Thursday, 18 January 2018

Mambosasa akanusha Polisi kuzuia Wanawake kuvaa nguo fupi




Dar es Salaam. Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,  Lazaro Mambosasa amekanusha kutoa tamko la kuzuia wanawake kuvaa nguo fupi zisizo na heshima kwa maelezo kuwa  jambo hilo ni la kimaadili siyo sheria.

Amesema Jeshi la Polisi lina kazi ya kushughulikia makosa ya kisheria na si maadili.

Mambosasa ametoa kauli hiyo leo Januari 18, 2018 wakati akihojiwa katika kipindi cha 360 kinachorushwa na Redio Clouds, ikiwa ni siku mbili baada ya kunukuriwa katika mkutano wake na wanahabari kuwa amezuia uvaaji wa nguo fupi jijini Dar es Salaam.

 “Niliwaeleza wazi kuwa suala la mavazi bado halijatungiwa sheria hivyo polisi hatuhusiki nalo mtu anayevaa kimini katika maeneo kama kanisani au msikitini  ni ukiukwaji wa maadili,” amesema na kuongeza,

“Niliwaeleza  kuwa katika nyumba hizo za ibada kuna kamati ya ulinzi na usalama za eneo husika wao watakushughulikia lakini si polisi.”

Amesisitiza, “Nilikwenda mbali zaidi na kuwaeleza kuwa hivyo vimini kuna mahali vinahitajika kama ufukweni, sehemu za starehe. Ikitokea mtu amepigwa, amedhalilishwa au amekamatwa na askari kwa kuwa amevaa kimini ana haki ya kulalamika kuwa ameshambuliwa.”

NHIF yakanusha taarifa hii

Waziri Mkuu atoa agizo kwa Mghwira kusitisha uuzwaji wa mali za KNCU



Tarime. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro  Anna Mghwira asitishe uuzwaji wa mali za Chama cha Ushirika cha Kilimanjaro (KNCU).

Ametoa agizo hilo jana jioni (Jumatano, Januari 17, 2018) wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Serengeti, wilayani Tarime.

Hatua hiyo imekuja baada ya KNCU kutangaza kuuza shamba lake kwa ajili ya kuiwezesha benki yake ya KCBL  kutimiza sharti la mtaji la Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Benki hiyo ya KCBL inatakiwa kutimiza sharti la kuwa na mtaji kamili unaotosha wa shilingi bilioni  tano (5) katika kipindi cha miezi sita tangu kutolewa kwa tangazo hilo.

Waziri Mkuu amesema  ni marufuku kuuza mali za Ushirika huo, hususan katika kipindi hiki ambacho Serikali inafanya uhakiki wa mali za vyama mbalimbali vya Ushirika nchini.

Amesema Serikali imedhamiria kuimarisha Ushirika nchini na sasa inafanya uhakiki wa mali za vyama vya Ushirika na watakaobainika kuhusika na ubadhilifu watachukuliwa hatua.

Januari 4, 2018 BoT ilizipa miezi sita benki tatu ili ziweze kuongeza kiwango cha mtaji unaohitajika kutokana na matakwa ya kisheria ya kuwa na mtaji kamili wa kutosha.

Benki hizo ni Kilimanjaro Co-Operative Bank Limited, Tanzania Women Banki Plc na Tandahimba Community Bank Limited, zitakaposhindwa kutekeleza agizo zitachukuliwa hatua.

BoT ni itazifutia leseni na kusimamisha shughuli za kibenki chini ya ufilisi, iwapo benki hizo zitashindwa kutekeleza agizo hilo hadi kufikia Juni 30, 2018.


Katibu UVCCM Iringa afunguka alivyonusurika kufa


KATIBU wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM), Alophance Myunga amenusurika kifo baada ya kitu chenye mlipuko kurushwa dirishani kwake na kufikia kitandani huku yeye akiwa amelala na kisha kusababisha moto ulioteketeza nyumba anayoishi yote.

