Sunday, 31 December 2017

Nikki wa Pili afunguka kuhusu Muziki wa Hip Hop





Msanii wa Hip Hop kutoka Weusi Kampuni, Nikki wa Pili amesema muziki wa sasa wa Hip Hop ushindani wake upo kibiashara zaidi kwa kuangalia jinsi ya kuwakonga mashabiki jukwaani na namna ya msanii mwenyewe anavyoweza kujiweka kibiashara.

Nikki wa Pili amedai kuwa kinachoangaliwa kwa sasa ni kuuza bidhaa yako na bidhaa nzuri ndiyo inayouza sokoni kwa hiyo ndio muziki wa Hip Hop ya sasa ulivyo.

Akizungumzia ushindani wa Hip Hop ulivyo wa kibiashara, Nikki wa Pili amesema ni ushindani ambao Msanii mwenzako akitoa video kali na wewe unatoa video kali zaidi au akifanya show nzuri na wewe unafanya show kali zaidi yake. Msikilize Nikki wa Pili kwenye mahojiano yake na Bongo5 hapa chini


Nape azungumzia kupokewa wanaohama vyama



Dar es Salaam. Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amehoji sababu za vyama vya siasa kuhangaika kupokea wanachama wa vyama vingine, badala ya kushughulika na Watanzania wasio na vyama.

Akizungumza leo Jumapili Desemba 31,2017 katika mahojiano na kituo cha televisheni cha Azam, Nape amesema siku zote amekuwa na msimamo tofauti na wanachama wanaovihama vyama vyao kwa maelezo kuwa unawajenga wanaohama, si vyama.

"Kama tunataka kujenga vyama viwe vya kitaasisi ni lazima kuhamahama lisiwe suala la kawaida. Yaani mtu mpaka anahama watu waseme kweli huyu alistahili kuhama," amesema Nape.

Amesema, "Watanzania wapo zaidi ya 50 milioni, wenye uwezo wa kujiunga na vyama kikatiba wanaweza kuwa zaidi ya 30 milioni, waliopo kwenye vyama wanaweza wasifike 10 milioni. Kwa nini tunakwenda kuhangaika na wanachama wa vyama vingine badala ya kushughulika na Watanzania wasio na vyama. Tushughulike kuwashawishi hawa."

Katika kipindi hicho, mwenyekiti wa kamati ya uongozi ya Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro na mwanahabari mkongwe, Dk Gideon Shoo waliungana na Nape kukosoa vitendo vya wanachama kuvihama vyama vyao.

Kwa mtazamo wao, hamahama ya wanasiasa ni miongoni mwa kasoro zilizojitokeza mwaka 2017.

"Bora wafute vyama vingi" - Mbowe



Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amefunguka na kusema kama Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na serikali haioni umuhimu na uwepo wa vyama vingi nchini watumie uwingi wao bungeni wavifute vyama hivyo.

Mbowe amesema hayo leo wakati akiongea na waandishi wa habari na kusema toka imeingia madarakani Serikali ya awamu ya tano watu wa upinzani wanaonekana ni maadui

"Tumemwambia Rais mara nyingi na chama chake kama wao wanaamini upinzani ni hasara kwa nchi na hawajaweza kuona faidi ya vyama vingi vya siasa, kama Chama Cha Mapinduzi hakijaona umuhimu vyama vingi vya siasa kwenye nchi hii kwa miaka 25 hii wana wingi wa kutosha bungeni ni bora wafute vyama vingi lakini ku pretend tupo kwenye vyama vingi wakati mnavikandamiza na kuvifunga mikono wakati nyinyi mnafanya siasa wenzenu wasifanye siasa" alisema Mbowe

Mbali na hilo Mbowe amesema kuwa kupitia chama chake cha CHADEMA kwa mwaka 2018 watakuwa na kazi ya kupigania mchakato wa Katiba Mpya pamoja Tume Huru ya Uchaguzi na kusema hilo wanaliweka wazi mapema ili ifahamike.



Msuva Arejea Nyumbani Kwa Mapumziko Baada Ya Kazi Nzuri Morocco



WINGA wa kimataifa wa Tanzania, Simon Happygod Msuva anatarajiwa kurejea nchini Alhamisi kwa mapumziko ya baada ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Morocco, maarufu kama Botola.

Akizungumza na Bin Zubeiry Sports – Online leo, Msuva amesema kwamba Ligi ya Morocco inakwenda mapumzikoni naye anarejea nyumbani kwa mapumziko na kujipanga kwa mzunguko wa pili.

“Natarajia kurudi nyumbani kuanzia Alhamisi kwa mapumziko ya baada ya mzunguko wa kwanza Ligi Kuu huku, na pia kujipanga kwa mzunguko wa pili kabla ya kurudi kambini,”amesema.

