Sunday, 4 February 2018

Samatta arejea kwenye ubora wake



Mchezaji wa kimataifa wa Tanzania Mbwana Ally Samatta amerejea kwenye ubora wake baada ya jana kucheza kwa dakika 68 na kuisaidia timu yake ya KRC Genk kuibuka na ushindi wa 1-0 ugenini.

Samatta ambaye amekuwa nje ya uwanja kwa takribani miezi mitatu jana amecheza mchezo wake wa tatu tangu apone majeraha ya mishipa ya paja ambayo aliyapata Novemba 4 mwaka jana.

Genk jana imeshinda mchezo wake wa Ligi kuu nchini Ubelgiji dhidi ya wenyeji Royal Excel Mouscron kwenye uwanja Le Canonnier mjini Mouscron, Ubelgiji.

Baada ya Samatta kutoka nafasi yake ilichukuliwa na mshambuliaji kutoka DR Congo, Dieumerci N'Dongala ambaye alifunga bao pekee la ushindi katika mchezo huo dakika ya 83.

Jumanne wiki hii Samatta aliichezea Genk na kutoa pasi ya bao la kwanza la timu yake lakini bao hilo halikusaidia timu hiyo kushinda kwani ilifungwa 3-2 ugenini dhidi ya Kortrijk katika mechi ya Kombe la Ubelgiji.

Hii ndio Ratiba ya Mazishi ya Mzee Kingunge kesho

Mzee Kingunge Ngombale Mwiru enzi za uhai wake.

Ratiba ya mazishi ya Baba yetu mpendwa Mzee Kingunge Ngombale Mwiru(Baba Kinje)
Jumapili tarehe 4/2/2018
– Saa 10:00 jioni mwili kutoka Hospitali kuelekea nyumbani Victoria/Makumbusho Kingunge street.
-Saa 11:00 jioni mwili kuwasili nyumbani na taratibu za ibada mila na desturi kuendelea usiku mzima(mkesha)

Jumatatu tarehe 5/2/2018
– Saa 1:00 asubuhi mpaka saa 2:00 asubuhi waombolezaji kuwasili nyumbani Kwa ajili ya kuanza taratibu za mazishi.
– Saa 2:00 asubuhi mpaka saa 3:30 asubuhi Kupata kifungua kinywa/Chai Kwa waombolezaji wote
– Saa 4:00 asubuhi mpaka saa 5:00 misa nyumbani Kwa marehemu
– Saa 6:00 mwili kuwasili karemjee halll Kwa kuagwa
– Saa 6:00 mchana 9;00 kuaga mwili wa marehemu
– Saa 9:00 aalasiri mpaka 9:30 kuelekea makaburini kinondoni
– Saa 9:30 mpaka 11:30 maziko
– Saa 11:30 jioni 12:30 kuelekea nyumbani Kwa chakula cha jioni.
waombolezaji wote
1:30 usiku mpaka. 2:45 chakula cha usiku waombolezaji wote
3:00 usiku- waombolezaji wote hitimisho la shughuli ya Mzee wetu

Tunawashukuru sana Kwa ushiriki wenu wa Hali na mali katika wakati huu mgumu
Mungu awazidishie
Bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe🙏

Omary A kimbau( Mwenyekiti wa kamati ya mazishi)

 Facebook  Twitter  Google+  Pinterest  Linkedin
Newer Post Older Post
POPULAR
TAZAMA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2017
TAZAMA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2017
Breaking News:NECTA wanatangaza matokeo ya Kidato cha Nne
Breaking News:NECTA wanatangaza matokeo ya Kidato cha Nne
VIDEO: Ifahamu Dini Ya Kingunge Na Mengine Usioyajua
VIDEO: Ifahamu Dini Ya Kingunge Na Mengine Usioyajua
Ufafanuzi wa Serikali kuhusu uhamisho wa walimu
Ufafanuzi wa Serikali kuhusu uhamisho wa walimu
Mama afunguka kuhusu Nabii Tito na Kanumba
Mama afunguka kuhusu Nabii Tito na Kanumba
VIDEO: EXCLUSIVE Katambi aichana CHADEMA Amtaja LISSU
VIDEO: EXCLUSIVE Katambi aichana CHADEMA Amtaja LISSU
VIDEO: Aunty Ezekiel ahaidi kuwalipa shilawadu
VIDEO: Aunty Ezekiel ahaidi kuwalipa shilawadu
Serikali yafuta kifungu umri wa kustaafu
Serikali yafuta kifungu umri wa kustaafu
Dalili Hizi Zinaashiria Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI
Dalili Hizi Zinaashiria Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI
BREAKING: Mzee Kingunge Ngombale Mwiru Amefariki Dunia
BREAKING: Mzee Kingunge Ngombale Mwiru Amefariki Dunia

Zidane:kumtoa Ronaldo lilikuwa ni suala la kiufundi sio kumpumzisha

Kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane amesema kitendo cha kumtoa Cristiano Ronaldo kwenye mchezo wa jana dhidi ya Levante dakika ya 82 haikuwa kwasababu ya kumpumzisha.

