mpya,Mfaransa Pierre Lechantre.

Kocha huyo mzoefu ataanza kazi mara moja na atasaidiwa na kocha msaidizi wa sasa Masoud Djuma ambae alikuwa akikaimu nafasi hiyo

Kocha Lichantre keshawahi kufundisha vilabu kadhaa duniani kikiwemo kikosi cha Timu ya Taifa ya Cameroun kilichotwaa ubingwa wa Africa 2000.

Kocha huyo pia alipata kuwa kocha bora wa Afrika mwaka 2001 na pia barani Asia mwaka 2012.

Lechantre amekuja pia na kocha wa viungo Mmorocco Mohammed Aymen Hbibi, Na leo jioni kocha Lechantre ataishuhudia Simba ikicheza na Singida United kwenye Uwanja wa Taifa.


VIDEO: Kiwanda Kikubwa Afrika Chatua Kigamboni



Dar es Salaam kujenga kiwanda kikubwa zaidi ya mara tatu ya ya Kiwanda cha Ethiopia chenye  mita za mraba Milion Tano na uwekezaji huu utafanyika wilayani Kigamboni.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI.......USISAHAU KU SUBSCRIBE

VIDEO: Mwenyekiti Bavicha Amvaa Magufuli


Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema Patrick Ole Sosopi amesema kitendo cha Rais John Pombe Magufuli Kumuita Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowasa Ikulu na Kumshawishi kujiunga na CCM sio kitendo ambacho kinafaa kufumbiwa macho.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI.......USISAHAU KUSUBSCRIBE


Mtulia sasa kupambana na meneja wake Kinondoni


Aliyekuwa meneja kampeni wa Maulid Mtulia kwenye uchaguzi wa 2015 Kinondoni, Rajabu Salim Jumaa leo Alhamisi amechukua fomu kugombea ubunge jimbo hilo.

Mwaka 2015 mgombea wa CUF Mtulia alishinda ubunge wa jimbo hilo lakini alijivua uanachama wa CUF na kuhamia CCM na hivyo kupoteza sifa ya ubunge.

Akizungumza leo Alhamisi, Juma amesema atamshinda Mtulia katika nafasi hiyo kwa sababu anaisababishia Serikali hasara.

"Gharama kubwa za uchaguzi zinasababishwa na Mtulia ambaye alishakuwa mbunge lakini amejiuzulu na kutaka tena ubunge.”


Afariki Dunia kwa kugongwa na ndege Mwanza



Mkazi mmoja wa mkoa wa Mwanza amefariki dunia baada ya kuigonga ndege ya Fastjet iliyokuwa ikiruka katika Uwanja wa Ndege Mwanza kuelelea jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Mwananchi leo Januari 18, 2018 Kaimu MKurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Richard Mayongela amesema tukio hilo la aina yake limetokea jana usiku.

Amesema ndege hiyo ilikuwa njia moja kuelekea jijini Dar es Salaam, kubainisha kuwa mtu huyo ndiye aliyeigonga ndege hiyo.

“Ingawa ndege ndio ilimgonga mtu huyo ambaye jina lake hatulifahamu, kisheria mtu au kitu chochote kinachokuwa kwenye njia ya kurukia  na kutua ndege ndiyo kinahesabiwa kuigonga ndege. Ni kama ilivyo kwa treni,” amesema Mayongela.

Amesema kabla ya ndege hiyo kuruka,  taratibu zote za kiusalama zilifuatwa ikiwemo kukagua njia kujiridhisha hakuna kitu chochote.

“Haijulikani mtu huyo alitokea wapi. Vyombo vya ulinzi na usalama vipo eneo la tukio kuchunguza tukio hilo kwa kina na tutatoa taarifa kamili uchunguzi utakapokamilika,” amesema kaimu mkurugenzi huyo.

Amesema kitendo cha mtu huyo kuwepo katika njia ya kurukia ndege licha ya ukaguzi kufanyika kinawaumiza vichwa viongozi na wataalam wa usalama uwanjani hapo.

