Monday, 20 November 2017

Aliyeongoza mauaji ya kiitikadi Marekani Charles Manson amefariki jela


Kiongozi wa kikundi chenye itikadi kali za imani Charles Manson - ambaye aliongoza mauaji ya kikatili miaka ya 1960 - amefariki dunia katika jimbo la California baada ya kuwa gerezani kwa zaidi ya miongo minne .

Alikuwa na umri wa miaka 83.

Mwezi Agosti 1969 wafuasi wa kundi lake waliwauwa watu saba, akiwemo mcheza filamu wa Hollywood actress Sharon Tate, ambaye alikuwa akitarajia kupata mtoto na mumewe mwongozaji wa filamu Roman Polanski.

Waandamana tena Marekani kupinga mauaji

Maadhimisho ya mauaji ya mweusi Marekani

Kwa Picha: Mauaji Las Vegas, Marekani

Manson alihukumiwa kifo mwaka 1971, lakini kifungo chake kilibadilishwa na kuwa cha maisha jela.

Aliamuini mauaji hayo yangeanzisha vita vya kijamii na hivyo kumuwezesha kuchukua mamlaka.
Manson alilazwa katika hospitali ya Bakersfield iliyoko California mapema mwezi huu na baadae akafa kifo cha kawaida Jumapili.

Mmoja wa wafuasi wa Manson, Susan Atkins, alimdunga kisu Tate hadi kufa na kuuburuza mwili wake uliokuwa ukichuruzika damu hadi mbele ya mlango wa nyumba ya mchezaji filamu huyo.

Wengine wanne waliokuwa nyumbani kwa Tate waliuliwa kinyama kwa kuchomwa visu.

Siku iliyofuatia, matajiri wawili wa Los Angeles- mke na mume , Leno na Rosemary LaBianca, pia waliuliwa na wafuasi wake.

Mauaji hayo yalitambuliwa kwa ujumla kama mauaji ya Tate-LaBianca.

Katika tukio jingine tofauti Donald Shea, mchezaji filamu mwingine wa Hollywood , na Gary Hinman, pia waliuliwa na wajumbe wa familia ya Manson.

Manson hakuwepo kwenye tukio la mauaji, lakini alipatikana na hatia ya kuongoza mauaji ya wafuasi wake katika mauaji yote saba.
Alihukumiwa mwaka 1971.



Mkenya ashinda taji la malkia wa urembo Afrika



Shindano la malkia wa urembo duniani la 2017 lilikamilika mjini Sanya China siku ya Jumamosi huku Mkenya Magline Jeruto akishinda taji la malkia wa urembo barani Afrika.

Hatua hiyo inajiri baada ya mwanadada huyo kutoka eneo la Elgeyo Marakwet nchini Kenya kuchukua nafasi ya tano.

Taji la malkia wa urembo duniani lilichukuliwa na mwanadada wa India Manushi Chhillar.

Andrea Meza wa Mexico alichukuwa nafasi ya pili akifuatiwa na Muingereza Stephanie Hill huku naye Aurore Kichenin wa Ufaransa akishinda nafasi ya nne.




Magline Jeruto ambaye ndiye malkia wa urembo wa Elgeyo Marakwet alichukua nafasi ya tano miongoni mwa wagombea 118 katika shindano la malkia mrembo dunia.

Mwanadada mwengine wa Afrika ambaye aliorodheshwa katika nafasi kumi bora ni Ade van Heerden wa Afrika Kusini ambaye alimaliza katika nafasi ya tisa.

Mahakama ya Kenya yafanya uamuzi huu



Mahakama ya Juu nchini Kenya imetupilia mbali kesi zilizofunguliwa na wafuasi wa NASA za kupinga ushindi wa Urais wa Uhuru Kenyatta, kwenye uchaguzi wa marudio wa Oktoba 26, 2017

Kesi hiyo ambayo ilikuwa moja kwa moja kwenye vyombo vya habari, iliongozwa na majaji 6 akiwemo Jaji Mkuu David Maraga, na kutoa uamuzi kuwa Uhuru Kenyatta ni mshindi halali wa uchaguzi wa Oktoba 26.

