Wednesday, 7 February 2018

New VIDEO: Mesen Selekta Ft Rayako – Kinanda

New VIDEO: Mesen Selekta Ft Rayako – Kinanda

New VIDEO: Mesen Selekta Ft Rayako – Kinanda


DOWNLOAD VIDEO


Audio | Chemical ft Beka Flavour – Asali | Mp3 Download

Audio | Chemical ft Beka Flavour – Asali | Mp3 Download

Audio | Chemical ft Beka Flavour – Asali | Mp3 Download

DOWNLOAD

New Video | Maromboso ( Mbosso ) _ Riziki | Official Video

New Video | Maromboso ( Mbosso ) _ Riziki | Official Video

New Video | Maromboso ( Mbosso ) _ Riziki | Official Video


Sunday, 4 February 2018

DOWNLOAD: Vigour – Pande Zote

DOWNLOAD: Vigour – Pande Zote
Vigour - Pande Zote
DOWNLOAD: Vigour – Pande Zote


Sheria ndogo ya kunyonyesha ndani ya miezi minne kuundwa

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt Rehema Nchimbi amewataka viongozi wa vijiji na kata mkoani humo kuhakikisha wanatunga sheria ndogo ya kunyonyesha ndani ya miezi minne ili kuondokana na tatizo la ukosefu wa lishe kwa watoto.

Dkt Nchimbi ametoa agizo hilo Juzi Ijumaa kwenye hafla ya kukabidhiwa vifaa vya kutambua hali ya lishe kwa watoto na akinamama wajawazito katika kijiji cha Saranda wilayani Manyoni.

“Kunyonyesha ni lazima, Wenyeviti wa vijiji na kata hakikisheni mmetunga sheria ndogo kwa ajili ya kudhibiti akinamama wote wasionyonyesha watoto wao kulingana na taratibu za afya,”amesema Dkt. Nchimbi.

Mhe Nchimbi amelazimika kutoa agizo hilo baada ya kusomewa taarifa inayoonesha kuwa ni asilimia 54 pekee ya watoto mkoani Singida ndio hubahatika kunyonyeshwa maziwa ya mama pekee kwa kipindi cha miezi sita.

Akisisitizia suala hilo Dkt. Nchimbi amesema kuwa ulazima huo usibakie kuwa ni wa majukwaani tu bali utekelezwe kisheria na atakayepatikana aadhibiwe, hata hivyo, mhakikishe adhabu hiyo haisababishi mama kumkimbia mtoto.

Sheria ndogo ya kunyonyesha ndani ya miezi minne kuundwa

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt Rehema Nchimbi amewataka viongozi wa vijiji na kata mkoani humo kuhakikisha wanatunga sheria ndogo ya kunyonyesha ndani ya miezi minne ili kuondokana na tatizo la ukosefu wa lishe kwa watoto.

Dkt Nchimbi ametoa agizo hilo Juzi Ijumaa kwenye hafla ya kukabidhiwa vifaa vya kutambua hali ya lishe kwa watoto na akinamama wajawazito katika kijiji cha Saranda wilayani Manyoni.

“Kunyonyesha ni lazima, Wenyeviti wa vijiji na kata hakikisheni mmetunga sheria ndogo kwa ajili ya kudhibiti akinamama wote wasionyonyesha watoto wao kulingana na taratibu za afya,”amesema Dkt. Nchimbi.

Mhe Nchimbi amelazimika kutoa agizo hilo baada ya kusomewa taarifa inayoonesha kuwa ni asilimia 54 pekee ya watoto mkoani Singida ndio hubahatika kunyonyeshwa maziwa ya mama pekee kwa kipindi cha miezi sita.

Akisisitizia suala hilo Dkt. Nchimbi amesema kuwa ulazima huo usibakie kuwa ni wa majukwaani tu bali utekelezwe kisheria na atakayepatikana aadhibiwe, hata hivyo, mhakikishe adhabu hiyo haisababishi mama kumkimbia mtoto.

Aubameyang aanza kuonyesha makali yake Arsenal

STAA mpya wa Arsenal Pierre-Emerick Aubameyang jana alianza mchezo wake wa kwanza kwenye timu hiyo na kufanikiwa kuifungia bao moja kwenye ushindi wa 5-1 dhidi ya Everton katika mchezo wa Ligi Kuu England.

