Thursday, 28 December 2017

Video | Samir – Zuzu.| Mp4 Download

Video | Samir – Zuzu.| Mp4 Download

Video | Samir – Zuzu.| Mp4 Download

DOWNLOAD


Audio | Mercy Masika – Upendo | Mp3 Download

Audio | Mercy Masika – Upendo | Mp3 Download



Audio | Mercy Masika – Upendo | Mp3 Download

DOWNLOAD

Audio | Saida Karoli – Kabaka | Mp3 Download

Audio | Saida Karoli – Kabaka | Mp3 Download

Audio | Saida Karoli – Kabaka | Mp3 Download

DOWNLOAD

Audio | Orbit – 1000 -100,000 “Buku kuwa Laki | Mp3 Download

Audio | Orbit – 1000 -100,000 “Buku kuwa Laki | Mp3 Download

Audio | Orbit – 1000 -100,000 “Buku kuwa Laki | Mp3 Download


DOWNLOAD

Audio | Chemical – Struggle | Mp3 Download

Audio | Chemical – Struggle | Mp3 Download

Audio | Chemical – Struggle | Mp3 Download

DOWNLOAD

Audio | B2k – Tunaendana | Mp3 Download

Audio | B2k – Tunaendana | Mp3 Download

Audio | B2k – Tunaendana | Mp3 Download

DOWNLOAD

Video | Tiwa Savage – SugarCane | Mp4 Download

Video | Tiwa Savage – SugarCane | Mp4 Download

Video | Tiwa Savage – SugarCane | Mp4 Download


DOWNLOAD

Guardiola afunguka asema Barcelona yapewa jeuri na Messi


Kocha wa Manchester City Pep Guardiola amesema Lionel Messi ndio mtu anayeifanya Barcelona iwe timu yenye nafasi kubwa ya kutwaa Ligi ya mabingwa Ulaya msimu huu.

Guardiola ameyasema hayo alipokuwa akijibu swali kutoka kwa mwandishi wa habari ambaye alimuuliza kuhusu timu yake ya Man City kama ina nafasi kubwa ya kushinda ubingwa wa Ulaya msimu huu.

Pep alimjibu mwandishi kwa kumuuliza swali kuwa, “Ni timu gani anachezea Lionel Messi”, ? Baada ya mwandishi kujibu kuwa ni Barcelona ndipo Guardiola akamwambia kuwa ndio timu yenye nafasi ya kutwaa UEFA.

Guardiola alifafanua kuwa aina ya uchezaji wa Barcelona kwa sasa ni hatari zaidi kwani wanaanza kumiliki mpira kwenye eneo la ushambuliaji kwa kumtumia zaidi Messi.

“Hakuna asiyejua ubora wa Messi, na kama Barcelona inamtumia kwenye eneo la adui unategemea nini kama sio kukumaliza tu mpinzani”, ameeleza Guardiol



Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB atangaza kujiuzulu


MTENDAJI Mkuu wa CRDB Bank, Dr Charles Kimeo, leo ametangaza kustaaafu ifikapo Mei 2019. Dkt. Kimei aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kwamba hatua hiyo ni kwa ajili ya kuanzisha mchakato wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo kupata mtu atakayeshika nafasi yake kwa mujibu wa taratibu na kanuni zilizopo.

Kabla ya kujiunga na benki hiyo, Dk Kimei alifanya kazi Benki Kuu ya Tanzania kama Mkurugenzi Mfawidhi wa Shughuli za Benki, Mkurugenzi wa Sera, Uchumi na Utafiti, Meneja wa Idara ya Utafiti wa Uchumi na Sera na nyadhifa nyingine mbalimbali katika Idara ya Utafiti. Hivi sasa ni Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki Mabenki nchini.

Amewahi pia kufanya kazi katika bodi mbalimbali ikiwemo ya Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Mamlaka ya Elimu nchini, Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kampuni ya Huduma za Mikopo Midogo ya CRDB na tawi la CRDB nchini Burundi.

Dkt. Kimei ana Shahada ya Uzamivu katika Uchumi aliyoipata Chuo Kikuu cha Uppsala cha Sweden, Shahada ya Uzamili katika Uchumi aliyoipata Chuo cha Uchumi cha Stockholm na Shahada ya Sayansi (Uchumi) aliyoipata Chuo Kikuu cha Taifa cha Moscow.