Kufuatia uamuzi huo wa mahakama ya Juu nchini Kenya, Uhuru Kenyatta anatarajiwa kuapishwa wiki ijayo, na kuwa Rais wa Jamhuri ya Kenya kwa muhula wa pili.

Ikumbukwe uchaguzi wa marudio ulifanyika baada ya Mahakama ya Juu kufuta matokeo ya Urais ya uchaguzi wa kwanza wa Agosti 8, 2017 na kutaka urudiwe mara ya pili.

Upimaji afya waibua msongamano




 Upimaji afya bure unaofanywa na madaktari kutoka China katika Bandari ya Dar es Salaam umesababisha foleni kwa watumiaji wa barabara.

Upimaji wa afya unafanyika kwenye meli iliyotia nanga katika Bandari ya Dar es Salaam.

Katika Barabara ya Kilwa, magari yanayoelekea Posta na Gerezani yamekuwa yakitembea mwendo wa taratibu na kusimama kwa takriban kwa dakika 20 kabla ya kusogea.

Kondakta wa daladala linalofanya safari kati ya Mbagala Rangi Tatu na Stesheni, Yasin Yusuph amesema leo Jumatatu Novemba 20 kuwa wametumia zaidi ya saa mbili kwa safari.

"Sisi tumetoka Mbagala saa 1:30 hadi sasa saa 3:40 hatujafika na mwendo ni huuhuu unaouona wa taratibu. Magari yakishasimama unasahau. Tatizo ni kuwa hakuna utaratibu maalumu, watu wamejaa kila sehemu na wanaruhusu magari njia mbili," amesema Yusuph.

Amesema ni vyema lingetafutwa eneo kubwa ambalo watu wanaweza kukaa na kusubiri huduma badala ya kusimamishwa pembezoni mwa barabara.

"Watu ni wengi, eneo la kupumzika hakuna. Hapa hakuna miti ya kutosha jua likiwa kali litawachoma," amesema.

Mtoto wa Rais Mugabe amkingia kifua baba yake



Mtoto wa Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe na mkewe Grace, Chatunga Bellarmine Mugabe amemsifu baba yake na kukitukana chama cha Zanu-PF.


Rais Robert Mugabe akiwa na mkewe Grace pamoja na mtoto wao wa tatu Chatunga

Mtoto huyo ambaye ni watatu katika familia ya Rais huyo ametoa maneno hayo kupitia mtandao wake wa Facebook kwa kukiambia chama hiko kuwa hakiwezi kufanya lolote bila Rais Mugabe.

Kupitia mtandao huo, Chatunga ameandika:

“You can’t fire a Revolutionary leader ! Zanu Pf is nothing without President Mugabe ✊ Gushungo will always remain the champion of champions! Proud of you Gushungo Proud of Dad. Gushungo always and forever to death✊ People like Wellence Mujuru celebrate and march became of Jealous and ruchiva acting as if he cares for the people and unnecessary attacks !

We all grow up in life and take up our responsibility to serve our country. We all have a responsibility to keep this country safe and guard our sovereignty. God bless all who sacrifice for our nation Zimbabwe

Chama cha Zanu-PF kimemtaka Mugabe kujiuzulu Urais wa nchi hiyo mpaka kufikia leo mchana.

Nafasi za kazi leo November 20

Huu ndio muonekano mpya wa Dkt Shika

Huu ndio muonekano mpya wa Dkt Shika

Maisha ya Dk Louis Shika ambaye hivi karibuni aliingia kwenye headline baada ya kushindwa kutoa asilimia 25 ya mnada wa nyumba za Lugumi muda mchache baada ya kushinda mnada huo, yameanza kubadilika taratibu kutokana na kupata deal kadhaa za matangazo.

DK Shika ambaye alikuwa katika muonekano ambao haufananii na utajiri anaoutangaza kuwa nao, weekend hii ameonekana akiwa amevaa suti kali.

Wadau wa mambo wanadai kuwa mzee huyo mashuhuri mitandaoni amepata deal kubwa katika kampuni moja kubwa la michezo ya kubashiri.

Huwenda akapata deal nyingi zaidi kutoka na umaarufu alionao kwa sasa

Kala Jeremiah ataka kufanya kazi na Dk Shika



Msanii wa muziki wa Hip Hop, Kala Jeremiah amedai atafanya jitihada za kumtafuta Dk Louis Shika ili apate madini kutoka kwa mzee huyo ambaye anadaiwa kuwa  ni msomi wa udaktari.