Aubameyang amejiunga na Arsenal kwenye dirisha hili la usajili na huu ulikuwa mchezo wake wa kwanza kuitumikia timu hiyo ya London na kupata ushindi mnono hata hivyo Aaron Ramsey aligeuka nyota kwenye timu hiyo baada ya kufunga mabao matatu ‘hat trick’.

Arsenal ilianza mchezo huo kwa kasi ya hali ya juu na ndani ya dakika 20 za kwanza timu hiyo ilikuwa mbele kwa mabao 4-0.

Ramsey, alifanikiwa kuifungia Arsenal bao la kwanza katika dakika ya sita ya mchezo akimalizia pasi safi ya Henrikh Mkhitaryan, ambaye alipata pasi kutoka kwa Mesut Ozil.

Dakika ya 14, Laurent Koscielny, alifanya kazi kubwa baada ya kuifungia Arsenal bao la pili baada ya kumalizia pasi iliyopigwa na Shkrodan Mustafi.

Iliwachukua Arsenal dakika sita tu kujipatia bao la tatu ambalo liliwekwa tena kimiani na Ramsey na kuwafanya waendelee kutakata.

Dakika ya 36 ya mchezo, Mkhitaryan alifanya kazi kubwa na kutoa pasi yake ya pili ya bao baada ya kumtengea Aubameyang mpira safi ambaye hakufanya kosa na kuuchopu akaifungia timu yake bao la nne.

Hata hivyo, Theo Walcott ambaye anaitumikia Everton akiwa anacheza mchezo wake dhidi ya timu yake ya zamani alionyesha kiwango kizuri kipindi cha kwanza ambapo alitolewa uwanjani katika dakika ya 63 na kupigiwa makofi na wachezaji pamoja na mashabiki wa timu hiyo ya London kuonyesha heshima kwake.

Dakika mbili baada ya kutolewa Everton walifanikiwa kujipatia bao moja kupitia kwa Calvert Lewin na kufanya matokeo kuwa 4-1.

Kipa wa Arsenal, Petr Cech aliumia na kutolewa kwenye mchezo huo na nafasi yake kuchukuliwa na David Ospina katika dakika ya 69.

Dakika ya 74, Ramsey alikamilisha `hat trick’ yake baada ya kupata pasi safi kutoka kwa Mkhitaryan ambaye naye alitoa pasi ya tatu ya bao kwenye mchezo huo.

Katika mchezo wa awali, Manchester United walipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Huddersfield, huku staa mpya wa timu hiyo, Alexis Sanchez akiifungia timu yake bao moja likiwa ni la kwanza kwake kuanzia ajiunge nayo akitokea Arsenal.

Bao lingine la United liliwekwa kimiani na Romelu Lukaku, huku Manchester City wao wakitoka sare ya bao 1-1 na Burnley.

TANO Z IJAZO ARSENAL

Tottenham -UGENINI- Feb 10

Ostersund -UGENINI- Feb 15

Ostersund -NYUMBANI- Feb 22

Man City -UGENINI- Feb 25

Man City -NYUMBANI- Mar 1

Arsenal: Cech (Ospina 69), Bellerin, Koscielny, Mustafi, Monreal (Kolasinac 45), Ramsey (Wilshere 74), Xhaka, Mkhitaryan, Ozil, Iwobi, Aubameyang.

Subs: Lacazette, Chambers, Maitland-Niles, Elneny.

Scorers: Ramsey 6, 19, 73, Koscielny 14, Aubameyang 37

Booked: Koscielny, Mustafi

Everton: Pickford, Keane (Davies 45), Williams, Mangala, Kenny, Schneiderlin, Gueye, Martina, Walcott (Calvert-Lewin 60), Niasse (Tosun 77), Bolasie.

Subs: Rooney, Tosun, Sigurdsson, Holgate, Robles.

Scorers: Calvert-Lewn 64

Referee: Neil Swarbrick

Tunda amfungukia Aunt Ezekiel

Tunda Sebastian ‘Tunda’.

MUUZA nyago maarufu Bongo na mwenye visa kila kukicha Tunda Sebastian ‘Tunda’ amefunguka kuwa kamwe hawezi kuirudisha heshima yake aliyokuwa akiitoa kwa staa maarufu wa filamu Aunt Ezekiel, kama ilivyokuwa huko nyuma.
Staa maarufu wa filamu Aunt Ezekiel akiwa na mpenzi wake Moze Iyobo.

