Sunday, 31 December 2017

Msuva Arejea Nyumbani Kwa Mapumziko Baada Ya Kazi Nzuri Morocco



WINGA wa kimataifa wa Tanzania, Simon Happygod Msuva anatarajiwa kurejea nchini Alhamisi kwa mapumziko ya baada ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Morocco, maarufu kama Botola.

Akizungumza na Bin Zubeiry Sports – Online leo, Msuva amesema kwamba Ligi ya Morocco inakwenda mapumzikoni naye anarejea nyumbani kwa mapumziko na kujipanga kwa mzunguko wa pili.

“Natarajia kurudi nyumbani kuanzia Alhamisi kwa mapumziko ya baada ya mzunguko wa kwanza Ligi Kuu huku, na pia kujipanga kwa mzunguko wa pili kabla ya kurudi kambini,”amesema.

Msuva anaweza kuwa kwenye mapumziko marefu, kwa sababu michuano yote nchini Morocco sasa itasimama kupisha Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) zinazohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee zinazotarajiwa kuanza Januari 13 hadi Februari 4, mwakani.

Simon Msuva (kulia) amefunga mabao matano katika mechi 13 za ligi ya Morocco na ametoa pasi za mabao matatu

Msuva anarejea nyumbani akitoka kuifungia bao pekee Difaa Hassan El-Jadidi ikishinda 1-0 dhidi ya Hassania Agadir Ijumaa.

Msuva, mchezaji wa zamani wa Yanga alifunga bao hilo dakika ya 52 katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Ben Ahmed El Abdi mjini El Jadida, Mazghan nchini Morocco na sasa anafikisha mabao matano katika mechi 13 za ligi ya Morocco, akiwa pia ametoa pasi za mabao matatu.

Msuva anazidiwa mabao mawili mawili na Mehdi Naghmi wa Ittihad Tanger na Jalal Doudi wa Hassania Agadir wanaoongoza kwa mabao yao saba kila mmoja, wakifuiatiwa na Mouhcine Lajour wa Raja Casablanca mabao sita sawa na Bilal El Magri, Hamid Ahadad wote wa Difaa Hassan El-Jadidi na Abderrahim Makran.

Mbali na Msuva aliyewahi pia kuchezea Moro United baada ya kupita akademi ya Azam FC, mwingine mwenye mabao matano ni Badr Kachani wa Hassania Agadir.

Ikumbukwe Msuva yupo katika msimu wake wa kwanza Difaa Hassan El-Jadidi baada ya kujiunga na timu hiyo kutoka Yanga SC ya Tanzania.


Mwaka Mpya wa 2018, Watanzania wakumbushwa kudumisha amani


Katika kuelekea mwaka Mpya wa 2018 watanzania wamekumbushwa kuenzi na kudumisha Mshikamano, Amani na Upendo hususani kwa makundi ya wasiojiweza, yatima na wazee kutokana na kwamba, vitendo hivyo vimeendelea kuwa mhimili na kichocheo muhimu katika kufikia Maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.

Haya yanajidhihirisha kwa vitendo baada ya kikosi cha Jeshi la wananchi 313 Monduli kufika katika kituo cha watoto yatima Global Cha Arusha ambapo kwa pamoja wameshiriki katika shughuli za usafi wa mazingira ya kituo hicho, kufua shuka na mablanket ya watoto lakini pia kutoa msaada wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni Tatu na fedha taslimu shilingi laki tano ikiwa ni ishara ya Upendo kwa yatima hao .

Mkurugenzi wa kituo hicho Mack Donald Kavishe anasema ni kwa mara ya kwanza kupata ugeni kama huo na kuongeza kuwa kitendo cha kushiriki usafi na kutoa msaada huo ni tiba ya kisaikolojia kwa watoto hao ili wasijisikie upweke.

Baadhi ya msaada wa vitu vilivyokabidhiwa ni Sukari, mchele, mafuta ya kujipaka na kupikia, magodoro, chumvi, vifaa vya usafi, madaftari, unga na maharagwe.


Ajali mbaya ya Barabarani Kenya, Yaua watu 36 na wengine zaidi ya 11 kujeruhiwa



Watu 36 wamepoteza maisha na wengine 11 kujeruhiwa katika ajali mbaya ya barabarani nchini Kenya iliyotokea mapema usiku wa kuamkia leo.

Polisi wameeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni basi la abiria ambalo lilikuwa linatokea Busia mpani na nchi yaUganda lililokuwa likielekea jijini Nairobi kugongana ana kwa ana lori lililokuwa linatokea mjini Nakuru.

Mkuu wa kitengo cha trafiki katika eneo la Bonde la Ufa, Zero Arijme, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo amesema ilitokea saa tisa alfajiri katika barabara kuu ya kutoka Nakuru kwenda mjini Eldoret.

