Wednesday, 18 October 2017

Breakfast news : Kocha Wa Simba ajiuzulu

Kocha Jackson Mayanja ameamua kuachana na klabu ya Simba nrejea kwao Uganda.
Mayanja ambaye bado yuko jijini Dar es Salaam, ameamua kuachana na Simba akidai ana matatizo yake binafsi.
“Ni matatizo ya kifamilia lakini suala hilo siwezi kulizungumzia kwa sasa,” alisema.
Lakini habari kutoka Simba zimeeleza kuwa sasa wako katika hatua za mwisho kuvunja mkataba wake baada ya kukubaliana naye kutokana na uamuzi wake huo.

Moto waacha wanafunzi bila nguo bwenini

PICHA HII HAIHUSIANI NA TUKIO LA KUUNGUA SHULE YA SEKONDARI YA NANDEMBO.
ZAIDI ya wanafunzi 70 wanaosoma katika Shule ya Sekondari ya Nandembo wilayani Tunduru Mkoa wa Ruvuma, wamekosa mahali pa kulala na kuhamishiwa eneo la kanisa, baada ya moto kuteketeza bweni lao.
Wanafunzi hao walinusurika kifo kutokana na kuwa darasani moto huo ulipoanza kuwaka Jumatatu.
Moto huo uliunguza na kuteketeza madaftari, nguo, mashuka na mali nyingine za wanafunzi.
Mashuhuda walisema bweni hilo walilokuwa wakilala wanafunzi wa kiume wa kidato cha kwanza na kidato cha nne lililipuka moto kati ya saa 1:30 na saa 2: 00 usiku.
Mkuu wa shule hiyo, Mary Ndunguru, alisema baada ya kuzuka kwa moto huo, walimu walishirikiana na wanafunzi kuuzima moto huo bila mafanikio.
Alisema wakati wa tukio hilo, wanafunzi walikuwa wakiendelea na masomo ya jioni katika madarasa yaliyopo zaidi ya mita 200, hivyo kuchelewa kubaini kilichokuwa kinaendelea.
Ndunguru alieleza baada ya kuudhibiti moto na kubaini kutokuwapo uwezekano wa wanafunzi kuendelea kulala katika bweni hilo, aliwasiliana na viongozi wa Kanisa Katoliki kijijini hapo na kuomba wanafunzi waende kulala eneo la kanisa kwa muda wakati uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ukiendelea na juhudi za kutafuta ufumbuzi wa kuwajengea bweni lingine.
Kaimu Ofisa Elimu wa Shule za Sekondari wilayani Tunduru, Habiba Mfaume, alisema takwimu zinaonyesha kuwa jumla ya wanafunzi 72 walikuwa wanalala katika bweni hilo na hakuna aliyepata madhara.
Alisema amemuagiza mkuu wa shule hiyo kuwaita wazazi wote katika kikao kilichopangwa kufanyika kesho, ili kuomba msaada wa awali kwao na kila mzazi ajitahidi kufika na nguo zitakazosaidia kuwasitiri watoto wao katika kipindi hicho cha mpito.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Chiza Marando, alisema ili kuwasaidia wanafuzni wanaojiandaa kufanya mitihani ya kuhitimu masomo ya kidato cha nne inayotarajiwa kuanza Oktoba 30 mwaka huu, ameshawatuma wataalamu kupitia masomo yote waliyosoma, ili kuwasaidia kuwatolea nakala wanafunzi wote kuwasaidia waendelee kujisomea.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Tunduru ambaye ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Kaimu Ofisa Tawala wa wilaya hiyo, Agustino Maneno, alisema amemuagiza Kamanda wa Polisi wa wilaya hiyo kupeleka wataalamu wake kupeleleza chanzo cha moto huo.

Askari Aliyekuwa Akifanya Mapenzi na Mfungwa Ajinyonga.....