''Kumtoa Ronaldo lilikuwa ni suala la kiufundi wala si kumpumzisha kwaajili ya mchezo dhidi ya PSG kama inavyodaiwa, tulikuwa tunaongoza kwa 2-1 na hatukuweza kuongeza bao licha ya kushambulia, hivyo tulitaka kuingiza kiungo Marco Asensio ili tumiliki mpira'', amesema.

Zidane amelazimika kutoa ufafanuzi huo baada ya kuwepo kwa malalamiko mengi kutoka kwa mashabiki ambao wanadai kutoka kwa Ronaldo kulisababisha Levante kushambulia na kusawazisha bao la pili dakika ya 89 na kufanya mchezo umalizike kwa sare ya 2-2.

Baada ya sare ya jana Real Madrid imesalia katika nafasi ya nne ikiwa na alama 39 huku vinara Barcelona wakiwa na alama 57 kileleni.

Mwanamke ajifanya muuguzi na kuiba mtoto wa siku moja Mbeya

Picha ya mtandao

Polisi mkoani hapa wanamsaka mwanamke ambaye aliyejifanya muuguzi na kuiba mtoto wa kike wa siku moja kwenye wodi ya wazazi katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya.

Mtoto huyo alizaliwa kwa njia ya upasuaji na Sarah Mwasanga (40), mkazi wa Iganzo jijini hapa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mohamed Mpinga alisema tukio hilo lilitokea juzi alfajiri kabla ya ndugu na jamaa kuingia kuona wagonjwa.

Mpinga alisema mwanamke huyo alifika hospitalini hapo kwa pikipiki huku akiwa amebeba kitu mithili ya mtoto na alipohijiwa na walinzi getini, alieleza ana mgonjwa ameandikiwa sindano za masaa hivyo akaruhusiwa kuingia.

“Alitumia mbinu ambayo kwa namna moja au nyingine ilifanikisha azma yake jambo ambalo hata wakati anatoka walinzi hawakumtilia shaka kwa kutambua tayari kapatiwa huduma,” alisema.

Mpinga alisema awali alipoingia kwenye wodi ya wazazi, aliwahoji kinamama waliojifungua kuwa anahitaji mtoto wa kike kwa ajili ya kumpatia chanjo, ndipo mzazi wa mtoto huyo alimkabidhi kwa kutambua ni muuguzi kutokana na mavazi aliyokuwa amevaa.

Alisema hilo ni tukio kubwa lililotokea mkoani hapa tangu aliporipoti na kwamba wanaendelea na uchunguzi.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Yahaya Msuya amekiri kutokea kwa tukio hilo, na kwamba kwa sasa lipo kwenye uchunguzi zaidi.

Mama wa mtoto huyo, Sarah Mwasanga aliomba msaada wa jeshi la polisi kufanya jitihada za haraka kuhakikisha mtoto wake anapatikana.

Audio | Chidinma X Young D X Toby Grey X Daphne – Egwu | Mp3 Download

Audio | Chidinma X Young D X Toby Grey X Daphne – Egwu | Mp3 Download
Audio | Chidinma X Young D X Toby Grey X Daphne – Egwu | Mp3 Download


Audio | Marisa – UKARONDA | Mp3 Download

Audio | Marisa – UKARONDA | Mp3 Download

Audio | Marisa – UKARONDA | Mp3 Download

Audio | Nuh Mziwanda – Upofu | Mp3 Download

Audio | Nuh Mziwanda – Upofu | Mp3 Download

Audio | Nuh Mziwanda – Upofu | Mp3 Download

VIDEOS New VIDEO: Fally Ipupa ft. R. Kelly – Nidja

VIDEOS New VIDEO: Fally Ipupa ft. R. Kelly – Nidja
VIDEOS New VIDEO: Fally Ipupa ft. R. Kelly – Nidja


New VIDEO: Seyi Shay – Bia

New VIDEO: Seyi Shay – Bia

New VIDEO: Seyi Shay – Bia

Nigerian music star Seyi Shay has released the visuals for her current song BIA and it’s a must-see.

