Wednesday, 7 February 2018

Chadema yasema mgombea Udiwani wa Chama hicho alipewa fedha ajitoe

Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji amesema mgombea udiwani wa chama hicho Kata ya Buhangaza Wilaya ya Muleba mkoani Kagera, Athanas Makoti (28) alilazimishwa kupokea rushwa ya Sh8milioni na watu waliomteka na kumjeruhi ili ajitoe kwenye uchaguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 7, 2018 makao makuu ya Chadema, Kinondoni jijini Dar es Salaam, Dk Mashinji ameliomba Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa tukio hilo na kuchukua hatua.

Makoti alitekwa Februari 2, 2018 katika mazingira ya kutatanisha na kupatikana Februari 5, 2018 saa moja asubuhi akiwa ametelekezwa na watu wasiojulikana jirani na Hospitali ya Kagando iliyopo Wilaya ya Muleba. Mgombea huyo amelazwa katika hospitali hiyo mpaka sasa.

Dk Mashinji amesema Makoti alikuwa anatoka kwenye maandalizi ya uchaguzi, akaita bodaboda ili arejee nyumbani lakini likatokea gari nyuma yake na kumchukua kwa nguvu.

“Watekaji hao walimfunga kitambaa usoni akapoteza fahamu. Walimzungusha maeneo mbalimbali na alipozinduka hakujua aliko. Walimtaka akubali kupokea Sh8 milioni na ajitoe kwenye uchaguzi, hata hivyo alikataa ndipo wakaanza kumtesa,” amesema Dk Mashinji,

“Hizi ni njama za kisiasa kutaka kuvuruga uchaguzi katika kata ya Buhangaza,” amesema.

Amesema kwa mujibu wa maelezo ya mgombea huyo, alitekwa kwa madhumuni ya kisiasa.

“Tunalaani  kitendo cha mgombea wetu kutekwa, kuteswa na kulazimishwa kupokea fedha ili ajitoe kwenye uchaguzi,” amesema.

VIDEO: BAKWATA Watoa Tamko

Baraza la Waislamu Tanzania BAKWATA, kupitia kwa Msemaji wa Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Khamis Mataka leo wametoa  majina ya Taasisi 15 ambazo zimekubaliwa na kupewa idhini ya kupeleka Mahujaji ambao wataenda kuhiji na pia zimeratibiwa na kupewa hisa ya kufanya safari.

Sheikh Mataka amewataka waislamu wote nchini kuzingatia taratibu zote zilizowekwa na BAKWATA ili kuepuka usumbufu ama matapeli ambao wanajitokeza kwa kipindi cha kuelekea HIJJA.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHU KUSUBSCRIBE


VIDEO: Uchumi wa Tanzania umepanda na nakuongoza kuwa na Uongozi Bora

Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas, amesema hali ya uchumi wa Tanzania imeimarika ikilinganishwa na awamu zilizopita ambapo imeshika nafasi ya 48 kwa nchi zenye uchumi jumuishi duniani, pia ni ya pili Afrika ikifuatiwa na Tunisia ambapo kusini mwa jangwa la Sahara ni ya kwanza.

Abbas alikuwa akizungumza leo jijini Dar es Salaam na  waandishi wa habari ambapo mambo mengine aliyozungumzia ni kuhusu kifo cha mkongwe wa siasa nchini marehemu Kingunge Ngombale-Mwiru aliyemuita kuwa ni msahafu wa siasa za Tanzania.
Pia Abbas alitumia fursa hiyo akisema kwamba atakuwa na utaratibu maalum wa  kuzungumza na waandishi wa habari kila mwisho wa mwezi ambao utatolewa karibuni.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI.....................USISAHAU KUSUBSCRIBE...................

Audio | Timbulo – Promise | Mp3 Download

Audio | Timbulo – Promise | Mp3 Download

Audio | Timbulo – Promise | Mp3 Download

DOWNLOAD

New VIDEO: Mesen Selekta Ft Rayako – Kinanda

New VIDEO: Mesen Selekta Ft Rayako – Kinanda

New VIDEO: Mesen Selekta Ft Rayako – Kinanda


DOWNLOAD VIDEO


Audio | Chemical ft Beka Flavour – Asali | Mp3 Download

Audio | Chemical ft Beka Flavour – Asali | Mp3 Download

Audio | Chemical ft Beka Flavour – Asali | Mp3 Download

DOWNLOAD

New Video | Maromboso ( Mbosso ) _ Riziki | Official Video

New Video | Maromboso ( Mbosso ) _ Riziki | Official Video

New Video | Maromboso ( Mbosso ) _ Riziki | Official Video


Sunday, 4 February 2018

DOWNLOAD: Vigour – Pande Zote

DOWNLOAD: Vigour – Pande Zote
Vigour - Pande Zote
DOWNLOAD: Vigour – Pande Zote


Sheria ndogo ya kunyonyesha ndani ya miezi minne kuundwa

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt Rehema Nchimbi amewataka viongozi wa vijiji na kata mkoani humo kuhakikisha wanatunga sheria ndogo ya kunyonyesha ndani ya miezi minne ili kuondokana na tatizo la ukosefu wa lishe kwa watoto.

