Saturday, 25 November 2017

Wastara ateswa na macho yake




STAA wa filamu za Kibongo, Wastara Juma ameibuka na kueleza jinsi macho yake yanavyomtesa kwani watu wamekuwa wakimsema vibaya kuwa anajilegeza makusudi akitaka kutupia picha mtandaoni.

Akipiga stori na Risasi Jumamosi,Wastara alisema kuwa macho yake ndivyo yalivyo kwani amezaliwa hivyo ni macho yaliyolegea kama mtu mwenye usingizi wakati wote na kutokana na vichambo anavyovipata amejikuta akitamani kuhama Insta lakini hawezi kwa sababu ana manufaa na page yake.

“Jamani haya macho yananitesa kwani kutwa kucha natukanwa mitandaoni kuwa nalegeza macho hawajui kuwa nimeumbwa hivi kwani hata nikijitahidi kuyafanya yawe magumu nashindwa, hivyo watu wakisema najifanyisha huwa najisikia vibaya kusema ukweli,” alisema Wastara.

Baada ya kimya kirefu, Jokate afunguka kuhusu Lulu



MWANAMITINDO Jokate Mwegelo hivi karibuni baada ya kukaa kimya bila kumposti msanii mwenzake Elizabeth Michael ‘Lulu’ wala kuongea lolote kuhusiana na hukumu yake ambapo mastaa kibao walionesha kumuhurumia na k
umposti kwa kuweka maneno tofauti tofauti, yeye ameibuka na kusema kuwa anamuombea dua huko alikoenda kwani ndio jambo pekee ambalo anaweza kulifanya.

Akilonga na Risasi Jumamosi, Jokate alisema kuwa yeye anamuombea dua Lulu Mungu amfanyie wepesi huko alikokwenda kwani ndio njia pekee ya kumfariji.

Mwanamitindo huyo aliongea hayo baada ya kuulizwa sababu ya yeye kutomposti na maoni yake juu ya hukumu hiyo. “Kikubwa ni kumuombea na mimi namuombea ndicho ninachoweza kusema,” alisema Jokate.




Sikutarajia Dk Slaa kuwa balozi - Profesa Lipumba



   Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama cha CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amezungumzia uteuzi wa Dk Wilbroad Slaa kuwa balozi akisema hakutarajia.

Rais John Magufuli juzi alimteua Dk Slaa aliyewahi kuwa katibu mkuu wa Chadema kabla ya kukihama chama hicho wakati wa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Wakati wa mchakato wa uchaguzi huo, Profesa Lipumba na Dk Slaa ambao vyama vyao vilikuwa katika umoja uliojulikana Ukawa, walijiondoa baada ya Chadema kumpitisha Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kuwa mgombea wake wa urais.

Akizungumza na Mwananchi jana, Profesa Lipumba alisema, “Imekuwa kama surprise, sikutegemea kama Dk Slaa atateuliwa kwa sababu muda mwingi yupo Canada.”

Hata hivyo, Profesa Lipumba alisema hana shaka na uteuzi huo kwa kuwa Dk Slaa ni mzoefu wa siasa na mzalendo ambaye ataitumikia vyema nafasi hiyo mpya.

“Narudia, sikutegemea. Ila popote atakapopangiwa kazi Dk Slaa atafanya kwa sababu najua ni mchapakazi,” alisema.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema Rais Magufuli ana mamlaka kisheria ya kumteua mtu atakayemuona anafaa katika nafasi fulani.

“Huu ni uamuzi wa Rais sisi wengine hatuna comments zaidi ya kuwatakia kila heri katika utendaji wao wa kazi,” alisema Mbowe ambaye pia ni mbunge wa Hai mkoa wa Kilimanjaro.

Akizungumza uteuzi huo wa Dk Slaa, Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Profesa Abdallah Safari alisema Rais Magufuli amemuonea huruma Dk Slaa ndiyo maana akaamua kumpa nafasi ya ubalozi.

Profesa Safari alisema hawezi kumsema vibaya Dk Slaa lakini nafasi hiyo ni huruma na zawadi ya Rais Magufuli.

Amedai Dk Slaa alijaribu kuivuruga Chadema wakati wa uchaguzi mkuu mwaka 2015 lakini hakufanikiwa.

“ Hii ni huruma. Siku zilizopita Dk Slaa aliandikwa katika vyombo vya habari kuwa anafanya kazi Super Market. Mimi nimekaa Ulaya najua maisha ya kule na Dk Slaa ni rafiki yangu sana lakini kwa kitendo alichokifanya mwaka juzi, haya ndiyo matokeo yake,” alisema Profesa Safari.

Kwa upande wake, aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Urusi kuanzia mwaka 2002 hadi 2008, Patrick Chokala alimpongeza Rais Magufuli kwa kumteua Dk Slaa kuwa balozi.

“Sina shaka hata kidogo na Dk Slaa ana uwezo wa kufanya kazi nchi yoyote. Hii kazi anaiweza na ni mtu mwenye dhamira ya kweli,” alisema Balozi Chokala.

Alisema anamfahamu Dk Slaa kwa kipindi kirefu tangu akiwa padre na kwamba, amekuwa ni mchapakazi hodari na mwenye hekima kwa watu.

Akizungumza na kituo cha televisheni cha Azam TV, Dk Slaa alimshukuru Rais Magufuli kwa kumteua ili aungane naye kujenga nchi na hivyo atafanya kazi kwa uwezo wake wote.

