Sunday, 26 November 2017

Rais Magufuli aibua mapya bandarini


Magari 50 ambayo mwenyewe hajajulikana yamekamatwa bandarini na Rais Magufuli alipofanya ziara bandarini hapo, akitokea kwenye meli ya madaktari bingwa kutoka China.

Magari hayo amabyo yameelezwa kuletwa mwezi wa 6 mwaka 2015 yakiwa na magari ya jeshi la polisi, mpaka leo hayajatolewa bandarini hapo, yameelezwa kuwa na siri kuba ambayo Rais mwenyewe anaifahamu, huku mizgo wa lawama ukienda kwa Jeshi la Polisi.

“Inakuwaje rais nipate taarifa za magari kufichwa lakini Waziri, TRA, TPA msijuie? Mnatakiwa muwe na informer wenu sio hadi mimi nije ndo mnaaza kusema sijui. Nafahamu hata mletaji namfahamu, nataka mniletee ninyi ili nione kama tunaenda uelekeo mmoja au hatuendi", amesema Rais Magufli.

Raius Magufuli ameendelea kwa kusema ..."Kule Polisi kuna mambo ya hovyo. Polisi Mnadai hizi gari ni zenu, kwanini hamzifuatilii tangu 2015? Kuna magari yamekaa miaka 10 lakini sheria inasema gari likikaa zaidi ya siku 21 yapigwe Mnada, kwanini hampigi mnada? IGP kwenye Majambazi upo safi lakini huku kwenye Ufisadi bado sana. Kama mtu anakunanihii mtwange. Nilikuchagua ulikua such good guy lakini unaniangusha. Polisi kuna Uchafu mwingi sana".

Kufuatia tukio hilo Rais Magufuli ametoa siku saba kwa TAKUKURU, Polisi na Wizara ya Uchukuzi kumpatia taarifa kamili juu ya magari hayio, ambayo mpaka sasa mmiliki wake hajajulikana.

Waziri Mhagama aiagiza Halmashauri ya Bahi kukamilisha Ujenzi wa Soko la Kigwe


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Bahi kuhakikisha inamaliza ujenzi wa soko la Kigwe kwa kuhakikisha wanajenga vyoo na vibanda vidogo vitakavyo saidia soko hilo lililojengwa na Programu ya Miundo Mbinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF).

Ameyasema hayo alipofanya ziara yake Wilayani Bahi Novemba 21, 2017 kwa lengo la kujionea namna uboreshaji wa soko hilo ambalo tayari limekamilika kwa asilimia 90 na kukabiliwa na changamoto za vibanda na vyoo vya kudumu.

“Ninaiagiza Halmashauri hii kuhakikisha inaleta timu ya wataalamu kupima viwanja na kuvigawa kwa wananchi pamoja na kumalizia ujenzi wa Vyoo vya soko ili lianzae utekelezaji wake haraka na kuhakikisha umeme unafungwa ndani ya soko hili”.

Kwa upande wake Mbunge wa Bahi Mhe. Omary Badwel alieleza ujenzi wa soko ni jambo ja muhimu linalogusa wanakigwe wote kwani tangu enzi za mkoloni kumekuwa na changamoto ya soko na kuwataka wananchi kulitunza na kuhakikisha linakuwa msaada kwao wote.

“Soko hili toka utawala wa mkoloni kulikuwa na soko bovu hivyo hatua ya kulikamilisha litavutia wengi na kukuza uchumi wa wana Kigwe wote.”Alisisistiza Badwel

