Msanii wa muziki, Vanessa Mdee amedai ametumia gharama kubwa katika kuiandaa albamu yake mpya MoneyMonday.
Muimbaji huyo amesema kuwa albamu ya MoneyMonday mpaka kukamilika imemgharimu zaidi ya shilingi za Kitanzania Milioni 100.
“Nimetumia fedha nyingi lakini kwangu sioni tatizo lolote, niliangalia zaidi jinsi gani watu watatambua Vanessa kafika wapi katika kukua kimuziki, fedha hiyo nililipa idara zote kuanzia wasanii walioshiriki matangazo, video nk na bado naendelea kutoa kwa kuwa matangazo bado yanaendelea ,” Vanessa aliuambia mtandao wa Dar 24.
Ameongezea kuwa hajutii matumizi ya kiasi hicho kikubwa cha fedha kwa kuwa lengo lake hasa ni kutoa kazi itakayomwongezea heshima kwenye muziki wake sambamba na kuhakikisha inawifikia watu wa aina zote.
Hivi karibuni Vanesa ameachia albamu yake katika ukumbi wa Mlimani City.
Vanessa ni kati ya wasanii wachache ambao wanajaribu kurudisha utamaduni wa kutengeneza Albamu katika muziki wa Bongo fleva jambo ambalo kwa siku za nyuma limekuwa likififia na kupotea.
Naye Diamond Platinum anajipanga kuaachia albamu yake ya Mtoto wa Tandale ambapo juzi alitaja baadhi ya sababu zilizomfanya acheleweshe kutoka kwa albamu hiyo.
Waziri wa mambo ya ndani nchini, Mwigulu Nchemba leo ameongoza oparesheni ya kuteketeza jumla ya ekari sita za bangi zilizokuwa zimelimwa katikati ya msitu ndani ya kijiji cha Engalaoni wilayani Arumeru mkoani Arusha.
Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya CHADEMA, Mhe. Peter Msigwa amefunguka na kumchana Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala na kudai kuwa anafanya kazi kwa mizuka na mihemko na kuisumbua sekta ya Utalii na Maliasili nchini.
Arusha. Mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki (Chadema) Joshua Nassari, ameitaka Serikali kutoa tamko moja juu ya michango ya chakula shuleni kama ni halali ama la ili kuzuia migogoro ambayo imeanza kuibuka.
Wakulima wa mahindi mkoani Njombe wamedai kuwa bado hawajaanza kuona manufaa ya kufunguliwa kwa mipaka kutokana na wafanyabiashara kutochukua mahindi waliyonayo licha ya bei ya zao hilo ikiwa ni chini ya kawaida.
Habari kutoka Hispania zinaeleza kuwa meneja wa zamani wa klabu ya Barcelona, Luis Enrique ameonekana kukubali kurithi mikoba ya kocha Antonio Conte ndani ya Chelsea.
Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji amesema mgombea udiwani wa chama hicho Kata ya Buhangaza Wilaya ya Muleba mkoani Kagera, Athanas Makoti (28) alilazimishwa kupokea rushwa ya Sh8milioni na watu waliomteka na kumjeruhi ili ajitoe kwenye uchaguzi.
Baraza la Waislamu Tanzania BAKWATA, kupitia kwa Msemaji wa Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Khamis Mataka leo wametoa majina ya Taasisi 15 ambazo zimekubaliwa na kupewa idhini ya kupeleka Mahujaji ambao wataenda kuhiji na pia zimeratibiwa na kupewa hisa ya kufanya safari.
