Thursday, 28 December 2017

Kiwanda cha Alizeti chafungwa Singida


Serikali imekifungia Kiwanda cha kukamua mafuta cha  Alizeti Mount  Meru Millers Ltd kwa  muda usiojulikana kwa madai ya kukaidi agizo la kulipa faini ya Sh20milioni.

Uamuzi wa kukifunga kiwanda hicho umetolewa jana Jumatano na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira ,Kangi Lugola  alipokuwa kwenye kwanda hicho kilichopo  kijiji cha Manguanjuki Manispaa ya Singida.

Kabla ya kutoa uamuzi huo  mbele ya kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Singida, Lugola alisema Novemba 29 mwaka jana, mtangulizi wake Luhaga  Mpina, aliuagiza uongozi wa  kiwanda hicho ulipe  faini ya Sh20milioni kwa kosa la kutiririsha  maji taka yenye kemikali kwenye makazi ya watu .

“Maji taka yameelekezwa kwenye makazi ya wananchi wanaokizunguka kiwanda .Pia maji  hayo yenye kemikali, yameelekezwa kwenye ziwa la Singidani lenye viumbe hai wakiwemo samaki. lakini hadi leo, agizo la Waziri  Mpina, halijatekelezwa’’ amesema Lugola na kuongeza kwamba

‘’Kutokana na  ukiukwaji wa  sheria za mazingira, Mpina alikipa adhabu ya kulipa faini  Sh20milioni ambayo haijalipwa hadi leo”, amesema Waziri Lugola kwa masikitiko.

Lugola amesema kwamba  kiwanda hicho kimetekeleza agizo la kununua mashine ya kutibu maji taka, lakini maji taka hayo, hayajaelekezwa kwenye mashine hiyo.

 “Maji hayo yenye kemikali bado yameendelea kuwa kero kwa wananchi hadi leo, na yanaathiri viumbe hai vilivyopo kwenye ziwa Singidani. Hii dharau kwa serikali haikubaliki”, amesema

Naibu waziri huyo, amesema  wananchi wanaozunguka kiwanda hicho wamekuwa wakitoa kilio chao serikalini kwa miaka minne, kwamba wanaathiriwa na maji yenye kemikali  na moshi mnene wa kiwanda cha Maount Meru.

“Binafsi leo nimefika kwenye kiwanda hiki na baada ya kufanya ukaguzi wa kina, nakiri kwamba kilio cha wananchi wa Manguanjuki ni cha kweli na kinahitaji tiba ya kudumu. Mkuu wa wilaya ya Singida, naagiza kuanzia sasa, usimamie kufungwa kwa kiwanda hiki”,amesema na kuongeza;

“OCD pia nakuagiza uwatafute Wakurugenzi wa kiwanda hiki Atul Nittal, Arvind Mittal na Tarsem Aggarwal, popote walipo na kuwakamata na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria kwa kukaidi agizo la Serikali”.

Kwa upande wake meneja Uhusiano, Nelson Mwakambuta, amesema kiwanda hicho kimekuwa kikifanyiwa ukaguzi mara kwa mara na mamlaka mbalimbali. Lakini  wamekuwa wakiwaambiwa na viongozi hao kuwa   kiwanda hicho, hakina tatizo lolote linalohusiana na kwenda kinyume na sheria za  mazingira.

“Kufungwa kwa muda usiojulikana kwa kiwanda hiki, kutaathiri ustawi wa watumishi wengi wa kiwanda na familia zao. Pia  wakulima wa zao la alizeti ndani na nje ya mkoa wa Singida, nao watakuwa wamepata pigo. Hatupingani na serikali tutatekeleza yale yote tuliyoagizwa”,amesema meneja huyo.



Orodha ya wachezaji wanaolipwa mkwanja mrefu EPL



Ligi Kuu ya Uingereza ni miongoni mwa Ligi Kubwa Ulaya lakini ni miongoni pia mwa Ligi za Ulaya zenye mashabiki wengi ukanda wa Afrika husani Afrika Mashariki, inawezekana kuna mambo mengi ambayo huyafahamu katika Ligi Kuu England.

Hii hapa chini ni orodha ya mastaa wa Soka kwenye Ligi hiyo wanaolipwa mkwanja mrefu zaidi kwa wiki.

1- Paul Pogba analipwa pound 290000/Tsh 872,087,739 (ManUnited)

2- Romelu Lukaku pound 250000/Tsh 752,068,375 (ManUnited)

3- Sergio Aguero pound 220000/Tsh 661,820,170 (ManCity)

= Yaya Toure pound 220000/Tsh 661,820,170 (ManCity)

= Zlatan Ibrahimovic pound 220000/Tsh 661,820,170 (ManUnited)

6-Kevin De Bruyne pound 200000/Tsh 601,609,900 (Man City)

= David De Gea pound 200000/Tsh 601,609,900 (ManUnited)

= Eden Hazard pound 200000/Tsh 601,609,900 (Chelsea)

9-Virgil van Djik pound 180000/Tsh 541,448,910 (Liverpool)

= Philippe Coutinho pound 180000/Tsh 54,1448,910 (Liverpool)


Familia yafukua kaburi la Baba yao




Familia ya watoto wanne wakiongozwa na mama yao mzazi Julieta Majaliwa wamelazimika kufukua kaburi la baba yao Stanford Gombo, wakidai kuwa na mashaka na sababu ya kifo cha baba yao.