Msuva anaweza kuwa kwenye mapumziko marefu, kwa sababu michuano yote nchini Morocco sasa itasimama kupisha Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) zinazohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee zinazotarajiwa kuanza Januari 13 hadi Februari 4, mwakani.

Simon Msuva (kulia) amefunga mabao matano katika mechi 13 za ligi ya Morocco na ametoa pasi za mabao matatu

Msuva anarejea nyumbani akitoka kuifungia bao pekee Difaa Hassan El-Jadidi ikishinda 1-0 dhidi ya Hassania Agadir Ijumaa.

Msuva, mchezaji wa zamani wa Yanga alifunga bao hilo dakika ya 52 katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Ben Ahmed El Abdi mjini El Jadida, Mazghan nchini Morocco na sasa anafikisha mabao matano katika mechi 13 za ligi ya Morocco, akiwa pia ametoa pasi za mabao matatu.

Msuva anazidiwa mabao mawili mawili na Mehdi Naghmi wa Ittihad Tanger na Jalal Doudi wa Hassania Agadir wanaoongoza kwa mabao yao saba kila mmoja, wakifuiatiwa na Mouhcine Lajour wa Raja Casablanca mabao sita sawa na Bilal El Magri, Hamid Ahadad wote wa Difaa Hassan El-Jadidi na Abderrahim Makran.

Mbali na Msuva aliyewahi pia kuchezea Moro United baada ya kupita akademi ya Azam FC, mwingine mwenye mabao matano ni Badr Kachani wa Hassania Agadir.

Ikumbukwe Msuva yupo katika msimu wake wa kwanza Difaa Hassan El-Jadidi baada ya kujiunga na timu hiyo kutoka Yanga SC ya Tanzania.


Mwaka Mpya wa 2018, Watanzania wakumbushwa kudumisha amani


Katika kuelekea mwaka Mpya wa 2018 watanzania wamekumbushwa kuenzi na kudumisha Mshikamano, Amani na Upendo hususani kwa makundi ya wasiojiweza, yatima na wazee kutokana na kwamba, vitendo hivyo vimeendelea kuwa mhimili na kichocheo muhimu katika kufikia Maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.

Haya yanajidhihirisha kwa vitendo baada ya kikosi cha Jeshi la wananchi 313 Monduli kufika katika kituo cha watoto yatima Global Cha Arusha ambapo kwa pamoja wameshiriki katika shughuli za usafi wa mazingira ya kituo hicho, kufua shuka na mablanket ya watoto lakini pia kutoa msaada wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni Tatu na fedha taslimu shilingi laki tano ikiwa ni ishara ya Upendo kwa yatima hao .

Mkurugenzi wa kituo hicho Mack Donald Kavishe anasema ni kwa mara ya kwanza kupata ugeni kama huo na kuongeza kuwa kitendo cha kushiriki usafi na kutoa msaada huo ni tiba ya kisaikolojia kwa watoto hao ili wasijisikie upweke.

Baadhi ya msaada wa vitu vilivyokabidhiwa ni Sukari, mchele, mafuta ya kujipaka na kupikia, magodoro, chumvi, vifaa vya usafi, madaftari, unga na maharagwe.


Ajali mbaya ya Barabarani Kenya, Yaua watu 36 na wengine zaidi ya 11 kujeruhiwa



Watu 36 wamepoteza maisha na wengine 11 kujeruhiwa katika ajali mbaya ya barabarani nchini Kenya iliyotokea mapema usiku wa kuamkia leo.

Polisi wameeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni basi la abiria ambalo lilikuwa linatokea Busia mpani na nchi yaUganda lililokuwa likielekea jijini Nairobi kugongana ana kwa ana lori lililokuwa linatokea mjini Nakuru.

Mkuu wa kitengo cha trafiki katika eneo la Bonde la Ufa, Zero Arijme, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo amesema ilitokea saa tisa alfajiri katika barabara kuu ya kutoka Nakuru kwenda mjini Eldoret.

Kwa mujibu wa jeshi la Polisi nchini Kenya wamesema mwezi wa Desemba pekee, watu zaidi 100 wamepoteza maisha katika ajali za barabarani zilizotokea katika barabara kuu ya Nakuru kuelekea Eldoret hali ambayo inaashiria hatari kuwa katika eneo hilo ambalo limekuwa sugu kwa kutokea ajali za mara kwa mara.


Friday, 29 December 2017

Yanga yatua Mwanza Salama, kuivaa Mbao FC


Kikosi cha Yanga kimetua salama Mjini Mwanza tayari kwa pambano lake la Jumapili dhidi ya wenyeji Mbao FC, pambano la Ligi Kuu ambalo limepangwa kupigwa uwanja wa CCM Kirumba.