Amesema kutokana na kurushwa kwa kitu hicho ambacho kilisababisha mlipuko mkubwa chumbani kwake na kisha moto kuanza kuwaka alichofanikiwa ni kuchukua simu yake ya mkononi tu huku vitu vingine vyote vikiteketea kwa moto.

 Myunga amesema yeye ni moja kati ya wapangaji saba wanaoishi kwenye nyumba ambayo wanaishi na chumba ambacho kilianza kuwaka moto ni cha kwake.

Katibu huyo wa UVCCM Wilaya ya Iringa amesema kuwa kwenye mida ya saa saba usiku akiwa amelala chumbani kwake alisikia dirisha lililopo chumbani kwake likivunjwa.Hata hivyo aliogopa kuchungulia kwani hakujua wanaofanya hivyo wanalengo gani dhidi yake.

Ameongeza wakati anaendelea kutafakari huku akiwa bado yupo kwenye kitanda chake alishangaa kuona amerushiwa kitu ambacho hawezi kukielezea ni cha aina gani lakini ghafla kikaangukia chini na kusababisha kulipuka na moto kuanza kuwaka.

“Naogopa kusema ni kitu aina ya bomu au laa.Maana si mtaalamu wa kutambua aina ya kitu ambacho kimerushwa chumbani.Niseme tu baada ya kitu hicho kurushwa kitandani na kudondokea chini, moto ukaanza kufuka na kisha kulipuka.Nilichofanikiwa ni kuchukua simu na Kompyuta mpakato na kisha kukimbilia nje.

“Nilipotoka nje na wapangaji wenzangu nao wakatoka na kuanza kuulizana nani amefanya tukio hilo.Tayari tumetoa taarifa Polisi jana(juzi) usiku baada ya nyumba kuungua na hivyo tunasubiri watakachobaini kilichosababisha nyumba kuchomwa na waliohusika kufanya tukio hilo,”amesema.

Alipoulizwa anahisi nini baada ya tukio hilo, Myunga alijibu kuwa anachoamini sababu kubwa itakuwa ni mambo ya siasa kwani yeye si mfanyabashara na hana kazi nyingine zaidi ya siasa na siku za karibuni kuna moja ya kiongozi wa kisiasa wa upande wa upinzani alimtishia kwa bastola.

“Mbali ya kunitisha kwa bastola aliniambia kuwa nitakiona na lazima atanihamisha Iringa kwani najifanya mjanja kwa kuwa nimetoka Dar es salaam.Huyu kiongozi(jina tunalo) ndio atakuwa adui yangu namba moja na ndio namhisi atakuwa kafanya tukio hilo.

“Inaonesha kabisa walikuwa wamedhamiria kuniuua mimi na ndio maana walivunja dirisha la chumbani kwangu na kurusha kitu hicho ambacho kilisaabisha mlipuko uliofanya moto kuanza kuwaka.Hata hivyo acha Jeshi la Polisi Iringa nalo lifanye kazi yake ya kuchunguza na ukweli utapatikana,”amesema.


Fid Q atoa somo kwa Wasanii



Mkali wa muziki wa hip hop Bongo, Fid Q ametoa somo kwa wasanii namna ya kujiweka mbali na msongo wa mawazo (stress) kutokana na kuyumba kwa uchumi.

Rapper huyo ameiambia Dj Show ya Radio One kuwa wasanii wanatakiwa kuwa wabunifu katika kazi zao na kuwa na njia tofauti tofauti za kuwaingizia kupato.

“Katika suala la ubunifu inakupa nafasi kubwa sana kwa sababu unakuwa na akili iliyotulia ambayo haipelekwi pelekwi na stress ndogo ndogo kama za kukosa show za hapa na pale, ni kitu poa na kinapaswa kufuatwa na kila msanii,” amesema Fid Q.

“Pia kuhakikisha anakuwa na njia zaidi ya moja ya kujiingizia kipato yaani mbali na muziki awe na vitu vingine ambayo vitamsaidia kujiingizia kipato,” amesisitiza Fid Q.

