Thursday, 19 October 2017

Kifo Cha kanumba : Ushahidi Wa kwanza umetolewa Leo 19 October

Leo Oktoba 19, 2017 mahakama kuu chini ya Jaji Sam Rumanyika imeanza kuisikiliza shauri la kesi ya jinai namba 125 ya mwaka 2012, Inayomkabili Msanii Elizabethi Michael ya kumua msanii mwenzie Steven Kanumba bila kukusudia mbapo leo upande wa jamhuri ulikuwa na Mashahidi 2 na shahidi namba moja alikuwa ni Mdogo wake Steven Kanumba Aliyejimabulisha kama Seth Bosco, lakini shahidi wa pili aliomba udhuru wa kutofika leo.
Katika maelezo ya Shahidi Seth Bosco akiongozwa na wakili wa Jamhuri Faraja George ameieleza mahakama kuwa Kanumba ndiye aliye mfungulia mlango Lulu, na alipofika ndani baada ya muda kidogo yeye akiwa chumbani kwake alianza kusikia mvutano wa sauti ya Kanumba ikimwambia Lulu
"kwanini Unaongea na 'Boyfriend' wako mbele yangu?" Mabishano yalianzia kwenye korido, na baada ya kuingia chumbani zilianza kusikika kelele
Baada ya muda mfupi Lulu aliinita na kuniambia Kanumba ameanguka najaribu kumwagia maji naona haamki, nilipoingia chumbani nikweli nilikuta yuko chini akiwa ameegemea ukuta, nikamchukua nikamlaza chali na ndipo nilipoanza kumtafuta Daktari wake anayeitwa Paplas Kageiya, daktari alipofika alimfanyia 'Chek up' akasema ameshafariki, akashauri tumpeleke Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, niliendesha gari mpaka muhimbili, tulipofika muhimbili kwenye kitengo cha dharura walituambia tukatafute utaratibu wa kipolisi, wakati wao wanaandaa vibali vya kuruhusiwa apelekwe mochwari, Baada ya mahojiano ya Polisi katika kituo cha urafiki Ubungo, niliondoka na Askari kurudi nyumbani kwaajili ya uchunguzi, baada ya polisi kufika pale wakiwa chumbani wanaendelea na uchunguzi walikuta Panga chini ya kitanda" Alisema shahidi Seth Bosco
Baada ya ushahidi huo, mahakama imeahirisha shauri hilo hadi kesho Oktoba 20, 2017 kwaajili ya kuendelea kusikiliza mashidi wengine Wanne kutoka upande wa Jamhuri.
Upande wa mstakiwa unaongozwa na Wakili Msomi Peter Kibatala.
Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa kwa siku tatu mfulilizo, ingawa Jaji Rumanyika ameelekeza upande wa mstakiwa na Jamhuri kuona kama wnaweza kutumia hata siku mbili kuisikiliza na siku ya tatu ikatumika kuandika hukumu.

Mke Wa Mugabe Amshtaki Mfanyabiashara kwa kutomuuzia Pete ya $1.35m

Zimbabwe na mkewe Grace MUgabe
Mke wa rais nchini Zimbabwe Grace Mugabe amemshtaki mfanyibiashara mmoja kwa kushindwa kumpatia pete ya almasi yenye thamani ya $1.35m kulingana na chmbo cha habari cha Herald.
Jamal Ahmed alidaiwa kumpatia pete yenye thamni ya $30,000 badala ya ile aliyoagiza.
Ni mgogoro wa hivi karibuni kuhusu pete hiyo yenye Carat 100 iliotarajiwa kuwa zawadi ya rais Mugabe kwa mkewe wakati wa maadhimisho ya miaka 20 ndoa yao.
Mwaka uliopita, bwana Ahmed aliwashtaki Bi Grace Mugabe na mwanawe wa ndoa yake ya kwanza mahakamani baada ya kuchukua mali zake katika mgogoro wa pete hiyo.
Alisema katika nakala za mahakamani kwamba bi Mugabe alitaka kurudishiwa fedha zake baada ya pete hiyo ya almasi ilionunuliwa Dubai kukabidhiwa yeye baada ya kusafishwa na mtu mwengine.
Wakati aliposhindwa kulipa fedha hizo kwa akaunti moja huko Dubai, licha ya kusema kuwa fedha hizo zilitumwa kupitia benki moja ya Zimbabwe mke huyo wa rais alichukua kwa lazima nyumba zake.
Bwana Ahmed alisema kuwa alinyanyaswa, kutukanwa na kutishiwa na kuambia hawezi kuchukua hatua yoyote kwa kuwa walioshtakiwa ndio 'Zimbabwe'.
Disemba iliopita jaji mmoja alimuagiza bi Mugabe kurudisha mali hiyo.
Na sasa anamshtaki bwana Ahmed , ambaye ana kibali cha kuishi nchini Zimbabwe na biashara katika taifa hilo kwa $1.23m ili kulipa deni hilo.