Kwa mujibu wa jeshi la Polisi nchini Kenya wamesema mwezi wa Desemba pekee, watu zaidi 100 wamepoteza maisha katika ajali za barabarani zilizotokea katika barabara kuu ya Nakuru kuelekea Eldoret hali ambayo inaashiria hatari kuwa katika eneo hilo ambalo limekuwa sugu kwa kutokea ajali za mara kwa mara.


Friday, 29 December 2017

Yanga yatua Mwanza Salama, kuivaa Mbao FC


Kikosi cha Yanga kimetua salama Mjini Mwanza tayari kwa pambano lake la Jumapili dhidi ya wenyeji Mbao FC, pambano la Ligi Kuu ambalo limepangwa kupigwa uwanja wa CCM Kirumba.

Kocha msaidizi wa timu hiyo Shadrack Nsajigwa amesema, timu imewasili salama na leo wanatarajia kufanya mazoezi kwenye uwanja wa Kirumba, pamoja na kesho kabla ya kujiandaa na mchezo huo ambao wameupa umuhimu mkubwa.

“Nashukuru tumewasili salama Mwanza, hali ya hewa ni nzuri na kufika mapema siku mbili kabla ya mchezo kutatusaidia kufanya vizuri kwenye mchezo wetu wa keshokutwa kwasababu tumedhamiria kushinda mchezo huo ukizingatia Mbao ni timu nzuri na imeuwa ikitusumbua sana,” amesema Nsajigwa.

Kocha huyo amesema ukitoa wachezaji Ibrahim Ajibu na Obrey Chirwa wachezaji wote waliobaki na kusafiri na timu hiyo niwazima na wapo katika ari kubwa ya kuhakikisha wanacheza na kuhakikisha wanapata pointi tatu.


Yanga inashika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, ikiwa na pointi 21, huku mahasimu wao Simba wakiwa ndiyo vinara wa ligi hiyo wakiwa na pointi 23 huku Azam FC wakishika nafasi ya pili wakiwa na pointi sawa na Simba.

VIDEO: Rais Magufuli amwagiwa sifa na Sheikh Kishki


Mhadhiri wa Kimataifa wa Kiislamu, Sheikh Nurdeen Kishki amemmwagia sifa Rais wa DK John Magufuli kutokana na uamuzi wake wa kupiga vita uvaaji wa nguo zisizo na maadili katika video za muziki nchini.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI..USISAHAU KUSUBSCRIBE




VIDEO: KAKOBE Aendelea Kupeta Mtaani



Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amefunguka na kusema kuwa jeshi la polisi mpaka sasa halijamkamata Askofu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zakaria Kakobe kama baadhi ya taarifa zinavyosamabazwa.

Kamanda Mambosasa amesema hayo leo wakati akiongea na waandishi wa habari na kusema kuwa bado hawajamtia nguvuni Askofu huyo na pindi watakapomkamata kwa makosa aliyotenda basi watatoa taarifa hizo.

"Baba Askofu Kakobe bado hatujamkamata pale atakapokuwa amekamatwa kwa makosa aliyotenda nitawaambia lakini kwa sasa hajakamatwa mchungaji huyo, jeshi la polisi huwa halipangi kumkamata mtu bali mtu anapofanya kosa la jinai ndipo anakamatwa hivyo na yeye kama amefanya kosa hili basi tutamkamata" alisisitiza Mambosasa

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE


Dk Mollel awaomba msamaha wanachama wa Chadema



Siha. Aliyekuwa mbunge wa Siha, Dk Godwin Mollel amewaomba msamaha wanachama wa Chadema kwa uamuzi wake wa kujivua ubunge na kujiunga na CCM.

Dk Mollel aliyetangaza uamuzi wa kujivua ubunge Desemba 14,2017 na kukabidhiwa kadi ya CCM Desemba 15,2017 amesema upepo wa kisiasa umebadilika na safari aliyoianzisha ni ya kusafisha upinzani kanda ya kaskazini.

Amesema hayo wakati wa kukabidhiwa kadi za CCM madiwani wawili waliojiuzulu nyadhifa zao na kuhama Chadema hivi karibuni, ambao ni wa Donyomurwak, Lwite Ndosi na wa Gararagua aliyekuwa pia mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Siha, Zakaria Lukumay.

Dk Mollel alisema jana Alhamisi Desemba 28,2017 kuwa amelitazama goli na ndiko alikokwenda ili kuweza kufunga.

“Natambua kuna watu walipoteza muda mwingi, walitumia fedha zao kunichangia na wengine walimwaga damu ili niweze kuwa mbunge lakini hivi majuzi nilijivua ubunge hatua ambayo iliwaumiza wengi. Niombe mnisamehe kwa kuwa nilishindwa kuwafuata siku ile nikihama kwa kuwa nilijua mngeweza kunipiga au kusababisha sintofahamu kubwa,” amesema Dk Mollel.

