Friday, 22 December 2017

Tanzania yapolomoka katika viwango vya FIFA



TANZANIA imezidi kuporomoka katika viwango vya soka vinavyotolewa kila mwezi na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) ambapo hivi sasa inashika nafasi ya 147 kutoka 142 ya mwezi Oktoba.
Jana Alhamisi, Fifa ilitoa viwango hivyo ambapo inaonyesha ndani ya miezi mitano kuanzia Julai, mwaka huu, Tanzania imeshuka kwa jumla ya nafasi 33.
Ikumbukwe kuwa, kwa siku za hivi karibuni, Tanzania ilifanya vizuri kwenye viwango vya Juni baada ya kushika nafasi ya 114 kutoka nafasi ya 139 ya mwezi Mei. Baada ya hapo, Julai ikashika nafasi ya 120, Agosti 125, Septemba 136, Oktoba 142 na sasa Novemba ni 147.
Kushuka huko kwa Tanzania kunatokana na Novemba, mwaka huu, Taifa Stars kutoka sare ya bao 1-1 na Benin katika mchezo wa kirafiki uliopigwa kwenye Uwanja wa l’Amitie, Benin.
Katika 10 Bora ya duniani, Ujerumani inaongoza ikifuatiwa na Brazil, Ureno, Argentina, Ubelgiji, Hispania, Poland, Uswisi, Ufaransa na Chile.

Waziri Kigwangalla kuwakutanisha Joketi Na Wema Sepetu





Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk.Hamisi Kigwangalla jana Desemba 21, 2017 aliteua majina mengine ya Kamati ya Kitaifa ya kuandaa mwezi maalum wa maadhimisho ya Urithi wa Tanzania. Miongoni mwa wajumbe walioteuliwa ni makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jokate Mwegelo na Wema Sepetu ambao wataungana na wajumbe 23 aliowateua awali kuunda Kamati ya Kitaifa ya Kuandaa Mwezi Maalumu wa Maadhimisho ya Urithi wa Tanzania.

Mashindano Ya Miss Tanzania kutokuwepo 2017



WAANDAAJI wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania, Kampuni ya Lino International Agency Limited, wamesema kwamba hakutakuwa na Fainali za Taifa za shindano la Miss Tanzania kwa mwaka 2017.
Katika taarifa iliyotolewa na kampuni hiyo leo imeeleza kuwa sababu kubwa ya kuahirishwa kwa shindano hilo ni ukosefu wa Wadhamini ambao kwa njia moja au nyingine huwezesha kufanyika kwa mashindano hayo kwa kulipa gharama mbalimbali ikiwemo zawadi za washiriki.
Aidha waandaaji hao pia wamesema kuwa kuchelewa kupata kibali cha kuanza mchakato wa Miss Tanzania 2017, ambacho kilitolewa na BASATA mwezi Septemba mwaka huu pia kimechangia kukosa kwasababu muda ulikuwa umeshaenda.
Mashindano ya kutafuta warembo wa Miss Tanzania yamekuwa yakifanyika kila mwaka na baadae kuibua mastaa mbalimbali kama Wema Sepetu, Lulu Diva, Jokate Mwegelo na wengine 