Shot by Clarence Peters, the Afro Pop jam with salsa elements is sure to capture minds from start to finish. It dropped officially on Thursday, February 1, 2018 and is a complete dose of freshness, energy and entertainment from the sexy singer. Seyi’s charm and creativity are infectious in this clip and fans can rest assured there’s more to come.


MAGAZETI YA LEO 4/2/2018































Shelisheli waanza mchecheto dhidi ya Yanga

St Louis ya Shelisheli

WAKATI wakiwa wanajiandaa kuvaana na Yanga kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, uongozi wa klabu ya St Louis ya Shelisheli umeanza mchecheto.

Timu hiyo inakuja nchini kucheza na Yanga Febrauri 11, mwaka huu katika Uwanja wa Taifa jijini Dar. Meneja wa St Louis, Davis Khan aliidai kuwa; “Kucheza michuano hii wakati ligi yetu imeisha kunachangia sisi kufanya vibaya tena ukiangalia wapinzani wetu wao wanaendelea kucheza na wanashinda katika michezo yao migumu.”
Yanga wakiendelea na mazoezi yao.

“Pia katika wakati huu tunasaka kocha mwingine baada ya yule wa awali kujiuzulu, ambapo kocha huyo atakuwa na muda mdogo sana kabla ya kucheza kwa mchezo wetu huo na Yanga, ila tunajaribu kuwa na mtu haraka iwezekanavyo,” alisema Khan kupitia kwenye moja ya mitandao ya nchini kwao.

St Louis watacheza na Yanga kwenye michuano hiyo baada ya kuwa mabingwa wa Ligi ya Shelisheli ambayo ilimalizika mwezi Novemba mwaka jana.

Panya wawapa Wakulima wakati mgumu Morogoro



Wakulima wa Kata ya Kiberege Wilayani Kilombero mkoani Morogoro, wamejikuta katika wakati mgumu, baada ya mazao yao kuvamiwa na panya waharibifu, na kusababisha uharibifu mkubwa katika  mazao ya mpunga na mahindi ambayo wameyapanda katika msimu huu.

Wakulima wa kata hiyo wamesema tatizo hilo limeanza kwa muda mrefu, na cha kushangaza licha ya mvua kunyesha bado panya hao wameendelea na uharibifu, hali ambayo inawapa mashaka juu ya hali ya chakula itakavyokuwa msimu huu.

Aidha wakulima hao kutoka katika vijiji vya Nyamwezi na Misufini, wamedai ndiyo  mara ya kwanza kuwanaona panya hao wakiharibu mazao yao.

Naye Afisa Kilimo wa Kata ya Kiberege amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na ameeleza kuwa Serikali ya Wilaya hiyo imeanza kuchukua hatua mbalimbali katika kuhakikisha inakabiliana na tatizo hilo.

Lulu Diva apokonywa kila kitu na Mpenziwe?



IMEVUJA! Ukiachana na habari ya kudaiwa kupangishiwa nyumba na kununuliwa gari mpya aina ya Jeep na kigogo, imebainika kuwa msanii huyo amepokonywa kila kitu alichokuwa amepewa na mpenzi wake wa zamani aitwaye Joho.

Hivi karibuni, Lulu Diva aliripotiwa kuwa amepangiwa nyumba na kupewa gari jipya ambapo aliibuka sosi mwingine na kudai kuwa Lulu si mkweli, aliyenunua gari hilo ni mpenzi wake Joho ambaye alikuwa akiishi naye kinyumba kwa takriban miaka mitatu kiasi cha kufikia hatua ya kutolewa mahari ambayo ilirudishwa hivi karibuni na hata hivyo gari hilo amepokonywa hayuko nalo tena.

Akipiga stori na Risasi Jumamosi kwa sharti la kutotajwa jina sosi huyo alisema kuwa anawajua vilivyo Lulu na Joho kwa sababu Joho ni rafiki yake hivyo anachokisema yeye ana uhakika nacho kwamba Lulu hajanunuliwa gari bali ni lile lile alilopewa na Joho.

“Hivi mnajua kuwa huyo Lulu ni muongo mbona gari analosema amepewa na kigogo ni la rafiki yangu Joho alimnunulia na walikuwa wakiishi pamoja ila kwa sasa ameachana naye na ninavyojua amechukua vitu vyake.

“Hii yote ilikuja baada ya jamaa kumshtukia kuwa Lulu anatembea na msanii mwenzake, Rich Mavoko,” alisema sosi huyo.