Wednesday, 7 February 2018

Hii ndio gharama aliyotumia Vanessa Mdee kuandaa albamu yake mpya ‘MoneyMonday’

Msanii wa muziki, Vanessa Mdee amedai ametumia gharama kubwa katika kuiandaa albamu yake mpya MoneyMonday.

Muimbaji huyo amesema kuwa albamu ya MoneyMonday mpaka kukamilika imemgharimu zaidi ya shilingi za Kitanzania Milioni 100.

“Nimetumia fedha nyingi lakini kwangu sioni tatizo lolote, niliangalia zaidi jinsi gani watu watatambua Vanessa kafika wapi katika kukua kimuziki, fedha hiyo nililipa idara zote kuanzia wasanii walioshiriki matangazo, video nk na bado naendelea kutoa kwa kuwa matangazo bado yanaendelea ,” Vanessa aliuambia mtandao wa Dar 24.

Ameongezea kuwa hajutii matumizi ya kiasi hicho kikubwa cha fedha kwa kuwa lengo lake hasa ni kutoa kazi itakayomwongezea heshima kwenye muziki wake sambamba na kuhakikisha inawifikia watu wa aina zote.

Hivi karibuni Vanesa ameachia albamu yake katika ukumbi wa Mlimani City.

Vanessa ni kati ya wasanii wachache ambao wanajaribu kurudisha utamaduni wa kutengeneza Albamu katika muziki wa Bongo fleva jambo ambalo kwa siku za nyuma limekuwa likififia na kupotea.

Naye Diamond Platinum anajipanga kuaachia albamu yake ya Mtoto wa Tandale ambapo juzi alitaja baadhi ya sababu zilizomfanya acheleweshe kutoka kwa albamu hiyo.

Waziri Nchemba aongoza oparesheni ya kuteketeza ekari sita za bangi

Waziri wa mambo ya ndani nchini, Mwigulu Nchemba leo ameongoza oparesheni ya kuteketeza jumla ya ekari sita za bangi zilizokuwa zimelimwa katikati ya msitu ndani ya kijiji cha Engalaoni wilayani Arumeru mkoani Arusha.

Mwigulu akishirikiana na kamanda wa jeshi la polisi mkoani Arusha,(RPC)Charles Mkumbo pamoja na vikosi vya askari wa jeshi la polisi mkoani hapa walilazimika kuacha magari yao njiani na kutembea umbali wa kilomita 5 milimani kufika katikati ya msitu huo ambapo wamiliki wa mashamba hayo walitokomea kusikojulikana.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa zoezi hilo Mwigulu alisema kwamba serikali itaendelea na oparesheni pande zote za nchi na haitasita kuwakamata wahusika wote na kutaifisha magari yatakayotumika kusafirisha bangi.

Akizungumza na askari waliokuwa wakishiriki katika zoezi hilo Mwigulu mbali na kuwapongeza kwa kazi wanayofanya lakini aliwambia kwamba pamoja na kufanikiwa kuteketeza madawa ya kulevya yanayolimwa mashambani lakini waongeze juhudi pia katika kupambana na madawa ya kulevya yanayotengenezwa viwandani.

“Niwapongeze sana songeni mbele na kazi ya kukamata madawa yote ya kulevya mmefanya kazi kubwa sana ya kukabiliana na madawa ya kulevya yanayolimwa mashambani ongezeni bidii kukamata na yale yanayozalishwa viwandani,” alisema Waziri Mwigulu.

Hata hivyo, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Arusha(RPC),Charles Mkumbo alisema kwamba jumla ya ekari sita za mashamba ya bangi zimeteketezwa na kusisitiza kwamba oparesheni hiyo ni endelevu katika mkoa wa Arusha na wilaya zake.

Aidha Kamanda Mkumbo alifichua mbinu mpya wanayotumia wamiliki wa mashamba hayo kwamba kwa sasa wameamua kulima mashamba hayo katikati ya misitu kwa lengo la kujificha ili kukwepa mkono wa sheria.

“Walidhani kulima bangi katikati ya misitu hatutawakamat sisi tuna mbinu nyingi na hatutakubali kuona vijana wetu wanaharibikiwa kwasababu ya bangi.”

Vanessa Mdee atoa ufafanuzi kuhusu ngoma zake na Diamond kuchezwa Nigeria



Msanii wa muziki Bongo, Vanessa Mdee ametolea ufafanuzi kauli yake iliyodai alipofika Nigeria alikuta ngoma za wasanii toka Bongo zinazochezwa ni zake na za Diamond.