Dkt Nchimbi ametoa agizo hilo Juzi Ijumaa kwenye hafla ya kukabidhiwa vifaa vya kutambua hali ya lishe kwa watoto na akinamama wajawazito katika kijiji cha Saranda wilayani Manyoni.

“Kunyonyesha ni lazima, Wenyeviti wa vijiji na kata hakikisheni mmetunga sheria ndogo kwa ajili ya kudhibiti akinamama wote wasionyonyesha watoto wao kulingana na taratibu za afya,”amesema Dkt. Nchimbi.

Mhe Nchimbi amelazimika kutoa agizo hilo baada ya kusomewa taarifa inayoonesha kuwa ni asilimia 54 pekee ya watoto mkoani Singida ndio hubahatika kunyonyeshwa maziwa ya mama pekee kwa kipindi cha miezi sita.

Akisisitizia suala hilo Dkt. Nchimbi amesema kuwa ulazima huo usibakie kuwa ni wa majukwaani tu bali utekelezwe kisheria na atakayepatikana aadhibiwe, hata hivyo, mhakikishe adhabu hiyo haisababishi mama kumkimbia mtoto.

Sheria ndogo ya kunyonyesha ndani ya miezi minne kuundwa

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt Rehema Nchimbi amewataka viongozi wa vijiji na kata mkoani humo kuhakikisha wanatunga sheria ndogo ya kunyonyesha ndani ya miezi minne ili kuondokana na tatizo la ukosefu wa lishe kwa watoto.

Dkt Nchimbi ametoa agizo hilo Juzi Ijumaa kwenye hafla ya kukabidhiwa vifaa vya kutambua hali ya lishe kwa watoto na akinamama wajawazito katika kijiji cha Saranda wilayani Manyoni.

“Kunyonyesha ni lazima, Wenyeviti wa vijiji na kata hakikisheni mmetunga sheria ndogo kwa ajili ya kudhibiti akinamama wote wasionyonyesha watoto wao kulingana na taratibu za afya,”amesema Dkt. Nchimbi.

Mhe Nchimbi amelazimika kutoa agizo hilo baada ya kusomewa taarifa inayoonesha kuwa ni asilimia 54 pekee ya watoto mkoani Singida ndio hubahatika kunyonyeshwa maziwa ya mama pekee kwa kipindi cha miezi sita.

Akisisitizia suala hilo Dkt. Nchimbi amesema kuwa ulazima huo usibakie kuwa ni wa majukwaani tu bali utekelezwe kisheria na atakayepatikana aadhibiwe, hata hivyo, mhakikishe adhabu hiyo haisababishi mama kumkimbia mtoto.

Aubameyang aanza kuonyesha makali yake Arsenal

STAA mpya wa Arsenal Pierre-Emerick Aubameyang jana alianza mchezo wake wa kwanza kwenye timu hiyo na kufanikiwa kuifungia bao moja kwenye ushindi wa 5-1 dhidi ya Everton katika mchezo wa Ligi Kuu England.

Aubameyang amejiunga na Arsenal kwenye dirisha hili la usajili na huu ulikuwa mchezo wake wa kwanza kuitumikia timu hiyo ya London na kupata ushindi mnono hata hivyo Aaron Ramsey aligeuka nyota kwenye timu hiyo baada ya kufunga mabao matatu ‘hat trick’.

Arsenal ilianza mchezo huo kwa kasi ya hali ya juu na ndani ya dakika 20 za kwanza timu hiyo ilikuwa mbele kwa mabao 4-0.

Ramsey, alifanikiwa kuifungia Arsenal bao la kwanza katika dakika ya sita ya mchezo akimalizia pasi safi ya Henrikh Mkhitaryan, ambaye alipata pasi kutoka kwa Mesut Ozil.

Dakika ya 14, Laurent Koscielny, alifanya kazi kubwa baada ya kuifungia Arsenal bao la pili baada ya kumalizia pasi iliyopigwa na Shkrodan Mustafi.

Iliwachukua Arsenal dakika sita tu kujipatia bao la tatu ambalo liliwekwa tena kimiani na Ramsey na kuwafanya waendelee kutakata.

Dakika ya 36 ya mchezo, Mkhitaryan alifanya kazi kubwa na kutoa pasi yake ya pili ya bao baada ya kumtengea Aubameyang mpira safi ambaye hakufanya kosa na kuuchopu akaifungia timu yake bao la nne.