Dk Slaa ambaye hivi sasa anaishi Canada alisema, “Ni mapenzi ya Mungu, nashukuru kwa uteuzi. Ninachoweza kusema katika hatua hii, huu ni wajibu mkubwa kwenye kipindi cha kulijenga Taifa letu.”    

Mwananchi:

Wema Sepetu asema ameirudisha heshima ya Bongo Movie

Wema Sepetu asema ameirudisha heshima ya Bongo Movie


Msanii wa filamu nchini Tanzania, Mrembo Wema Sepetu ambaye yupo nchini Rwanda tangu Jumatano ya wiki hii, amesema ndiye aliyeifufua tasnia ya Bongo Movie iliyokufa baada ya kifo cha Kanumba.

Wema amesema marehemu Kanumba alipofariki  hata kiwanda cha Bongo Movie kilionekana kuyumba kwani alikuwa ndiye nguzo muhimu kwenye ramani ya filamu Tanzania.

“Zamani Bongo Movie ilikuwa inafanya vizuri sana enzi za marehemu Steven Kanumba, alivyofariki kama na yenyewe ikafa. Tumekuwa tukiomboleza kifo chake na kifo chake kimetusababishia mazingira mabaya sisi kama waigizaji  kwa sababu tuko kwenye fani moja. Wengi wetu tumejikuta watu wanaona Bongo Movie haina mashiko.“amesema Wema Sepetu kwenye mkutano na Waandishi wa Habari jijini Kigali nchini Rwanda na kuelezea jinsi alivyoinyanyua Bongo Movie baada ya kifo cha Kanumba.

“Kwa bahati nzuri mimi nimeweza kuirudisha tena Bongo Movie back to where it was (ilipokuwa enzi za Kanumba) baada ya kutoa filamu yangu ya Heaven Sent. Bongo Movie kama Bongo Movie zilikuwa zimelala kiukweli kabisa mpaka nilipozindua filamu yangu hiyo na nimeweza kuiweka kwenye application yangu kumekuwa kuna muhemko, yaani waigizaji wengi hata mkiwaona kwenye mitandao ya kijamii wanashoot, wanafanya vipindi, yaani Bongo Movie haijafa ni kazi nzuri tu tumeshindwa kuziweka sokoni. Tukiwa tuna kazi nzuri tukafanya vitu ambavyo vitapendwa na watu Bongo Movie itakuwa imara tena Inshallah!“.

Steven Charles Kanumba almaarufu The Great alifariki katika mazingira ya kutatanisha mnamo mwezi Aprili 2012 akiwa chumbani kwake na mpenzi wake Elisabeth Michael ‘Lulu’ ambaye mwezi huu amehukumiwa kifungo cha miaka miwili jela kwa kosa la kumuua Kanumba bila kukusudia.

Waziri Kigwangalla awajibu wanaosema vyuma vimekaza




Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Hamisi Kigwangalla amesema maisha yataendelea kuwa magumu kwa watu wasio na shughuli maalum ambao wamezoea kuishi kwa ujanja ujanja.

Ameyasema hayo wakai akijibu maswali ya wananchi kupitia mtandao wa ‘Twitter’ ambao wengi walitaka kujua kuhusu utendaji kazi wake na hali halisi ya maisha yalivyo wakidai kuwa ni magumu.

“Wanaofanya shughuli zao halali hawatoona vyuma vimekaza, badala yake watafurahia sema watoto wa mjini, wasanii sanii na wajanja wajanja ndiyo watapata shida! Hawa wajanja wajanja ni wangapi? Na wenye shughuli halali ni wangapi?”, alisema Kigwangalla akiacha maswali kwa mmoja wa watu waliomuuliza.

Waziri Kigwangalla aliendelea kwa kutoa ufafanuzi juu ya namna ya kujenga uchumi kupitia kufanya kazi na sio kutegemea kupata pesa kwa njia rahisi rahisi.

“Mfumo wa uchumi unataka watu tufanye kazi kwa ubunifu ndipo tupate maisha mazuri siyo kufanya usanii kidogo tayari ukatajirika! Kukaza vyuma maana yake kuziba mianya ya wasanii ili walio kwenye uchumi halisi na wasanii wawe sawa siyo kuonea watu!” alimaliza.

Waziri Kigwangalla hivi sasa yupo jimboni kwake Nzega vijijini akiwa amepiga kambi kwaajili ya kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata ya Nata.

Audio | Stino Ft Beka Flavour – Shikamoo Pesa | Mp3 Download

Audio | Stino Ft Beka Flavour – Shikamoo Pesa | Mp3 Download

Audio | Stino Ft Beka Flavour – Shikamoo Pesa | Mp3 Download



                                                   DOWNLOAD HERE

Audio | Flavour – Turn by Turn | Mp3 Download

Audio | Flavour – Turn by Turn | Mp3 Download


Flavour – Turn by Turn

Audio | Flavour – Turn by Turn | Mp3 Download



                                            DOWNLOAD HERE.



Video | Beka Flavour – Sarafina | Mp4 Download

Video | Beka Flavour – Sarafina | Mp4 Download

Video | Beka Flavour – Sarafina | Mp4 Download



Audio Gospel | Precious P.I – Shikilia | Mp3 Download

                         
Precious P.I – Shikilia




             https://cloudup.com/files/iNyhsBVNj49/download

                                                               

MAGAZETI YA LEO 25/11/2017

MAGAZETI YA LEO 25/11/2017


MAGAZETI LIVE: Vurugu zatawala, Lipumba ashamgaa Dr. Slaa kuteuliwa Balozi


Davido - Like Dat (Official Video)


Stino Ft Beka Flavour Pesa Hajizclassictz com