Baada ya kauli hiyo Vanessa amekuwa akishambuliwa na mashabiki hasa wa team Kiba kuwa kauli yake ni yenye upendeleo kwa upande mmoja. Kupitia Instagram Vanessa ameamua kumjibu shabiki aliyehoji kuhusu hilo.

vanessamdee @ze_masta my love hiyo issue nilikuwa nazungumza kitu kikubwa zaidi lakini wenye akili zao wamegeuza imekuwa hivyo. Na Ukiangalia lengo la jibu langu ilikuwa kuwahamasisha waTanzania wathamini na waPromote zaidi mziki wa home maana wenzetu ndivyo wanavyofanya.

Sasa wapi hapo nimemdiss kaka? Kaka anajua mimi shabiki yake sasa tutafika kweli kila neno linageuzwa kuwa negative when in truth I was just shedding light on what I was seeing. Jamani.

Hapo Jux Vanessa aliiambia Clouds Fm alipoenda Nigeria kwa ajili ya kutangaza albamu yake ‘Money Mondays’ katika moja club alizopita alikuta ngoma zinazochezwa kutoka Bongo ni ya Patoranking na Diamond ‘Love You Die’ na ile aliyoshirikiana na Reekado ‘Move’.

Msigwa amfungukia Kigwangalla Bungeni

Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya CHADEMA, Mhe. Peter Msigwa amefunguka na kumchana Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala na kudai kuwa anafanya kazi kwa mizuka na mihemko na kuisumbua sekta ya Utalii na Maliasili nchini.

Msigwa amesema hayo wakatii alipokuwa akichangia bungeni taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji, mjini Dodoma na kudai kuwa Mawaziri vijana wamekuwa na mihemko.

"Niwashauri hawa Mawaziri vijana fursa 'opportunity is atrracted by talent, skills, perfomance and abillity. Show your talent and abillity people will love you' hawa Mawaziri wa zamani hawa kwa mfano Lukuvi, Tizeba tunawaona wakijibu hoja wanajibu hoja siyo za kimihemko kiasi kwamba unaridhika hata Waziri akikujibu unapenda lakini Mawaziri vijana wengi mnaonekana mnayofanya katika Serikali hii kiasi kwamba Serikali ijayo muonekane hamna tija" kwa sababu mna mihemko sana"

Mbali na hilo Msigwa alikwenda mbali zaidi na kumnyooshea mkono Waziri wa Maliasili na Utalii na kudai amekuwa na maamuzi ya ajabu jambo ambalo linapelekea kiongozi huyo kuivuruga Wizara hiyo.

"Utalii huu umejengwa kwa muda mrefu sana na akitokea mtu mmoja anaamua kufanya tu kwa kutafuta umaarufu atauvuruga kwa muda mfupi sana, Utalii kwenye pata la taifa unaingiza asilimia 20 na forex ni kubwa inatokana na utalii kwa hiyo hicho si kitu kimoja mtu anaweza kuamka leo anasema nimeharibu na hii diplomasia ya kiuchumi inategemea sana na kutabirika, wawezekaji huko nje wanataka kuona kunatabirika wao kufanya biashara zao. Haiwezekani huyu Waziri anatoa amri mpaka mapolisi wanamkataa anashindwa hata kuwasiliana na Waziri wake wa Mambo ya Ndani, huyu huyu Waziri anatoa amri anapingana na Waziri wa Ardhi, huyu huyu Waziri mmoja anapingana na Waziri wa Uvuvi hatuwezi kuwa na Mawaziri ambao wanakuwa na mizuka na kufanya kazi kwa mizuka wote kama tunalipenda taifa letu tufanye kazi kwa kupendana" alisisitiza Mchungaji Msigwa

. Nassari: katika Jimbo langu kumeanza kuibuka migogogro juu ya michango

Arusha. Mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki (Chadema) Joshua Nassari, ameitaka Serikali kutoa tamko moja juu ya michango ya chakula shuleni kama ni halali ama la ili kuzuia migogoro ambayo imeanza kuibuka.

Akizungumza na Mwananchi leo Februari 7 Nassari amesema  katika jimbo lake kumeanza kuibuka migogoro juu ya michango ya chakula kwani kuna wazazi ambao walikuwa wamechangia mara baada ya shule kufunguliwa na sasa wanataka warejeshewe michango yao.

‘’Hili  suala limeleta utata mkubwa na mgongano baina ya walimu, Kamati za shule na wazazi, kwani  baadhi ya wazazi wameaminishwa kuwa Serikali imetoa fedha kugharamia mahitaji yote ya shule," amesema

Amesema  ni muhimu kuwepo na tamko moja ni michango gani, ambayo ni marufuku na ipi ambayo inakubalika na hivyo kuwekwa utaratibu mzuri wa kuikusanya.