Askari mmoja wa Chuo cha Mafunzo ya Wafungwa cha Losperfontein, nchini Afrika Kusini amejinyonga hadi kufa mara baada ya kuzagaa kwa picha zilizomwonyesha akimpiga busu mfungwa kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii .
Taarifa iliyotolewa na Idara ya Magereza nchini humo imesema kuwa ilifahamishwa kuhusu picha zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na kwamba wakati wanafanya uchunguzi wa tukio hilo, tayari ofisa huyo alikuwa ameshajinyonga.
Aidha, Kamishna wa Magereza wa Limpopo‚ Mandla Mkabela amesema katika taarifa yao kwamba wameshtushwa sana na wamehuzunishwa mno na tukio hilo la kujinyonga kwa Askari huyo.
“Tumetuma timu ya mameneja waandamizi na wataalamu wa mpango wa ushauri kwa wafanyakazi kwa ajili ya kutoa msaada wowote muhimu,” amesema Mkabela.
Hata hivyo, Mkabela amelaani tukio la usambazaji wa picha zinazodaiwa kuwa ni za ofisa huyo ambazo zimeweza kumsababishia kuchukua maamuzi ya kujinyonga.

Moto Waendelea kuwaka CCM

Wakati Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole akiwataka wakuu wa wilaya nchini kuwa na hekima ya kuridhika na vyeo walivyonavyo moto umeendelea kuwaka ndani ya chama hicho, baadhi ya makada na wachambuzi wa siasa kukosoa pendekezo lake la wagombea kuwa wakazi wa majimbo husika.
Wiki iliyopita, Polepole alisema katika kipindi cha redio Times kuwa wanachama wanaotaka kugombea ubunge kwa tiketi ya CCM 2020, sasa watalazimika kuwa wakazi wa eneo wanalotaka kuliwakilisha, sharti ambalo linaweza kuwaondoa takriban nusu ya wabunge wa sasa.
Tamko hilo la Polepole lilizua mjadala mzito jambo lililosababisha Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Organaizesheni, Pereira Silima alitoa taarifa kueleza kuwa hakuna mahali popote katika mabadiliko ya katiba yao palipoandikwa kuwa wagombea wa udiwani na ubunge watajadiliwa kwa sifa ya kuishi jimboni.
Ukiacha hilo juzi usiku katika kipindi cha ‘Tuambie’ kinachorushwa na televisheni ya TBC, Polepole alizungumzia suala jingine la kuwa kanuni za uchaguzi haziwakatazi wakuu wa wilaya kuwa wajumbe wa mkutano mkuu wa Taifa wa CCM, wanapaswa kuwa na hekima.
Kauli ya Polepole imekuja wakati tayari kukiwa na wakuu wa wilaya wanne, mkuu wa mkoa na makatibu tawala walioshinda katika chaguzi za chama hicho zilizofanyika hivi karibuni.
Walioshinda ni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendego ambaye aligombea ujumbe wa mkutano mkuu wa CCM baada ya kupata kura 311.
Mwingine ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Nanyumbu, Salum Palango aliyepata kura 295.
Wakuu wa wilaya walioshinda ni Simon Odunga (Chemba) aliyeshinda kwa kura 432, Christina Mndeme (Dodoma) na Elizabeth Kitundu (Bahi) wote kutoka mkoani Dodoma.
Mkoani Morogoro, walioshinda ni Alhaji Mohamed Utaly (Mvomero) na Seriel Nchembe (Gairo).
Wakuu wengine wa wilaya walioshinda ni Raymond Mushi (Babati) mkoani Manyara, Herman Kapufi (Geita), katibu tarafa wa Makuyuni (Arusha), Paul Kiteleki na mkuu wa Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, Alexander Mnyeti.
“Ukienda kwenye kanuni za uchaguzi za 2017 fungu la 25: Nafasi ya uongozi ni kazi ya muda wote (inazitaja hapo), Mkutano Mkuu wa Taifa haujatajwa, lakini mkuu wa wilaya ni kiongozi wetu wa Serikali pia ni kiongozi wetu wa chama,” alisema Polepole na kuongeza:
Mkuu wa wilaya ni mjumbe wa kamati ya siasa ya wilaya ni mjumbe wa halmashauri kuu ya wilaya na ni mjumbe wa mkutano mkuu wa wilaya. Huyu pia ni kamisaa wa Serikali, ‘public officer’ anayefanya kazi zote za chama. Sasa nikasema hekima pale ituongoze, yaani mtu ujiongeze mwenyewe.”
Aliendelea kusema: “Kama wewe una dhamana zote hizi, kwa nini mkutano mkuu tusimwachie mwanachama mwingine asiye na dhama nyingine yeye ashiriki kwenye mkutano wa chama?”
Polepole aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Musoma mkoani Mara na baadaye Ubungo jijini Dar es Salaam alisema kwa sasa kuna wakuu wa wilaya wapatao 166 na kama wote wataomba nafasi hizo, watafurika kwenye nafasi za chama hicho.
“Kama wakuu wa wilaya wote watachukua kwa pamoja wako 166, zamani mkutano mkuu tulikuwa 2400 sasa hivi tumepunguza idadi tumekuwa 1,700, hao ni wanachama walioomba dhamana halafu kati ya hao 166 ni wakuu wa wilaya,” alisema Polepole na kuongeza:
“Upande wa pili ni hekima ya kuwa na kiasi. Wewe una nafasi kadhaa, hizi nafasi nyingine tumwachie mtu mwingine. Hiyo inakuja kutokana na maelekezo yetu kwenye fungu la 22 kwamba; mtu mmoja kofia moja. Ukiwa kiongozi una dhamana tayari basi hii nyingine waachie wengine nao waweke mawazo yao katika kupeleka mbele chama chetu.”
Mbunge wa Nzega Mjini(CCM), Hussein Bashe katika maoni yake alisema dhana ya ukazi imepitwa na wakati pamoja na kuwa inaenda kinyume na Katiba, kanuni na tamaduni za chama hicho.
“Nimeisikia kauli ya katibu wangu nadhani ni kauli ambayo inahitaji mjadala mpana, binafsi naamini chama chetu kina katiba, Kanuni na maadili. Utamaduni huu ndo msingi a chama chetu ambao unatuongoza,” alisema.
Bashe alisema dhana ya aina hiyo ikipewa fursa siku moja itakuja hoja ya kwamba anayetakiwa kugombea uchaguzi ni lazima awe mchaga, ikiwa hoja ya mkazi itakosa uhalali na nguvu kisiasa.
“Fursa aina hii ya mawazo ikipewa uhalali, siku moja hoja ya mkazi ikikosa uhalali na nguvu ipo siku tutatumia ukabila, ikiisha tutasema udini kwa kuwa ukiwa muislamu utayajua sana matatizo ya waislamu,” alisema.
Bashe alisema mbunge anayo majukumu yake nayo ni uwakilishi na kwamba, mbunge kuwa mkazi haiwezi kumfanya azifahamu shida za watu yapo mambo ya msingi ambayo yanatakiwa kutazwa.
“Je Mbunge ametimiza majukumu yake? Ametimiza ahadi zake? Amekuwa muwakilishi mzuri wa wananchi wake? Dhana hii binafsi naiona kama ni dhana ‘aoutdated’ (imepitwa na wakati),” alisema.
Alisema kuwa hoja ya mkazi haimfanyi mtu kuwa mwakilishi mzuri na ifahamike kwamba wabunge wengi wanafanya shughuli mbalimbali ikiwazo zao binafsi zinazosaidia maendeleo ya wananchi wake.
“Mwalimu Nyerere alitengeneza mifumo toka Tanu mpaka CCM ya kumuandaa kiongozi kuanzia Chipukizi, Yuth Legue.Haya ni maeneo ya majaribo na makosa
Alisisitiza kuwa zipo nafasi ambazo kiongozi hatakiwi kutoa kuli yenye Taswira ya kuwagawa watanzania kwa msingi wowote ule hata kama utakuwa na nia njema.
“Tumeona kauli ya Silima, ni kauli sahihi kabisa. Hivi karibuni kumekuwa na matamko controversial ambayo unajiuliza duh hivi Katibu Mkuu yupo wapi? Hata kama tunafanya reform, hii ni njia sahihi? Vitisho vimekuwa vingi sana,”alisema Bashe.
Alieleza kuwa CCM ni wanachama na wanachama
“Leo wana CCM wameanza kuwa wanyonge na hofu ya kukosa ari. Tumeanza kujenga tabaka la watawala na watawaliwa ndani ya chama, ni muhimu sana kila kiongozi aheshimu katiba na kupima kauli zetu,”.
Source: Mwananchi

