Friday, 27 October 2017

Burundi yajiondoa rasmi katika mahakama ya ICC

Burundi yajiondoa rasmi katika mahakama ya ICC

Rais Nkurunziza alichukua madaraka kwa awamu ya tatu, licha ya kuwepo kwa kipindi cha mihula miwili katika katiba ya taifa hilo.

Burundi limekuwa taifa la kwanza mwanachama wa mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa jinai kujiondoa katika mahakama hiyo.

Serikali ya taifa hilo la Afrika ya kati liliuarifu Umoja wa Mataifa UN kuhusu hatua hiyo mwaka mmmoja uliopita , na hii leo kujitoa kwao kunaanza kuidhinishwa rasmi.

Inaonekana kama kipimo cha jamii ya kimataifa kuhusu haki.

Ni hatua sio ya kawaida.

Je kutakuwa na athari zake na ni kwa nini ni muhimu?.

Kulingana na mwandishi wa BBC Anna Holligan kujiondoa kwa Burundi ni majuto makubwa.

Mahakama ya ICC imeanza kutathmini iwapo inaweza kuchunguza ghasia za kisiasa zilizoibuka baada ya rais Nkurunziza kuchukuwa madaraka kwa awamu ya tatu, licha ya kuwepo kwa kipindi cha mihula miwili katika katiba ya taifa hilo.

ICC bado ina uwezo kuchunguza uhalifu uliotekelezwa wakati Burundi ilipokuwa mwanachama wa mahakama hiyo.

Lakini haiwezi kuchunguza uhalifu wowote wa siku zijazo.

Hatua hiyo inaweza kuwa mfano na kuonyesha viongozi wengine kwamba kujiondoa katika mahakama hiyo ni njia mojawapo ya kuepuka jicho la kimataifa hadi pale Jamii ya kimataifa itakapochukua hatua na taasisi kama vile Umoja wa Afrika ama baraza la usalama la umoja wa mataifa litakapowafuatilia washukiwa na kuyakumbusha mataifa kwamba kujiondoa katika ICC hakumaanishi moja kwa moja kwamba waathiriwa hawatopata haki.

Simba vs Yanga kufa na kupona kesho

Simba vs Yanga kufa na kupona kesho

MECHI za Ligi Kuu Bara z i n a t a r a j i a kuendelea wikiendi hii kwa mzunguko wa nane kuchezwa, huku miamba miwili ya soka Tanzania, Simba na Yan­ga ikitarajia kukutana kwenye Uwanja wa Uhu­ru jijini Dar es Salaam, kesho Jumamosi.

Mchezo huu unatara­jiwa kuwa na ushindani wa hali ya juu kutokana na timu hizo kuwa katika nafasi sawa ya msimamo wa ligi licha ya Simba kuongoza kwa idadi ya mabao ya kufunga, huku kila moja ikihitaji kukaa kileleni.

Mechi hii inatarajiwa kuwa ni ya vita na kisasi kutokana na hali jinsi ilivyo katika mechi husika ambapo kila upande utahitaji ku­fanya vyema.

Yafuatayo ni baadhi ya mambo ambayo yanatarajiwa kuifanya mechi hiyo kuwa ni ya vita na kisasi.

MAKOCHA KUTETEA VIBARUA VYAO
Imekaa vibaya kwa upande wa makocha wa timu zote mbili, kutokana na historia za timu hizo ambapo mara nyingi makocha wamekuwa wakifungashiwa vi­rago vyao pale wanapofungwa na wapinzani wao.

Hivi karibuni kulizuka uzushi juu ya Yanga kutaka kumuondoa ko­cha wake, George Lwandamina kutokana na matokeo mabaya katika mechi za awali jambo am­balo uongozi wa klabu hiyo ulika­nusha, lakini waswahili husema lisemwalo lipo, hivyo mechi hiyo inaweza kuwa katika wakati mgu­mu kwa upande wake.

Vilevile kwa upande wa Simba, Kocha Joseph Omog amekalia kuti kavu kwa muda mrefu kuto­kana na uongozi wa klabu hiyo kutaka kumuondoa kutokana na madai ya kutokifundisha vyema kikosi hicho kwa kuona kuwa kimemzidi uwezo, lakini mkataba aliosaini umeonekana kumbeba kutokana na baadhi ya vipengele kuwabana waajili wake.