Alisema anachofahamu ni kuwa Serikali, haijapiga marufuku michango ya chakula, bali kinachotakiwa ni wazazi kutoa kwa hiari yao baada ya kukubaliana katika vikao lakini jambo hili linapaswa kuelimishwa.

Waraka namba 3 wa mwaka 2016 juu ya suala la elimu bure, pia umeeleza jukumu la chakula cha wanafunzi kwa shule za kutwa na sare za shule ni la wazazi.

Diwani wa kata ya Imbaseni, Gabriel Mwanda alisema katika kata yake, kuna wazazi walichanga chakula shuleni, lakini kutokana na tamko la serikali la kuzuia michango wameanza kuidai.

"Hili ni tatizo, tumejaribu kuwaeleza wazazi juu ya umuhimu wa michango baadhi wameelewa na wengine bado hawajaelewa" amesema

Mwanda amesema ni ukweli ni kuwa fedha ambazo zinapelekwa shuleni, hazitoshi mahitaji yote lakini sintofahamu iliyopo sasa isipopatiwa ufumbuzi itaathiri sekta ya elimu.

"Suala la chakula kwa watoto  shuleni ni muhimu sana hivyo tumekuwa tukishauri wazazi kuchanga kwa hiari lakini watoto wasirejeshwe nyumbani kwa wazazi wao kwa kushindwa kuchangia chakula," amesema.

Katika shule nyingi wilaya ya Arumeru, kamati za shule zilikuwa zimepitisha mchango wa debe mbili za mahindi na kilo tano za maharage kwa ajili ya chakula na tayari shule zilipofunguliwa wazazi walichanga.

Hata hivyo, kutokana na kuibuka utitiri wa michango shuleni, hivi karibuni Rais John Magufuli alitangaza kupigwa marufuku walimu kupokea michango mashuleni na akawataka wazazi ambao wanataka kujitolea kupeleka michango yao kwa  wakurugenzi.

Wakulima wa Mahindi watoa kilio chao kwa Serikali

Wakulima wa mahindi mkoani Njombe wamedai kuwa bado hawajaanza kuona manufaa ya kufunguliwa kwa mipaka kutokana na wafanyabiashara kutochukua mahindi waliyonayo licha ya bei ya zao hilo ikiwa ni chini ya kawaida.

Wakulima hao wamesema kuwa kufunguliwa kwa mipaka hakuna faida kwao kwa kuwa mazao hayanunuliwi kutokana na wafanyabiashara wanaotoa mazao nje ya nchi tayari wana mahindi ya kutosha.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti mkoani Njombe wakulima hao wamesema kuwa zao hilo sasa halina soko la uhakika na bei yake imekuwa ni ya chini mpaka shilingi 4500 kwa debe moja la kilo 20 ambazo pamoja na kushuka hakuna mteja anaye fika kununua.

Halmashauri ya wilaya ya Njombe nayo inalalamika kwa kutonunuliwa kwa mazao hayo ambayo ni moja ya chanzo chake cha mapato ambapo awali ilitegemewa wakala wa hifadhi ya chakula (NFRA), watanunua mazao hayo.

Kambale wa Singida United aiomba radhi klabu yake



Nyota wa kimataifa wa Singida United Kambale Salita gentil ameiomba msamaha klabu hiyo baada ya kumsimamisha kwa muda usiojulikana kutokana na utovu wa nidhamu uwanjani.

Taarifa ya klabu hiyo iliyotolewa leo na Mkurugenzi mtendaji Festo Richard Sanga imeeleza kuwa kiungo huyo aliyesajiliwa kwenye dirisha dogo ametambua kosa lake na kuomba kupunguziwa muda wa adhabu.

Sehemu ya taarifa hiyo pia imenukuu maneno ya Kambale ambaye amesema, ''Naomba sana mnisamehe, mimi ni mtoto wenu, mimi ni kijana wenu na mimi ni mfanyakazi wenu, naomba wachezaji wenzangu wanisamehe pamoja na uongozi wa klabu yangu, tukio hili halitajirudia tena''.

Kambale alimpiga mchezaji wa timu ya Green Worriors kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho kitendo kilichopelekea kuoneshwa kadi nyekundu. Singida United ilishinda mchezo huo na kusonga mbele.

Singida United leo jioni inashuka kwenye dimba la CCM Kirumba kukipiga na wenyeji Mbao FC kwenye mchezo wa ligi kuu. Singida United inashika nafasi ya nne ikiwa na alama 30.

Luis Enrique akubali kurithi mikoba ya Antonio Conte?

Habari kutoka Hispania zinaeleza kuwa meneja wa zamani wa klabu ya Barcelona, Luis Enrique ameonekana kukubali kurithi mikoba ya kocha Antonio Conte ndani ya Chelsea.

