Friday, 12 January 2018

Serikali kuchunguza madai ya Meli ya Tanzania kukamatwa Ugiriki

SERIKALI imesema inachunguza taarifa za meli iliyokamatwa nchini Ugiriki ikiwa na bendera ya Tanzania ikipeleka vilipuzi Libya.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Susan Kolimba, akizungumza na Nipashe jana kuhusu tukio hilo, alisema wanafuatilia kwa kina ili kupata ukweli wake.

“Kwa sasa ni kwamba jambo hilo tunalifuatilia ili kujua habari hizo kama zina ukweli na tutakapopata taarifa tutawajulisha, bado tunafuatilia,” alisema Kolimba.

Jana, Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) ilieleza kuwa maofisa wa Ugiriki wanaofanya doria baharini  wameizuia meli hiyo iliyokuwa inapeperusha bendera ya Tanzania ikiwa imebeba vilipuzi.




Taarifa hiyo ya BBC ilieleza kuwa meli hiyo inadaiwa kusafirisha vilipuzi hivyo kutoka Uturuki kwenda Libya, kinyume cha sheria iliyowekwa ya kutosafirisha silaha kwenda Libya.

Iliongeza kuwa maofisa hao wameeleza kwamba meli hiyo ilikuwa imebeba kreti 29 zilizojaa vilipuzi pamoja na kemikali zinazotumiwa kuunda vilipuzi.

"Maofisa wa kushika doria baharini wamezima bomu lililokuwa linasafiri," ofisa mkuu wa walinzi hao wa Ugiriki, Yiannis Sotiriou alikaririwa na BBC jana.

Taarifa ya BBC ilieleza kuwa Wizara ya Safari za Baharini ilisema meli hiyo ilisimamishwa ikiwa katika kisiwa cha Crete kusini mwa Ugiriki baada ya maofisa kupatiwa taarifa na ilisindikizwa hadi katika bandari ya kisiwa hicho na kufanyiwa ukaguzi.

Sotiriou alikaririwa katika taarifa hiyo akieleza kuwa meli hiyo ambayo ilinaswa Jumamosi ilikuwa pia na kasoro nyingi na haikufaa kuwa baharini.

"Ingesababisha madhara makubwa sana kwa watu na mazingira pia," alikaririwa katika ripoti hiyo ya BBC.

Ilielezwa zaidi katika ripoti hiyo kuwa nahodha wa meli hiyo ambaye alifahamika kwa jina moja la Andromeda, alidai meli hiyo ilikuwa inasafiri kuelekea Djibouti lakini baadaye ikabainika kwamba ilikuwa inasafiri kuelekea mji wa bandarini wa Misrata nchini Libya.

Kwa mujibu wa ripoti ya BBC, mabaharia wanane ambao ni raia wa India, Ukraine na Albania waliokuwa kwenye meli hiyo, walitarajiwa kufikishwa mbele ya mwendesha mashtaka jana.

TLS kimefanikiwa kukusanya mamilioni kugharamia matibabu ya Lissu




Dar es Salaam. Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kimesema kimefanikiwa kukusanya Sh138 milioni kugharamia matibabu ya Rais wa Chama hicho, Tundu Lissu aliyelazwa Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven nchini Ubelgiji.

Taarifa iliyotolewa na Makamu Mwenyekiti wa TLS, Godwin Ngwilimi amesema kiasi hicho wamekipata kutoka kwa watu mbalimbali walijitolea kuchangia wa ndani na nje ya nchi wakiwemo wanachama wa chama hicho.

Kuhusu mchanganuo wa fedha hizo, Ngwilimi amesema kimetumika kulipa gharama za matibabu ya Lissu katika Hospitali ya Nairobi, Leuven na visa kwa watu watatu wakiwa nchini Ubelgiji.

Ngwilimi ametoa shukuran kwa wale wote waliojitokeza kuchangia matibabu ya Lissu ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashariki na mwanasheria mkuu wa Chadema.

Lissu aliyeshambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa katika makazi yake mjini Dodoma ambapo alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na usiku wa siku hiyo alihamishiwa Hospitali ya Nairobi alikolazwa hadi Januari 6 baada ya kahamishiwa Leaven, Ubelgiji kwa mazoezi ya viungo na saikolojia.

Mzee akilimali amkingia kifua Chirwa


Ibrahim Akilimali.

MWENYEKITI wa Baraza la Wazee wa Yanga, Ibrahim Akilimali amemtetea mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga, Mzambia, Obrey Chirwa kufuatia kukosa penalti katika mechi ya juzi dhidi ya URA ya Uganda kwenye Kombe la Mapin­duzi.

Yanga iliondolewa katika nusu fainali kwa penalti 5-4 ambapo Chirwa alikosa kwa upande wa Yanga na kusaba­bisha kuwa gumzo kutokana na tukio hilo.


Mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga, Mzambia, Obrey Chirwa.