Shehena ya bangi yaibuka kwenye ajali

Kibaha. Majeruhi wawili wa ajali ya gari wanashikiliwa na polisi mkoani Pwani wakituhumiwa kuhusika na usafirishaji na biashara ya bangi kilo 7,500.
Majeruhi hao ni Gudluck Kundaeli maarufu Mbowe (24) mkazi wa Kiwalani na Ally Gebra maarufu Mtena (28) wa Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Jonathan Shanna amesema leo Alhamisi Oktoba 19,2017 kuwa watuhumiwa walikamatwa jana eneo la Kwa Mathias mjini Kibaha baada ya upekuzi kufanyika kwenye gari walilokuwa wakisafiria aina ya Toyota IST lililopata ajali.
Amesema gari hilo lilipata ajali eneo hilo saa tatu usiku na askari walifika kutoa msaada ikiwemo kuwaokoa majeruhi ambao walipelekwa Hospitali ya Tumbi kwa matibabu.
Kamanda Shanna amesema baada ya kuwaokoa majeruhi na askari kufanya upekuzi kwenye gari walikuta magunia saba yenye bangi.
"Tulipata taarifa ya ajali kutokea eneo la Kwa Mathias, askari wakaenda kwa ajili ya uokoaji na waliwaokoa vijana hawa. Baadaye walifanya upekuzi kwenye gari na kukuta bangi hiyo. Tumepima ina kilogramu 7,500 kwa hiyo tunawashikilia watusaidie katika uchunguzi," amesema Kamanda Shanna.

Kauli ya Ridhiwani kikwete kuhusu Tundu Lissu,,,,

Mbunge mpya wa Jimbo la Chalinze (CCM), Ridhiwani Kikwete amefunguka na kusema kuwa amefurahi kumuona Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu akiwa mwenye tabasamu na furaha na kuzidi kumuombea apone kabisa na kurudi kupambana.
Ridhiwani Kikwete amesema hayo kupitia mtandao wake wa Instagram na kusema Mungu siku zote anatenda wema kwa watu kufuata kushambuliwa kwa risasi nyingi Tundu Lissu na hatimaye kuweza kupona na sasa furaha yake kuanza kurejea.
"Mungu utenda wema siku zote. Ashukuliwe yeye kwa kazi ya kurejesha tabasamu katika sura yako na afya kwa wanaokuuguza. Nimefurahi kukuona tena msomi, Kiongozi wangu na mwana kamati mwenzangu wa Bunge ukitabasamu na mwenye Afya njema. Mungu akulinde na akusimamie katika matibabu yako .Looking forward to see you back into your good shape" aliandika Ridhiwani Kikwete
Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana mnamo Septemba 7, 2017 akiwa nyumbani kwake mjini Dodoma na kisha baadaye kusafirishwa na kupelekwa jijini Nairobi Kenya kwa matibabu ambapo mpaka sasa yupo nchini Kenya akiendelea kupatiwa matibabu