Akimzungumzia 'tajiri mtata' , Kala alisema mzee huyo anaonekana kuwa ni msomi mkubwa na tayari ana mambo mengi amejifunza akiwa nje ya nchi alipokuwa alisoma na kufanya kazi enzi za ujana wake.

“Binafsi nitamtafuta kwaajili ya kujifunza, yule ni mzee mwenye mambo mengi, aliyopitia, ni mafunzo tosha kwa vijana kama mimi na wengine. Kwahiyo nitamtafuta ili nijifunze,” alisema Kala.

Kala alidai kwa kuwa nyimbo zake ni za kijamii zaidi, ataangalia uwezekano wa kumtumia katika baadhi ya project zake kama akipata nafasi.

Pia rapa huyo aliitaka serikali kumtumia mzee huyo katika Tanzania ya Viwanda kwa kuwa anaonekana ana mambo mengi ambayo anayafahamu.

Dk Louis Shika hivi karibuni aliingia kwenye headline baada ya kushindwa kutoa asilimia 25 ya mnada wa nyumba za Lugumi muda mchache baada ya kushinda mnada huo na kudai pesa zake zipo Urusi.

Mtoto wa Rais Mugabe amkingia kifua baba yake na kuitukana Zanu-PF



Rais Robert Mugabe akiwa na mkewe Grace pamoja na mtoto wao wa tatu Chatunga

Mtoto wa Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe na mkewe Grace, Chatunga Bellarmine Mugabe amemsifu baba yake na kukitukana chama cha Zanu-PF.

Mtoto huyo ambaye ni watatu katika familia ya Rais huyo ametoa maneno hayo kupitia mtandao wake wa Facebook kwa kukiambia chama hiko kuwa hakiwezi kufanya lolote bila Rais Mugabe. Kupitia mtandao huo, Chatunga ameandika:

“You can’t fire a Revolutionary leader ! Zanu Pf is nothing without President Mugabe ✊ Gushungo will always remain the champion of champions! Proud of you Gushungo Proud of Dad. Gushungo always and forever to death✊ People like Wellence Mujuru celebrate and march became of Jealous and ruchiva acting as if he cares for the people and unnecessary attacks !
We all grow up in life and take up our responsibility to serve our country. We all have a responsibility to keep this country safe and guard our sovereignty. God bless all who sacrifice for our nation Zimbabwe

Chama cha Zanu-PF kimemtaka Mugabe kujiuzulu Urais wa nchi hiyo mpaka kufikia leo mchana.

Mahakama ya Kenya kuamua juu ya kesi ya urais leo

Jaji Mkuu wa Mahakama ya juu zaidi nchini kenya David Maraga

Mahakama ya juu zaidi nchini Kenya Jumatatu inatarajiwa kutoa uamuzi katika kesi zilizowasilishwa kwenye mahakama hiyo kupinga uchaguzi wa marudio wa tarehe 26 Oktoba ambapo rais wa sasa Uhuru Kenyatta alitangazwa kama mshindi.

Katika Kesi majaji watatakiwa kutoa uamuzi kuhusu masuala yafuatayo:

Wataamua iwapo tume huru ya taifa ya chaguzi na mipaka (IEBC ) ilifaa kuteuwa upya wagombea urais au la.

Uamuzi pia utatolewa na mahakama hiyo juu zaidi juu ya ya ikiwa kujiondoa kwenye uchaguzi huo kwa kiongozi Muungano wa upinzani Raila Odinga na Makamu wake Kalonzo Musyoka kuliathiri uchaguzi huo.

Majaji pia watatoa uamuzi kuhusu ikiwa baada ya tume ya IEBC kushindwa kuendesha uchaguzi katika ameneo bunge 25 kati ya 290 kunahalalisha ama kubatilisha matokeo ya uchaguzi.

Aidha Mahakama hiyo itawaeleza waKenya ikiwa tume ya uchaguzi (IEBC) ilikuwa na uwezo wa kuandaa uchaguzi wa haki na huru baada ya kugubikwa na mgawanyiko miongoni mwa wajumbe wake.

