Thursday, 14 December 2017

Waziri Nchemba amaliza mgogoro wa Ardhi uliodumu miaka 9 Kondoa


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amefanikiwa kumaliza mgogoro wa ardhi ambao umedumu kwa miaka zaidi ya tisa ambao ulifikia hadi kuhatarisha amani ya kijiji cha Hurui katika kata kikole jimbo la kondoa vijijini wilaya ya kondoa mkoa wa Dodoma.

Mgogoro huo ambao umesababishwa na baadhi ya watu ambao si wajumbe wa kijiji kuuza eneo la kijiji la malisho mwaka 2009 bila mkutano wa kijiji kushirikishwa na kusababisha hali ya sitofahamu mpaka leo. Jitihada za wananchi kutafuta haki ya eneo hilo kwa njia za kisheria hazikuzaa matunda kwani walishindwa katika kesi zote mbili walizofungua katika Mahakama ya ardhi ya wilaya na mkoa hali iliyopelekea sasa mbunge wa jimbo la kondoa vijijini Dr Ashatu Kijaji kumwita waziri wa mambo ya ndani kusaidia kutuliza taharuki hiyo.

Waziri Dr Mwigulu Nchemba baada ya kusikiliza pande zote za kijiji na serikali ya wilaya ameagiza eneo hilo liendelee kutumika kama lilivyopangwa tangu mwaka 1972 kuwa eneo la malisho, amewataka wananchi na viongozi wa vijiji waache kuuza maeneo kinyemela kwani ndio chanzo kikubwa cha migogoro ya ardhi katika vijiji nchini.

Naye mbunge wa jimbo la kondoa vijijini ambaye pia ni Naibu waziri wa fedha Dr ashatu kijaji amesema amechoka na migogoro ya ardhi katika jimbo lake,yule ambaye atawafikisha katika migogoro watashughulika naye kwa sheria na taratibu za nchi.

Aidha Dr Ashatu amesema kuwa kwasasa hawawezi fanya shughuli za maendeleo katika baadhi ya vijiji kama kujenga madarasa na miundombinu ya maji na umeme kwasababu ya migogoro ya ardhi iliyopo hivyo kwasasa migogoro basi ili wafanye kazi huku akimshukuru Mkuu wa wilaya kwa jitihada kubwa zakusaidia kumaliza migogoro hiyo anayoonyesha

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Hurui Ramadhani Selemani amesema migogoro hiyo imeletwa na baadhi ya wajumbe wa serikali ya vijiji waliopita kwa kuuza maeneo zaidi ya ekari 52 ya malisho bila kushirikisha mkutano wa kijiji hali ambayo imeleta mgogoro mkubwa na kuhatarisha amani ndani ya kijiji.

Wananchi wa kata ya kikole wamemshukuru waziri wa mambo ya Ndani ya nchi kwa kuwarudishia maeneo yao kwani kwasasa amani itarudi tena katika kata yao na maendeleo yatakuja kwani watafanya shughuli kwa amani

Takwimu NBS; Tatizo la ukosefu wa ajira lapungua mwaka hadi mwaka



Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imesema tatizo la ukosefu wa ajiri nchini limepungua.

Mkurugenzi wa Shughuli za Takwimu, NBS Irineus Ruyoby amesema kwa mujibu wa takwimu walizonazo kwa sasa zinaonyesha tatizo la ukosefu ajira linaenda likipungua mwaka hadi mwaka.

“Takwimu ambazo tunazo zinaonyesha kiwango cha watu ambao hawaja ajiriwa kimepungua mwaka hadi mwaka, sasa hivi tupo katika kufanya tafiti nyingine tutaweza kujua hali halisi sasa ikoje” amesema.

Ameongeza kuwa uchumi wa Tanzania kwa sasa unaendelea kukua kwa kiwango cha wastani wa asilimia saba kwa mwaka na imekuwa hivyo kwa muda mrefu sasa

Kidoa Adaiwa Kurudi kwenye Ufuska,,,



MSANII wa filamu Bongo Asha Salum ‘Kidoa’ ambaye kwa kipindi kirefu alipoa kama maji ya mtungi kutokana na mwandani wake kumpiga ‘stop’ mambo ya kifuska ikiwemo kupiga picha za nusu utupu, amedaiwa kurejea kwenye vitendo hivyo baada ya kumwagana na jamaa huyo.
Kwa mujibu wa chanzo, Kidoa awali alikuwa machachari lakini alivyompata pedeshee ambaye ni kigogo wa serikali
alimpiga ‘stop’ mambo ya kifuska ikiwemo kuuza sura mitandaoni akiwa nusu utupu, pamoja na skendo kwenye vyombo vya habari.
Baada ya kunasa ubuyu huo, mwanahabari wetu alipomtafuta Kidoa, aliangua kicheko na kusema: “Watu wanapenda sana kufuatilia maisha yangu, najua hayo yote yameibuka baada ya kuweka picha Instagram nikiwa na nguo za ndani pekee, mavazi hayo nilikuwa nayapenda kitambo na picha zangu nyingi zilikuwa za hivyo, nikaamua tu nipumzike, si kwamba nimeachwa.”
Kama hujeelekezwa kiotomatiki, bofya