Alichokifanya Kassim Mganga kwa Vanessa Mdee jukwaani

Alichokifanya Kassim Mganga kwa Vanessa Mdee jukwaani



FiestaDar2017: AliKiba na Ommy Dimpoz walivyowasha moto Fiesta

FiestaDar2017: AliKiba na Ommy Dimpoz walivyowasha moto Fiesta



FiestaDar2017: Aslay awashika pabaya mashabiki wake



FiestaDar2017: Aslay awashika pabaya mashabiki wake


Audio | Single Sally – Asuu | Mp3 Download

Audio | Single Sally – Asuu | Mp3 Download

Single Sally - Asuu

Audio | Single Sally – Asuu | Mp3 Download



                 DOWNLOAD HERE

Audio | Crazy Ninja – Komaa Na Mziki | Mp3 Download

Audio | Crazy Ninja – Komaa Na Mziki | Mp3 Download


Crazy Ninja - Komaa Na Mziki

Audio | Crazy Ninja – Komaa Na Mziki | Mp3 Download







                                                DOWNLOAD HERE

Video | Stino Ft Beka Flavour – Shokamoo Pesa | Mp4 Download

Video | Stino Ft Beka Flavour – Shokamoo Pesa | Mp4 Download

Stino Ft Beka Flavour - Shokamoo

Video | Stino Ft Beka Flavour – Shokamoo Pesa | Mp4 Download


                                                  DOWNLOAD

Singeli Audio | Mc Sudy Ft S Kide – Usitoe Mimba | Mp3 Download

Singeli Audio | Mc Sudy Ft S Kide – Usitoe Mimba | Mp3 Download

Mc Sudy Ft S Kide – Usitoe Mimba

Singeli | Mc Sudy Ft S Kide – Usitoe Mimba | Mp3 Download



                                                       DOWNLOAD HERE

Audio | Harrysong Ft Patoranking & Seyi Shay – Confession | Mp3 Download

Audio | Harrysong Ft Patoranking & Seyi Shay – Confession | Mp3 Download

Harrysong Ft Patoranking & Seyi Shay - Confession

Audio | Harrysong Ft Patoranking & Seyi Shay – Confession | Mp3 Download


                                           DOWNLOAD HERE

NEC yaomba amani itawale



Dar ,Mikoani. Tume ya Taifa ya Uchaguzi  (NEC) imevitaka vyama vya siasa kuhakikisha kuwa uchaguzi mdogo wa madiwani utakaofanyika leo Jumapili Novemba 26 unafanyika kwa amani na utulivu.

Akisoma risala kwa umma  jijini Arusha  Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage amesema kuwa wapigakura wapatao 333,309 wanatarajiwa kupiga kura.

Amesema uchaguzi huo utakaofanyika katika kata 43 za Tanzania Bara, utakuwa na  vituo 884  ambako ndipo wapigakura wamejiandikishia kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa Rais, wabunge na madiwani wa mwaka 2015.

Juzi Mkuu wa Jeshi la Polisi(IGP), Simon Sirro alisisitiza amani kipindi hiki cha uchaguzi kauli ambayo imeungwa mkono na makamanda wote wa polisi mikoani.

Leo Jumapili asubuhi wananchi wamejitokeza katika kutetea haki zao za kikatiba za kuwachagua viongozi wanaowataka.

"Wananchi wote wasitarajie vurugu zozote na kama zikitokea,wahusika watachukuliwa hatua stahili za kisheria," amesema  IGP Sirro.

Amesema  kwamba jeshi hilo lipo tayari kukabiliana na yeyote atakayejaribu kuvuruga amani na wala halitajali nafasi wala jina la mtu kwenye kuchukua hatua.

Mwananchi:

Yanga yamsajili beki Mkongo




KLABU ya Yanga jana imemsainisha mkataba wa miaka miwili, beki wa kati, Mkongo Fiston 'Festo' Kayembe Kanku ambaye alikuwa kwenye majaribio katika timu hiyo kwa muda mrefu.

Usajili huo unakuja siku moja baada ya safu ya ulinzi ya Yanga kuruhusu bao la tano katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jana wakilazimishwa sare ya 1-1 na Tanzania Prisons Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Usajili wa Kayembe unazima kabisa uwezekano wa beki Mtogo, Voncent Bossou kurejeshwa Jangwani, licha ya kupigiwa debe na wadau mbalimbali wa klabu hiyo, arejeshwe kikosini.

Bossou alimaliza mkataba wake msimu uliopita baada ya kuitumikia Yanga kwa miaka miwili alitarajiwa kuendelea kutokana na kufanya vizuri, lakini klabu haikumpa mkataba mpya baada ya mazungumzo ya muda mrefu.

