Thursday, 18 January 2018

Waombolezaji wasambaratika baada ya mtu aliyedhaniwa amekufa kuibukia msibani


Kenya: Wakazi wa kijiji cha Marindi huko Kaunti ya Migori walipaniki na kuchanganyikiwa baada mwanaume wa miaka 35 ambaye aliaminika kuwa amefariki kuibukia msibani nyumbani kwake ghafla

Familia ya mwanaume huyo walikuwa wakimalizia mipango ya mazishi ndipo Okelo Nyamwaga alipojitokeza

Kufika kwake huko kusikotarajiwa kulileta hofu na furaha katika familia yake na marafiki na waombolezaji wengine kukimbia

Nyamwaga alikuwa amepotea kwa miezi miwili na familia yake ilipoteza matumaini ya kumpata akiwa hai

Wiki moja iliyopita marafiki wa Nyamwanga walisema mwili wake ukiwa umeharibika ulikuwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Migori

Mwili huo uliokotwa mtoni ukiwa umeharibika na kupelekwa mochwari


Kimbitor kugombea Ubunge jimbo la Kinondoni



Dar es Salaam. Diwani wa kata ya Hananasifu (Chadema), Ray Kimbitor amepitishwa na mkutano mkuu wa wilaya ya Kinondoni kugombea ubunge jimbo la Kinondoni.

Akitangaza matokeo hayo jana usiku mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Kinondoni, Waziri Muhunzi amesema matokeo hayo watayawasilisha Kamati Kuu Taifa ya chama hicho kwa ajili ya kupata baraka.

Amesema Kimbitor amepata kura 40 na kuwashinda wagombea wengine sita.

Amesema wajumbe wa mkutano huo walikuwa 102 na kura zilizoharibika ni tano.

“Kimbitor amepata kura 40 na kufuatiwa na Mustapher Muro (diwani Kinondoni) aliyepata kura 33,” amesema.

Amesema Rose Moshi amepata kura 5, Nicolas Mkwama kura 16, David Asey kura 2, Moza Ally kura moja huku Juma Uloleulole ambaye ni diwani kata ya Kijitonyama akipata kura sifuri.

Hata hivyo, jana Katibu wa Mambo ya Nje na Itifaki wa Chadema, John Mrema alilieleza Mwananchi kuwa chama kingetoa msimamo huo jana baada ya kuunda kamati ndogo kufanya utafiti, lakini akasema Chadema haikutoa baraka za kufanyika kwa mchakato wa ndani wa kuchukua fomu na kupitisha wagombea.

Beki wa Liverpool ahukumiwa baada ya kumpiga mpenzi wake



Beki wa Liverpool ya England ambaye msimu wa 2016/2017 alikuwa akiichezea Burnley kwa mkopo Jon Flanagan amehukumiwa baada ya kukutwa na hatia ya kumpiga mpenzi wake.

Jon Flanagan amekutwa na hatia baada ya mahakama jijini Liverpool kujiridhisha na ushahidi, hivyo amehukumiwa saa 40 za kufanya kazi bila malipo na miezi 12 ya kufanya shughuli za kijamii.

Staa huyo mwenye umri wa miaka 25 alitenda kosa hilo kwa kumpiga Ms Wall ambaye ndio mpenzi wake December 22 wakiwa mtaa wa Duke jijini Liverpool.

Snura afunguka kuhusu kupigwa vibuti



MSANII wa filamu Bongo, Snura Mushi amesema kuwa, japo amekuwa akionekana kulalamika kuhusu masuala ya mapenzi, ukweli ni kwamba kinachomuuma ni kutompata mwanaume stahiki kwake, lakini hajawahi kuachwa, huwa anaacha.

Snura alifunguka hayo kutokana na kuibuka minong’ono ya mara kwa mara kuwa huenda anaongoza kwa kupewa vibuti kwenye mapenzi ndomana hachoki kulalamika kuwa na stress za mahusiano, jambo ambalo amelipinga vikali.

“Nani kakudanganya huwa naachwa hiyo haijawahi kutokea, nikiona mtu haeleweki huwa najiengua mwenyewe sisubiri anipasue kichwa changu, hivyo kinachoniliza ni kutopata mtu sahihi kwangu na siyo kuachwa na wanaume,”alisema.

Wednesday, 17 January 2018

BLT: What Holds Women Back? - BBC News

BLT: What Holds Women Back? - BBC News



Dozens of women describe abuse by ex-doctor Larry Nassar - BBC News

Dozens of women describe abuse by ex-doctor Larry Nassar - BBC News



US senator to Trump official: Your amnesia is complicity - BBC News

US senator to Trump official: Your amnesia is complicity - BBC News

Tanzia: Johari amefiwa na Mama yake mzazi


Muigizaji wa sinema za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’.