Miezi 11 Mbeya, Songwe yaongoza kwa vifo kwa Kipindupindu



Dar es Salaam. Watu 3,739 wameugua na wengine 71 kufariki dunia kutokana na kipindupindu katika kipindi cha miezi 11 iliyopita, huku mikoa ya Mbeya na Songwe ikiongoza kwa vifo.
Takwimu hizo za Januari hadi Novemba zinaonyesha mkoa wa Mbeya umekuwa na wagonjwa 710 na vifo 14 huku Songwe ikiwa nao wagonjwa 538 na vifo vinne.
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu jana aliitaja mikoa mingine iliyoathirika zaidi kuwa ni Morogoro (320 na vifo 11), Dar es Salaam (320 na vifo vitano) Iringa (332 na vifo tisa), Kigoma (314 na vifo vinne). “Takwimu zinatuonyesha bado maambukizi mapya ni tishio kwani kuna ongezeko la idadi ya mikoa na halmashauri zinazotoa taarifa za wagonjwa japokuwa idadi imepungua mwishoni mwa mwaka,” alisema.
Ummy alisema takwimu za tangu mwaka huu uanze zinaonyesha ongezeko la ugonjwa ambapo mikoa 17 ilitoa taarifa za kuwapo kwa wagonjwa.
Hata hivyo, waziri alisema mikoa saba haikuripoti kuwa na ugonjwa huo ikiwamo Mwanza, Shinyanga, Arusha, Lindi, Kagera, Simiyu, Kilimanjaro na Mtwara.
“Nchi yetu inaelekea katika majira ya mvua ambazo zinaweza kuongeza kuenea kwa maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu, hivyo tunahitaji kuzidisha juhudi za kuzuia kwa kusimamia kikamilifu maelekezo na miongozo stahiki inayotolewa,” alisisitiza.
Waziri huyo aliwataka wananchi kujenga na kutumia vyoo bora katika maeneo ya makazi, kunawa mikono kwa maji yanayotiririka na sabuni kabla ya kula, baada ya kutumia choo na baada ya kuwasafisha watoto waliojisaidia.
“Mamlaka za maji zilizopo nchini zihakikishe upatikanaji wa majisafi na salama kwa wananchi, kunywa majisafi na salama yaliyotakaswa kwa dawa (kama vile water guard) au yaliyochemshwa na kupoa,” alisema.
Ugonjwa wa kipindupindu unachangiwa pia na kutokuwa na vyoo bora, huku ofisa mtendaji wa Kijiji cha Humekwa kilichopo Chamwino mkoani Dodoma, Ashrey Myogoya akisema kampeni ya Taifa ya usafi wa mazingira yenye kaulimbiu “usichukulie poa nyumba ni choo” imesaidia kwa kuwa mpaka sasa kaya zote 349 zina vyoo vilivyoboreshwa. Mkazi wa kijiji hicho, Cecilia Isaya alisema choo chake amekijenga kwa gharama ya Sh55,000.
“Si gharama kubwa nimetumia kwani baadhi ya vifaa nimenunua lakini vingine nimetengeneza mwenyewe ikiwamo matofali,” alisema.
Kama hujeelekezwa kiotomatiki, bofya
hapa .

Wednesday, 13 December 2017

Real kumng’oa neymar psg


Timu ya Real Madrid inaripotiwa wamefikia makubaliano na staa wa Paris Saint-Germains, Neymar, ili akajiunge nayo ifikapo mwishoni mwa msimu ujao.

Mbrazili huyo amekuwa mchezaji ghali zaidi duniani majira ya joto msimu huu baada ya kuhamia PSG akitokea Barcelona kwa uhamisho wa pauni milioni 200.

Licha ya kuanza vizuri msimu huu akiwa na PSG baada ya kufunga mabao 15 na kutoa pasi zilizozaa mengine 11 katika mechi 18 tu, tetesi zimeibuka zikidai kuwa Neymar hana furaha kamili katika mazingira yake mapya.