Kocha msaidizi wa timu hiyo Shadrack Nsajigwa amesema, timu imewasili salama na leo wanatarajia kufanya mazoezi kwenye uwanja wa Kirumba, pamoja na kesho kabla ya kujiandaa na mchezo huo ambao wameupa umuhimu mkubwa.

“Nashukuru tumewasili salama Mwanza, hali ya hewa ni nzuri na kufika mapema siku mbili kabla ya mchezo kutatusaidia kufanya vizuri kwenye mchezo wetu wa keshokutwa kwasababu tumedhamiria kushinda mchezo huo ukizingatia Mbao ni timu nzuri na imeuwa ikitusumbua sana,” amesema Nsajigwa.

Kocha huyo amesema ukitoa wachezaji Ibrahim Ajibu na Obrey Chirwa wachezaji wote waliobaki na kusafiri na timu hiyo niwazima na wapo katika ari kubwa ya kuhakikisha wanacheza na kuhakikisha wanapata pointi tatu.


Yanga inashika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, ikiwa na pointi 21, huku mahasimu wao Simba wakiwa ndiyo vinara wa ligi hiyo wakiwa na pointi 23 huku Azam FC wakishika nafasi ya pili wakiwa na pointi sawa na Simba.

VIDEO: Rais Magufuli amwagiwa sifa na Sheikh Kishki


Mhadhiri wa Kimataifa wa Kiislamu, Sheikh Nurdeen Kishki amemmwagia sifa Rais wa DK John Magufuli kutokana na uamuzi wake wa kupiga vita uvaaji wa nguo zisizo na maadili katika video za muziki nchini.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI..USISAHAU KUSUBSCRIBE




VIDEO: KAKOBE Aendelea Kupeta Mtaani



Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amefunguka na kusema kuwa jeshi la polisi mpaka sasa halijamkamata Askofu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zakaria Kakobe kama baadhi ya taarifa zinavyosamabazwa.

Kamanda Mambosasa amesema hayo leo wakati akiongea na waandishi wa habari na kusema kuwa bado hawajamtia nguvuni Askofu huyo na pindi watakapomkamata kwa makosa aliyotenda basi watatoa taarifa hizo.

"Baba Askofu Kakobe bado hatujamkamata pale atakapokuwa amekamatwa kwa makosa aliyotenda nitawaambia lakini kwa sasa hajakamatwa mchungaji huyo, jeshi la polisi huwa halipangi kumkamata mtu bali mtu anapofanya kosa la jinai ndipo anakamatwa hivyo na yeye kama amefanya kosa hili basi tutamkamata" alisisitiza Mambosasa

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE


Dk Mollel awaomba msamaha wanachama wa Chadema



Siha. Aliyekuwa mbunge wa Siha, Dk Godwin Mollel amewaomba msamaha wanachama wa Chadema kwa uamuzi wake wa kujivua ubunge na kujiunga na CCM.

Dk Mollel aliyetangaza uamuzi wa kujivua ubunge Desemba 14,2017 na kukabidhiwa kadi ya CCM Desemba 15,2017 amesema upepo wa kisiasa umebadilika na safari aliyoianzisha ni ya kusafisha upinzani kanda ya kaskazini.

Amesema hayo wakati wa kukabidhiwa kadi za CCM madiwani wawili waliojiuzulu nyadhifa zao na kuhama Chadema hivi karibuni, ambao ni wa Donyomurwak, Lwite Ndosi na wa Gararagua aliyekuwa pia mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Siha, Zakaria Lukumay.

Dk Mollel alisema jana Alhamisi Desemba 28,2017 kuwa amelitazama goli na ndiko alikokwenda ili kuweza kufunga.

“Natambua kuna watu walipoteza muda mwingi, walitumia fedha zao kunichangia na wengine walimwaga damu ili niweze kuwa mbunge lakini hivi majuzi nilijivua ubunge hatua ambayo iliwaumiza wengi. Niombe mnisamehe kwa kuwa nilishindwa kuwafuata siku ile nikihama kwa kuwa nilijua mngeweza kunipiga au kusababisha sintofahamu kubwa,” amesema Dk Mollel.

Amesema uamuzi wenye tija siku zote lazima ulete machungu.

Dk Mollel amesema ameingia kwenye vita kuhakikisha anayafikia malengo ya kuwaletea wananchi wa Siha maendeleo waliyoyatarajia kwa kipindi kirefu.

“Niwahakikishie wananchi wa Siha kwamba hamtajuta mimi kuhama chama, kwa kuwa niliisoma ramani yote ya Siha na kuelewa maendeleo yaliko, hivyo sijawaaibisha, niungeni mkono sasa na ninaahidi sitawaangusha,” amesema.