Thursday, 21 December 2017

Orodha ya mastaa BONGO waliopata watoto mwaka huu 2017




Mwanamitindo wa kimataifa, Hamisa Mobeto
MWAKA 2017 ndiyo huo unayoyoma na zimebaki siku kumi tu kuingia mwaka 2018. Mwaka 2007, mengi yametokea kwa kila mtu katika maisha yake ya kawaida.
Wapo waliofanikiwa, waliofeli na wapendwa wetu wengine walitutoka kabisa. Kama ilivyo kwenye maisha ya kawaida kuwa na mengi yaliyotokea, vivyo hivyo kwenye ulimwengu wa burudani. Ukiachana na kiki zilizotikisa, matukio ya kuvutia na mengine mengi mazuri na mabaya tumeyashuhudia kwa staa mmojammoja.Miongoni mwa hayo mazuri ni kwa baadhi ya mastaa wa kike ambao walihabatika kuitwa mama kama ifuatavyo;
Muigizaji Faiza Ally akiwa na mtoto wake Lil Junior
MAMA KAIRO (HAPPINESS MILLEN MAGESE):
Mwishoni mwa Julai, mwaka huu, baada ya kutafuta mtoto kwa muda mrefu, mwanamitindo maarufu wa kimataifa, Happiness Millen Magese ‘Ladiva Millen’ alijibiwa kilio chake na Mungu wake.
Millen alijaliwa mtoto wa kiume aliyempa jina la Prince Kairo Michael Magese. Kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Instagram, Millen alionesha furaha yake kwa kuandika ujumbe matata ambapo pia alifafanua jina la mtoto wake huyo la Kairo kwamba, linamaanisha ‘utukufu kwa Mungu.’
MAMA JADEN (CHUCHU HANS):
Uhusiano wake na muigizaji Vincent Kigosi ‘Ray’ ulianza kama siri. Ghafla, muigizaji Chuchu Hans ni mjamzito. Baadaye mambo yalikuwa wazi hasa Mwezi Januari, Chuchu alipojifungua mtoto wa kiume ambaye yeye na mpenzi wake, Ray walimpa jina la Jaden.
MAMA GOLD (AIKA):
Baada ya kudumu kwenye uhusiano kwa zaidi ya miaka nane, Aika na mpenzi wake, Nahreel, mwanzoni mwa Mwezi Desemba walibahatika kupata mtoto wa kiume ambaye
walimpa jina la Gold.
MAMA PRINCE ABDUL (HAMISA MOBETO);
Mwanamitindo wa kimataifa, Hamisa Mobeto naye anaingia kwenye orodha hii baada ya Mwezi Agosti, mwaka huu kupata mtoto wa kiume aliyempa jina la Prince Abdul. Kwa Hamisa, huyu ni mtoto wa pili kufuatia awali kupata mtoto wa kike aitwaye Fantas.
MAMA CLARIBELL (ESHA BUHETI);
Wakati ikiwa imepita siku moja tu baada ya mwanamitindo Hamisa Mobeto kupata mtoto wa kiume, muigizaji Esha Buheti naye alibahatika kupata mtoto
wa kike ambaye alimpa jina la Claribell. Kama ilivyo kwa Hamisa, kwa Esha pia huyo naye ni mtoto wake wa pili. Mtoto wa kwanza anaitwa Clarisa.
MAMA LIL JUNIOR (FAIZA ALLY);
Muigizaji Faiza Ally naye yumo kwenye orodha hii. Mwaka 2017, kwake umekuwa na mafanikio mengi ikiwemo kupata mtoto wa kiume ambaye amemuita Lil Junior. Naye ni mtoto wake wa pili baada ya Sasha aliyezaa na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’. Wengine waliopata watoto kwa mwaka 2017 ni pamoja na staa wa Bongo Fleva, Estarlina Sanga ‘Linah’ Khadija Nito na muigizaji Welu Sengo.

Shilole afunguka kuhusu ndoa yake



STAA wa miondoko ya mduara, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ amefunguka kuwa, watu wasimfikirie ameamua kuingia kwenye ndoa kama maonyesho bali amedhamiria kwenda kuwa mke anayestahili kuwa mfano wa kuigwa.
Mrembo huyo anayesumbua na wimbo wa Hatutoi Kiki, alisema kuwa anajua wazi watu wengi wanamuhesabia siku za uhusiano wao kuvunjika kama ilivyo kwa mastaa wengine, lakini kwa jinsi alivyodhamiria kutulia kwenye ndoa atawashangaza walimwengu.
“Najua wazi watu watakuwa wananihesabia siku ndani ya ndoa yangu lakini ukweli ni kwamba nitawashangaza watu wengi na sina sababu ya kuacha kuwa mke bora na mwenye heshima kwa
mume,” alisema

Ben Pol awataka wasanii Wa bongo kuacha uvivu



Msanii wa kiume wa bongo fleva Ben Pol, amewataka wasanii wenzake kuacha uvivu na kufanya kazi kwa bidii, kwani licha ya sanaa kuwahitaji, pia wana majukumu ya kutimiza.
Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Ben Pol amesema wao kama wasanii wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii, kwani kuna watu wanawategemea, ikiwemo familia zao na mashabiki wao.
“Niwaambie wasanii wenzangu tuache uvivu hii ni kazi yetu, familia zinatutegemea, tuna-teams ambazo zinaishi kupitia sisi, tuna mashabiki wanatuangalia, turudi studio turudi studio tutoe albam, kama kuna changamoto tutakabiliana nazo mbele kwa mbele”, amesema Ben Pol.
Ben Pol hakuishia hapo aliendelea kwa kuitaka serikali kuhakikisha wanasimamia ipasavyo kazi zao za sanaa, kwani na wao tayari wameshaanza kuchangia pato la serikali kwa kukatwa kodi.
“Tushaanza kulipwa kodi, kwenye shows tunakatwa, mtu anakuja pale mlangoni na mashine, kwa hiyo na wao serikali watusaidie kwenye biashara yetu”, amesema Ben Pol.
Ifahamike kwamba Ben Pol ni miongoni mwa wasanii wachache ambao mwaka huu wameachia albam, kitendo ambacho wasanii wengi wanakiogopa.