 “Pengine tatizo la muda mrefu la kukosa uzio tunaloanza kukabiliana nalo kwa ujenzi na upanuzi wa uwanja linaweza kuwa chanzo cha mtu huyo kuingia katika njia ya kurukia ndege,” amesema.

Ili kukabiliana na matukio ya aina hiyo, amesema wataimarisha mifumo ya usalama kwenye viwanja vya ndege nchini.

Majaliwa ampa maagizo RC Mghwira kuhusu KNCU



Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira asitishe uuzwaji wa mali za Chama cha Ushirika cha Kilimanjaro (KNCU).

Ametoa agizo hilo jana jioni (Jumatano, Januari 17, 2018) wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Serengeti, wilayani Tarime.

Hatua hiyo imekuja baada ya KNCU kutangaza kuuza shamba lake kwa ajili ya kuiwezesha benki yake ya KCBL  kutimiza sharti la mtaji la Benku Kuu ya Tanzania (BoT).

Benki hiyo ya KCBL inatakiwa kutimiza sharti la kuwa na mtaji kamili unaotosha wa shilingi bilioni  tano (5) katika kipindi cha miezi sita tangu kutolewa kwa tangazo hilo.

Waziri Mkuu alisema ni marufuku kuuza mali za Ushirika huo, hususan katika kipindi hiki ambacho Serikali inafanya uhakiki wa mali za vyama mbalimbali vya Ushirika nchini.

Alisema Serikali imedhamiria kuimarisha Ushirika nchini na sasa inafanya uhakiki wa mali za vyama vya Ushirika na watakaobainika kuhusika na ubadhilifu watachukuliwa hatua.

Januari 4, 2018 BoT ilizipa miezi sita benki tatu ili ziweze kuongeza kiwango cha mtaji unaohitajika kutokana na matakwa ya kisheria ya kuwa na mtaji kamili wa kutosha.

Benki hizo ni Kilimanjaro Co-Operative Bank Limited, Tanzania Women Banki Plc na Tandahimba Community Bank Limited, zitakaposhindwa kutekeleza agizo zitachukuliwa hatua.

BoT ni itazifutia leseni na kusimamisha shughuli za kibenki chini ya ufilisi, iwapo benki hizo zitashindwa kutekeleza agizo hilo ihadi kufikia Juni 30, 2018.

Walcott atuma ujumbe wa mwisho kwa Arsenal



Inauma ukiondoka sehemu ambayo umeizoea kwa muda mrefu. Theo Walcott ametuma ujumbe kwa mashabiki wa klabu ya Arsenal baada ya kuhamia Everton.

Mchezaji huyo ambaye amesajiliwa na Everton kwa ada ya uhamisho wa paund milioni 20 na kukabidhiwa jezi namba 11, amedumu Arsenal kwa miaka 12 na ameichezea jumla ya michezo 397 na kushinda magoli 108.

Huu ndio ujumbe ambao Walcott amewatumia mashabiki wa Arsenal:
Ninataka tu kusema shukrani kubwa kwa mashabiki wote wa Arsenal. Nimekuwa nimesumbuliwa na ujumbe ambao nimepata leo kheri na siwezi kukushukuru kwa kutosha, na hasa kwa miaka 12 iliyopita. Nataka tu kuwatakia kila mmoja katika klabu kila la kheri kwa siku zijazo.

Mashindano ya elimu kuanza kutimua vumbi Februari 28



Katika kuonesha kwamba wanaunga mkono suala la elimu bora nchini Taasisi ya Teacher's Junction imeandaa mashindano kwa shule za binafsi nchini ambapo wanafunzi wa darasa la nne, sita la saba watafanya mitihani ya kujipima nguvu lengo likiwa ni kuongeza ufanisi baina ya wanafunzi hao na pia kuwarahisishia walimu kujua wapi wanapaswa kuongeza nguvu.

Mashindano hayo yamepangwa kufanyika kuanzia Februari 28 hadi Machi 1 na kushirikisha takribani shule 120 nchini.