Baada ya kuwashuku wachezaji kuiba blanketi, shirika la Ndege lawaomba radhi


Shirika la American Airlines limewaomba msamaha wachezaji wawili wa mpira wa kikapu ambao walifukuzwa kutoka kwa ndege kwa kuwashuku kuiba.

Marquis Teague na Trahson Burrell waliabiri ndege hiyo siku moja kabla ya krismasi wakielekea kucheza mechi.

Lakini kabla ya ndeye kuondoka uwanjani, mhudumu mmoja wa ndege alidai kuwa wanaume hao walikuwa mablanketi kutoka upande wa kifahari wa ndege ambapo walilazimishwa kushuka kutoka kwe ndege hiyo.

Baadaye ilibainika kuwa ni abiria walikuwa wamewapa mablanketi hayo.

Wachezaji hao wote walikuwa wa asilia ya Afrika akiwemo mhudumu wa ndege.

Hakuna mchezaji kati ya hao wanaochezea timu ya Memphis Hustle amezungumzia kisa hicho.

Laiki naibu kocha wa Hustle, Darnell Lazere aliandika katika twitter kuwa kitendo hicho kilichochewa na ubaguzi wa rangi.

Wachezaji walikuwa wakisafiri kutoka uwanja wa Dallas-Fort Worth kwenda Sioux Falls, South Dakota wakitumia ndege ya Envoy Air iliyo sehemu ya American Airlines.




Nikki wa Pili atupa dongo hili



 Msanii Nikki wa Pili ambaye ni miongoni mwa wasanii wachache wanaofanya uchambuzi wa masuala mbali mbali ikiwemo uchumi wa taifa, ametupa jiwe gizani kuhusu sera mpya ya viwanda.

Kupitia ukurasa wake wa twitter Nikki wa Pili ameandika ujumbe kuhusu sera mpya ya Tanzania ya viwanda inayotekelezwa na serikali ya awamu ya tano, na kusema kwamba ni vyema tukajitafakari kwa hili kwani nchi ambazo zimefanikiwa, zilitumia mfumo wa ruzuku na sio wawekezaji pekee.

"Kupitia ruzuku ya serikali, na ulinzi dhidi ya ushindani wa kisoko kwa miaka 40 ndipo Japan wakafanikiwa kuisimamisha secta ya viwanda vya magari, sasa tunao hubiri Tanzania ya viwanda kupitia wawekezaji na ushindani wa kisoko tujitafakari",ameandika Niki wa Pili.

Sasa hivi Tanzania inapambana kuleta mapinduzi ya viwanda ili nchi iweze kuzalisha vitu vingi yenyewe bila kuagiza nje, huku ikitoa fursa kwa wawekezaji mbali mbali kuja nchini kuwekeza kwenye sekta ya viwanda.




Lissu huenda akakaa hospitali miezi sita zaidi


Dar es Salaam. Siku moja baada ya mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kusimama kwa mara ya kwanza tangu Septemba 7, amesema huenda akakaa hospitalini kwa miezi sita zaidi.

Juzi, Lissu anayepata matibabu katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya alisimama kwa msaada wa madaktari.

Akijibu swali ni lini atarejea nchini na kama atasafiri nje ya Afrika kwa matibabu zaidi aliloulizwa jana na mwandishi wetu, Lissu alisema, “Ndio kwanza nimesimama jana (juzi), kuna miezi sita ya ‘rehabilitation’ (kumrudisha katika hali ya kawaida). Madaktari waliniambia kuna miezi sita au tisa.”

“Kwanza nimesimama kwa mara ya kwanza uamuzi wa je, nitamalizia hapa au nitakwenda bado, itategemea ushauri wa madaktari na kisha majadiliano na familia kwa sasa bado sijajua.”

Tangu mwanasheria huyo mkuu wa Chadema aliposhambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi akiwa katika makazi yake Area D mjini Dodoma Septemba 7, hakuwahi kusimama na wakati wote alikuwa akionekana amelala au amekaa hadi juzi.