Wednesday, 20 December 2017

Diwani CHADEMA Ajiuzulu na Kujiunga CCM



KILIMANJARO: Diwani wa Donyomurwak kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilayani Siha mkoani Kilimanjaro, Lwite Ndossi amejiuzulu nafasi yake na kujivua uanachama wake katika chama hicho na kijiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole amethibitisha hilo na kusema kuwa wamempokea diwani huyo ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Chama Cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) kimeendelea kupoteza baadhi ya viongozi wake katika ngazi mbalimbali ambao wamekuwa wakijiuzulu nafasi zao na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kile wanachosema wanaunga mkono juhudi za Rais John Pombe Magufuli na Serikali yake.

Kamati Ya Ushauri Wa Mazingira Yazindiliwa



Serikali imezindua kamati ya Taifa ya ushauri wa mazingira ambayo itakuwa ikijihusisha na uchunguzi wa masuala yanayohusu kulinda mazingira na kupendekeza hatua za kuchukua.
Akizungumza jana katika uzinduzi huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba alisema kamati hiyo inayoundwa na wataalamu kutoka sekta mbalimbali ina mchango wa kutatua changamoto za mazingira bila kuwa na misigano. “Yote hayo ni kumjengea uwezo waziri mwenye dhamana ya mazingira ili katika kutekeleza majukumu yake awe na imput za kitaalamu,” alisema.
Katibu mkuu wa wizara hiyo, Joseph Malongo alisema kamati hiyo imeanzishwa kwa mujibu wa sheria na kwamba wananchi wanapaswa kujua na kuzingatia umuhimu wa mazingira katika kila jambo.

Vyama Vya Upinzani Vyamkosoa Mzee Makamba



Baadhi ya vyama vya upinzani vimekosoa kauli iliyotolewa juzi na aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba vikisema imelenga kudhoofisha upinzani nchini.
Juzi, akihutubia Mkutano wa Mkuu wa CCM, Makamba alisema Rais mstaafu Jakaya Kikwete alikuwa ‘anabatiza’ kwa maji, lakini Rais John Magufuli anafanya hivyo kwa moto na mfano mzuri ni uchaguzi wa marudio wa kata 43 ambao CCM ilizoa viti 42.
“Huu si ubatizo wa moto? Kazi tunayoifanya leo ni kuchagua kocha ambaye ni wewe (Rais Magufuli), kocha msaidizi Mangula (Philip) na Dk Shein (Ali Mohamed). Kama haitoshi unatakiwa uchague dawati la ufundi Kamati Kuu, sasa wenzangu wajue nimlisikia rafiki mmoja alikwenda kwa jimbo la Mnyika (John) na kusema 2020 njia nyeupe,” alisema mwanasiasa huyo.
“Njia nyeupe kwa utaratibu huu, kwa matokeo haya na ubatizo huu wa moto 2020 mshindi ni CCM we’ lala. Naomba mniruhusu niwaambie kina Mrema (Lyatonga), ubatizo ni uleule na leo sitaki kutabiri.Natabiri 2020 mheshimiwa Lowassa (Edward), Mbowe (Freeman) na Mapesa (John Cheyo ), John Shibuda wajue njia si nyepesi.”
Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano, Uenezi na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema alisema hakutarajia kama Makamba angetoa kauli hiyo kutokana na alichodai kuwa ni kuminywa kwa demokrasia nchini.
Alisema kinachofanyika sasa dhidi ya wapinzani ni sawa na refa anayechezesha mpira wa miguu kuwapa kadi nyekundu wachezaji wote wa timu husika, halafu timu nyingine inaendelea kucheza.
Naibu Katibu wa CUF (Bara), Magdalena Sakaya alisema kauli hiyo haileti picha nzuri kwa siasa.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema alisema Makamba yupo sahihi na upinzani unabidi kufanya kazi ya ziada kama wanataka kushinda 2020.
“Tulikosea na tulichelewa kuunda upinzani, mwaka 1995 tulikuwa na nafasi nzuri sana ya kuungana kwa sababu hakukuwa na rais kama Magufuli, lakini sasa hivi yupo na sisi wapinzani tusipobadilika na siasa zetu za kususa watatuchapa kweli 2020,” alisema Mrema.
Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen-Kijo Bisimba alisema Makamba alisema ukweli kutokana na hali na mazingira ya siasa nchini.