Akizungumza na wandishi wa habari leo, Afisa Mradi wa taasisi hiyo, Njama Salum alisema walianzisha mradi huo ili kuongeza kiwango cha elimu nchini kwa wanafunzi wa shule za msingi lakini pia wakiwa na mpango wa kupeleka mradi huo hadi kwenye shule za Sekondari.

" Kiu ya taasisi yetu ni kuona kiwango cha elimu kinaongezeka nchini, hivyo kwa kushirikiana na wadau wa elimu hasa wamiliki wa shule tukaja na wazo hili la kufanya mashindano ambayo tunaamini yanawajenga wanafunzi kuanzia kiakili hadi kujiamini pale wanapofanya mitihani ya Kitaifa.

" Kikubwa tunatoa zawadi za medali kwa wanafunzi wanaofanya vizuri lakini shule ambazo zitafanya vizuri tunatoa zawadi za ngao. Na mitihani hii hufanyika mara tatu kwa mwaka ambapo kwa kuanzia tunaanza mwezi Machi kisha tutafanya mwingine Mei halafu Agosti tutafanya mwingine," alisema Njama.

Alisema tayari washapata zawadi lakini bado anatoa fursa kwa wadau wengine wa elimu kujitokeza kwa wingi kuwaunga mkono ili kuweza kuzalisha kizazi bora cha vijana wenye elimu ambao watakuja kuwa msaada mkubwa kwa Taifa hapo baadaye.

Akizungumzia sababu za kutohusisha Shule za Serikali, Njama alisema sio kwamba wamezitenga shule hizo lakini wao kama taasisi waliangalia ni wapi wanaweza kupenyeza wazo lao kwa haraka zaidi na kwamba taratibu za kuonana na viongozi wa kiserikali ili kuangalia uwezekano wa kupeleka mradi huo kwenye shule hizo unafanikiwa kusudi kila mwanafunzi nchini aweze kunufaika nao.

Kwa upande mwingine Njama alisema taasisi yake pia imekuwa ikisaidia walimu ambao wapo mitaani bila ajira kwa kuwatafutia kazi kwenye shule za binafsi ambazo wana ushirika nazo lengo likiwa ni kumaliza tatizo la ajira nchini.

" Sisi pia tunasaidia vijana wenzetu ambao wana taaluma ya ualimu ambao wapo mitaani ambapo kwa mwaka uliopita zaidi ya vijana 356 ambao wana taaluma ya ualimu tuliwatafutia kazi katika shule mbalimbali nchini," alisema Njama.

Mwanamke mjamzito atolewa kopo la mafuta sehemu za siri



Veronica Paschal (29) mkazi wa Kishili jijini Mwanza ametolewa kopo la mafuta ya kujipaka mwilini katika sehemu za siri, ikiwa ni muda mfupi baada ya kuwaeleza ndugu zake kuwa anataka kujifungua kopo.

Licha ya kutolewa kopo hilo, daktari aliyekuwa zamu katika kituo cha afya Igoma jijini hapa, Zaitun Lionge amelieleza Mwananchi leo Januari 18, 2018 kuwa mimba ya miezi sita ya mwanamke huyo ipo salama.

Tukio hilo la aina yake limetokea jana Januari 17, 2018 baada ya Veronica kufikishwa katika kituo hicho cha afya na ndugu zake waliomtoa kwenye zahanati binafsi.

“Mwanzoni hawakuonyesha ushirikiano ndio tukawambia tutafanyaje. Wakasema kuna kopo kwamba ndugu yao anataka kujifungua kopo, tukauliza kopo linazaliwaje? Amehoji na kuongeza,

“Tukawambia hilo kopo halijaingia lenyewe mtakuwa mmeliweka wenyewe. Kopo lilikuwa halionekani lakini anavyojaribu kusukuma likatokezea.”

Amesema walipomchunguza kwenye vipimo ndipo walipolibaini kopo hilo la mafuta ya kujipaka mwilini, kwamba baada ya kulitoa waliita Polisi kuchukua maelezo ya mhusika na ndugu zake.

Amesema ujauzito wa mwanamke huyo uko salama kutokana na njia kutofunguka baada ya kuondolewa kopo hilo.