Hivyo basi, mechi hii ndiyo itakayotoa maamuzi juu ya kuen­delea kuwepo katika kikosi hicho kwa kuwa inadaiwa kuna kipenge­le alichosaini kinaeleza kuwa iwapo t i m u haitaongoza msimamo wa ligi, itawapa nguvu viongozi kuweza kuvunja kandar­asi hiyo.

Mshambuliaji wa Simba, Haruna Niyonzima akiopambana na wachezaji wa Simba.
Hivyo, atakuwa na kibarua kigumu kuhakikisha anafanikiwa kushinda mchezo huo ambao utakuwa na upinzani mkubwa.

KILA TIMU ITAHITAJI KUKAA KILELENI
Simba na Yanga zimefungana katika msimamo wa ligi kuto­kana na zote kuwa na pointi 15, huku Simba ikiongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya mabao ya kufunga. Simba ina mabao 19 na Yanga ina mabao 10.

Hivyo, kutokana na jinsi msi­mamo ulivyo, timu ambayo itashinda katika mchezo huo ndiyo itakayopata nafasi ya kuongoza msimamo wa ligi na iwapo itatokea wakatoa sare na Mtibwa Sugar yenye pointi 15 ikishinda mechi yao ya Ju­mapili dhidi ya Singida United basi itakaa kileleni.

KUONYESHANA UBORA WA VIKOSI
Kila timu inajinadi kuwa na kikosi bora ambacho imekisa­jili msimu huu, hivyo mashabiki wanasubiri kwa hamu kubwa kuona timu gani itaonyesha ufundi zaidi katika mchezo huo.

AJIBU, NIYONZIMA & OKWI VIVUTIO
Kwa sasa habari ya mjini ka­tika timu hizo ni kuhusiana na viwango vya wachezaji Ibrahim Ajibu wa Yanga na Haruna Niy­onzima na Emmanuel Okwi wa Simba, hivyo kila mmoja atahi­taji kuona wanafanya nini ka­tika mechi hiyo ya kesho.

Kwa upande wa Okwi, ndiye mchezaji kinara wa mabao kwenye ligi akiwa na mabao nane ambayo yameifanya kiko­si hicho kukaa kileleni kwa to­fauti ya mabao.

Aidha, wachezaji Ajibu na Niyonzima, kwa sasa ni gumzo kutokana na viwango wana­vyoonyesha. Mashabiki wa timu hizo wamekuwa waki­rushiana maneno huku wale wa Yanga wakidai Simba wamepoteza mchezaji (Ajibu) kwani amekuwa muhimu Jang­wani na Niyonzima akipondwa kwa kuonyesha uwezo wa ka­waida tofauti na ule aliokuwa akionyesha Yanga.

HOFU YA MASHABIKI
Hofu kubwa ya mashabiki kuelekea mchezo huo, itakuwa namna ya kuingia uwanjani kwani kwa muonekano wa haraka Uwanja wa Uhuru jinsi ulivyo hauwezi kukidhi mahitaji ya mashabiki kutokana na udo­go wa uwanja huo tofauti na ule wa Taifa ambao ni mkubwa.

Kuna uwezekano mkubwa kwa mashabiki wengi kuanga­lia mpira huo kupitia runinga kutokana na kushindwa ku­ingia uwanjani licha ya kuhitaji kuwaona wachezaji ‘live’ uwan­jani.

Dongo la Haji Manara

Dongo la Haji Manara

TIMU ya Simba leo imetua kwa ndege jijini  Dar wakitokea Unguja walipokuwa wameweka kambi ya wiki moja kabla ya mchezo wa kesho na watani wao wa jadi, Yanga SC.

Timu hiyo imepokelewa na viongozi mbalimbali wa Simba wakiongozwa na msemaji wa timu hiyo, Haji Manara, huku akirusha kijembe kwenda kwa watani hao  kupitia akaunti yake ya Instagram akisema: Mara paap,,tumetua dar,,,,okey mnaweza kupitia njia ya kilwa,,au ya kisarawe,,au daraja la kiluvya lishajengwa??Swaumu oyeeeee😊😊

Diamond Azua Gumzo Mitandaoni Baada Ya Kuonekana Akimpiga Kiss Mtoto Wake Wakike,,,,