“ Mimi nilikuwa najua ni mwenye busara lakini hakuna kitu hivyo siwezi kumuheshimu tena hata kidogo maana zamani nilikuwa namchukulia kama dada lakini nimemvua cheo hicho kabisa kwangu hakipo,” alisema

Tunda.

Mtemela: baadhi ya Viongozi wa Kanisa wanaweza kuwa chanzo cha migogoro

Askofu mstaafu wa Kanisa Anglikana, Donald Mtetemela amesema baadhi ya viongozi wa kanisa wanaweza kuwa chanzo cha migogoro kutokana na tamaa ya mali na madaraka.

Askofu Mtetemela amesema hayo leo Jumapili Februari 4,2018 wakati ya misa ya kuwekwa wakfu na kusimikwa Askofu mteule Jackson Sosthnes wa kanisa hilo Dayosisi ya Dar es Salaam.

Amesema migogoro makanisa ni kazi ya shetani anayevuruga huduma ya Mungu ili isifanikiwe, hivyo kuwa katika hali ya hatari muda wote.

Askofu Mtetemela amesema migogoro haiwahusu waumini wa kanisa hilo pekee bali makanisa yote.

“Migogoro ni njia ya shetani ili kudhoofisha huduma ya kanisa, kazi yake ni kuingiza watu wasiofaa ili waweze kuwa viongozi. Utakuta mtu amevaa ngozi ya kondoo kumbe mbwa mwitu na wengine wanaingiza maandiko ambayo si maneno yaliyoandikwa kwenye vitabu vya dini,” amesema.

Amesema migogoro huleta chuki na roho ya kulipiza kisasi.

Amemweleza Askofu Jackson kuwa kazi yake si nyepesi, hivyo anatakiwa awe imara.

Askofu Jackson anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk Valentino Mokiwa aliyeondolewa madarakani na uongozi wa juu wa kanisa hilo takriban mwaka mmoja uliopita.

Hospitali ya Aga Khan yaandaa Kampeni kuhamasisha Wananchi kupima saratani ya Utumbo



Hospitali ya Aga Khan kwa kushirikia na Mpango wa Taifa wa Damu Salama imeandaa kampeni kuhamasisha wananchi kupima saratani ya utumbo ili kujihami na ugonjwa huo.

Upimaji wa saratani ya utumbo ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya saratani duniani ambayo huadhimishwa kila Februari 4.

Akizungumza leo Jumapili Februari 4,2018 daktari bingwa wa magonjwa ya saratani wa Hospitali ya Aga Khan, Dk Harrison Chuwa amesema hospitali hiyo imeamua kuhamasisha upimaji wa ugonjwa huo baada ya kuona kuna ongezeko la wagonjwa.

Amesema ili kujua kama una ugonjwa huo, kuna kipimo ambacho kinauzwa kwenye maduka ya dawa.

"Kipimo hiki unaweza kujipima mwenyewe ukiwa nyumbani, ukibainika kuwa na saratani ya utumbo ndipo unaweza kuwaona madaktari kwa uchunguzi zaidi," amesema.

Daktari bingwa wa magonjwa ya saratani wa hospitali hiyo, Dk Aleesha Adatia amesema ugonjwa huo unatibika iwapo mgonjwa atawahi kutibiwa.

"Wagonjwa wengi huwa wanafika hospitali wakiwa wamechelewa, tunashauri watu kujipima kwa kutumia kipimo hicho angalau mara moja kila mwaka," amesema.

Kuhusu dalili, Dk Adatia amesema ni kutoka damu wakati wa kujisaidia haja kubwa, kuchoka na kupungua uzito.

Ofisa kutoka Mpango wa Damu Salama Kanda ya Mashariki, Fatma Mjungu amesema wanashirikiana na hospitali hiyo kwa kuwa kuna mahitaji makubwa ya damu kwa wagonjwa wa saratani.

"Ndiyo maana tupo hapa wakati wenzetu wanahamasisha upimaji wa saratani ya tumbo sisi tunahamasisha watu wajitolee kuchangia damu," amesema.