CHADEMA Waliamsha Dude

Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimeweka wazi kwamba hakimuhitaji Mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru Bw. Christopher Kazeri kuwa msimamizi wa uchaguzi mdogo kwa madai hawana imani naye pia hana sifa kwani anaweza kusababisha umwagikaji wa damu.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimeweka wazi kwamba hakimuhitaji Mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru Bwana Christopher Kazeri kuwa msimamizi wa uchaguzi mdogo kwa madai kwamba hawana imani naye pia hana sifa kwani anaweza kusababisha umwagikaji wa damu.
Akiitoa taarifa hiyo Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini Amani Golugwa amesema kwamba Mkurugenzi huyo alipoteza sifa za kusimamia uchaguzi tangu Juni, 24 walipokuwa kwenye uchaguzi wa vitongoji na vijiji kwa kufoji matokeo katika vijiji kadhaa na kuwalazimisha wasimamizi wabadilishe namba kwenye fomu.
Golugwa amesema kwamba vitendo ambavyo Mkurugenzi huyo alivifanya anavitafsiri kama mambo ya kihuni kwani yalipelekea kugombanisha watu ambao ni ndugu hivyo hofu yao ni kwamba anaweza kusababisha umwagikaji damu katika uchaguzi mdogo wa marudiano Arumeru Mashariki.
"Tumeishauri Tume iweze kuwasiliana na mamlaka ya uteuzi kwamba hatumtaki ndg Kazeri awe msimamizi wa uchaguzi huu mdogo Arumeru Mashariki, kwanza aliingilia uchaguzi wa vitongoji na vijiji na kulazimisha kubadilishwa matokeo ambayo yalionyesha Chadema wameshinda, jambo ambalo lilileta ugombanishi kwa wagombea, na hata wagombea wa CCM walikataa matokeo kwa kukubali kwamba walishindwa na hata wasimamizi na askari waliokuwepo hapo walithibitisha kwamba Chadema walikuwa wameshindwa" Golugwa
Ameongeza "Kama uchaguzi wa vitongoji Mkurugenzi ametumia mabavu na kufanya uhuni ambao tumeumbatanisha kwa Tume, kwenye uchaguzi huu wa madiwani si ataleta hata vifaru au kusababisha umwagaji wa damu? Kwa busara na hekima ya kawaida matendo aliyoyafanya Kazeri hayampi sifa ya kuwa msimamizi.
Hata hivyo Golugwa amefafanua na kusema kwamba wamewasilisha ushahidi wa wagombea wa CCM wakikataa kupokea ushindi huo wa vitongoji kwa madai kwamba hawawez kupokea ushindi wa mtutu wa bunduki.

Mwigamba avuta 'jeshi' kujiunga CCM

Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo Samsoni Mwigamba na wanachama wengine 10 wametangaza kujiunga na chama cha CCM baada ya kujivua uanachama wa ACT Wazalendo leo.
Taarifa za Mwigamba kujiunga na CCM zimetolewa leo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, na kusema kwamba wameamua kufanya hivyo ili kujitenga na upinzani unaokerwa na maendeleo ya nchi, na pia kuunga mkono juhudi za serikali za mapambano dhidi ya rushwa.
“CCM ya sasa ndicho chama kinachotekeleza kwa karibu itikadi, falsafa na sera za ACT Wazalendo ambazo mimi na wenzangu tulishiriki kukiasisi, nchi yetu ndio kinara wa mapambano dhidi ya rus
hwa sasa hivi, sera ambazo ndio misingi ya ACT Wazalendo, tumeamua kujitenga na upinzani unaokerwa na mafanikio ya nchi ili tuendelee kuwa sehemu ya mapambano katika kurejesha nchi kwenye misingi yake”, amesema Mwigamba.
Samson Mwigamba atakuwa kiongozi wa pili ACT Wazalendo kujivua uanachama wa ACT Wazalendo kwa mwaka huu baada ya Prof. Kitila Mkumbo ambaye naye alifanya hivyo wiki kadhaa zilizopita.