Kwa upande mwingine Wakenya watasubiri kusikia uamuzi wa mahakama kuhusu kama ghasia zilizotokea kabla na baada ya uchaguzi wa marudio wa urais ziliathiri ama hazikuathiri matokeo ya uchaguzi na kuufanya kuwa usio wa haki na huru au la.

Mahakama itatoa ufafanuzi juu ya dosari ya karatasi za kupigia kura, maarufu kama form 34A ziliathiri matokeo ya uchaguzi.

Hukumu hii inasubiriwa kwa shauku kubwa na raia wa Kenya pamoja na kwingineko duniani, huku wengio wakijiuliza hatma ya Kenya.

Tangu kufanyika kwa uchaguzi wa marudio wa urais tarehe 26 Oktoba, baadhi ya miji mikuu nchini Kenya ukiwemo mji mkuu Nairobi, pamoja na mji wa magharibi wa Kisumu imekuwa ikikumbwa na ghasia za maandamano ambazo zilizosababisha mauaji ya watu na wengine kujeruhiwa.

Kansela Merkel awekwa njia panda



Mazungumzo kuunda serikali ya mseto nchini Ujerumani yamevunjika, hali ambayo inaweka njia panda mstakabali wa Kansela Angela Merkel.

Baada ya wiki nane ya majadiliano chama chenye mrengo wa kati cha Centrist Free Democrats -FDP- kimejitoa kikilalamikia tofauti zisizoweza kusuluhishwa na chama cha Merkel cha Christian Democrats na vyama vingine katika mazungumzo.

Baadaye leo bibi Merkel atakutana na Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier, ambaye ndiye mwenye nguvu kuitisha uchaguzi mpya.

Bibi Merkel ameonya kuwepo kwa magumu katika wiki zijazo, Kiuhalisia makubaliano9 ya muungano huo yanawezekana lakini bado haijawa wazi iwapo kuna uwezekano wowote washiriki kufanya umuhimu wa kupata suluhu

Waliolipukiwa na bomu wapata tatizo la kuona


Ikiwa ni siku moja baada ya mlipuko wa bomu uliotokea Shule ya Msingi Kihinga mkoani Kagera, majeruhi wawili wamerejeshwa hospitali baada ya kupata tatizo la kuona.

Watoto hao wawili ni miongoni mwa majeruhi 43, akiwemo mwalimu, wa mlipuko wa bomu uliotokea Novemba 8 na kuua wanafunzi watano baada ya mmoja wao kuliokota na kwenda nalo shuleni akidhani kuwa ni chuma chakavu ambacho angekiuza.

Mganga mkuu wa Hospitali ya Misheni ya Rulenge, Dk Mariagoreth Frederick alisema jana kuwa watoto hao waliruhusiwa kurejea nyumbani Novemba 10 na walirejeshwa Novemba 14 kutokana na kuathirika machoni.

Aliwataja watoto hao kuwa ni Irene Sherehe na Domina Wabandi (10).

Dk Mariagoreth alisema Domina anafanyiwa utaratibu na Halmashauri ya Wilaya ya Ngara ili apelekwe Hospitali ya Rufaa ya KCMC ili kuwekewa jicho la bandia.

Bomu hilo lililipuka wakati wanafunzi wa darasa la kwanza wakiingia darasani na liliokotwa na mwanafunzi ambaye alilihifadhi kwenye begi lake la madaftari kwa lengo la kwenda kuliuza kwa wafanyabiashara wa vyuma chakavu.

Mbali ya hao, Dk Mariagoreth alisema watoto wengine wawili jana walihamishiwa Hospitali ya Kagondo wilayani Muleba ambako kuna madaktari bingwa wa mifupa.

Pia, alisema leo watawaruhusu majeruhi watano kurejea nyumbani kutokana na afya zao kuimarika, hivyo watabaki watano.

Majeruhi waliohamishiwa Hospitali ya Kagondo ni Emanuel Hilali (13) ambaye anahitaji uchunguzi zaidi wa mguu wa kushoto na ambaye pia alipoteza jicho la kulia lililoondolewa kutokana na kuharibika.

Mwingine ni Simon Boniface (10), mwenye tatizo kwenye kidevu na anahitajiwa kuchunguzwa meno yake. Pia, ana maumivu mguu wa kulia.