MAGAZETI YA LEO 27 OCTOBER








Audio | Qboy Msafi Ft Mr Blue _ Kamoyo | Mp3 Download

https://my.notjustok.com/track/download/id/285110/by/g0k
8FWrgxq

Audio | Bracket Ft Korede bello _ Just Like That | Mp3 Download

https://my.notjustok.com/track/download/id/285158/by/OkoOtyDjTu

Audio | Coyo _ Tulipotoka | Mp3 Download

https://my.notjustok.com/track/download/id/285103/by/_zrbwPKpuO

Wednesday, 25 October 2017

Audio | Baraka Da Prince _ Sometimes | Mp3 Download

https://my.notjustok.com/track/download/id/284708/by/A0yGnzN9Zr

AUDIO | RICH MAVOKO FT PATORANKING _ RUDI | MP3 DOWNLOAD

https://my.notjustok.com/track/download/id/284754/by/MtTPFaHxVR

TPA yasema idadi ya meli zinazoingia nchini imeshuka


TPA yasema idadi ya meli zinazoingia nchini imeshuka Muungwana Blog 1 Wednesday, October 25, 2017 Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) imesema idadi ya meli zinazoingia nchini imeshuka kutoka 1,200 hadi 1,000 huku mapato yanayotokana na biashara hiyo yakiongezeka. Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo Mhandisi Deusdedit Kakoko alisema kwamba hata mizigo inayoingia nchini pia imepungua. Kakoko alilazimika kuyasema hayo wakati akijibu swali liloulizwa na Mbunge wa Kilindi, Omary Kigua ambaye alitaka kupata ufafanuzi wa kuhusu hali ikoje katika biashara ya bandari. “Kuna speculation (minong’ono) kuwa idadi ya meli zinazoingia nchini zimepungua. Nilitaka kufahamu hali biashara ikoje?”alihoji Kigua. Kakoko alisema hatua wanazochukua zinalenga ufanisi , tija, gharama wanazotoza na huduma kwa mteja na kwamba kwa kukamilisha mambo hayo kutawezesha meli nyingi kuingia nchini. “Uchunguzi wetu umejionyesha kuwa unapochukua hatua matokeo yake yanakuwa mbele hizi hatua ambazo tunachukua zinazaa matunda. Alitaja sababu nyingine ya kupungua kwa meli ni uwezo wa kutia nanga kwa meli ambao hutegemea kina cha maji na kwamba kuna meli nyingi ambazo zinasubiri nje ya gati. Alisema kina cha maji kuna mahali ni mita saba wakati kwingine ni mita 10.5 na meli nyingi duniani ni kubwa hivyo nyingine kusababisha meli kutofika nchini. “Kwa hiyo kuna meli zinasubiri siku saba na meli inatengeneza hela ikitembea ikisimama inatumia hela kwasababu ni kama gari, hiyo ndio sababu inayotuathiri lakini sasa tumeanza ujenzi wa kuchimba gati zetu,”alisema. Alisema sababu nyingine za usalama ambapo kuna baadhi ya watu wamekuwa wakiibiwa hadi betri na kwamba nyingine ni usimamizi wa sera ambapo awali kulikuwa kuna baadhi ya watu wanaleta mizigo hawalipii. Alisema pia kampeni za masoko zilienda chini licha ya miaka 1960 ilikuwa ni bandarini yenye nguvu. Mbunge wa Magomeni, Jamal Kassim alisema hoja nyingi za ukaguzi kwa mamlaka hiyo zinatoka na mfumo mbuvu walionao taasisi hiyo. “Mwenyekiti (Mwenyekiti wa Bodi ya Bandari Profesa Ignas Rubaratuka) ulituambia kuwa mmevuka malengo kutoka Shilingi 632 bilioni hadi 705 bilioni lakini kutokana na mfumo mbovu Serikali wharfag (fedha za mizigo) zikusanywe na TRA ( Mamlaka ya Mapato Nchini),”alisema. “Mkurugenzi atuambie hizo fedha walizokusanya zinajumuisha pia fedha za wharfag na atumbie pia ukoje huo utaratibu?”alihoji. Akijibu Mhandisi Kakoko alisema wamerejeshewa Sh 112bilioni ambazo ni mapato yanayotokana na mizigo ya kipindi cha Agostihadi Desemba mwaka jana na kwamba walishazitumia. Hata hivyo, alisema wanadai Serikali Sh 183 bilioni ambazohazijarejeshwa katika mamlaka hiyo. “Awali makubaliano kati ya TRA na mamlaka kuwa watakusanya mapato hayo ya mizigo lakini hili lilifutika baada ya sheria ya bandari kufanyiwa marekebisho na kutoa mamlaka kwa TRA kukusanya mapato hayo ya mizigo na kisha kurejeshwa kwa TPA,”alisema. Akisoma maazimio ya kamati hiyo Mwenyekiti wa Kamati hiyo Kaboyoka aliagiza mamlaka kuwasilisha mpango kazi wa kusimika na kuanza kutumika kwa mfumo wa Tehama katika ofisi ya Katibu wa Bunge. “Bodi ikamilishe zoezi la uthaminishaji wa mali katika mwaka wa fedha 2017/18,”alisema. Chanzo Mwananchi.