Amesema uamuzi wenye tija siku zote lazima ulete machungu.

Dk Mollel amesema ameingia kwenye vita kuhakikisha anayafikia malengo ya kuwaletea wananchi wa Siha maendeleo waliyoyatarajia kwa kipindi kirefu.

“Niwahakikishie wananchi wa Siha kwamba hamtajuta mimi kuhama chama, kwa kuwa niliisoma ramani yote ya Siha na kuelewa maendeleo yaliko, hivyo sijawaaibisha, niungeni mkono sasa na ninaahidi sitawaangusha,” amesema.

Pia, ametaka viongozi wa CCM kutambua kuwa wana kazi kubwa ya kuhakikisha walio nje ya chama hicho wanavutiwa na matendo ya chama na si kukatishwa tamaa.

Katibu wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Jonathan Mabihya amesema, “Kuna watu wanawatisha watu kuwa wakiondoka na kuja CCM hawatapata nafasi, tunawakaribisha kwa kuwa nafasi ziko wazi na wakihitaji kugombea watapata nafasi.”

Mabihya amesema CCM imeongeza idadi ya wapambanaji ambao wameamua wenyewe kuungana na timu ya maendeleo.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Patrick Boisafi amesema milango iko wazi kwa anayetaka kujiunga na chama hicho.

“Wanaorudi CCM wanarudi nyumbani, ninaomba Watanzania waelewe kuwa hakuna biashara ya binadamu na CCM hatuwezi kufanya biashara hiyo,” amesema.

Ndosi aliyekuwa diwani wa Donyomurwak ametaka maneno yanayoendelea kuhusu kuhama kwake Chadema yaishe, kwa kuwa haitaji mashindano ya maneno bali kufanya kazi ili kuyafikia maendeleo.


Ronaldo amtaka Philippe Coutinho kutojiunga na Barcelona



Aliyekuwa mshambuliaji hatari wa timu ya taifa ya Brazil na vilabu vikubwa vya Ulaya, Ronaldo Luís Nazário de Lima amemuonya kiungo wa Liverpool, Philippe Coutinho kuhusu kujiunga na Barcelona.

Coutinho ambaye amekuwa akiwindwa na vinara hao wa La Liga tangu msimu uliopita, ameambiwa na Ronaldo kuwa Barca ni timu ambayo imekuwa na matatizo makubwa na wachezaji wa kutoka nchini Brazil.

Nilijisikia furaha zaidi na zaidi nilipojiunga na Real Madrid, licha ya kuwa nilikuwa na mwaka mzuri huko Barcelona,” Ronaldo amesema hayo wakati akiongea na kituo cha runinga cha Esporte Interativo


Ronaldo de Lima

“Mwishoni, historia yangu na Barça ilikuwa mbaya sana, sawa na ile Neymar aliyokuwa nayo. Barcelona daima imekuwa na matatizo na wachezaji wa Brazil: Neymar, Romario, Ronaldinho na mimi. Sisi wote tulitendewa vibaya na klabu mwishoni licha ya michango yetu yote na kujitolea,” ameongeza.

De Lima aliichezea Barca kwa msimu mmoja wa mwaka 1996–1997 katika mechi 37 na alifanikiwa kufunga magoli 34 na baadaye alihamia Inter Milan ambapo alicheza kwa misimu mitano.



VIDEO: Diamond Platnumz Awakabidhi mashabiki zawadi ya Pikipiki


Msanii wa bongo fleva nchini Tanzania ambae amefanikiwa pia kuvuka boda kwa hatua kubwa Nasibu Abdul alimaarufu kama Diamond Platnumz amewapa mashabiki wake zawadi za pikipiki na zawadi nyingi ikiwemo chibu perfume na nyingine kibao.

Angalia Full Video Hapa na Usisahau ku Subscribe......



Thursday, 28 December 2017

Serikali yapiga hodi mgodi wa Geita



Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Luhumbi ameunda kamati maalumu ya kuchunguza wanaofuja fedha za wananchi, huku akiwaagiza mkuu wa wilaya hiyo Herman Kapufi, Mkurugenzi wa mji Modest Apolinary kuwasiliana na mgodi wa Geita (GGM) waharakishe kuikabidhi serikali ya mkoa huo majengo yaliyojengwa kwa ufadhili wa mgodi huo yaliyopo magogo ili yabadilishwe kuwa chuo kikubwa cha ufundi kwa lengo la kuwasaidia vijana na watoto katika mkoa wa Geita.

