Thursday, 7 December 2017

VIDEO: Siku 17 za Kutoweka kwa Mwandishi wa Mwananchi



Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), imelaani vikali huku ikipaza sauti ya kutaka arejeshwe akiwa hai mwandishi wa habari wa kujitegemea wa gazeti Mwananchi, Azory Gwanda aliyechukuliwa na watu wasiojulikana.
Gwanda ambaye kituo chake cha kazi ni Kibiti na Rufiji mkoani Pwani, alitoweka katika mazingira ya kutatanisha Novemba 21, 2017 baada ya kuchukuliwa na watu wasiojulikana akiwa Kibiti majira ya saa 4:00 asubuhi.

MCL ilipata taarifa za kupotea kwa mwandishi huyo Novemba 30, 2017 kutoka kwa ndugu zake na mkewe baada ya kushindwa kumpata kwenye simu yake.

Juhudi za kuhakikisha Gwanda anapatikana chini ya uongozi wa kampuni hiyo ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa kwa vyombo vya ulinzi na usalama, wizara husika na wadau wa tasnia hiyo ya habari hazijafanikiwa hadi leo.

Kutokana na mazingira hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa MCL, Francis Nanai akiwa ameongozana na timu ya wafanyakazi wa kampuni hiyo pamoja na viongozi wa Jukwaa la Wahariri(TEF) leo Alhamisi asubuhi ameitisha mkutano wa vyombo vya habari kueleza jinsi kampuni inavyoendesha harakati za kumtafuta mwandishi huyo kupitia jeshi la polisi na wizara ya habari.



“Tumefuatilia tukio hilo hadi kwa Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Kanda Maalumu ya Rufiji ambaye amesema hawana taarifa na kwamba atafuatilia kisha kutoa taarifa. Mpaka leo hatujapata taarifa yoyote,” amesema Nanai.

Katika tukio hilo, waandishi wote na wafanyakazi wa kampuni hiyo inayochapisha magazeti ya Mwananchi, Mwanaspoti na The Citizen wamevalia mavazi meusi huku wakiwa wameinua juu magazeti na mabango yenye ujumbe unaosema kwa maandishi makubwa ‘Bring Back Azory’, #MrudisheniAzory.

Waandishi wa habari walihitaji kujua ni sababu au dalili gani ambazo kampuni inaamini zimesababisha kupotea kwa Gwanda, aina ya habari alizokuwa amepewa kufuatilia za uchunguzi na habari ya mwisho kuripoti katika gazeti la Mwananchi ilikuwa ya aina gani.

Nanai amejibu maswali hayo kwa nyakati tofauti lakini akasema habari ni nyingi zinazoandikwa na vitisho vimekuwapo kwa waandishi wa habari katika mazingira tofauti.

Kupotea kwake

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Nanai amesema kwa mujibu wa Anna Pinoni, ambaye ni mke wake, Azory alichukuliwa na watu ambao hawafahamu waliomfuata eneo ambalo hupenda kukaa kwa ajili ya maongezi na wenzake katika mji wa Kibiti.



Amesema kwa maelezo ya Anna watu hao waliokuwa na gari nyeupe aina ya Toyota Land Cruiser walienda naye shambani kumfuata. Walipofika shambani, Azory alimuuliza mkewe mahali zilipo funguo za nyumba yao na kuelezwa sehemu zinapowekwa siku zote.

Nanai amesema baadaye watu hao na Azory wakaondoka na kumuacha mkewe shambani. Kabla ya kuondoka, Azory alimwambia mkewe kwamba anaenda kazini na atarudi jioni ya siku hiyo (Jumanne Novemba 21, 2017) au siku inayofuata (Jumatano Novemba 22, 2017).

“Mkewe aliporudi nyumbani alikuta nyumba imefungwa na funguo zikiwa mahali alipoziweka, lakini alipoingia ndani alikuta dalili za kupekuliwa kwani vitu mbalimbali vilikuwa vimerushwa shaghalabaghala ndani ya nyumba. Mkewe anasema hakuwa na wasiwasi mpaka siku iliyofuta baada ya kuona simu zake zote hazipatikani,” anaendelea kusimulia Nanai.