Audio | Jygga Lo Ft. Becka Tittle – Hawaniwezi | Mp3 Download

Audio | Jygga Lo Ft. Becka Tittle – Hawaniwezi | Mp3 Download

https://hearthis.at/baraka-matara-junior-vu/jyyga-lo-ft-becka-tittle-hawaniwezi/download/

AUDIO | Lady Jay Dee _ Penzi la kweli | Download

Audio | Lady Jay Dee _ Penzi la kweli | download

https://hearthis.at/baraka-matara-junior-vu/lady-jay-dee-penzi-la-kweli/download/

Audio | King Kaka FT Didge _ Lote | Download

https://hearthis.at/baraka-mat
ara-junior-vu/king-kaka-ft-didge-lote/download/

Audio | DJ Olu ft Davido, Mayorkun & Danagog – Bambiala | Mp3 Download

Audio | DJ Olu ft Davido, Mayorkun & Danagog – Bambiala | Mp3 Download

https://hearthis.at/baraka-matara-junior-vu/dj-olu-ft-davido-mayorkun-danagog-bambiala/download/

MAGAZETI YA LEO 18/10/2017













Mji Wa Raqqa Wa Syria Wakombolewa,,,,

Bendera ya wanamgambo wa kupambana na kundi la wanamgambo wenye msimamo mkali la I-S imekuwa ikipepea juu ya mji wa Raqqa, baada ya kuuweka mji huo wa Syria katika himaya yake baada ya mapambano ya nguvu ya miezi minne mfululizo.
Wanamgambo hao wenye asili ya Kurdi na Uarabuni wametoa tamko la kwamba sasa wanaudhibiti mji wa Raqqa, lakini wasaidizi wao Marekani wameonya kuwa wapiganaji hao wa Kiislam wanaokadiriwa kufikia mia moja wanaishi katika mji huo na kwamba Marekani imesema kwamba iko tayari kutoa usaidizi wowote utakao hitajika.
Tatizo lingine kubwa lililopo kwa sasa ni ukusanyaji na uondoaji wa mabomu yaliyosimikwa kwatika makazi ya watu na kwenye mji wote wa Raqqa.
Waangalizi wa masuala ya kimataifa wamearifu kuwa zaidi ya watu elfu tatu wameuawa katika kipindi cha mapambano ya kuukomboa mji huo, na miongoni mwao theluthi moja ni raia.

Nassari Awavimbia Takukuru......