Fid Q kwa sasa anafanya vizuri na remix ya ngoma Fresh aliyowashirikisha Diamond na Rayvanny.


Davido kuwaanika anaowadai



Unaweza ukasema ugumu wa mwezi Januari kwa upande wa uchumi ni kwa watu wakawaida lakini kumbe haipo hivyo hili ni janga hata kwa watu maarufu, Hii ni baada ya msanii wa muziki kutoka Nigeria, Davido kutangaza kuwa ataweka hadharani majina ya watu wote anaowadai kama hawatarudisha fedha zake kuanzia leo.

Davido kupitia ukurasa wake wa Snapchat amesema ametoa siku ya leo Jumatano kwa watu wote anaowadai ambao wapo jijini Lagos kutii amri hiyo la sivyo atatangaza majina hayo bila kuogopa ukubwa wa majina yao.

“Kupitia posti hiyo Davido amesema “Nitaweka orodha ya majina ya watu wote ninao wadai hapa Lagos, Watu wengi nimewakopesha pesa lakini hawataki kunilipa mimi sio serikali, Kama hutanilipa leo jina lako nitaliweka hadharani,” ameandika Davido.

Hata hivyo, watu wengi wanasema huenda hasira hizo zimekuja kutokana na Mamlaka ya mapato jijini Lagos kumtaka Davido atoe risiti za malipo ya kodi aliyolipa kwenye tamasha lake la 30 Bilioni Concert.


Pluijm awafungukia Simba




KUELEKEA mchezo wa Alhamis hii dhidi ya vinara Simba, kocha mkuu wa timu ya Singida United, Hans van der Pluijm amesema anawachukulia mabingwa hao wa zamani kama washindani wake wengine katika ligi na atakiingiza kikosi chake katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa ‘tahadhari’ kubwa licha ya ukweli haihofii timu hiyo iliyofunga magoli 12 katika michezo 12 iliyopita.

“Naichukulia Simba kama timu nyingine. Siwezi kuweka akili yangu yote kwao.” Anasema Hans nilipofanya naye mahojiano Jumanne hii. Inatakiwa tuwe makini na tucheze mchezo wetu kwa kujitambua na kuimarisha morali ya timu nzima. Inatakiwa tufanye kazi yetu vizuri katika kila nafasi na katika uchezaji wa mpira pia.”

Singida wamepanda daraja msimu huu lakini namna timu hiyo inavyoendeshwa imesaidia kwa  kiasi kikubwa kusajili wachezaji mahiri kutoka ndani na ng’ambo, ikiwemo kumtwaa kocha Hans ambaye aliipa Yanga mataji mawili mfululizo ya ligi kuu.

Mudathir Yahya, Ken Ally, Deus Kaseke, Kiggy Makassy, Daniel Lyanga, golikipa Peter Manyika ni baadhi ya nyota wazawa ambao wamesajiliwa na klabu msimu huu. Mzimbabwe, Tafadzwa Kutinyu, Mganda, Shafiq Batambuze,  Wanyarwanda, Michael Rusheshangoga, Danny Usengimana wamefanya kikosi hicho kuwa imara na ushindi wowote utawafanya kuwa pointi sawa na Simba.

Hans ni kocha mwenye uzoefu mkubwa sasa hadi katika soka la Tanzania. Amewahi kuishinda Simba katika michezo yote miwili ya ligi kuu msimu wa 2015/16 ameendeleza aina ya soka lake la kushambulia katika kikosi cha Singida. Atawavaa Simba kwa mara ya kwanza akiwa nje ya kikosi cha Yanga huku akiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo mmoja tu vs Simba.

“Mpira hautabiriki. Kila kitu kinawezekana, Simba bado ni timu kubwa na nawaheshimu lakini siwaogopi. Tunajiandaa vizuri na timu ipo katika morali, natumaini tunaweza kuwashangaza siku ya mchezo. Hii mechi wachezaji wanatakiwa wawe makini wao wenyewe ili tupate matokeo mazuri. Ni mechi yetu muhimu.” Anasema Hans ambaye atamkosa mfungaji wake namba moja Usengimana.