Amesema Alhamisi ya Novemba 23, 2017 alikwenda(mkewe) kuripoti Kituo cha Polisi Kibiti na kupewa RB Na:Kibiti/RB/1496/2017 ambako walimweleza kuwa  hawajui alipo na kumwomba awape namba yake ya simu ili wampigie iwapo watapata taarifa zinazomhusu, lakini mpaka sasa hajapewa taarifa yoyote wala kuitwa.



“Baada ya hapo, juhudi za kumtafuta ziliendelea ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa kwa vyombo vya habari vya ndani na nje, baadhi vikatangaza na kuchapisha. Pia kampuni ilituma ujumbe wake kwa mkewe Kibiti kumpa pole na kupata taarifa zaidi ili kujua kinachoendelea.”

Nanai amesema pamoja na hatua hiyo, MCL imeshaandika barua rasmi kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo; Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF).

Wengine waliopata barua ni Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari (MOAT), Taasisi ya MISA-TAN, Baraza la Habari Tanzania (MCT), Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) na wadau wengine kuhusu kupotea kwa mwandishi huyo.


Audio | D’Banji – As I Dey Go | Mp3 Download

Audio | D’Banji – As I Dey Go | Mp3 Download

Audio | D’Banji – As I Dey Go | Mp3 Download

                DOWNLOAD

Audio | Makihiyo Ft. Ben Pol – Ni wako | Mp3 Download

Audio | Makihiyo Ft. Ben Pol – Ni wako | Mp3 Download


Audio | Makihiyo Ft. Ben Pol – Ni wako | Mp3 Download

                  DOWNLOAD

LIVE: Hotuba ya waziri mkuu kwenye ufunguzi wa ofisi za Umoja wa Mataifa Dodoma


Jackline Wolper amwaga machozi mbele ya Watoto


LIVE: Cha kufahamu kuhusu Tamasha la ''DR SHIKA'' Usiku wa 900 itapendeza

LIVE: Cha kufahamu kuhusu Tamasha la ''DR SHIKA'' Usiku wa 900 itapendeza

Odinga apewa onyo na Marekani



Raila Odinga

Marekani imemtaka kiongozi wa upinzani nchini kenya Raila Odinga kuacha mpango wake wa kuapishwa kama raisi wan nchi hiyo wiki ijayo.

Odinga aliwasilisha Malalamiko juu ya mapungufu katika uchaguzi mkuu uliopita na kusababisha uchaguzi wa marudio ambapo Uhuru Kenyata alishinda kwa kura nyingi.

Msaidizi wa katibu wa masuala ya Afrika Marekani , Donald Yamamoto ambae ametembelea nchini kenya.

Ametaka majadiliano ya pande zote mbili kati ya upinzani na serikali ilioko madarakani.

Baadhi ya viongozi wa serikali wameonya kuwa tukio hilo la kuapishwa linaweza kuhusishwa na uhaini.

Trump ameutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel



Rais Trump amefanya maamuzi ya kihistoria ya kuipindua sera za miaka mingi ya Marekani kwa kuutambua mji wa Yerusalem kuwa ndio mji mkuu wa Israel.

Rais huyo pia ametangaza kuwa Ubalozi wa Marekani utahamishwa kutoka katika eneo la sasa la Tel Aviv kwenda Yerusalem. Amesema kuwa uamuzi huu haulengi kujiondoa kwa Marekani katika juhudi zake za kuleta amani katika eneo hilo la mashariki ya kati.

Trump amesema uamuzi huu haulengi kujiondoa kwa Marekani katika juhudi zake za dhati za kuleta amani ya kudumu bali inataka kutafuta suluhu ya mgogoro wa miaka mingi kati ya Israel na Palestina ambao .Marekani haifungaman na upande wowote na kuingilia mipaka ya Israel na mamlaka zake ,na hatuko tayari kuingilia katika migogoro yao ,hayo ni mambo yao wenyewe.