Katika picha iliyomwonyesha Lissu akiwa amesimama, madaktari wawili walimshika huku mmoja akiurekebisha mguu wake wa kulia.

Lissu alituma ujumbe kwa wapigakura wa Singida Kaskazini akisema; “Wajiandae kwa mapambano makubwa ya kisiasa… kila mmoja atimize wajibu wake na kuacha visingizio.”

Akizungumzia hatua ya Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS) kusimama, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema, “Ni jambo la kumshukuru Mungu, tulikuwa tunapigania mwenzetu asimame, tunamshukuru Mungu kwa hatua hii.

“Itachukua muda kidogo ili aweze kurejea katika hali yake, lakini tumshukuru sana Mungu kwa kutupa Lissu, lakini tuwashukuru sana madaktari waliomuuguza na hili ni funzo kwetu,” alisema.

Alipoulizwa iwapo wanamkumbuka Lissu katika harakati zake, Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni alisema, “Kila kiongozi ana wajibu wake wa kiharakati, uongozi si shule unakwenda kujifunza, kila mmoja ana vipawa vyake, wengine ni wazuri katika kuhoji, wengine katika mikutano ya hadhara, wengine mikakati na kila mmoja ana wajibu wake.

“Lissu ni moja ya wanasiasa makini na mahiri hasa linapokuja suala la kuhoji, amekuwa msaada mkubwa katika kambi ya upinzani bungeni na zaidi katika masuala ya sheria na Mahakama, kila mmoja anajua hivyo, kwa hiyo ni kweli tunaposema ‘tumemmisi’ ni kweli tumemmisi sana,” alisema.

Mbowe alisema, “Tunawashukuru Watanzania walio wengi walioshiriki kumuuguza Lissu, kumwombea, kutoa michango na salamu zao hadi amefikia hatua ile ambayo wengi hawakutegemea.Tunawashukuru viongozi wa dini na watu waliomwombea kamanda wetu aweze kupona.”



Sakata la Airtel, Wafanyakazi TTCL wajitosa


Chama cha Wafanyakazi wa Sekta ya Huduma za Mtandao wa Mawasiliano Tanzania (Tewuta) kimepongeza hatua ya Rais John Magufuli kumtaka Waziri wa Fedha kuanza uchunguzi kubaini ukweli kuhusu ubinafsishwaji wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL).

Katibu Mkuu wa Tewuta, Junus Ndaro amesema chama hicho kinatambua fika kuwepo mchezo mchafu uliosababishwa na Watanzania wachache wenye uchu wa fedha wakisaidiana na wawekezaji kupora rasilimali hiyo ya Taifa.

Ndaro amesema leo Alhamisi Desemba 28,2017 kuwa, kwa muda mrefu chama hicho kimekuwa kikitoa malalamiko kuhusu ufisadi huo serikalini lakini hakikusikilizwa.

“Tunampongeza Rais Magufuli kwa kuthubutu kutamka pasipo shaka kuwa taarifa alizonazo zinaonyesha kampuni ya Airtel ni mali ya TTCL, jambo hili tulilipigia kelele kwa muda mrefu,” amesema.

Ndaro amesema mara zote hawakusita kutamka kuwa Celtel ambayo sasa ni Airtel ni mali ya TTCL iliyoporwa pasipo kulipwa chochote.

“Wafanyakazi tunatambua kuwa TTCL haikuporwa Celtel pekee bali ilinyang’anywa pia Chuo cha Posta na Simu hali iliyosababisha tukose mahali pa kupata mafunzo,” amesema Ndaro.

Kutokana na kuanza uchunguzi wa sakata hilo, Ndaro amesema viongozi wa Tewuta wako tayari kutoa kila aina ya ushirikiano kuhakikisha Serikali inashinda na kuirudisha Airtel mikononi mwa TTCL.

JPM aagiza TCRA kuzifuta kampuni za simu zitakazoshindwa kujiunga na soko la hisa

“Tuna ushahidi wa kutosha na tuko tayari kutoa ushirikiano kwa Serikali katika hatua zote kuleta haki iliyopotea ya Kampuni ya Simu Tanzania,” amesema.