Amesema asilimia 25 ya damu inayokusanywa na mpango huo inatumiwa na wagonjwa wa saratani.

Amesema asilimia 42 ya damu inayokusanywa na mpango huo inatumiwa na watoto, huku asilimia 21 ikitumiwa na akina mama.

"Hivyo, ongezeko la saratani ya utumbo inasababisha matumizi makubwa ya damu, tunaomba jamii ichangie damu," amesema.

Sugu atembelewa na Wabunge wa Chadema, CUF Mahabusu



Wabunge wamefika Gereza Kuu la Ruanda jijini Mbeya kumjulia hali mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi 'Sugu'.

Waliomtembelea Sugu ni mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema na wa Tandahimba (CUF), Katani Katani.

Sugu na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga wapo mahabusu wakikabiliwa na kesi ya kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.

Lema na Katani wakiongozwa na mwenyeji wao Mbunge wa  Viti Maalumu, Sophia Mwakagenda pia wamefika nyumbani kwa Desderia Mbilinyi, mama mzazi wa Sugu eneo la Sae jijini Mbeya kwa ajili ya kumfariji na kumtia moyo kutokana na misukosuko anayopitia mtoto wake.

Wakizungumza na familia ya Sugu, wabunge hao wamesema yupo gerezani kwa kuwa anapigania haki za wananchi.

Lema amemtaka mama huyo kuwa na moyo wa uvumilivu.

Shamsa Ford afunguka kuhusu ndoa yake



MSANII mwenye uwezo mkubwa anapokuwa mbele ya kamera Shamsa Ford, amefunguka kuwa kama angeamua kufuata mambo ya mjini na kujivika ustaa mwingi kama wafanyavyo wengine ingewezekana mpaka leo hii ndoa yake isingekuwepo kabisa.

Akizungumza na gazeti hili Shamsa, alisema kuwa ameamua kujishusha kabisa kwasababu anaamini kwenye ndoa hakuna ufundi wala ustaa wowote zaidi ya kujiheshimu na kutambua kuwa unapopewa heshima ya kuwa mke na wewe lazima uibebe ipasavyo.

“Siwezi kufanya ujinga wa kuichezea ndoa yangu kabisa kwani ndoa ni kitu adimu mno hivyo unapoipata lazima uilinde na kama ustaa uuache mlangoni unapoingia nyumbani la sivyo itakuwa ni shida na ndoa haiwezi kudumu,” alisema Shamsa.

Rais Magufuli asema anaposikia matatizo yametokea huwa anajiuliza akimbilie wapi

Rais Dkt. John Magufuli amesema mara zote anaposikia matatizo yametokea eneo fulani fulani huwa anajiuliza akimbilie wapi ili aweze kupata msaada wa utatuzi wa jambo hilo bila ya kuleta athari yeyote katika taifa.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo (Jumapili Februari 04, 2018) wakati alipohudhuria hafla ya kumweka wakfu na kumsimika Mchungaji Jackson Sosthenes kuwa Askofu wa tano wa Kanisa la Anglikana Dayosis ya Dar es Salaam.

"Sisi viongozi wa serikali mara nyingi huwa tunawategemea viongozi wa makanisa na misikiti katika kutuongoza, nafahamu serikali haina dini lakini naheshimu sana dini na kuthamini mawaidha pamoja na mafundisho yanatolewa na viongozi wa dini wawe waislamu, wakristo hata wahindu tunayaheshimu sana", alisema Rais Magufuli.

Pamoja na hayo, Rais Magufuli aliendelea kwa kusema "siku zote sisi viongozi ndani ya serikali huwa tunafurahi sana kuona makanisa na misikiti ikiwa imetulia, unaposikia mahali fulani fulani kuna migogoro sisi viongozi na hasa mimi huwa najiuliza ninapopata matatizo ntakimbilia wapi. Kwa sababu makanisa na misikiti ni sehemu ya uponyaji wa roho zetu. Uponyaji wa roho ni mahali ambako kuna manufaa zaidi kuliko kwenye uponyaji wa mwili".

Kwa upande mwingine, Dkt. Magufuli amedai endapo mahali kwenye uponyaji wa mwili ukisikia kumeanza matatizo basi unapaswa kutazambua jinsi taifa unaloliongoza roho zake zitakavyopotea.