MBUNGE wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (Chadema), amepinga onyo alilopewa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) la kutoweka hadharani taarifa anazowafikishia kuhusiana na flashi za tuhuma za rushwa na kusisitiza kuwa hataacha kufanya hivyo.
Akizungumza jana ikiwa muda mfupi baada ya kupata taarifa za onyo alilopewa na Takukuru, Nassari alisema haoni kama anavunja sheria kwa kuuarifu umma juu ya kila hatua anayoichukua kuhusiana na taarifa za rushwa anazozifikisha Takukuru.
Hivi karibuni, kwa nyakati tofauti, Nassari amekuwa akizungumza na waandishi wa habari kuelezea anavyofikisha taarifa Takukuru kuhusiana na kile anachodai kuwa ushahidi juu ya tuhuma za rushwa za baadhi ya viongozi mkoani Arusha.
Jana, Takukuru kupitia kwa Mkurugenzi Mkuu wake, Kamishna wa Polisi Valentino Mlowola, ilitoa onyo lililotajwa kuwa la nne kwa mbunge huyo kuhusu mwenendo wake wa kuzungumza na vyombo vya habari juu ya tuhuma za rushwa anazowafikishia na kumtaka kukaa kimya wakati uchunguzi wa suala lake ukiendelea.
Nassari amekuwa akiwasilisha kwenye ofisi za Takukuru ‘flashi’ na CD zenye video anazodai zinaonyesha jinsi viongozi wa serikali jijini Arusha walivyokuwa wakiwashawishi kwa rushwa madiwani kadhaa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ili wahamie Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Siwezi kukaa kimya. Nitaendelea kuzungumza na vyombo vya habari… wananchi wana haki ya kupata taarifa,” alisema Nassari kuiambia Nipashe jana baada ya kusikia onyo alilopewa na Takukuru.
Katika hoja yake, Nassari alidai kuwa aliamua kuwasilisha ushahidi Takukuru kuthibitisha madai yake kwamba kuna madiwani wawili wa Chadema waliotangaza kujiunga na CCM hivi karibuni walishawishiwa kwa rushwa.
Nassari aliwasilisha kile alichodai kuwa ni ushahidi wa vitendo vya rushwa kwa mara ya kwanza Oktoba 2, 2017 akisindikizwa na wabunge wenzake wa Chadema, Peter Msigwa (Iringa Mjini) na Godless Lema (Arusha Mjini). Alienda tena Takukuru kuwasilisha ushahidi wake wa pili Oktoba 4, 2017 kabla ya juzi kuwasilisha ushahidi wake wa tatu.
ONYO LA TAKUKURU
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamishna Mlowola alisema wameshamwonya Nassari mara tatu juu ya kitendo chake cha kuzungumza na waandishi wa habari na kueleza kile kinachojiri wakati wa mazungumzo kati yao na mbunge huyo.
Mlowola alimtaka mbunge huyo kukaa kimya na ‘akome’ kuzungumzia suala hilo kwenye vyombo vya habari kwa sababu vinginevyo, anaweza anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari jana, Kamishna Mlowola alisema:
"Oktoba 2 mwaka huu, Nassari akiwa na wabunge wenzake Mchungaji Peter Msigwa na Godbless Lema, walikuja ofisini kwetu. Wakatoa taarifa zao na tukapokea… na tukawaambia hicho kilichowasilishwa tutafanyia kazi.