Tukio hilo limetokea huko katika cha kijiji cha Kilimani wilayani Gairo mkoani Morogoro ikiwa ni utekelezaji wa amri ya Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani humo baada ya familia hiyo kutaka mwili huo kufanyiwa uchunguzi.

Wanafamilia hao walifika kijijini hapo wakiwa na ulinzi wa polisi kwa ajili ya kusimamia utekelezaji wa amri ya mahakama inayoelekeza kufukuliwa kwa kaburi hilo, ili watoto wapate nafasi ya kuhakiki mwili uliozikwa kama ni wa baba yao pamoja na kufanyiwa uchunguzi kubaini sababu zilizopelekea kifo chake.

Kwa upande wake Mke wa marehemu ,Bi. Julieta Majaliwa amesema mara ya mwisho kuwasiliana na mumewe walikua  nyumbani kwao jijini Dar es salaam ambapo alimuaga anaenda kijiji kwao kuwajulia hali lakini tangu alivyo ondoka hawa kuwa na mawasiliano hadi kifo chake.

Chifu ashambuliwa kwa kupiga vita pombe haramu



Chifu wa eneo la Elburgon, Kaunti ya Nakuru nchini Kenya alijikuta akishambuliwa na kundi la vijana wenye hasira alipoongoza msako dhidi ya pombe haramu.

Chifu huyo anayejulikana kwa jina la Francis Ngacha, alikuwa ameongozana na wanachama wa kundi la nyumba kumi aliposhambuliwa na vijana hao, wakimlaumu kwa kuwaharibia sherehe zao za Krismasi.

“Nilikuwa nimeongoza kikundi hicho kufanya msako dhidi ya vijiwe vya kuuza pombe haramu katika eneo hilo, na ndipo kundi la vijana zaidi ya 10 lilipoanza kuturushia mawe,” amesema Bw. Ngacha.

Kwa upande mwengine Naibu Kamishna wa Kaunti hiyo Bw. Naftaly Korir, alituma kikosi cha polisi kufanya msako huo, lakini hawakufanikiwa kuwakamata vijana waliomshambulia chifu, kwani walitoroka eneo hilo.

Polisi wamesema wanawatafuta vijana hao waliohusika kumshambulia chifu, ili wachukuliwe hatua za kisheria.



Audio | Joh Makini – Mipaka | Mp3 Download

Audio | Joh Makini – Mipaka | Mp3 Download


Audio | Joh Makini – Mipaka | Mp3 Download

DOWNLOAD

Video | Nancy Hebron ft Vanessa Mdee, Mimi Mars – Beautiful Jesus | Mp4 Download

Video | Nancy Hebron ft Vanessa Mdee, Mimi Mars – Beautiful Jesus | Mp4 Download


Video | Nancy Hebron ft Vanessa Mdee, Mimi Mars – Beautiful Jesus | Mp4 Download


Video | Joh Makini – Mipaka.| Mp4 Download

Video | Joh Makini – Mipaka.| Mp4 Download

Video | Joh Makini – Mipaka.| Mp4 Download

DOWNLOAD

Video | Samir – Zuzu.| Mp4 Download

Video | Samir – Zuzu.| Mp4 Download

Video | Samir – Zuzu.| Mp4 Download

DOWNLOAD


Audio | Mercy Masika – Upendo | Mp3 Download

Audio | Mercy Masika – Upendo | Mp3 Download



Audio | Mercy Masika – Upendo | Mp3 Download

DOWNLOAD

Audio | Saida Karoli – Kabaka | Mp3 Download

Audio | Saida Karoli – Kabaka | Mp3 Download

Audio | Saida Karoli – Kabaka | Mp3 Download

DOWNLOAD

Audio | Orbit – 1000 -100,000 “Buku kuwa Laki | Mp3 Download

Audio | Orbit – 1000 -100,000 “Buku kuwa Laki | Mp3 Download

Audio | Orbit – 1000 -100,000 “Buku kuwa Laki | Mp3 Download


DOWNLOAD

Audio | Chemical – Struggle | Mp3 Download

Audio | Chemical – Struggle | Mp3 Download

Audio | Chemical – Struggle | Mp3 Download

DOWNLOAD

Audio | B2k – Tunaendana | Mp3 Download

Audio | B2k – Tunaendana | Mp3 Download

Audio | B2k – Tunaendana | Mp3 Download

DOWNLOAD