Thursday, 7 December 2017

Bill Nas apata dili la Mamilion



MWANAMUZIKI ambaye alitamba kwenye gemu la muziki wa Bongo Fleva na ngoma ya Chafu Pozi, Bill Nas baada ya kula dili la Coce Studio Africa pamoja na kufanya matamasha mbalimbali, hivi karibuni amekula dili lingine la mtandao wa simu, ambalo amesema litampigisha hatua kubwa kwenye muziki wake.

Akichonga na ukurasa huu wa burudani, Bill Nas alisema kwamba, dili hilo ni la mkwanja mrefu na hivi karibuni atalifungukia moja kwa moja pale ambapo tangazo alilofanya litaachiwa na wenye nalo.

“Nimepiga dili ambalo nafikiri kwa mashabiki wangu litakuwa ni habari nzuri, sina uhuru wa kulizungumzia tu kwa sababu bado niliofanya nao hawajaliachia, lakini hivi karibuni wataliachia na nitakuwa wazi kusema ni milioni ngapi nimedaka,” alimaliza Bill Nas.

Pam D afunguka kuhusu Ney Wamitego


MWANADADA ambaye anafanya vizuri kwenye gemu la Muziki wa Bongo Fleva, Pamela Daffa ‘Pam D’, amefunguka juu ya skendo ya kujichimbia na mwanamuziki Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ hotelini wakiwa kwenye ziara ya kimuziki katika mikoa mbalimbali hivi karibuni na kudai hazina ukweli.


Akichonga na Showbiz-Xtra kuhusiana na ishu hiyo, Pam D alisema mara nyingi wakiwa na Nay, kila mmoja anakuwa analala kwenye chumba chake na kilichokuwa kimewapeleka kwenye mikoa hiyo ni kazi na wala si kitu kingine.

“Hayo maneno si ya kweli kabisa bhana, mimi nilikuwa ninalala kwenye chumba changu na Nay kwenye chumba chake kwa hiyo hakuna ukweli wowote ule, sisi ni washkaji tu sijui kwa nini watu wamejiaminisha kwamba sisi ni wapenzi,” alisema Pam D.

Audio | Baraka the Prince – Nipe Nguvu | Mp3 Download

Audio | Baraka the Prince – Nipe Nguvu | Mp3 Download
Baraka the Prince - Nipe Nguvu
Audio | Baraka the Prince – Nipe Nguvu | Mp3 Download

DOWNLOAD NOW

Audio | Destiny – Wakata | Mp3 Download

Audio | Destiny – Wakata | Mp3 Download
Destiny - Wakata
Audio | Destiny – Wakata | Mp3 Download


DOWNLOAD NOW

Audio | Centano – Hisia | Mp3 Download

Audio | Centano – Hisia | Mp3 Download
Centano - Hisia
Audio | Centano – Hisia | Mp3 Download

Audio | Gazza ft Madee – Nani | Mp3 Download

Audio | Gazza ft Madee – Nani | Mp3 Download
Gazza ft Madee - Nani
Audio | Gazza ft Madee – Nani | Mp3 Download

DOWNLOAD NOW

Audio | Christian Bella – Shuga Shuga | Mp3 Download

Audio | Christian Bella – Shuga Shuga | Mp3 Download
Christian Bella - Shuga Shuga
Audio | Christian Bella – Shuga Shuga | Mp3 Download

DOWNLOAD NOW

Video | Christian Bella – Shuga Shuga | Mp4 Download

Video | Christian Bella – Shuga Shuga | Mp4 Download
Christian Bella – Shuga Shuga
Video | Christian Bella – Shuga Shuga | Mp4 Download


DOWNLOAD NOW

Video | Shetta Ft G Nako – Vumba | Mp4 Download

Video | Shetta Ft G Nako – Vumba | Mp4 Download
Shetta Ft G Nako - Vumba
Video | Shetta Ft G Nako – Vumba | Mp4 Download



                              DOWNLOAD NOW

Audio | Shetta Ft G Nako – Vumba | Mp3 Download

Audio | Shetta Ft G Nako – Vumba | Mp3 Download
Shetta Ft G Nako - VumbaShetta Ft G Nako - Vumba
Audio | Shetta Ft G Nako – Vumba | Mp3 Download

DOWNLOAD NOW

Audio | Tid ft Rich Mavoko – We Dada | Mp3 Download

Audio | Tid ft Rich Mavoko – We Dada | Mp3 Download
Tid ft Rich Mavoko - We Dada
Audio | Tid ft Rich Mavoko – We Dada | Mp3 Download


MAGAZETI YA LEO 7/12/2017



Mauaji ya halaiki makubwa zaidi kuwahi kutokea duniani



Ukisikia mauaji ya Halaiki (genocide) akili inakimbilia Rwanda , Soweto na Holocaust (waisrael walivyouliwa na WANAZI). Leo tunakupa Mauaji yaliyosahaulika lakini nayo ni makubwa mno.

1. WAJERUMANI WALIVYOSAFISHA KABILA LA WAHERERO.
Baada ya kusikia fununu ya madini Namibia, Wajerumani walikuja na kutawala pwani ya nchi hiyo na kukaa katikati ya kabila la waherero. Kosa kubwa wenyeji walipojifanya wabishi. Walizungukwa pande zote, Upande uliobaki ulikuwa ni jangwa ambalo visima vyote vya maji mjerumani alivitia sumu. Ukimbie unywe maji ya sumu au ufe na kiu jangwani au ukutane na risasi. Asilimia 80 ya wenyeji wote waliuwawa kikatili sana bila huruma.