"Lakini kwa mshtuko baada ya kupokea taarifa, tukashangaa wanaongea na waandishi wa habari kuhusu kilichojiri wakati awali tuliwaambia tukio hili wasilifanye kisiasa. Na tuliwaonya wasiongee na waandishi.”
Mlowola alisema kuwa kwa mara nyingine, Oktoba 4, 2017, Nassari alifika tena Takukuru na kutoa maelezo kwao na alipotoka ofisini kwao, aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kueleza yale yaliyojiri kwenye mazungumzo yao, licha ya ukweli kuwa awali walishamkanya aache kufanya hivyo.
Alisema Oktoba 16 (juzi), Nassari alifika tena katika ofisi za Takukuru kuwasilisha taarifa zingine na alipomaliza, alifanya kitendo kile kile cha kuzungumza na waandishi wa habari na kueleza hatua ambazo zimeshanza kuchukuliwa, ijapokuwa alipewa angalizo kwa mara nyingin e la kutokufanya jambo hilo.
“Tunamwonya Nassari, ameshaleta taarifa kwetu na atuache tufanye kazi kwa mujibu wa sheria na siyo kutushinikiza,” alisema Kamishna Mlowola na kuongeza:
“Natoa onyo lingine… endapo ataendelea na tabia hii tutazingatia sheria na tutachukua sheria dhidi yake, bila kuathiri taarifa yake aliyotupa kuifanyia kazi."
Mlowola aliongeza kuwa Sheria ya Takukuru inawapa mamlaka ya kufanya kazi kwa uhuru bila ya shinikizo.
Alisema Takukuru inapokea taarifa zinazohusiana na rushwa au makosa ya rushwa kutoka vyanzo mbalimbali vikiwamo vya wazi na vya siri.
Alisema taarifa wanaipokea kutoka kwa mtu yeyote na anaweza kuwa mtakatifu, shetani, mwendawazimu au mwenye akili timamu, lakini hatua ya kwanza kwao inakuwa ni kupokea taarifa na mengine hufuata baadaye.
Alisema Takukuru inapopeleleza huwa inaangalia kama kuna kosa limetendwa na kufikishwa katika chombo kingine kilichotengwa ambacho ni mahakama kupitia kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).
“Hatukutarajia kuwa na drama (maigizo) na watu wanapaswa kufahamu kuwa Nassari ameleta taarifa na siyo ushahidi… ushahidi una sifa zake,” alisema Kamishna Mlowola.
Alibainisha kuwa kifungu cha 37 cha makosa ya rushwa, kinaeleza kuhusu makosa ya jinai yanayoweza kutendwa na mtoa taarifa.
Alisema Nassari alikuwa ni mtoa taarifa na Takukuru ina wajibu wa kumlinda mtoa taarifa na kwamba kinyume chake, Nassari amejionyesha mwenyewe katika vyombo vya habari kuwa ndiye aliyewapatia taarifa.
“Tunachokiona sisi hapo, Nassari na wenzake wanataka kulifanya suala hili kama la kisiasa badala ya sheria. Tuzingatie sheria. Chombo chenye mamlaka tukiache kifanye kazi yake,” alisema Kamishna Mlowola.
Alisema kuihusisha Takukuru katika malumbano na ulingo wa kisiasa si vizuri kwa kuwa jukumu la Takukuru siyo kufanya siasa.
Alisema uchunguzi unaweza kuonyesha kilichotokea katika tukio hilo ni kosa au siyo kosa kwa kuwa inawezekana kuna makosa yanafanyika mtu akadhani ni ya jinai, kumbe ni makosa ya kawaida ambayo yanahitaji utaratibu mwingine wa kuyashughulikia.