Singida wamekusanya alama 23 katika michezo 12 iliyopita. Wakiwa nafasi ya nne ya msimamo pointi  tatu nyuma ya Simba, timu hiyo kutoka mkoani Singida imeonyesha mwanga kuwa huenda wakawa washindani wa kweli katika mbio za ubingwa msimu huu kutokana na uimara wa timu yao.

“Njia bado ngumu, chochote kinaweza kutokea muda wowote. Tunaichukulia ligi ‘mchezo kwa mchezo’ mwishoni tutajua tulipofika. Inatakiwa tufanye kazi yetu vizuri.” Anamaliza kusema Hans.



Meli zilizokamatwa na madawa ya kulevya zafutiwa usajili




picha ya Mtandao

Serikali ya Tanzania imezifutia usajili meli mbili zilizokamatwa zikiwa na shehena ya madawa ya kulevya na silaha, huku ikikana kuhusika na mzigo uliokamatwa nao.

Taarifa hiyo imetolewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu, na kusema kwamba meli hizo zilisajiliwa chini ya mamlaka ya usajili wa usafiri wa baharini, lakini hata hivyo zilishasajiliwa kinyume na sheria.

“Tanzania haihusiki na shehena za silaha wala mdawa ya kulevya yaliyokamatwa ndani ya meli hizo, bali ilitoa usajili wa meli hizo chini ya mamlaka za usajili ambao ni utaratibu wa kawaida wa kimataifa wa kusajili meli duniani, kwa hiyo kufuatia tukio hilo, tumezifutia usajili meli zote mbili, usajili ulitolewa chini ya taasisi ambayo ilishanyimwa kibali cha kusajili meli, na sasa meli zote zimeshusha bendera ya Tanzania ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa”, amesema Mama Samia Suluhu

Sambamba na hilo serikali imesema kuanzia sasa mamlaka husika inapitia taarifa za meli zote zilizosajiliwa nchini ili kuhakiki taarifa zake, na kutoa mapendekezo ya ushauri kwa serikali.

Meli hizo zenye namba za usajili IMO 6828753 ikiwa na kilo 1600 za dawa za kulevya kutoka Jamhuri ya Dominika, na nyingine yenye namba IMO 7614966 iliyokamwa ikiwa na silaha zilizokuwa zikisafirishwa kwenda Libya kinyume na sheria za kimataifa, zilikamatwa Desemba, 2017.

Theo Walcott atuma Ujumbe kwa mashabiki wa Arsenal


Inauma ukiondoka sehemu ambayo umeizoea kwa muda mrefu. Theo Walcott ametuma ujumbe kwa mashabiki wa klabu ya Arsenal baada ya kuhamia Everton.

Mchezaji huyo ambaye amesajiliwa na Everton kwa ada ya uhamisho wa paund milioni 20 na kukabidhiwa jezi namba 11, amedumu Arsenal kwa miaka 12 na ameichezea jumla ya michezo 397 na kushinda magoli 108.

Huu ndio ujumbe ambao Walcott amewatumia mashabiki wa Arsenal:

Ninataka tu kusema shukrani kubwa kwa mashabiki wote wa Arsenal. Nimekuwa nimesumbuliwa na ujumbe ambao nimepata leo kheri na siwezi kukushukuru kwa kutosha, na hasa kwa miaka 12 iliyopita. Nataka tu kuwatakia kila mmoja katika klabu kila la kheri kwa siku zijazo




Amber Rose anatarajia kufanya upasuaji wa matiti



Mwanamitindo wa kimataifa Amber Rose anatarajiwa kufanya upasuaji wa matiti yake hivi karibuni.

Mrembo huyo ambaye alitangaza kuchoshwa na ukubwa matiti hayo ameamua kutilia mkazo suala lake la kuyapunguza ili yaweze kuendana na mwili wake kama yeye mwenyewe alivyodai.