2. WASOVIETI/USSR WALIPOHAMISHA JAMII NZIMA YA WACHECHNYA.
Kulizuka fununu kuwa Wachechya na Wainguish walikuwa wanawasaliti warusi wenzao vita ya pili ya dunia. Kuwapa adhabu serikali iliamuwa kubeba wote kwenye magari na kuwafukizilia maporini bila kumsamehe hata mmoja. Kila aliyebisha alikutana na Risasi . Wachechnya waliuwawa karibu 50% kutokana na sakata hili lililoitwa “Operation Lentil.”.

3. (HAITI) MAUWAJI YA PARSLEY/EL CORTE AU (KUKATWA).
Ukabila usikie tu redioni. Hii ilikuwa ni vita ya Kikabila, Wadominika walipanga kuwauwa Wahaiti karibu wote nchini mwao chini ya dikteta Rafael Leonidas Trujillo. Njia pekee ya kumtofautisha Mdominika na Muhaiti kwa walioleta utata kuwatambua ilikuwa matamshi ya hili neno "PARSLEY". Wahaiti walikuwa hawawezi kulitamka vizuri kutokana na Lugha yao. Wote walioshindwa waliuwawa kinyama. Kuepusha risasi zisiishe mapema, Hapa ilikuwa ni Mapanga na marungu asubuhi na mchana.

4. (TAIPEI REBELION) CHINA WATU ZAIDI YA 20 MILLION WALIPOTEZA MAISHA.
Hapa ilikuwa ni vita kati ya jamaa aliwaaminisha watu kuwa yeye ni Mdogo wake YESU. Akitawala karibu 1/3 ya nchi yote Hong Xiuquan. Akiongoza jeshi dhaifu kabisa kwa nia ya kuondoa kamali, uonevu, ndoa za wake wengi nk, China ilijikuta chini aya vita vya miaka 10 na kuacha raia zaidi ya 200 million wakifa na mamia kupotea.

5. UTURUKI DHIDI YA WANAVIJIJI WAASI.
Wanakijiji wa eneo la Dersim , walipoleta ubishi kuwa chini ya serikali ya Uturuki badala yake wakang'ang'ania sheria na taratibu zao, Jeshi lilitumwa, Makabila matatu yaliyojisalimisha yaliuliwa wote, Wakina mama na watoto waliokimbilia kwenye Mapango, Yalifunikwa na mawe, moto ukawashwa na wakafa kwa moshi. Inakadiliwa kwa siku moja watu karibu 2 MILLION waliuliwa na wengine kutekwa.

6. DICTETA WAKIRUSI STALIN ALIPOUA MAMILIONI UKRAIN KWA NJAA.
Waukraini walipata upenyo baada ya kuanguka utawala wa Czar Urusi wakataka kujitawala. Jenelali Stalin alipochukua Madaraka akaliona hilo. Pia Vradmil Lenin alikuwa kaishaweka mikakati ya kurudisha maeneo yote. Wao wakambishia na kuendelea na Harakati. Kwanza alikamata wasomi waliokuwa wanahojihoji 5000 na kuwaua wote, Akachukua mashamba ya raia yote. Akawapa adhabu ya njaa hadi nchi nzima isalimu amri kwake. Inasadikiwa kwa sababu ya njaa kila siku watu 2500 walikuwa wanakufa, na walifika watu karibu million 5.

7. MAUAJI YALIYOFANYA NA WAZUNGU DHIDI YA WAMAREKANI ASILIA (WAHINDI WEKUNDU).
Mamilioni ya hawa jamaa waliuliwa bila huruma. Ila hapa tutazaungumzia kabila dogo tu la MOQUI katika mji ulioitwa AWATOVI huko ALIZONA. Wahispania Makasisi walifika wakawalazimisha kuwa wakristo wakagoma. Ikabidi liitwe jeshi, maana wakazi waliwachukia wahispania na wachache waliobadili dini. Wanaume wakiwa kwenye sherehe Walivamiwa na kuuliwa. Wanaume wote. Wanawake na watoto wakachukuliwa mateka. Wakiwa njiani wakabishana wawapeleke wapi, wakaamua kuwaua woote ili kujipunguzia mizigo.

8: JEAN JACQUES DESSALINES ALIPOIGEUZA HAITI KUWA TAIFA LA WATU WEUSI ASILIMIA MIA.
Kile alichoshindwa kinjekitile wa Maji maji Haiti iliwezekana. Mzungu alikimbizwa na watumwa nchi ikapatia uhuru chini ya mkono wa watu weusi. Baada ya kiongozi wa mapinduzi kuuawa aliyemfuatia alipinga idea zake za kuwavumilia wazungu na machotara. Amri ilitolewa Kuua wazungu wote nchi nzima. Hakuishia hapo tu alipita kila mji kuhakikisha agizo linafuatwa. Katika mji mkuu tu wazungu zaidi ya 800 waliuawa kama wanyama na wengine kukimbia. Ilikuwa revenge ya aina yake. Hadi kesho haiti ni nchi ya watu weusi tu asilimia karibu mia kwa baara la Barani Amerika.

9: VITA VYA BIAFRA - NIGERIA.
Tofauti na tanzania tuna makabila mengi yanayopendana, na Nyerere alisaidia kikubwa, Hii haikuwa hivyo Nigeria. Wanamakabila zaidi ya 300 na yalikuwa karibu karibu kilichosababisha ugomvi mara kwa mara.Tatizo lilianza pale Kabila/kundi kubwa la IGBO walipojikatia nchi na kutengeneza nchi yao ya BIAFRA eneo tajiri kwa mafuta. Serikali haraka ikataka kuwarudisha. Kwa mbinu katili kabisa hata kuzuia chakula na maji yasielekee BIAFRA. Inasemekana kila siku walikuwa wanakufa watu zaidi ya 5000 wengi wao IGBO. Watu zaidi ya Milioni 3 walikufa hadi vita kuisha.