Amesema hayo wakati akizungumza na wananchi wa kata ya kalangalala katika shughuli ya uchimbaji misingi ya majengo ya shule ya secondary GEITA,na kwamba baada ya GGM kukabidhi majengo hayo,ndani ya mwezi mmoja watahakikisha wanakamilisha taratibu za kuwa chuo ili watoto wapate kujiunga hasa wale wanaotaka kusomea kozi mbalimbali zikiwemo computer ,makanika,ujenzi, kuchomelea vyuma na madini hakuna haja ya kuwatoa mkoani hapa kuwapeleka kusoma kwenye mikoa mingine.

Katika hatua nyingine baadhi ya wananchi wa kata ya Nyankumbu wamelalamikia baadhi ya viongozi kukwamisha shughuli za maendeleo na kumlazimu mkuu wa wilaya kuahidi kula nao sahani moja.


Manyara bado inasumbuliwa na uhaba wa Walimu



Waalimu na wanafunzi katika shule ya Umbur iliyopo wilayani Mbulu mkoa wa Manyara wanakabiliwa na changamoto kutembea umbali mrefu upatao kilomita 20 kufuata shule,ikiwemo kukosekana uwiano wa walimu na wanafunzi ambapo mwalimu mmoja anafundisha darasa moja lenye watoto zaidi ya 100.

Akizungumza kwa njia ya simu na kunukuliwa na channel ten Mkuu wa wilaya ya mbulu Chelestino Mofuga ameiambia kituo hiki kuwa sera ya elimu inaeleza juu ya uwiano wa wanafunzi wanaopaswa kufundishwa katika chumba kimoja cha darasa kuwa ni kati ya 45 kwa shule za sekondari na 35 kwa shule za msingi ambapo shule ya umbur hali hiyo ni mara tatu zaidi kwa mujibu wa waalimu shuleni hapa wameeleza kuwa wanakailiwa na upungufu wa vyumba vitatu vya madarasa pamoja na waalimu ambapo wanafundisha hadi wanafunzi zaidi ya mia moja.

Umburu shule ya msingi pia kwa sasa inakumbwa na wasi wasi juu ya umiliki wa eneo la shule kwakuwa shule hii haina hati miliki ya ardhi ya eneo iliyopo shule hii.

Watoto hawa licho ya umri wao hutembea kilomita zaidi ya 20 kufuata huduma itakayowapa mwanga kwenye maisha yao jambo linalowaacha wazazi katika maswali mengi wakijiuliza uwezekano wa watoto wao kufanya vizuri katika masomo.

Uzinduzi wa madarasa mawili kwenye shule hii inayofanywa na halmashauri kupitia mkurugenzi wa mbulu vijijini inaongeza idaidi ya vyumba vya madarasa na kufikia vinne lakini haimalizi tatizo uhitaji wa vyumba zaidi vya madarasa kutokana na watoto kutoka wilaya ya karatu mkoa wa arusha pamoja na wilaya ya mbulu mkaoni Manyara kuendelea kuongezeka zaidi.

Benki Kuu yaipa Serikali Bilioni 300


Benki Kuu ya Tanzania imetoa gawio la Shilingi Bilioni 300 kwa Serikali kutokana na faida iliyopatikana kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017.

Taarifa iliyotolewa na Benki Kuu imesema kwamba gawio hilo kutoka benki kuu kwenda kwa Serkali linafikisha jumla ya Bil 780  kwa kipindi cha miaka mitatu (2014/2015- 2016-2017)

Hata hivyo taarifa hiyo imewekwa wazi kwamba majukumu ya msingi ya Benki Kuu siyo kutengeneza faida na inapotokea faida imepatikana , sehemu kubwa hutolewa kama gawio kwa serikali.



Harmorapa amuomba msamaha Master Jay


Msanii wa muziki wa bongo fleva Harmorapa amefunguka na kumuomba radhi mtayarishaji mkongwe wa muziki wa bongo fleva na mmiliki wa studio za Mj Records, Master J na kusema kuwa amegundua kuwa alimkosea mkongwe huyo kwenye muziki.

Harmorapa alifunguka hayo alipohojiwa kwenye kipindi cha eNewz cha EATV na kusema katika mwaka 2017 amemkosea sana Master J kufuatia kauli yake aliyoitoa kipindi cha nyuma kupitia kipindi hicho kuwa hamjui wala hamtambua mtayarishaji huyo mkongwe wa bongo fleva.

"Nimegundua kuwa nilifanya makosa sana, unajua kipindi kile nasema vile nilikuwa bado sijamjua vizuri Master J hivyo naomba anisamehe tu kwani ulikuwa ugeni katika tasnia hivyo nilikuwa sijamjua vizuri" alisikika Harmorapa.

Harmorapa alishawahi kumkana mtayarishaji huyo kuwa hamfahamu baada ya Master J kunukuliwa akisema kuwa msanii huyo hana kipaji cha muziki na kuimba labda kama atakwenda kufanya vichekesho, jambo ambalo lilionesha kumkwaza Harmorapa.