Huku kwa upande wake Rais Mahmoud Abbas wa Palestina amesikitishwa na maamuzi ya rais Trump na kudai kuwa Marekani imepoteza haki ya kusimamia hatua ya kupatana kwa amani ambayo imekuwa ikitafutwa miongo kadhaa iliyopita.

Huku waziri mkuu wa Israel ,Benjamin Natanyau ameonekana kuunga mkono hatua ya rais Trump kwa kuelezea kuwa ni maamuzi ya kihistoria licha ya kuwa wapalestina wamemkosoa na huku Uingereza na nchi nyingine wanachama wa baraza la usalama wa umoja wa mataifa wameitisha kikao cha dharura ili kujadili maamuzi yaliyofanywa na rais Trump.

Polepole Awapiga Dongo CHADEMA



Katibu wa itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole amesema  CHADEMA wamefanya kikao cha dharura  kususia uchaguzi wa marudio wa majimbo na kata unaotarajiwa kufanyika January 13 mwakani.

Polepole amewatuhumu  CHADEMA  kuwa wanatumia mgongo wa kuminywa kwa Demokrasia nchini kususia uchaguzi huo wakati ukweli ni kwamba wamefulia baada ya kutumia vibaya hela ya mfuko wa chama chao.

"Watani wanakutana leo, agenda ni kutoshiriki uchaguzi unaokuja wa marudio kwa kisingizio cha demokrasia lakini ukweli ni matumizi mabaya ya fedha yamefuja mfuko wa chama. Tafuteni visingizio vingine lakini sio demokrasia. Watu wamechoka siasa za matukio. Kikao chema!" Ameandika polepole katika ukurasa wake wa Twitter.




Mtatiro akanusha kuhamia CCM



Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro amekanusha uvumi unaonea kwenye mitandao ya kijamii kwamba ana mpango wa kukihama chama hicho na kuhamia Chama tawala cha CCM.

Kupitia taarifa yake kwa umma aliyoitoa jana  Disemba 6,2017, Mtatiro pia hana mpango wa kugombea jimbo la Kinondoni lililo achwa wazi kufuatia aliyekuwa Mbunge wake kupitia CUF, Maulid Mtulia kujiuzulu na kujiunga na CCM.

“Ndugu zangu, nimeona propaganda nyingi kwenye mitandao juu ya mimi kuhamia CCM au kuwa na mipango ya kuhamia CCM.

"Nataka niwahakikishie watanzania kuwa SIJAPANGA mipango hiyo na sina nia hiyo. Na naomba niwajulishe kuwa mtu akiwa anahamia CCM, hamuwezi kuwa na tetesi, na mimi sina kawaida ya kufanya maamuzi ghafla na kwa kujificha.

"Ningelikuwa na nia ya kuhamia CCM ningewataarifu hapa hadharani, miezi kadhaa kabla ya kufanya hivyo, walau jambo moja ambalo Mungu alinijalia ni kutokuwa mwoga na mnafiki na alinipa uwezo mkubwa wa kufanya jambo naloliamini,” alisema na kuongeza.

“Pili, nimepokea meseji nyingi sana zikiniomba nigombee ubunge jimbo la Kinondoni baada ya Mbunge wa (CUF – Lipumba), Ndugu yetu Maulid Mtulia kuhamia CCM. Nataka niweke msimamo wangu mapema, kwamba sina na sikuwahi kuwa na ndoto za kugombea ubunge wa jimbo la Kinondoni,

Masuala ya kugombea ubunge kwenye majimbo ni masuala mapana, yanahitaji maandalizi, ukaribu wako na wapiga kura na historia yako na jimbo hilo. Kwa kiasi kikubwa hakuna kigezo hata kimoja kati ya hivyo ambacho nimekikaribia, kwa hiyo sitoweza kugombea kama nilivyoona baadhi ya fikra za watu mitandaoni.”

Mtatiro amewahakikisha wanachama wa CUF kwamba anaendelea na majukumu yake ya Kamati ya Uongozi CUF, pamoja na kushirikiana na kila mtanzania kwa njia mbalimbali katika kuijenga nchi.