Pia, ametaka viongozi wa CCM kutambua kuwa wana kazi kubwa ya kuhakikisha walio nje ya chama hicho wanavutiwa na matendo ya chama na si kukatishwa tamaa.

Katibu wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Jonathan Mabihya amesema, “Kuna watu wanawatisha watu kuwa wakiondoka na kuja CCM hawatapata nafasi, tunawakaribisha kwa kuwa nafasi ziko wazi na wakihitaji kugombea watapata nafasi.”

Mabihya amesema CCM imeongeza idadi ya wapambanaji ambao wameamua wenyewe kuungana na timu ya maendeleo.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Patrick Boisafi amesema milango iko wazi kwa anayetaka kujiunga na chama hicho.

“Wanaorudi CCM wanarudi nyumbani, ninaomba Watanzania waelewe kuwa hakuna biashara ya binadamu na CCM hatuwezi kufanya biashara hiyo,” amesema.

Ndosi aliyekuwa diwani wa Donyomurwak ametaka maneno yanayoendelea kuhusu kuhama kwake Chadema yaishe, kwa kuwa haitaji mashindano ya maneno bali kufanya kazi ili kuyafikia maendeleo.


Ronaldo amtaka Philippe Coutinho kutojiunga na Barcelona



Aliyekuwa mshambuliaji hatari wa timu ya taifa ya Brazil na vilabu vikubwa vya Ulaya, Ronaldo Luís Nazário de Lima amemuonya kiungo wa Liverpool, Philippe Coutinho kuhusu kujiunga na Barcelona.

Coutinho ambaye amekuwa akiwindwa na vinara hao wa La Liga tangu msimu uliopita, ameambiwa na Ronaldo kuwa Barca ni timu ambayo imekuwa na matatizo makubwa na wachezaji wa kutoka nchini Brazil.

Nilijisikia furaha zaidi na zaidi nilipojiunga na Real Madrid, licha ya kuwa nilikuwa na mwaka mzuri huko Barcelona,” Ronaldo amesema hayo wakati akiongea na kituo cha runinga cha Esporte Interativo


Ronaldo de Lima

“Mwishoni, historia yangu na Barça ilikuwa mbaya sana, sawa na ile Neymar aliyokuwa nayo. Barcelona daima imekuwa na matatizo na wachezaji wa Brazil: Neymar, Romario, Ronaldinho na mimi. Sisi wote tulitendewa vibaya na klabu mwishoni licha ya michango yetu yote na kujitolea,” ameongeza.

De Lima aliichezea Barca kwa msimu mmoja wa mwaka 1996–1997 katika mechi 37 na alifanikiwa kufunga magoli 34 na baadaye alihamia Inter Milan ambapo alicheza kwa misimu mitano.



VIDEO: Diamond Platnumz Awakabidhi mashabiki zawadi ya Pikipiki


Msanii wa bongo fleva nchini Tanzania ambae amefanikiwa pia kuvuka boda kwa hatua kubwa Nasibu Abdul alimaarufu kama Diamond Platnumz amewapa mashabiki wake zawadi za pikipiki na zawadi nyingi ikiwemo chibu perfume na nyingine kibao.

Angalia Full Video Hapa na Usisahau ku Subscribe......



Thursday, 28 December 2017

Serikali yapiga hodi mgodi wa Geita



Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Luhumbi ameunda kamati maalumu ya kuchunguza wanaofuja fedha za wananchi, huku akiwaagiza mkuu wa wilaya hiyo Herman Kapufi, Mkurugenzi wa mji Modest Apolinary kuwasiliana na mgodi wa Geita (GGM) waharakishe kuikabidhi serikali ya mkoa huo majengo yaliyojengwa kwa ufadhili wa mgodi huo yaliyopo magogo ili yabadilishwe kuwa chuo kikubwa cha ufundi kwa lengo la kuwasaidia vijana na watoto katika mkoa wa Geita.

Amesema hayo wakati akizungumza na wananchi wa kata ya kalangalala katika shughuli ya uchimbaji misingi ya majengo ya shule ya secondary GEITA,na kwamba baada ya GGM kukabidhi majengo hayo,ndani ya mwezi mmoja watahakikisha wanakamilisha taratibu za kuwa chuo ili watoto wapate kujiunga hasa wale wanaotaka kusomea kozi mbalimbali zikiwemo computer ,makanika,ujenzi, kuchomelea vyuma na madini hakuna haja ya kuwatoa mkoani hapa kuwapeleka kusoma kwenye mikoa mingine.

Katika hatua nyingine baadhi ya wananchi wa kata ya Nyankumbu wamelalamikia baadhi ya viongozi kukwamisha shughuli za maendeleo na kumlazimu mkuu wa wilaya kuahidi kula nao sahani moja.