Muigizaji wa sinema za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amepata pigo kwa kuondokewa na mama yake mzazi. Mungu ailaze roho ya mama Johari mahala pema peponi, Amina.



Daktari wa White House afunguka kuhusu afya ya akili ya Trump



Rais Trump hajaonyesha dalili zozote za matatizo ya kiakili kufuatia uchunguzi wa kiafya na yuko la afya nzuri, daktari wa White House amesema.

"Sina wasi wasi wowote kuhusu afya ya akili ya Trump," Ronny Jackson alisema Jumanne.

Wiki iliyopita Trump alifanyiwa uchunguzi wa afya wa saa tatu, ambao ni wake wa kwanza tangu awe rais wa Marekani.

Hii ni baada ya kutolewa kitabu chenye utata kulichoeneza uvumi kuhusu afya ya kiakili ya Rais Trump.

Akiongea na waandishi wa habari wakati wa mkutano huko White House, Dkt Jackson alisema kuwa kwa jumla afya ya rais ni nzuiri.

"Anaendelea kufurahia moyo wenye afya na afya yote kwa jumla kutokana na kutovuta sigara na kutokunywa pombe," aliongzea.

Hata hivyo Dkt Jakcson alisema kuwa Bw Trump, 71, atanufaika kwa kupunguza vyakula vyenye mafuta na mazoezi zaidi.

Siku ya Ijumaa rais alichunguzwa na madaktari wa kijeshi katika kituoa cha afya cha Walter Reed huko Bethesda, Maryland katika uchunguzi uliotajwa kuwa uliofanikiwa.

Kulingana na Michael Wolf ambaye ni mwandishi wa kitabu cha Fire and Fury: Inside the Trump White House, ni kuwa wafanyakazi wote wa White House walimuona Trump kama mtoto.

Trump alijibu kwa kusema kwa kitabu hicho kimejaa uongo huku naye waziri wa mashauri ya nchi za kigeni akikana madai kuwa afya ya rais ilikuwa inafeli.

Kitendo cha Tanesco kuikatia Dawasco umeme, kwazua taharuki



Deni la zaidi ya Sh25 bilioni ambalo Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) linalidai Shirika la Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (Dawasco) jana lilizua kizazaa cha upatikanaji wa maji kwa muda jijini hapa na baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Pwani.

Kizaazaa hicho kimetokana na jana mchana Tanesco kukata umeme kwa saa kadhaa katika mitambo ya Dawasco ya Ruvu Chini na Ruvu Juu kutokana na deni hilo lililotajwa kuwa linatokana na malimbikizo ya nyuma.

Baada ya taarifa za kuzimwa kwa mitambo ya umeme kuanza kusambaa, jioni Dawasco ililipa benki kiasi cha Sh2 bilioni huku kiasi kingine kama hicho ikiahidi kulipa kabla ya Ijumaa hivyo Tanesco kurejesha umeme.

Kukatwa kwa umeme katika mitambo hiyo kulizua hofu kwa wateja zaidi ya 200,000 wa Jiji la Dar es Salaam, Mlandizi na Bagamoyo waohudumiwa na mitambo hiyo.

Machi 5 mwaka jana, Rais John Magufuli wakati akizindua kituo cha kupooza umeme cha Tanesco mjini Mtwara, alitoa maagizo kwa shirika hilo kuwakatia umeme wateja wote wenye madeni bila kujali kama ni taasisi ya umma au binafsi.

Tanesco walikata umeme Dawasco ikiwa ni utekelezaji wa agizo ililolitoa Januari 11 kwa wadaiwa wake sugu, ikiwataka wawe wamelipa madeni wanayodaiwa ndani ya siku nne kabla ya jana.

Akizungumza na Mwananchi jana kabla ya umeme kurejeshwa, Kaimu Mkurugenzi wa Tanesco, Dk Tito Mwinuka alisema operesheni hiyo ya kuwakatia umeme wateja sugu itakuwa endelevu.

“Kazi hii hatujaianza leo (jana) tunaendelea nayo, lazima wadaiwa wote sugu watulipe madeni tunayowadai, ila ukiniuliza ni nani na nani wanaodaiwa na wameshakatiwa, jibu sina,” alisema Dk Mwinuka na kuongeza;

“Kama mmesikia watu wanasema yamewakuta, basi wafuateni wao watawaambia kilichowakuta ila siwezi kuwataja wateja wetu kwa majina. Huduma tunayoitoa sisi ni sawa na daktari na mgonjwa na daktari haruhusiwi kutoa siri za mgonjwa wake.”