IlifikiRIwa hali mbaya ya kiuchumi ilisababisha Yanga kumwaka kumpa mkataba mpya Bossou, lakini kitendo cha klabu kumsajili Kayembe anayetokea Balende FC ya kwao, Jamhuri ya Kidemkrasia ya Kongo (DRC) kinaashiria imeamua kuachana na Mtogo huyo kwa vyovyote.

Licha ya kucheza pungufu ya mchezaji mmoja, Tanzania Prisons imefanikiwa kupata sare ya ugenini ya kufungana 1-1 na wenyeji, Yanga SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliofanyika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Sare hiyo inaifanya Yanga SC iendelee kukamata nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu, nyuma ya Simba na Azam ambazo pia zina mechi moja moja mkononi.

Katika mchezo huo uliochezeshwa na Shomary Lawi wa Kigoma aliyesaidiwa na Abdallah Rashid wa Pwani na Sylvester Mwanga wa Kilimanjaro, hadi mapumziko tayari timu hizo zilikuwa zimekwishafungana mabao hayo.

Prisons walitangulia kwa  bao la Eliuter Mpepo dakika ya tisa akitumia makosa ya mabeki wa kati wa Yanga, Andrew Vincent ‘Dante’ na Nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’ waliochanganyana na kipa wao, Mcameroon, Youth Rostande na kushindwa kuokoa.

Prisons walipata pigo dakika ya 36 baada ya mchezaji wake, Lambert Sibiyanka kutolewa kwa kadinyekundu na refa Lawi kufuatia kumpiga kiwiko beki wa Yanga, Juma Abdul.

Yanga walitumia mwanya huo kuongeza mashambulizi kusaka bao la kusawazisha na wakafanikiwa kupata bao dakika ya 41, lililofungwa na kiungo Raphael Daudi aliyemalizia krosi ya mshambuliaji Ibrahim Ajib.

Kwa sare hiyo, Yanga inabaki na pointi zake 20 baada ya kucheza mechi 12, ikizidiwa pointi mbili mbili na zote, Simba na Azam. Simba watawakaribisha Lipuli ya Iringa Uwanja wa Uhuru kesho na Azam watakuwa wenyeji wa Mtibwa Sugar Chamazi Jumatatu.  

Bondia Ibrahim Class atetea taji La GBC




 BONDIA Mtanzania, Ibrahim Class Mgendera usiku wa kumkia leo amefanikiwa kutetea taji lake GBC uzito wa Light baada ya kumshinda kwa pointi Koos Sibiya wa Afrika Kusini.

Mgendera alishinda kwa pointi za majaji wote, ingawa ushindi wake ulilalamikiwa na mpinzani wake baada ya pambano hilo.

Haukuwa ushindi wa mashaka, kwani Mgendera alipigana vizuri kwa tahadhari kuanzia raundi ya kwanza hadi ya 10 akipiga ngumi za kudonoa kwa wingi katika staili yake ya Orthodox.

Mgendera hakuwa na kazi nyepesi ulingoni, kwani alikutana na bondia mzoefu na mwenye ngumi nzito – lakini akahimili vishindo vyote na kuwafurahisha Watanzania wachache waliojitokeza Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kumshangilia kwa mchezo mzuri.

Dalili za Mgendera kushinda pambano hilo zilianza kuonekana raundi ya nane baada ya kumjeruhi kwenye pua Sibiya ambaye alichafuka damu eneo hilo hadi mdomoni.

Na ni kuanzia raundi hiyo bondia wa Tanzania alianza kutawala pambano baada ya wawili hao kuonekana kupigana sawa katika raundi zilizotangulia. 

Mgendera aliyezaliwa Oktoba 10, mwaka 1990 eneo la Ipogolo, wilayani Mufundi mkoani Iringa, alitwaa taji hilo Julai 1, mwaka huu baada ya kumpiga Jose Luis Forero Atencio wa Panama kwa pointi Jijini Berlin, Ujerumani. 

Hilo linakuwa pambano la 21 Mgendera kushinda kati ya 25 aliyocheza, akiwa amepoteza mapambano manne.