Daktari ahukumiwa kifo Iran

Daktari ahukumiwa kifo Iran

Mahakama nchini Iran inaaminika kumhukumu kifo daktari mmoja mzaliwa wa Iran aliye na kibali cha kuishi nchini Sweden wakimtuhumu kwa kuifanyia ujasusi Israel.

Mkuu wa mashtaka nchini Iran alisema mtu alipatikana na hatia ya kuwapasha habari majasusi wa Israel anuani 30 za wanasayansi wa nyuklia, wawili kati yao waliouawa kwenye mashambulizi ya mabomu mwaka 2010.

Lakini mke wake daktari Ahmadreza Djalali, alisema kwa mume wake alikuwa amekuhukumiwa kwa mashtaka sawa na hayo.

Shirika la kupigania haki za binadamu la Amnety International, lilisema kwa hukumu hiyo ilitolewa baada ya mateso ya kisaikolojia na hukumu isiyo ya haki.

Mkuu wa mashtaka huko Tehran Abbs Jafari-Dowlatabadi, aliuambia mkutano wa maafisa wa mahakama kuwa mtu ambaye hakutajwa jina aliwapa majasusi wa Isreal anuani za watu 30 muhimu.

Alisema kuwa anuani hizo ni za wanasayansi wa nyuklia Massoud Ali-Mohammadi na Majid Shahriari, ambao waliuawa kwenye milipuko ya mabomu mjini Tehran mwezi Januari na Novemba mwaka 2010.Mkuu wa mashtaka alisema kuwa mtuhumiwa alitoa taarifa hizo kwa Israel ili alipwe pesa na msaada wa kupata kibali cha kuwa mkaazi wa Sweden.

Amnesty international ilisema kuwa Bw. Djalali ambaye ni daktari na muathiri kwenye taasisi ya Karolinska mjini Stockholm, alikuwa kwenye ziara ya kibishara nchini Iran mwezi Aprili mwaka 2016, wakati alikamatwa na maafisa wa ujasusi na kuzuiliwa bila ya kuruhusiwa kukutana na wakili kwa muda wa miezi saba.

Bw. Djalali anasema kuwa wakati akiwa kuzuizini alilazimishwa mara mbili kukiri mbele ya kamera kwa kusoma taarifa zilizokuwa zimeandikwa na wale waliokuwa wakimhoji.

Anasema alikuwa chini ya shinikizo kali kupitia mateso ya kisaskolojia na vitisho vya kumuua na kuwakamata watoto wake ili aweze kukiri kuifanyia ujasusi serikali ya Israel.

Mawaziri watatu wapigwa STOP

Mfalme wa Morocco Mohammed VI Mfalme wa Morocco Mohammed amewafuta kazi mawaziri wake wa elimu, makaazi na afya kwa kuchelewesha maendeleo ya kiuchumi katika jimbo la Rif lililopo kaskazini.

Eneo hilo lilishuhudia maandamano mwaka jana ambayo yalisababishwa na kifo cha muuza samaki katika makabiliano na polisi - tukio ambalo liliashiria matumizi ya nguvu kupitiliza, rushwa na hali ya kutojali.

Mwezi July, Mfalme Mohammed aliwasamehe watu ambao awali walikamatwa wakati maandamano hayo yakiendelea, huku akiwalaumu maafisa wa serikali kushindwa kupeleka miradi ya maendeleo katika jimbo la Rif.

Eneo hilo lilikuwa kati kati ya vuguvugu ya kisiasa ya mwaka 2011 ambayo ilichochea maandamano nchini Morocco.