Nafasi za kazi Leo 19

Bonyeza Links Zifuatazo Kusoma zaidi na Kuapply
Nafasi zingine ingia Nafasi za kazi leo October 19
2 Job Opportunities at Vodacom Tanzania
Job Opportunity at Energy and Water Utilities Regulatory Authority (EWURA)
Job Opportunity at Alliance for a Green Revolution in (AGRA), Finance & Administration Officer
Job Opportunity at Multinational
Bank, Branch Manager
Job Opportunity at TAPBDS CO LTD, Accountant
Job Opportunity at The Belgian Red Cross, Regional Cash Delegate, Tanzania
Job Opportunity at EngenderHealth Tanzania, Research Coordination Advisor
Job Opportunity at NMB Tanzania, Senior Manager Branch Technology Support
Job Opportunity at ILO, Technical Officer
www.ajirayako.co.tz

Picha ya faru aliyeuawa yashinda tuzo ya picha bora

Picha ya kutisha ya uhalifu wa mazingira imetangazwa kuwa mshindi katika tuzo za shindano la wapiga picha la mwaka huu
Picha ya kutisha ya uhalifu wa mazingira imetangazwa kuwa mshindi katika tuzo za shindano la wapiga picha la mwaka huu.
Picha hiyo iliopigwa na mpiga picha wa Afrika Kusini Brent Stirton inaoyesha hali ya faru mweusi katika mbuga ya wanyama pori ya Hluhluwe Imfolozi.
Wawindaji haramu walimuua mnyama huyo usiku kabla ya kumtoa pembe zake.
Stirton alipiga picha hiyo ikiwa miongoni mwa uchunguzi kuhusu biashara haramu ya bidhaa za faru.
Mpiga picha huyo alizuru zaidi ya maeneo 30 uliofanyika uhalifu huo wakati wa uchunguzi wake ambao aliutaja kuwa wa kuogofya.
Mwanangu wa kwanza atazaliwa mnamo mwezi Februari ; nina umri wa miaka 48. Unaweza kupoteza utu mara nyengine.
Stirton, ambaye alipokea tuzo hiyo katika tamasha la chakula cha jioni lililofanyika katika jumba la kumbukumbu mjini London , anaamini kwamba unyama huo aliofanyiwa faru huyo ulitekelezwa na wakaazi wa eneo hilo.
Lengo kubwa la uwindaji huo ni kuuza pembe mbili za faru huyo kwa wafanyibiashara.
Wafanyibiashara hao baadaye huzipeleka pembe hizo hadi Afrika Kusini kupitia Msumbiji hadi China ama hata Vietnam.
Katika mataifa hayo ya bara Asia, pembe za faru zina thamani ya juu ikilinganishwa na dhahabu ama dawa ya kulevya ya Cocaine.
Biashara hiyo hupata msukumo wa imani kwamba sawa na kucha za vidole vya mguuni, zinaweza kutibu ugonjwa wowote kutoka saratani hadi mawe ya figo.
Brent Stirton aliambia BBC : Kwa mimi kushinda tuzo hii, kwa majaii kuweza kutambua kazi yangu ni wazi kwamba tunaishi katika muda tofauti na kwamba hili ni swala nyeti.
''Swala la kuangamia kwa baadhi ya wanyama ni la kweli na faru ni mojawapo ya aina ya wanyama wanaoendelea kuangamia kwa kiwango kikubwa na ninashukuru kwamba majaji waliweza kutambua picha yangu kwa kuwa inaliangazia swala hili kwa hatua nyengine''.
Lewis Blackwell, mwenyekiti wa jopo la majaji hao wa WPY, alisema kuwa picha hiyo ya faru ilikuwa na athari kubwa katika jopo lake.
''Watu wanaweza kusinywa ama kushtushwa lakini ukweli ni kwamba picha hiyo inakuvutia na kukufanya kuhisi kana kwamba unataka kujifunza mengi.Unataka kujua habari kuihusu. Na huwezi kuitoroka kwa sababu inakuangazia yale yanayoendelea duniani''.