Hata hivyo, Theo Walcott ambaye anaitumikia Everton akiwa anacheza mchezo wake dhidi ya timu yake ya zamani alionyesha kiwango kizuri kipindi cha kwanza ambapo alitolewa uwanjani katika dakika ya 63 na kupigiwa makofi na wachezaji pamoja na mashabiki wa timu hiyo ya London kuonyesha heshima kwake.

Dakika mbili baada ya kutolewa Everton walifanikiwa kujipatia bao moja kupitia kwa Calvert Lewin na kufanya matokeo kuwa 4-1.

Kipa wa Arsenal, Petr Cech aliumia na kutolewa kwenye mchezo huo na nafasi yake kuchukuliwa na David Ospina katika dakika ya 69.

Dakika ya 74, Ramsey alikamilisha `hat trick’ yake baada ya kupata pasi safi kutoka kwa Mkhitaryan ambaye naye alitoa pasi ya tatu ya bao kwenye mchezo huo.

Katika mchezo wa awali, Manchester United walipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Huddersfield, huku staa mpya wa timu hiyo, Alexis Sanchez akiifungia timu yake bao moja likiwa ni la kwanza kwake kuanzia ajiunge nayo akitokea Arsenal.

Bao lingine la United liliwekwa kimiani na Romelu Lukaku, huku Manchester City wao wakitoka sare ya bao 1-1 na Burnley.

TANO Z IJAZO ARSENAL

Tottenham -UGENINI- Feb 10

Ostersund -UGENINI- Feb 15

Ostersund -NYUMBANI- Feb 22

Man City -UGENINI- Feb 25

Man City -NYUMBANI- Mar 1

Arsenal: Cech (Ospina 69), Bellerin, Koscielny, Mustafi, Monreal (Kolasinac 45), Ramsey (Wilshere 74), Xhaka, Mkhitaryan, Ozil, Iwobi, Aubameyang.

Subs: Lacazette, Chambers, Maitland-Niles, Elneny.

Scorers: Ramsey 6, 19, 73, Koscielny 14, Aubameyang 37

Booked: Koscielny, Mustafi

Everton: Pickford, Keane (Davies 45), Williams, Mangala, Kenny, Schneiderlin, Gueye, Martina, Walcott (Calvert-Lewin 60), Niasse (Tosun 77), Bolasie.

Subs: Rooney, Tosun, Sigurdsson, Holgate, Robles.

Scorers: Calvert-Lewn 64

Referee: Neil Swarbrick

Tunda amfungukia Aunt Ezekiel

Tunda Sebastian ‘Tunda’.

MUUZA nyago maarufu Bongo na mwenye visa kila kukicha Tunda Sebastian ‘Tunda’ amefunguka kuwa kamwe hawezi kuirudisha heshima yake aliyokuwa akiitoa kwa staa maarufu wa filamu Aunt Ezekiel, kama ilivyokuwa huko nyuma.
Staa maarufu wa filamu Aunt Ezekiel akiwa na mpenzi wake Moze Iyobo.

“ Mimi nilikuwa najua ni mwenye busara lakini hakuna kitu hivyo siwezi kumuheshimu tena hata kidogo maana zamani nilikuwa namchukulia kama dada lakini nimemvua cheo hicho kabisa kwangu hakipo,” alisema

Tunda.

Mtemela: baadhi ya Viongozi wa Kanisa wanaweza kuwa chanzo cha migogoro

Askofu mstaafu wa Kanisa Anglikana, Donald Mtetemela amesema baadhi ya viongozi wa kanisa wanaweza kuwa chanzo cha migogoro kutokana na tamaa ya mali na madaraka.

Askofu Mtetemela amesema hayo leo Jumapili Februari 4,2018 wakati ya misa ya kuwekwa wakfu na kusimikwa Askofu mteule Jackson Sosthnes wa kanisa hilo Dayosisi ya Dar es Salaam.

Amesema migogoro makanisa ni kazi ya shetani anayevuruga huduma ya Mungu ili isifanikiwe, hivyo kuwa katika hali ya hatari muda wote.

Askofu Mtetemela amesema migogoro haiwahusu waumini wa kanisa hilo pekee bali makanisa yote.

“Migogoro ni njia ya shetani ili kudhoofisha huduma ya kanisa, kazi yake ni kuingiza watu wasiofaa ili waweze kuwa viongozi. Utakuta mtu amevaa ngozi ya kondoo kumbe mbwa mwitu na wengine wanaingiza maandiko ambayo si maneno yaliyoandikwa kwenye vitabu vya dini,” amesema.

Amesema migogoro huleta chuki na roho ya kulipiza kisasi.

Amemweleza Askofu Jackson kuwa kazi yake si nyepesi, hivyo anatakiwa awe imara.

Askofu Jackson anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk Valentino Mokiwa aliyeondolewa madarakani na uongozi wa juu wa kanisa hilo takriban mwaka mmoja uliopita.