Bila kufafanua kiasi kilicholipwa, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco, Cyprian Luhemeja alisema umeme umerejeshwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Profesa Kitila Mkumbo alisema aliwaagiza Dawasco kukutana na Tanesco ili kujadiliana jinsi ya kulipa deni hilo

“Nimewaagiza Dawasco na Tanesco wakae wajadiliane walipe deni hilo haraka kesho (leo) ili huduma zirudi na wananchi wapate maji kwani deni hilo haliwahusu na wanapaswa kupata huduma ya maji kama kawaida,” alisema Profesa Mkumbo.

Chanzo kutoka Tanesco kililidokeza Mwananchi kuwa ‘baada ya kukatiwa umeme, kiasi hicho cha fedha kilipwa.“Kesho (leo) watalipa Sh500 milioni na Ijumaa watalipa Sh500 milioni lakini sisi (Tanesco) lengo letu wangepunguza deni kwa kiwango kikubwa.”

“Kuna (anamtaja kigogo wa wizara ya nishati) ameingilia kati kutokana na kupigiwa simu na watu wengi kuhusu tatizo la maji hasa maeneo ya Pwani hivyo kuagiza yarudishwe na deni hilo lilipwe haraka.”

Ronaldinho ametangaza kustaafu soka



Mwanasoka wa kimataifa wa Brazil Ronaldinho Gaucho leo ametangaza rasmi kustaafu kucheza soka la ushindani baada ya kudumu katika soka la ushindani kwa zaidi ya miaka 15, Ronaldinho amefikia maamuzi hayo baada ya kucheza soka kwa muda mrefu na sasa anaamini inatosha.

Ronaldinho hadi anatangaza kustaafu kucheza soka akiwa na umri wa miaka 37, amecheza vilabu zaidi ya saba toka aanze kucheza soka vikiwemo vilabu vya Paris Saint Germain ya Ufaransa, FC Barcelona na AC Milan.

Kama hufahamu Ronaldinho alizaliwa mwaka March 21 1980 Porto Alegre kwao Brazil na alinza kucheza soka katika timu ya vijana ya Gremio 1987, jina lake halisi ni Ronaldo lakini aliitwa Ronaldinho kutokana na kuwa na umbo dogo kuliko wote katika timu ya vijana aliyokuwa anacheza wakati huo akiwa na umri wa miaka 8.

Ronaldinho alianza kuingia kwenye headlines za vyombo vya habari akiwa na umri wa miaka 13, hiyo ni baada ya kufanikiwa kuipatia ushindi timu yake wa magoli 23-0 lakini magoli yote 23 alifunga yeye, hivyo nyota yake ya kuja kuwa staa wengi wanaamini walianza kuiona mapema.

Follow Me : Instagram  Twitter

Ronaldo kurejea Man United



STAA wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo hana furaha Real Madrid na anataka kurejea Manchester United. Ronaldo amekasirishwa na kitendo cha uongozi wa klabu hiyo kushindwa kuzungumza naye ili kuongeza mkataba wake.

Kwa mujibu wa magazeti ya Hispania ni kuwa Rais wa klabu hiyo, Florentino Perez alimwahidi kumwongeza mshahara mapema lakini ameshindwa kutimiza ahadi yake.

Ronaldo amehuzunishwa kujikuta kuwa yupo nje ya listi ya wachezaji watatu nyota duniani wanaopata mishahara mikubwa. Mwanasoka huyo bora wa dunia mara tano, anapata kiasi cha pauni milioni 19 kwa mwaka.

Kufuatia hali hiyo, nyota huyo ameuambia uongozi wa Real Madrid anataka kuondoka mwishoni mwa msimu huu. Hata hivyo, mreno huyo msimu huu amekuwa na kiwango kibovu, ambapo amefunga mabao manne tu.

Kauli ya Jokate kuhusu kugombea CCM



Mjasiriamali na Mwanamitindo maarufu Bongo, Jokate Mwegelo amesema hana mpango wa kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Jokate ameiambia Clouds Fm kuwa anachofanya sasa hivi ndani ya chama hicho ni kuhamasisha ili kiweze kuwasaidia wananchi wa Kitanzania kwa ueledi na kwa usahihi.

“Tunajitolea kwa ajili ya chama naamini kuwa chama ndio serikali, kwa hiyo mimi nasaidia tu, naishia hapo, ni mapenzi wangu kwa vijana,” amesema.

Kuhusu kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani CCM, alijibu, “Sijui, haipo kwenye plan, haipo kwenye ramani yangu,”.