MAGAZETI YA LEO 19/10/2017














AUDIO | Rayvanny _ Tabia | Np3 Download

https://my.notjustok.com/track/download/id/282350/by/nUXzBDbVsZ

Msami afunguka ishu ya kutoka na Nandy Kimapenzi

Msanii wa Bongo Flava, Msamii amesema si kweli kwamba ameshawahi kutoka kimapenzi na Nandy.
Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma katika mahojiano na Bongo5 amesema Nandy ni kama dada yake hivyo hawezi kufanya hivyo.
“Nandy sijawahi kupita naye ni kama mdogo wangu, dada yangu, kwa hiyo kwa sasa hivi mimi na Nandy ni kaka na dada, let say mimi ni mtu ambaye nimetoka kwenye familia ya THT Nandy pia kwenye familia hiyo hiyo, tupo familia moja” amesema Msami.
Msami anaungana na rapper Bill Nass ambaye amekuwa akidaiwa kuwa na mahusiano na Nandy kitu ambacho amekuwa akikikanusha kila mara.

Wema Afunguka sababu za kutokwenda kumuona lissu Nairobi

Mrembo wa Tanzania na Kada wa Chadema Wema Sepetu ametoa ya Moyoni kwa nini hakwenda kumuona mapema Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu baada ya kupigwa risasi septemba 7 ni kwamba asingeweza kumuona akiwa kwenye maumivu.
Wema ameweka wazi maneno hayo kwenye ukurasa wake wa Instagram ikiwa ni baada ya dakika chache tangu kuachiwa kwa picha za kwanza za Mbunge huyo akiwa hospitali ya Nairobi nchini Kenya.
Wema ameandika "Kisichokuua kinakufanya uwe na nguvuz zaidi....Utarudi tena ukiwa na nguvu kuliko ulivyokuwa awali...Shujaa wetu. ... Picha hii imenifanya nipate hisia. Sasa naweza andaa safari ya Nairobi kuja kukuona.. Awali nisingeweza kuvumilia kukuona ukiwa kwenye maumivu".
Wema Sepetu ametajwa na Chama cha Chadema kama mmoja wa wahamasishaji aliyeweza kuhamasisha watu kutoa michango kwa ajili ya matibabu ya Mbunge Tundu Lissu aliyelazwa Hospitali ya Nairobi baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana alipokuwa kwenye gari lake nje ya makazi yuke huko mjini Dodoma.

Beka Flavour : Siwezi kurudi yamoto band,,

Msanii wa Bongo Fleva, Beka Flavour amefunguka na kusema kuwa yeye kwa sasa hayupo tayari kurudi kwenye kundi la Yamoto Band na kudai ukweli ni kwamba kundi hili lilishakufa na kila msanii sasa anasimama kivyake.
Beka alisema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Planet bongo na kusema kuwa wakati wanaondoka kwenye kundi hilo hawakuwa na pesa zozote zile kwani enzi zao wakati wanafanya show mbalimbali walikuwa wanapewa fedha za matumizi tu na wao walipendekeza kwa uongozi fedha zinapopatikana wafanyiwe mambo kadhaa ikiwa pamoja na kujengewe nyumba.
"Mimi saizi ukisema nitoke kwenye uongozi wangu mpya nirudi Yamoto Band sidhani kama itawezekana unajua watu hawajui tu lile kundi ndiyo limeshakufa kwa sababu saizi kila msanii yupo na uongozi wake, sidhani kama wanaweza kukubaliana watoke walipo na kurudi kule" alisema Beka Flavour
Mbali na hilo msanii huyo aliweka wazi kuwa anafurahi kuona Aslay msanii ambaye alikuwa naye kwenye kundi moja na yeye saizi anakuwa ni kati ya wasanii wanaozungumziwa sana kwa kazi nzuri.
"Mimi nazidi kumuombea kwani mwenzangu saizi amekuwa ni kati ya wasanii ambao wanazungumziwa sana kutokana na kazi zake, lakini napenda kuwaambia Watanzania kuwa wasanii ambao tulikuwa tunaunda kundi la Yamoto Band Mungu alitupa kitu ndani yetu hivyo muda si mrefu mtakuja kuona haya nayosema kwani kila mmoja ana upekee wake katika kazi zake" alisisitiza Beka