Akizungumza na Championi Ijumaa, Akilimali alisema Chirwa hakufan­ya makosa katika kupiga penalti ya mwisho kwani alidhamiria kufunga na kilichotokea ni bahati mbaya na kudai kuwa, kocha ndiye anayepaswa kulaumiwa kutokana na kumtumia licha ya kutokuwa na ma­zoezi ya pamoja na wenzake.

“Yanga tumetolewa kiume katika michuano ya Mapinduzi kwani hadi tunatoka tumefanikiwa kufanya vyema hadi dakika 90 lakini kili­chotokea hakipaswi kulaumiwa mchezaji.

“Timu ilicheza vizuri ilipamba­na na hatimaye kuweza kufikia hapo tulipofikia na ilikuwa ni lazima timu moja isonge mbele.

“Siwezi kumlaumu Chirwa, kilichotokea ni bahati mbaya kwani, hata wachezaji wa­zuri Ulaya wanakosa penalti sembuse yeye, anayepaswa kulaumiwa ni kocha kwanini amemchezesha mchezaji akiwa hana mazoezi, naona anayarudia yaleyale ya Kocha Hans Pluijm,” alisema Akilimali.


Ronaldo amfungukia Neymar




Mshambuliaji wa zamani wa Barcelona Ronaldo Luís Nazário de Lima, amesema uhamisho wa nyota wa sasa wa Brazil Neymar Jr kutoka Barcelona kwenda PSG ni kama amepiga hatua moja nyuma.

Ronaldo ameyasema hayo kwenye mahojiano na chaneli ya 'Youtube' ya mchezaji wa zamani wa Brazil Arthur Antunes Coimbra maarufu kama Zico, alipoulizwa juu ya hatua alizopiga Neymar baada ya kuondoka Barcelona.

"Kwangu mimi uamzi huo ni kama kapiga hatua kurudi nyuma, lakini kila mtu huwa anatafuta changamoto mpya kama ilivyokuwa kwangu nilipoondoka Barcelona wakati huo nikajiunga na Inter Milan lakini ligi ya Italia ilikuwa na ushindani zaidi kuliko ilivyosasa ligi ya Ufaransa'', amesema Ronaldo.

Neymar aliondoka Barcelona kwenye majira ya kiangazi 2017 na kuhamia Paris Saint-Germain ya Ufaransa kwa dau la rekodi ya dunia € 222, zaidi ya shilingi bilioni 600. Neymar ameshaifungia PSG jumla ya mabao 20 katika michuano yote msimu huu ikiwemo 11 katika ligi kuu ya Ufaransa Ligue 1.

Hatua hii ya Ronaldo imekuja ikiwa ni siku mbili tu tangu Neymar mwenye miaka 25 aachwe kwenye kikosi cha UEFA mwaka 2017, huku nyota wawili Lionel Messi na Cristiano Ronaldo wakijumuishwa.






Wednesday, 3 January 2018

Audio | Ivan Ft Bibi Cheka – Diamond na Zari | Mp3 Download

Audio | Ivan Ft Bibi Cheka – Diamond na Zari | Mp3 Download

Audio | Ivan Ft Bibi Cheka – Diamond na Zari | Mp3 Download

DOWNLOAD

Audio | Ruby – Are You Ready | Mp3 Download

Audio | Ruby – Are You Ready | Mp3 Download

Audio | Ruby – Are You Ready | Mp3 Download

DOWNLOAD

Audio | Dudu Baya – Nimeshasema | Mp3 Download

Audio | Dudu Baya – Nimeshasema | Mp3 Download

Audio | Dudu Baya – Nimeshasema | Mp3 Download


DOWNLOAD

Video | Dully Sykes – Coconut | Mp4 Download

Video | Dully Sykes – Coconut | Mp4 Download
Video | Dully Sykes – Coconut | Mp4 Download


Audio | Dully Sykes – Coconut | Mp3 Download

Audio | Dully Sykes – Coconut | Mp3 Download

Audio | Dully Sykes – Coconut | Mp3 Download

DOWNLOAD

Sunday, 31 December 2017

Audio | Miss Rizy – Am Done | Mp3 Download

Audio | Miss Rizy – Am Done | Mp3 Download

Audio | Miss Rizy – Am Done | Mp3 Download

DOWNLOAD

Audio | Magic Soldier Ft. Kolly The Magic – Vunja Goti | Mp3 Download

Audio | Magic Soldier Ft. Kolly The Magic – Vunja Goti | Mp3 Download



Audio | Magic Soldier Ft. Kolly The Magic – Vunja Goti | Mp3 Download

DOWNLOAD

Audio | Msamaria Danielo – Yari Wewe | Mp3 Download

Audio | Msamaria Danielo – Yari Wewe | Mp3 Download

Audio | Msamaria Danielo – Yari Wewe | Mp3 Download

DOWNLOAD

Video | Mr 2Kay – Pray For Me | Mp4 Download

Video | Mr 2Kay – Pray For Me | Mp4 Download

Video | Mr 2Kay – Pray For Me | Mp4 Download