Nafasi ya Conte ndani ya kikosi cha Blues imeonekana kuwa mashakani tangu wiki iliyopita baada ya kupata matokeo mabaya ya kufungwa 3 – 0 dhidi ya Bournemouth na yale ya 4-1 mbele ya Watford siku ya Jumatatu.

Kufuatia mwenendo wa kusuasua kwa kikosi cha Chelsea mmiliki wa timu hiyo Mromania Abramovich anampango wa kumpatia mkataba wa miaka miwili na nusu kocha Enrique mwenye umri wa miaka 47 ambao atakuwa the blues hadi mwaka 2020 hii ni kwa mujibu wa chombo cha Sports.

Chadema yasema mgombea Udiwani wa Chama hicho alipewa fedha ajitoe

Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji amesema mgombea udiwani wa chama hicho Kata ya Buhangaza Wilaya ya Muleba mkoani Kagera, Athanas Makoti (28) alilazimishwa kupokea rushwa ya Sh8milioni na watu waliomteka na kumjeruhi ili ajitoe kwenye uchaguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 7, 2018 makao makuu ya Chadema, Kinondoni jijini Dar es Salaam, Dk Mashinji ameliomba Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa tukio hilo na kuchukua hatua.

Makoti alitekwa Februari 2, 2018 katika mazingira ya kutatanisha na kupatikana Februari 5, 2018 saa moja asubuhi akiwa ametelekezwa na watu wasiojulikana jirani na Hospitali ya Kagando iliyopo Wilaya ya Muleba. Mgombea huyo amelazwa katika hospitali hiyo mpaka sasa.

Dk Mashinji amesema Makoti alikuwa anatoka kwenye maandalizi ya uchaguzi, akaita bodaboda ili arejee nyumbani lakini likatokea gari nyuma yake na kumchukua kwa nguvu.

“Watekaji hao walimfunga kitambaa usoni akapoteza fahamu. Walimzungusha maeneo mbalimbali na alipozinduka hakujua aliko. Walimtaka akubali kupokea Sh8 milioni na ajitoe kwenye uchaguzi, hata hivyo alikataa ndipo wakaanza kumtesa,” amesema Dk Mashinji,

“Hizi ni njama za kisiasa kutaka kuvuruga uchaguzi katika kata ya Buhangaza,” amesema.

Amesema kwa mujibu wa maelezo ya mgombea huyo, alitekwa kwa madhumuni ya kisiasa.

“Tunalaani  kitendo cha mgombea wetu kutekwa, kuteswa na kulazimishwa kupokea fedha ili ajitoe kwenye uchaguzi,” amesema.

VIDEO: BAKWATA Watoa Tamko

Baraza la Waislamu Tanzania BAKWATA, kupitia kwa Msemaji wa Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Khamis Mataka leo wametoa  majina ya Taasisi 15 ambazo zimekubaliwa na kupewa idhini ya kupeleka Mahujaji ambao wataenda kuhiji na pia zimeratibiwa na kupewa hisa ya kufanya safari.

Sheikh Mataka amewataka waislamu wote nchini kuzingatia taratibu zote zilizowekwa na BAKWATA ili kuepuka usumbufu ama matapeli ambao wanajitokeza kwa kipindi cha kuelekea HIJJA.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHU KUSUBSCRIBE


VIDEO: Uchumi wa Tanzania umepanda na nakuongoza kuwa na Uongozi Bora

Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas, amesema hali ya uchumi wa Tanzania imeimarika ikilinganishwa na awamu zilizopita ambapo imeshika nafasi ya 48 kwa nchi zenye uchumi jumuishi duniani, pia ni ya pili Afrika ikifuatiwa na Tunisia ambapo kusini mwa jangwa la Sahara ni ya kwanza.

Abbas alikuwa akizungumza leo jijini Dar es Salaam na  waandishi wa habari ambapo mambo mengine aliyozungumzia ni kuhusu kifo cha mkongwe wa siasa nchini marehemu Kingunge Ngombale-Mwiru aliyemuita kuwa ni msahafu wa siasa za Tanzania.
Pia Abbas alitumia fursa hiyo akisema kwamba atakuwa na utaratibu maalum wa  kuzungumza na waandishi wa habari kila mwisho wa mwezi ambao utatolewa karibuni.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI.....................USISAHAU KUSUBSCRIBE...................

Audio | Timbulo – Promise | Mp3 Download

Audio | Timbulo – Promise | Mp3 Download

Audio | Timbulo – Promise | Mp3 Download

DOWNLOAD

New VIDEO: Mesen Selekta Ft Rayako – Kinanda

New VIDEO: Mesen Selekta Ft Rayako – Kinanda

New VIDEO: Mesen Selekta Ft Rayako – Kinanda


DOWNLOAD VIDEO