Wanaochakachua Pesa Za Tasaf waonywa



KAIMU Katibu Tawala Mkoa wa Tabora, Natalis Linuma, ameiomba serikali kusaidia vijiji ambavyo havijaingizwa kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini katika mkoa na vijiji.
Aliyasema hayo wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tasaf III kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika.
Linuma alisema vijiji vingi ambavyo havijaingizwa kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini, watu wake wana hali duni na baadhi wameachwa na watoto yatima.
Aidha, alisema kutokana na kaya hizo kutoingizwa katika mpango huo, kumesababisha malalamiko.Linuma alimwambia Waziri Mkuchika kuwa kaya 953ziliondolewa wakati wa uhakiki wa kubaini kaya zisizokuwa nasifa.
Alisema, Mkoa wa Tabora una jumla ya wilaya saba na tarafa 19, kata 174 na vijiji 696, mitaa148 ambayo mpango huo unatekeleza uhawilishaji katika kaya zenye sifa.
Lengo lilikuwa ni utambuzi na uandikishwaji wa kaya 52,558 na kaya 47,805 ziliandikishwa, kuanzia mwezi Agosti 2017.
Aidha, jumla ya Sh. 20,038,121.000 zilihawilishwa kwa walengwa 39,293.
Katika halmashauri zote za mkoa wa Tabora, mpango wa kunusuru kaya maskini umesaidia kuwapatia elimu watoto wenye wazazi wasio na uwezo.
Waziri Mkuchika alisema amepokea taarifa hiyo, lakini alipata fununu kuwa kuna baadhi ya viongozi wasio waaminifu.
Mkuchika alisema kuwa taarifa alizozipata ni baadhi ya viongozi kuomba rushwa na kuwaonya wakiendelea na tabia hiyo watakiona cha mtemakuni.

Hamisa Mobeto Anasa kwenye mtego Wa Zari



Mwanamitindo Hamisa Mobeto.
Mwanamitindo Hamisa Mobeto anadaiwa kunasa mtegoni baada ya ‘kuuvaa mkenge’ ulioratibiwa na hasimu wake wa siku za hivi karibuni, Zarinah Hassan ‘Zari’.
Kwa mujibu wa chanzo kilicho karibu na Zari, inadaiwa kuwa mjasiriamali huyo alimtumia mtu aitwaye William Bugeme ambaye pia ana ukaribu naye wa damu, ili aweze kumchukua mwanamitindo huyo, ambaye amezaa na baba wa watoto wake wawili.
Inadaiwa lengo la Zari ni kuona wawili hao wakiwa karibu, basi ni dhahiri kuwa ukaribu kati ya Hamisa na baba watoto wake utaisha, kwani uhusiano wa kimapenzi na William hauwezi kukubalika.
“Mnajua kuwa huyo Hamisa amenasa kwa Bugeme lakini hajui kuwa huo ni mpango wa Zari ili amtoe kwa baba mtoto wake, asipoangalia atatumika tu kisha atabwagwa kwani jamaa yupo kimaslahi zaidi kwa ajili ya kuokoa penzi la dada yake,” alisema Sosi huyo.
Kwa mujibu wa sosi huyo, picha za wawili hao wakiwa katika pozi tofauti zilinaswa hivi karibuni zikiwa zimerushwa mtandaoni.
Zarinah Hassan ‘Zari’
Sosi huyo alikwenda mbali zaidi na kuvujisha siri ya Zari kuwa ndiye anayemtuma ndugu yake huyo ili akifanikisha kuwa naye kimapenzi itakuwa rahisi kuachana na baba wa watoto wake.
Hata hivyo sosi huyo alidai fungu kubwa na zuri limeandaliwa kuhakikisha Hamisa hakwepi mtego huo.
“Mwanamke ni mjanja sana sana haongei ni pesa ndio inaongea, Bugeme toka zamani anafahamiana na Hamisa sasa ameamua kumtumia huyo huyo ili kuumaliza mchezo wake kabisa, unadhani mzazi mwenzake akiona ameingia kwenye penzi na Bugeme ataendelea naye, amecheza kwelikweli,” kilitiririka chanzo.
Risasi Jumatano lilimtafuta hewani Hamisa ili azungumzie sakata hilo kama ameshalifahamu au anajipanga vipi, lakini pia kuzungumzia picha zake zinazomuonesha akiwa na kaka huyo, lakini alipopokea simu yake alisikiliza madai yote kisha akakata simu.

Video | Rayvanny ft Maphorisa x Dj Buckz – Makulusa | Mp4 Download

Video | Rayvanny ft Maphorisa x Dj Buckz – Makulusa | Mp4 Download



DOWNLOAD

Audio | Rayvanny ft Maphorisa x Dj Buckz – Makulusa | Mp3 Download


Audio | Rayvanny ft Maphorisa x Dj Buckz – Makulusa | Mp3 Download