Dk Mariagoreth alisema bado wanahitaji dawa na vifaa tiba.

Alisema gharama za matibabu zilizotumika kwa majeruhi 33 walioruhusiwa ni Sh1.827 milioni na kwa waliopo hadi Novemba 14 wamefikisha Sh4.061 milioni.

“Wazazi wa majeruhi hawajiwezi kiuchumi, hivyo uongozi wa wilaya ulishauri watafutwe madaktari bingwa watoe huduma hapa badala ya kuwasafirisha kwenda hospitali za rufaa ili kupunguza gharama,” alisema.

Alisema majeruhi wanne ambao kila mmoja amepoteza jicho moja, hivyo wanatibiwa majeraha na mipango inafanywa ili fedha zikipatikana pia wapatiwe miwani ili kuongeza uwezo wao wa kuona kwa jicho lililobaki.

Dk Mariagoreth alisema wanahitaji dawa za antibiotiki kwa ajili ya kukausha vidonda vya majeruhi.

Jukwaa la Maendeleo ya Wakazi wa Rulenge na Murusagamba wilayani Ngara zlmechangia Sh1.07 milioni kusaidia mahitaji mbalimbali kwa ajili ya majeruhi hao.

Mkuu wa Wilaya ya Ngara, Michael Mntenjele aliyefika hospitalini kuwajulia hali majeruhi mwishoni mwa wiki, aliwataka wazazi na walezi kuwa na imani na madaktari wanaoshughulikia afya za watoto wao.

Alisema Serikali ya wilaya inafanya kila jitihada kuhakikisha huduma muhimu zinatolewa kwa majeruhi na baada ya kupona kutafanyika utaratibu wa kuhakikisha wanaendelea na masomo.

Pia, aliwashukuru wananchi wanaojitokeza kutoa misaada kupitia ofisi yake na kwa uongozi wa hospitali kwa kuonyesha uzalendo na kuwajali wenye shida.

Mwananchi.



Mugabe kushitakiwa

Mugabe kushitakiwa


Mtandao wa Twitter unaofuatilia taarifa za vyombo vya habari nchini Zimbabwe unaripoti kuwa Kiongozi wa chama tawala Cha ZANU PF anaamini mchakato wa kumshtaki Bwana Mugabe utaendelea kama ilivyopangwa Jumanne , wakati ambapo chama bunge linatarajiwa kukaa.

Hii ni kama muda wa makataa uliowekwa wa kujiuzulu kwake ambao ni Jumatatu saa sita adhuhuri utakwisha kabla Bwana Mugabe hajajiuzulu

Halikuwa tangazo ambalo baadhi ya waZimbabwe walilisubiri. Bwana Mugabe bado ni rais na haijawa wazi ikiwa bunge sasa litaanza mchakato wa kumshitaki.

Watu wa Zimbabwe walikuwa wanatarajia kusikia mugabe akijiuzulu kulingana na madai yao.

Baadhi ya wale waliokusanyika kufuatilia hotuba yake kwenye vilabu waliiambia BBC kuwa wamekatishwa tamaa na kutojiuzulu kwa rais Mugabe.

Hata hivyo hali ya imeendelea kuwa tulivu katika maeneo mengi ya Zimbabwe, huku wengi waliendelea kusubiri mchakato utakaofuata.

Duru kutoka ndani ya mazungumzo ya hatma ya Mugabe zimeiambia BBC kuwa Mugabe mwenye umri wa miaka 93 alikuwa amekubali kuondoka madarakani , lakini baadae akabadili mawazo yake
Jeshi linatarajiwa kuwa na mkutano na waandishi wa habari Jumatatu asubuhi pamoja na Muungano wa Wapiganaji waliopigania Uhuru wa Zimbabwe.

Katika hotuba yake ya kwanza kwa taifa tangu jeshi lichukue madarakwa Jumatano, Mugabe hakujiuzulu na alisema kuwa ameazimia kuongoza kongamano lijalo la Zanu-PF.

Hatma yake sasa iko mashakani kwani kulingana na mbunge wa Zanu-PF Terence Mukupe anasema kongamano hilo ni mahala panopofaa kumuidhinisha kiongozi mpya anayependelewa na chama cha Zanu-PF