Kwa mujibu wa mtandao wa Page Six imeelezwa kuwa baby mama huyo wa Wiz Khalifa na girlfriend wa rapper 21 Savage, atafanyiwa upasuaji wa kifua chake na Dr. Garth Fisher mapema leo.

Dkt. Fisher ameeleza kuwa Amber anahitaji kupunguza matiti hayo ili aweze kuwea huru “She wants to downsize so she can have more freedom.” Na kwa upande wa mrembo huyo ameeleza kuwa akipunguza matiti hayo atakuwa huru na ataweza kuvaa nguo zake amabzo hajazivaa takribani miaka 10 iliyopita.

MAGAZETI YA LEO 18/1/2018














Daktari wa kienyeji akamatwa na Polisi kwa kuwalaghai wanawake kuwa watashika mimba



Polisi nchini Guinea wanasema kuwa wamemkamata daktari mmoja wa kienyeji kwa kuwalaghai mamia ya wanawake na kuwafanya kuamini kuwa wao ni wajawazito.

N'na Fanta Camara aliwapa wanawake ambao hawakuwa na uwezo wa kuwa wajawazito , dawa ya kienyeji ambayo ilisababisha tumbo zao kufura na kuonekana kuwa wao ni wajawazito.

Kutokana na huduma hizo wagonjwa walilipa dola 33 kwenye nchi ambayo kipato cha kila mwezi kinakadiriwa kuwa dola 48.

Polisi wanaamini kuwa Bi Camara alipata maelfu ya dola kila mwezi licha ya yeye kusema kuwa alijaribu tu kusaidia.

Siku ya Jumanne zaidi ya wanawake 200 waliandamana nje ya kituo cha polisi kwenye mji mkuu wa Guinea Conakry ambapo Bi Camara alikuwa akizuiliwa.

Zaidi ya wanawake 700 walio na kati ya umri wa miaka 17 na 45 wanaamiwa kuathiriwa na matibabu ya Bi Camara.

Idadi hiyo kubwa inaashiria jinsi Guinea na nchi zingine za Afrika zinawategemea madaktari wa kienyeji

Mwaka 2006 shirika la afya duniani lilisema kuwa asilimia 80 ya waafrika walitumia matibabu ya kienyeji

Baadhi ya wanawake walisema kuwa walionekana kuwa wajawazito kwa kati ya miezi 12 na 16.
Wanawake hao walisema kuwa Bi Camara aliwashauri wasimuone daktari, na mara alipothibitisha kuwa wamekuwa wajawazito walistahili kumpa kuku na vitambaa kama njia ya kumshukuru.

Baadhi ya wanawake walisema kuwa walionekana kuwa wajawazito kwa kati ya miezi 12 na 16.

Daktari aliyewachunguza 47 kati ya wanawake walioathiriwa alisema wako kwenye hatari ya kukumbwa na matatizo ya kiafya ya muda mrefu kutokana na matibabu hayo.

Bi Camara hata hivyo anasema kuwa hajafanya lolote baya.

"Ninafanya kazi ngumu sana kuwasaidia wanawake kuweza kutimiza ndoto zao lakini mengine yako mikononi mwa Mungu, aliwambia waandishi wa habari mjini Conakry.

Nini amkana Ney wa Mitego




MSANII chipukizi wa Bongo Fleava, Nini amefunguka kuhusu uhusiano wake na Nay wa Mitego na kueleza kuwa hajawahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na rapper huyo.

Kauli ya Nini anakuja baada ya hapo awali kuwepo taarifa kuwa sababu ya kutimuliwa MJ Record ni kuwa na mahusiano na Nay.

“Sina mahusiano ya kimapenzi na Nay, halafu hata kama ningekuwa nayo, kiupande wangu I don’t real think hiyo ni sababu ambayo ingeweza kumfanya yeye afanye kile alichokifanya,” amesema.

“Seriously sidhani kama mahusiano ya kimapenzi yanaweza kuathiri muziki, sina uhakika may be according to me navyofikiria lakini sidhani kama hiyo it can be specific reason,” amesisitiza.