“Na kupitia michango yangu hiyo naendelea kuijenga Tanzania na hata kuunga mkono juhudi chanya za Rais wetu kuijenga Tanzania huku zile juhudi hasi za Rais huyo huyo hasa kwenye eneo la Demokrasia, Utawala Bora na Uchumi, nikizikemea kila siku.

"Mwisho, wapo wendawazimu wanachekelea, wanafurahia na ama kutamani vyama vya upinzani vife. Ukiona elimu ni ghali, hebu jaribu ujinga,” amesema.

Hata hivyo, Mtatiro amesema anaendelea kuwaheshimu wanaohamia CCM, kwa uhuru, utashi na mapenzi yao au kwa kununuliwa, kutokana kwamba sio wa kwanza wala hawatakuwa wa mwisho kufanya hivyo.

Yanga kutoa pigo Simba



MMOJA WA WACHEZAJI WA TIMU YA SIMBA, JUUKO MURSHEED ANAYEWANIWA NA TIMU YA YANGA

KAMA mazungumzo yanayoendelea kati ya uongozi wa klabu ya Yanga na wachezaji wawili wa klabu ya Simba yatakamilika, Wanajangwani hao kwa mara ya nyingine watakuwa wametoa pigo kwa vinara hao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Yanga inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa kama ilivyo kwa Simba na Singida United,  ipo kwenye mazungumzo ya siri na kiungo Muzamir Yassin na beki wa kati raia wa Uganda, Juuko Mursheed, ikijaribu kuwashawishi kutua kwenye timu hiyo katika kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili.

Yanga imetuma wajumbe wake wa kamati ya usajili jijini Nairobi inapofanyika michuano ya Kombe la Chalenji, kufanya mazungumzo na nyota hao.

Mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alimwambia mwandishi wetu kuwa, kwa upande wa Muzamir mazungumzo ya awali yanatoa ishara ya mchezaji huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar kuweza kutua kwenye kikosi chao hivi karibuni.

"Kuhusu Juuko, bado wapo kwenye mazungumzo, nafikiri baada ya siku chache lolote linaweza likatokea... wachezaji hawa wawili, kimkataba wanaruhusiwa kufanya mazungumzo na klabu nyingine kwa sababu mikataba yao imebaki miezi sita kumalizika," alisema Mjumbe huyo.

Aidha, taarifa zilieleza kuwa wachezaji hao wanasakwa vilivyo na Yanga kwa ajili ya kwenda kuchukua nafasi za kiungo Thaba Kamusoko ambaye ni majeruhi pamoja na beki Vincent Bossou aliyeamua kuachana na Yanga.

Muzamir yupo kwenye kikosi cha Kilimanjaro Stars kwenye michuano hiyo ya Chalenji inayoandaliwa na Baraza la Vyama vya Soka Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (Cecafa), huku Juuko akiwa na kikosi cha timu ya Taifa ya Uganda 'The Crane'

Wastaafu wa TRL wamuomba Rais Magufuli kuwasaidia wapate Mafao yao


Morogoro. Baadhi ya wastaafu wa Shirika la Reli Tanzania (TRL) wamemuomba Rais John Magufuli kuingilia kati na kuwasaidia ili waweze kulipwa mafao yao na fedha za kusafirishia mizigo ambazo wanadai kwa zaidi ya miaka mitano sasa.

Wastaafu hao ambao wameungana kudai stahiki zao walistaafu tangu mwaka 2012 hadi Juni, miaka yote wamekuwa wakidai stahiki hizo bila mafanikio.

Wakizungumza na gazeti hili jana, wastaafu hao walisema madai yao makubwa ni fedha za kusafirisha mizigo na familia ili kurejea vijijini kwao.

Katibu wa wastaafu hao, Selungwi Ubwe alisema wapo zaidi ya 100 katika mikoa mbalimbali nchini ambao wameshindwa kurejea makwao kwa kukosa fedha.“Madai yetu ni nauli za kusafirisha familia na mizigo, mafao ya kustaafu, kuna utaratibu wa wastaafu kulipwa tuzo za ustaafu ambazo ni mabati na mifuko 50 ya saruji na fedha taslim kulingana na kiwango chako cha mshahara na muda uliotumikia shirika,” alisema Ubwe.