Mtambo Wa kuchomea taka unavyohatarisha afya za wananchi Mkuranga,,,

Wakazi wa kijiji cha Dundani wilayani Mkuranga wako katika hatari ya kupata magonjwa yanayosababishwa na moshi mzito unaozalishwa na mtambo mkubwa wa kuchoma takataka za hospitali ulio jirani na makazi yao.
Uchunguzi wa Mwananchi umegundua kuwa mtambo huo mkubwa kuliko yote nchini kwa kazi hiyo ulijengwa kabla ya kufanyika kwa tathmini ya athari ya mazingira (EIA) na sasa umegeuka kero kwa wakazi hao. Mbali na uchomaji wa taka za hospitali, tanuru hilo linaloendeshwa na kampuni ya Safe Waste Incinerator linatumika pia kuchomea dawa zilizoisha muda wa matumizi na zile zinazogundulika kuwa si halisi (feki).
Kutokana na hali hiyo, wakazi wa Dundani wameziomba mamlaka zinazohusika kuingilia kati ili kunusuru afya zao na mazingira.
Kabla ya kiwanda hicho kuanza kuteketeza kiwango kikubwa cha taka hizo hakuna mkazi aliyehisi hatari iliyokuwa mbele, lakini sasa uteketezaji wa kiwango kikubwa umewafanya wakasirishwe.
Wakati mwekezaji huyo akijenga mtambo huo kati ya mwaka 2013 na 2014 hakukuwa na wakazi eneo hilo, lakini kwa sasa mtambo huo umezungukwa na makazi ya watu ambao sasa wanataka ama uhamishwe au zibuniwe mbinu mpya za kudhibiti moshi na harufu kali.
Kadhia hiyo imewaweka viongozi wa kisiasa na maofisa afya wilayani Mkuranga katika wakati mgumu kutokana na lawama za wananchi.
Malalamiko kila kona
“Hatujui hizi takataka ni kabila (aina) gani kwa sababu hatushirikishiwi na wala hajafika mwenye kiwanda kutuambia anachoma kitu gani,” alisema Mbarka Salumu mkazi wa Dundani.
“Ile harufu tunayoisikia ukisema ni mtu anachomwa ni sawa tu! Ukisema wadudu wanachomwa sawa! Na ukisema sumu inachomwa sawa tu kwa sababu ni harufu chafu kabisa.” Kwa mujibu wa Salumu, mtambo huo unapowashwa, moshi husambaa na kuingia mpaka ndani ya nyumba zao. “Tunataka tusaidiwe ili hii kero itutoke, ifike wakati huyu bwana atolewe sehemu hii ili tusidhurike,” anaongeza.
Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linasema halijapokea taarifa rasmi kuhusu kero hiyo. “Hili tatizo tumelisikia juzi tu na ndio tunakwenda kukagua. Ni mpaka tutakapofika na kuona hali halisi ndipo nitakapokuwa katika nafasi ya kulizungumzia hili zaidi,” alisema ofisa wa NEMC, Alfred Msokwa.
Alisema Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga ilimpa kibali mwekezaji kujenga mtambo huo, ambao hauwashwi kila siku kabla ya kufanyika kwa tathmini ya athari za mazingira. “Halmashauri zetu wakati mwingine huruhusu kujengwa kwa mitambo kama hii zikilenga kuongeza mapato na kusahau suala la mazingira na afya za watu. Wakati mwingine vibali vinatolewa katika ngazi ya halmashauri, halafu wanashindwa kuwasimamia,” alisema. Ofisa mmoja wa kampuni inayolalamikiwa aliyeomba kutotajwa jina, alisema wamepata malalamiko hayo kupitia vyombo vya habari, akisema ni “changamoto za kawaida katika biashara”.
“Tumepigiwa simu na watu kadhaa kutoka Mkuranga wakitaka tu-surrender documents (tusalimishe nyaraka). Tumewaandikia kutafuta muda mwafaka ili tukae na mamlaka zote husika na kuwajibu wanayoyataka kwetu kwa pamoja,” alisema ofisa huyo. Mkazi mwingine wa Dundani, Saidi Hamisi, alisema haelewi kinachochomwa.
“Ni kama (harufu) ya dawa za hospitali. Na watu ukiwauliza wengine wanasema zinachomwa simu za zamani, wengine wanasema dawa za hospitali zinazotoka Bohari Kuu, sasa hatuelewi ni kitu gani,” alisema. “Moshi ni mzito sana na harufu inayokuja inakuwa ya mchangayiko, sasa kwa kuwa lile bomba halijaenda juu sana ule moshi unaishia kusambaa chini.
“Kipindi alivyonunua huku palikuwa bado pori, kwa ushauri wangu kwa sababu huku mji umeshaingia basi hiki kiwanda kihamishwe au bomba liende hewani ili ule moshi unapotoka sisi tusiathirike.”
Kero ya moshi mzito na harufu kali imelalamikiwa pia na wanawake wakiwemo wajawazito.
“Harufu kama hii inatuumiza sana sisi wajawazito, tunaumia, tunaombwa tusaidiwe,” alilalamika mwanamke mjazito aliyeomba kutotajwa jina. Malalamiko ya mjamzito huyo yaliakisiwa pia na Rajma Saidi.
“Mtu unaweza kupika chakula na usikile kwa sababu harufu inayotoka huko ni mbaya kupita kiasi kwa hiyo tunakereka sana. Tunashukuru umefika ukatoe salamu huku hali si nzuri,” alisema Rajma
Ofisa msaidizi wa afya wilayani Mkuranga, Juma Shari alisema wamefuatilia malalamiko na kuthibitisha kuwa ni ya kweli.
“Kiwanda kipo kwa chini na maeneo ya makazi yako juu. Kwa hiyo katika uchomaji wao, moshi husambaa kwa urahisi zaidi kwenye eneo la makazi,” alisema Shari.

AUDIO | Sharpa tz Ft Brown Punch_hawa watu | Download

https://hearthis.at/djmwanga/sharpa-tz-ft-brown-punch-hawa-watu/download/