Ripoti kutoka kwenye chanzo cha habari nchini Hispania Diario Gol, zinadai kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 amekubaliana na Real Madrid na anatarajiwa kutua Bernabeu mwishoni mwa msimu wa 2018-19.

“Neymar anatamani sana kushinda tuzo ya Ballon d’Or na anaamini kuwa atakuwa na nafasi nzuri kutimiza ndoto zake akiwa katika Jiji Kuu la Hispania,” kilieleza chanzo hicho.

Manchester United na Manchester City pia zinasemekana zinavutiwa na mchezaji huyo, ambaye mkataba wake Parc des Princes utafika ukomo mwaka 2022.


Sababu za Wapinzani kuhamia CCM hizi hapa

Sababu za Wapinzani kuhamia CCM hizi hapa

New VIDEO: J Gold Wenga – Yonella

New VIDEO: J Gold Wenga – Yonella

New VIDEO: J Gold Wenga – Yonella

DOWNLOAD


Askofu Niwemugizi azungumza na JPM, Baada ya kuhojiwa uraia


Baada ya kuhojiwa na Idara ya Uhamiaji kuhusu uhalali wa uraia wake Askofu wa Jimbo la Ngara - Rulenge, Severine Niwemugizi ameeleza kwamba amezungumza na Rais John Magufuli.

Askofu Niwemugizi akizungumza na Mwananchi kwa simu jana kujua kile walichozungumza na Rais Magufuli hasa baada ya kuandika ujumbe wa kumpongeza Rais kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Facebook, kiongozi huyo wa kiroho alisema, “Ni kweli leo (jana) nilizungumza na Rais Magufuli, alinipigia simu na tumekuwa tukiwasiliana kujuliana hali.”

Jana, askofu huyo alikaririwa akisema amehojiwa mara mbili na Uhamiaji katika kile kinachoelezwa ni utata wa uraia wake huku akieleza kuwa amezaliwa wilayani Biharamulo mkoani Kagera.

Alipoulizwa kama mazungumzo hayo ni baada ya taarifa za kuhojiwa na Uhamiaji, Askofu Niwemugizi alijibu huku akianza kwa kucheka, “Hahahahaha!! Ni kweli Rais kataka kujua hasa kuna nini, yeye amesema atalifuatilia na kukiwa na... nitamfahamisha.”

Askofu huyo ambaye Septemba mwaka huu aliibua mjadala wa Katiba Mpya na kusema kuwa yuko tayari kuitwa mchochezi endapo kundi la watetezi wa haki za binadamu watachukuliwa kama wachochezi alisema kuhojiwa huko hakutamrudisha nyuma katika misimamo yake, “Siwezi kurudi nyuma, nimetumwa na Kristo, Nabii anaweza kupendwa au kuchukiwa na mimi siwezi kunyamaza.”

Askofu Niwemugizi aliyewahi kuwa Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) alisema, “Mimi nazungumza lakini kuna Watanzania wengine wanazungumza sana. Lakini mimi kuhojiwa mara mbili hakutaninyamazisha.”

Ujumbe aliouweka Facebook, unasema, “Nasali Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki, uniokoe na mtu wa hila asiye haki. Kwa kuwa wewe ndiwe Mungu uliye nguvu zangu; kwa nini umenitupa?

Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea? ...Nafsi yangu, kwa nini kuinama, na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; kwa maana nitakuja kumsifu, aliye afya ya uso wangu na Mungu wangu” (Zab 43:1-2,5). Asante Rais wangu JPM kwa faraja uliyonipa.”

Wakichangia ujumbe huo, Deusdedit Mwombeki alisema “Amina Baba Askofu Severine Niwemugizi kwa ujumbe wako wa faraja nami umenigusa. Pole sana na hongera kwa faraja uliyopewa na Rais Magufuli.”

Prosper Mallya alisema, “Kweli humuweka mtu huru, kiongozi hukutana na misukosuko ila kwa kuwa wewe unawasemea wanyonge na Roho wa Bwana yu nawe, hutaogopa wala hutarudi nyuma. Mwenyezi akutie Roho wa hekima na akili uendelee kunena yale unayoona ni kwa manufaa na ustawi wa taifa letu.”

Katibu Mkuu wa Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania, Askofu David Mwasota akizungumzia kitendo cha Uhamiaji kumhoji askofu huyo alisema kila nyakati na utendaji wake kikubwa ni kuliombea Taifa.

“Serikali ina macho na taarifa nyingi na labda inajua kwa nini inamhoji, lakini kwa heshima ilibidi hata taarifa zake zisijulikane...” alisema Askofu Mwasota na kuongeza:

“Tunawapa pole wenzetu wa Kanisa la Katoliki na tunawaomba kila mtu kwa nafasi yake tuliombee Taifa… lakini tuelewe kipindi hiki ni tofauti na kile cha Jakaya Kikwete.”

Mwananchi lilipomtafuta Rais wa TEC, Askofu Tarcisius Ngalalekumta kujua hatua ambazo baraza lake imechukua alisema “Kwanza ndiyo nasikia kutoka kwako, lakini kanisa linajiongoza, Serikali kama kuna kitu inakitafuta hatuwezi kuizuia.”

Ngalalekumtwa ambaye pia ni Askofu wa Jimbo Katoliki la Iringa alisema “Hilo sisi halina tatizo, Kanisa Katoliki halina mipaka, kuna maaskofu kutoka nchi mbalimbali.”

Source: Mwananchi


Unajua Kibiriti hutengenezwa na nini ?



 Unga wa muhogo umeelezwa kuwa na matumizi mbalimbali, zaidi ya kupikia ugali pia hutumika kutengeza Kibiriti ambapo unga huo hutengeneza kile kishungi cha kuwashia moto kinachokaa mbele ya kijiti cha kibiriti.


Hilo limethibitishwa na Mkurugenzi wa Kiwanda cha kusaga muhogo cha Ukaya, Mkuranga, Mkoani Pwani, Ibrahim, mbele ya uongozi wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita) uliotembelea kiwanda hicho.

Akiongea na uongozi wa Mkikita Ibrahim amesema kuwa miongoni mwa wateja wakubwa wa unga wao ni viwanda vya kutengenezea Vibiriti ambavyo vinautumia kwa kutengenezea kishungi cha njiti ya kibiriti kinachotumika kuwasha moto.

“Unga wetu wa muhogo tunaosaga hapa una wateja wengi sana kutokana na matumizi mbalimbali ambayo unaweza kufanya, ukitoa wateja kwaajili ya chakula, lakini Unga wa muhogo hununuliwa sana viwanda vya kutengeneza Kibiriti kwasababu hutumika kutengeneza kile kishungi cha kuwashia moto”, ameeleza Ibrahim.

Mbali na kupikia ugali na kutengeneza kishungi cha Kibiriti Ibrahim amebainisha kuwa Unga huo pia hutumika kutengenezea dawa ya kuzuia kuhara, Pombe, Mafuta pamoja na chakula cha wanyama.


Bifu la Wolper na Husna kwishaaa


Jacqueline Wolper

 MASTAA wawili waliokuwa na bifu kwa sababu ya kuchangia bwana Mkongo ajulikanaye kama Mwami Radjabu, Jacqueline Wolper na Husna Maulid wamemaliza uhasama kati yao na sasa ni full vicheko.

Hali hiyo ilijidhihirisha juzikati kwenye sherehe ya kumbukumbu ya kuzaliwa ya Wolper, walipoonekana wakiwa karibu na

kufurahi huku vyanzo vikisema warembo hao walielewana baada ya Husna kumwagana na bwana huyo.

“Si unajua Husna alishamwagana na Mwami ambaye alimvisha mpaka pete ya uchumba lakini hawakufanikiwa kufunga ndoa, kwa hiyo walimaliza tofauti zao,” kilisema chanzo.

Baada ya kuona na kupata habari kutoka kwa chanzo, Za Motomoto News

ilimtafuta Husna ambaye awali alikuwa hapendi kabisa kumsikia Wolper ambaye alikiri kumaliza tofauti zao.

“Tulishamaliza tofauti zetu, sina bifu na Wolper maana aliyekuwa anatugombanisha ni mwanaume na sisi ni wanawake hivyo wanawake tujifunze kuwa wanaume ni watu wa kupita tu,” alisema Husna.


Husna Maulid.

Serikali yatoa taarifa hii kuhusu kufanyika kwa mnada wa madini ya Tanzanite



Baada ya Wema kukutana na Makonda, Steve Nyerere afunguka


 Wema Sepetuakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Siku tatu baada ya muigizaji maarufu wa filamu, Wema Sepetu kumuangukia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, mchekeshaji nyota, Steve Mengere ‘Steve Nyerere’ amebwatuka vibaya kuhusiana na ishu hiyo.

Akizungumza na Risasi Mchanganyiko kwa njia ya simu juzi akiwa njiani kurejea Dar es Salaam akitokea Dodoma, msanii huyo anayedhaniwa kufanikisha kwa kiwango kikubwa kurejea CCM kwa Wema Sepetu, alikiri wawili hao kumaliza tofauti zao kwa njia ya amani, nyumbani kwa bosi huyo wa mkoa.

“Hakuna uadui wa kudumu katika haya maisha, isitoshe wale wote ni vijana, wamekutana wameombana msamaha na mambo yamebakia kuwa historia. Wanaangalia maisha mengine ya huko mbele kwa sababu safari bado ni ndefu,” alisema mchekeshaji huyo ambaye pia ni mmoja wa viongozi wa kundi linalohamasisha uzalendo kwa watanzania.

Kuhusu kama kuna ahadi yoyote iliyo nyuma ya makubaliano baina ya wawili hao ambao kabla ya kutofautiana wanaripotiwa kuwa marafiki, Steve alisema hakuna kitu chochote zaidi ya wao kuamua kuachana na mambo ya zamani na kufungua ukurasa mpya.

“Hili ni funzo kubwa sana kwa wapambe, hasa wasanii, watu wakikorofishana wawe na akiba ya maneno, kuna watu walikuwa wanatoa maneno ya ovyo kwa mkuu wa mkoa kupitia kwa Wema, sasa leo hawa wamepatana, hivi sura zao wanazipeleka wapi?

“Haya mambo ya maisha, ukiona kuna jambo limewatokea watu, ni vizuri mtu ukawa na kiasi cha maneno, au wengine walikuwa wanamponda Wema kwa kupitia kwa mkubwa, sasa leo hii wanajisikiaje?” alisema.

Alipoulizwa kuhusu kutoonekana kwa mama mzazi wa msanii huyo, Miriam Sepetu nyumbani kwake Sinza Mori, ikidaiwa kuwa huenda amefichwa sehemu kwa malengo maalum, Steve Nyerere alisema kada huyo wa Chadema yupo nyumbani kwake.

“Nani amekuambia mama hayupo? Yupo palepale nyumbani kwake na mambo yanaenda vizuri tu, wala watu hawana haja ya kumtafuta popote,” alisema Steve, akipinga habari za kutokuwepo nyumbani hapo kwa siku kadhaa sasa, ambako kumeripotiwa na magazeti ya Global Publishers.

Uhusiano wa Makonda na Wema uliingia dosari baada ya mkuu huyo wa mkoa kumtaja katika orodha ya kwanza ya watu wanaojihusisha na madawa ya kulevya, Februari mwaka huu.

Mchekeshaji nyota, Steve Mengere ‘Steve Nyerere’.



Ukarabati wa nyufa za majengo ya UDSM waanza


Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umeanza ukarabati wa mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) yenye ufa.

Taarifa za kuwepo nyufa hizo zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii usiku wa Desemba 3,2017 na baadaye ufafanuzi ulitolewa na TBA.

Uchunguzi uliofanywa na MCL Digital umebaini ukarabati umeanza, huku ikielezwa kuwa hauwaathiri wanafunzi wanaotumia mabweni hayo.

“Ukarabati umeanza, mafundi wanafanya kazi nje ya jengo kwa kuondoa plasta ili kuangalia tatizo liko wapi,” kimesema chanzo cha habari kilichozungumza na MCL Digital.

TBA iliyojenga majengo hayo ambayo bado yako katika usimamizi wake imeelezwa pia inaangalia dosari nyingine zilizopo.

Mtendaji Mkuu wa TBA, Mhandisi Elius Mwakalinga Desemba 4,2017 akizungumzia nyufa zilizoko kwenye jengo la Block A alisema hazina madhara na walizitarajia.

Alisema nyufa katika jengo hilo la hosteli ambalo ni kati ya sita yaliyopo Block A zimetokea eneo walilotarajia ambalo kitaalamu linajulikana (expansion joint) hivyo hazina madhara.

Mwakalinga alisema kwa kawaida udongo unaobeba jengo hutitia baada ya muda fulani, hivyo wakati wa ujenzi huacha nafasi kuliwezesha jengo kupumua bila kusababisha nyufa.

Mwakalinga alisema kuna makosa yalifanyika ya kuziba nafasi zilizoachwa (expansion joint) kwa kutumia saruji badala ya mbao au plastiki maalumu hivyo kuonyesha nyufa kwenye jengo hilo.

Kutokana na kusambaa kwa picha kuonyesha nyufa katika majengo hayo, mbunge wa serikali ya wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso), Kumbusho Dawson alishikiliwa na polisi kitengo cha makosa ya mtandao kwa kuhojiwa na baadaye aliachiwa.