Naye mstaafu mwingine, Ally Makubi alisema shirika halina budi kuwalipa stahili zao zote kwani walikuwa waadilifu kipindi chote cha utumishi.

“Mfanyakazi anapostaafu hana tegemeo lolote zaidi ya mafao na tuzo ili aweze kuendeleza maisha mengine, hivyo ni vyema Serikali ikaona umuhimu wa kutulipa tena kwa haraka,” alisema Makubi.

Akizungumzia suala hilo, katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Reli Tanzania (Trawu), Christopher Kaziyo alisema kwa sasa wameomba kuwasiliana na mkurugenzi wa Mfuko wa Pensheni (PPF) ili kujua tatizo, kwa kuwa ndio unaopaswa kuwalipa pensheni wastaafu hao. “Suala la mafao sheria zipo wazi kama mwajiriwa akithibitisha makato ya fedha hizo kwenye mshahara wake anastahili kulipwa bila kusumbuliwa,” alisema Kaziyo.

Naye mkurugenzi wa TRL, Masanja Kadogosa alisema hakuna mstaafu yeyote anayedai fedha za kusafirisha mizigo na familia kwani hulipwa baada tu mtumishi anapostaafu.

“Hakuna mtumishi anayetudai fedha za kusafirisha mizigo, kwani fedha hizi hulipwa mwanzo kabisa na kuhusu mafao mifuko ya hifadhi ndio inayopaswa kuwalipa,” alisema Masanja.

Mkurugenzi huyo alisema fedha ambazo wastaafu hao hawajalipwa ni za tuzo ambazo zina utata kidogo, hivyo wapo katika majadiliano ili zilipwe.

Uboreshaji TRL

Kampuni hiyo ilianza uendeshaji wa shughuli zake Oktoba 2007 chini ya umiliki wa mwekezaji kampuni ya Rites ya India ambayo ilikuwa inamiliki hisa 51 na Serikali ya Tanzania hisa 40. Hatua hiyo ilifuatia kuvunjwa kwa Shirika la Reli Tanzania (TRC) na kukaribisha wawekezaji ambao baadaye walishindwa na kuanzia Julai 22, 2011 hisa zote za kampuni hiyo zinamilikiwa na Serikali.

Kwa sasa Serikali imedhamiria kuboresha wa miundombinu ya treni na kupitia kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli Tanzania (Rahco), tayari imeingia mkataba na kampuni ya Yapi Merkezi ya Uturuki kujenga kipande cha pili cha reli ya kisasa ya Standard gauge (SGR) kutoka Morogoro hadi Makutopora yenye umbali kilomita 336 za njia kuu na kilomita 86 za njia za kupishana treni zitakazogharimu Sh4.3 trilioni.

Mkuu wa Mkoa mstaafu wa Manyara afariki dunia



Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Manyara mstaafu, Joel Bendera amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).

Akizungumza na MCL Digital leo Jumatano Desemba 6,2017 msemaji wa MNH, Aminiel Aligaesha amesema, “Ni kweli Joel Bendera amefariki. Aliletwa leo na gari la wagonjwa saa 6:30 mchana na ilipofika saa 10:24 jioni alifariki.”

Aligaesha amesema Bendera alipokewa hospitalini hapo akitokea Bagamoyo mkoani Pwani.

Kuhusu chanzo cha kifo chake Aligaesha amesema, ‘’Hilo sasa ni suala la familia lakini kwa wakati huu itoshe kusema amefariki.”

Bendera pia amewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Mbali ya ukuu wa mkoa, amewahi kuwa mbunge wa Korogwe Mjini na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo katika utawala uliopita wa Rais mstaafu, Jakaya Kikwete.

Katika mabadiliko ya wakuu wa mikoa yaliyofanywa na Rais John Magufuli Oktoba 26,2017, Bendera alikuwa miongoni mwa waliostaafu.

Nafasi yake imechukuliwa na Alexander Mnyeti aliyepandishwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara akitokea kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru.