Wednesday, 27 December 2017

Serikali yatoa taarifa hii kuhusu kuzimwa kwa 'chaneli' za bure kwenye ving'amuzi



Kufuatia uwepo wa malalamiko ya mara kwa mara kutoka kwa wananchi kuhusu kukosa huduma ya runinga za bure pindi vifurushi katika visimbusi (ving’amuzi) vyao vinapomalizika, serikali imetolea ufafanuzi suala hilo kwa kueleza namna mfumo wa utendaji unavyotakiwa kufanya kazi.
Akijibu maswali ya watumiaji mbalimbali wa mtandao wa Twitter kuhusu urushwaji wa runinga za bure, Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Abbas alisema, kwa mujibu wa sheria iliyopo sasa, vituo vyote vya runinga ambavyo vimepewa leseni ya FTA (Free to Air) vinapaswa kuonekana hata baada ya kifurushi kwenye kisimbusi kwisha.
Dkt. Abbas alisema kwamba, hadi sasa kuna vituo 16 vya runinga vya ndani ya nchi vilivyopewa leseni hizo, vikiwemo vituo vya ITV, Clouds TV na Channel 10.
Aidha, alifafanua kuwa, ili mtumiaji aweze kutazama hata baada ya kufurushi chake cha malipo kwisha, kituo cha runinga (mfano ITV) kinapaswa kuwalipa warushaji wa masafa (mfano Azam) ili ITV iweze kuonekana kwa wananchi hata ambao hawajalipia visimbusi vyao.
“… mfumo uko hivi: ili wewe uone bure hizo channeli kuna mzalishaji wa vipindi ambaye ni kituo cha TV na msafirisha masafa mfano StarMedia. Ili wewe uone bure kuna gharama huyo wa kwanza anatakiwa kulipia kwa wa pili. Asipolipia akakatiwa huduma hautaona. Kwa sasa ndio mfumo.”
Pia, Dkt. Abbas alitahadharisha kuwa, endapo kituo cha runinga hakutawalipa wasafirishaji wa masafa, watakatiwa huduma na hivyo kuwafanya wananchi washindwe kuweza kutazama runinga bure.
Kuhusu TBC kuonekana katika visimbusi vyote hata bila malipo, msemaji alifafanua kuwa, kila kisimbusi kinatakiwa kuweka TBC kupitia sera ya ‘must carry’ ambayo inaiwezesha kuonekana kwa wananchi bila malipo yoyote.
“Unapata TBC mda wote kwa sababu TBC anahadhi inayoitwa “must carry” ambaye mrusha masafa yeyote Tz lazima aioneshe TBC. Kama hupati channeli zingine za FTA muulize mtoa huduma wako. Majibu atakayokupa nijulishe na unipe jina la mtoa huduma wako,” aliandika Dkt. Abbas.
Alisema kuwa, kwa sasa serikali haina mfumo wa kuwaadhibu wamiliki wa vituo vya runinga wenye leseni za FTA lakini hawawalipi warusha masafa ili wananchi waweze kuona runinga hizo bure, badala yake, warusha matangazo hayo wanatawakati huduma kama hawajalipwa.
“…kwa kanuni iliyoanza Machi mwaka huu, mtoa huduma za TV asipolipa kwa msafirisha masafa anaweza kukatiwa huduma.”
Kuhusu Dstv na Azam kukata matangazo ya runinga za ndani baada ya kifurushi kwisha, Dkt Abbas alisema suala hilo lipo Baraza la Ushindani hivyo wananchi wasubirie majibu, na kwamba asingependa kulizungumzia kwa 

Mwaka 2017 Umekuwa mwaka Wa Majonzi kwa Wapinzani Nchini



Ukiwa ni mwaka wa pili kwa Rais John Magufuli kuwa madarakani, uelekezo wa siasa za upinzani umekuwa shakani kutokana na mazingira magumu huku baadhi ya makada wa vyama hivyo wakijiunga na CCM.
Awali kulikuwa na katazo la kufanya mikutano ya hadhara na maandamano licha ya Katiba na Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992 kuruhusu. Katazo hilo limedumu hadi mwaka huu.
Mwaka 2017 umeendelea kuwa wa misukosuko kwa vyama vya upinzani kutokana na kuendelea kukamatwa na mara nyingine kushitakiwa.
Miongoni mwa wabunge waliokamatwa ni pamoja na Halima Mdee (Kawe), Ester Bulaya (Bunda), John Heche (Tarime Vijijini), Esther Matiko (Tarime), Pascal Haonga (Mbozi), Godbless Lema (Arusha) na Freeman Mbowe (Hai).
Licha kukamatwa, Halima Mdee na Ester Bulaya walifukuzwa bungeni kwa kipindi cha mwaka mmoja kwa madai ya utovu wa nidhamu bungeni.
Mbali na wabunge, mjumbe wa kamati kuu ya Chadema Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa aliitwa kuohojiwa Polisi mara kadhaa, kutokana na kauli zake kuhusu viongozi wa kundi la Uamsho waliokamatwa tangu mwaka 2012, huku Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye akinyang’anywa shamba lake lenye hekta 83 lililoko wilayani Mvomero Mkoa wa Morogoro.
Novemba 26 mwaka huu Mbunge wa Chadema, Susan Kiwanga (Mlimba) alikamatwa akiwa na makada 41 wa chama hicho, huku mbunge mwenzake Peter Lijualikali wa Kilombero naye akisakwa wakidaiwa kufanya fujo na kuchoma moto ofisi ya mtendaji baada ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi mdogo wa udiwani katika Kata ya Sofi wilayani Malinyi.
Baada ya kukamatwa, wabunge na makada hao walifikishwa mahakamani na kunyimwa dhamana, walirejeshwa mahabusu hadi Desemba 8, kesi iliposikilizwa na kuachiwa kwa dhamana.
Mwaka 2017, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji naye hakusalimika alijikuta akikamatwa akiwa wilayani Mbamba Bay Mkoa wa Ruvuma hivi karibuni akiwa na baadhi ya wabunge wa chama hicho, wakidaiwa kufanya mkusanyiko bila kibali.
Licha ya kukamatwa mara kwa mara na kushitakiwa, Tundu Lissu (Singida Mashariki) ameendelea kupata umaarufu mkubwa, akiibua hoja zinazoitesa Serikali.
Miongoni mwa mambo aliyoibua Lissu ni kukamatwa kwa ndege ya Tanzania aina ya Bombardier Q400 iliyoshikiliwa nchini Canada kutokana na deni la Dola za Marekani 38 milioni (Sh87 bilioni ) ambazo Serikali inadaiwa na kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd baada ya kukatishiwa mkataba wake wa kujenga barabara ya Bagamoyo mwaka 2009.
Lissu pia alitangaza kumpiga Rais Magufuli katika mikakati yake ya kukamata mchanga wa dhahabu (makinikia) bandarini wa kampuni ya Acacia Mining akimtaka Rais kufanya marekebisho ya mikataba ya madini, huku pia akiponda ripoti za uchunguzi wa michanga hiyo akiita upuuzi wa kitaaluma.
Jambo lingine lililompa umaarufu Lissu ni hatua yake ya kuwania urais wa chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), ambapo Serikali ilionyesha kupinga.
Awali Rais Magufuli akihutuibia katika siku ya Sheria Februari 4, 2016 aliitahadharisha TLS kutoingiliwa na wanasiasa.
Hata baada ya tahadhari hiyo, ilibainika kuwa Lissu ana mpango wa kugombea uongozi wa chama hicho.
Aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria wakati huo, Dk Harrison Mwakyembe pia aliwatahadharisha viongozi wa TLS kutojihusisha na siasa, huku baadhi ya wanasheria akiwamo Godfrey Wasonga wakifungua kesi kumpiga Lissu kugombea urais wa TLS. Hata hivyo Lissu alishinda kesi hiyo.
Siku moja kabla ya uchaguzi wa TLS uliofanyika jijini Arusha, Lissu alishikiliwa na Jeshi la Polisi na kufikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam kesho yake.
Baada ya kusomewa mashitaka alijidhamini na kwenda Arusha kushiriki uchaguzi na kuibuka na ushindi wa kishindo kwa kupata asilimia 85 ya kura zote Machi 18. Tukio la Lissu kupigwa risasi Septemba 7 limefungua ukurasa mpya wa mapambano, huku Chadema, Bunge na Serikali wakisutana.
Lissu alipigwa risasi akiwa mjini Dodoma saa 7:30 mchana ikiwa ni takribani mwezi mmoja tangu alipoeleza kufuatiliwa na watu wasiojulikana huku akitaja namba za gari wanalotumia.
Kabla ya Lissu kubainisha hivyo, Mbunge wa Nzega (CCM) Hussein Bashe alitahadharisha kuwepo kwa wabunge 11 waliohatarini kuuawa huku akidai kuwepo kwa kikundi kinachotekeleza mauaji hayo ndani ya Idara ya Usalama wa Taifa.
Mwezi mmoja kabla Bashe hajatoa tahadhari hiyo, aliyekuwa Waziri wa Habari, Nape Nnauye alishikiwa bastola na watu ambao hadi leo hawajulikani walikotokea, ikiwa ni siku aliyoondolewa kazi ya uwaziri ya Machi 28.
Tukio la kushambuliwa kwa Lissu ambaye bado amelazwa jijini Nairobi nchini Kenya, limetumiwa na kambi ya upinzani hasa Chadema kuieleza dunia jinsi demokrasia inavyokandamizwa nchini.
Walau Oktoba 30, vyama vya upinzani walipumua baada ya aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyaladu alitangaza kujitoa CCM na kuomba kujiunga Chadema.
Hilo lilikuwa pigo kubwa kwa CCM ambayo imeonekana kujibu mapigo kwa kazi kubwa.
Kabla ya Nyalandu, tayari kulikuwa na madiwani sita kutoka jimbo la Arumeru Mashariki waliojitoa Chadema na kujiunga na CCM.
Madiwani hao ni pamoja na diwani wa Ngabobo, Solomon Laizer, Credo Kifukwe wa Kata ya Murieti jijini Arusha, Anderson Sikawa (Leguruki), Emmanuel Mollel (Makiba), Greyson Isangya (Maroroni) na Josephine Mshiu (Viti Maalumu).
Hata hivyo, Mbunge wa jimbo hilo, Joshua Nassari alidai kuwa na ushahidi wa rushwa kwa ajili ya kuwarubuni madiwani hao, ambao aliupeleka makao makuu ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) jijini Dar es Salaam.
Baada ya kuwaonyesha waandishi wa habari video hizo, walizipeleka makao makuu ya Takukuru jijini Dar es Salaam na kukabidhi ushahidi wao.
Madiwani hao walipokelewa na Rais John Magufuli wakati wa sherehe za kukamisheni maofisa wapya wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijiniArusha.
Novemba 21 baada ya vikao vya Kamati Kuu ya CCM, waliokuwa makada wa Chadema akiwamo Lawrence Masha, aliyekuwa mwenyekiti wa Bavicha, Petrobras Katambi na waliokuwa makada wa chama cha ACT Wazalendo Alberto Msando, Samson Mwigamba na Profesa Kitila Mkumbo walijiunga na CCM na kupokelewa na Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli wakati wa mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa iliyofanyika ikulu, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Kama hiyo haitoshi, Novemba 22 aliyekuwa kada wa Chadema, David Kafulila alikihama chama hicho na kutangaza kujiunga na CCM.
Siku mbili baadaye alikabidhiwa kadi ya CCM na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole katika mkutano wa kumnadi aliyekuwa mgombea wa udiwani wa chama hicho, Kata ya Mbweni jijini Dar es salaam.
Kafulila ambaye ni mume wa Mbunge wa Viti Maalumu wa Chadema, Jesca Kishoa aliwahi kuwa mwanachama wa chama hicho kisha kufukuzwa, baadaye akajiunga na NCCR- Mageuzi ambapo alifanikiwa kuwa Mbunge wa Kigoma Kusini mwaka 2010-2015 na baadaye kurudi tena Chadema 2016 kabla ya kuondoka kwa madai upinzani hauna nia ya kupambana na ufisadi.
Hata hivyo, Kishoa alipinga madai ya mumewe akimtaka kusema ukweli na kwamba sababu alizozisema sizo zilizomuondoa ndani ya chama hicho huku akiongeza kwamba mume wake hana msimamo.
Baada ya Kafulila, zamu ikaingia kwa aliyekuwa Mbunge wa Kinondoni Dar es Salaam kwa tiketi ya CUF, Maulid Mtulia alijiengua chama hicho na kutangaza kujiunga na CCM akidai kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli. Mtulia alisema amefikia uamuzi huo kwa kuwa mambo yote waliyoahidi tayari yanafanywa vizuri zaidi na CCM, hivyo ni vigumu kuwa mpinzani.
Kama hiyo haitoshi pia Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira naye ametangaza kujiunga na CCM katika mkutano wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM (UWT) uliofanyika mjini Dodoma uliofunguliwa na Rais John Magufuli.
Mghwira aliyekuwa Mwenyekiti wa ACT Wazalendo aliteuliwa kuwa mkuu wa mkoa Juni 3, 2017 na kukabidhiwa ilani ya uchaguzi ya CCM, japo awali alisema ataendelea kuwa mwanachama wa chama chake cha awali.
Mbali na wanasiasa, wasanii nao hawakuwa nyuma kwani mwigizaji wa filamu Wema Sepetu naye alitangaza kukihama chama chake na kurudi CCM alikokuweko awali.
Mbunge aliyefunga kazi ni wa Jimbo la Siha, Godwin Ole Mollel Desemba 14, 2017 alitangaza kuihama Chadema na kujiunga na CCM.
Mbali na hamahama iliyoitikisa kambi ya upinzani, kushindwa vibaya kwenye uchaguzi mdogo wa madiwani kwa kupata kata moja kati ya kata 43 zilizokuwa zikishindaniwa Novemba 26, limekuwa pigo kubwa la kufungia mwaka.
Chadema iliambulia kata moja tu ya Ibighi iliyoko mkoani Mbeya, huku ikilalamikia vitendo vya ukatili kwenye kata walizodai kuwa na nguvu ya kushinda.
Ni kutokana na hatua hiyo, vyama vya upinzani vilivyo chini ya mwavuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na chama cha ACT Wazalendo wamesusia uchaguzi mdogo wa ubunge na udiwani utaofanyika Januari 13, 2018.
Japo kususia huko kumetafsiriwa na baadhi ya wachambuzi kuwa ni kukimbia ushindani, lakini pia kumepeleka ujumbe wa manyanyaso wanayodai kufanyiwa na chama tawala cha CCM.

Mlela Afunguka bado ajapata mwanamke Wa kuowa



MUIGIZAJI wa Bongo Muvi, Yusuf Mlela amefunguka kuwa bado hajamuona mwanamke wa kumshawishi kuoa hadi pale Mungu atakapomuonesha.
Akizungumza na Za Motomoto News, Mlela alisema kuoa ni kudra za Mwenyezi Mungu, akipatikana wa kuoa ataoa ila kwa sasa bado hajampata kwa kuwa kila anayemtazama hana vigezo wala sifa.
“Kuoa ni kudra za Mwenyezi Mungu, wakati wangu ukifika na nikampata mwanamke wa kuoa itapendeza, nitaoa ila kwa sasa bado naendelea kumtafuta, nikipata mwanamke yeyote anayejua thamani ya mume na anayeji

NEC Yathibitisha Kujitoa Kwa Mgombea Jimbo la Nyarandu



Dar es Salaam. Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imethibitisha kumtoa kwenye kinyang’anyiro cha ubunge Singida Kaskazini mgombea kwa tiketi ya Chadema, David Djumbe.
Mgombea huyo ameondolewa kwenye orodha baada ya kutimiza masharti kujitoa katika uchaguzi kwa mujibu wa sheria.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Ramadhan Kailima alisema jana kuwa Djumbe alifuata maelekezo kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi.
“Kama Sheria inavyosema Kifungu cha 49(1)(2) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura 343 mgombea anaweza kujitoa kwa kuandika barua na kuisaini yeye mwenyewe pamoja na ahadi ya kiapo cha sheria alichoapa mbele ya hakimu.
“Tume haimkubalii wala haimkatalii sababu ni hiari yake. Amewasilisha taarifa hizo na Tume imemfuta katika orodha ya wagombea,” alisema Kailima alipoulizwa jana kuhusu hatima ya mgombea huyo.
Desemba 20, Djumbe aliwasilisha nyaraka za kujitoa katika uchaguzi huo uliopangwa kufanyika Januari 13 mwakani akieleza kuwa jina lake lilipelekwa kimakosa.
Mkanganyiko ndani ya Chadema ndiyo uliosababisha jina la Djumbe kupelekwa NEC na kupitishwa kuwa mgombea ubunge Singida Kaskazini.
Wakati Chadema ngazi ya Taifa ikisema haitashiriki katika uchaguzi huo mpaka NEC itakapokutana na wadau kujadili changamoto zilizojitokeza katika uchaguzi wa udiwani katika kata 43, uongozi wa chama hicho mkoani Singida ulipeleka Tume jina la Djumbe kuwa mgombea.
Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Singida, Shaban Limu alisema Djumbe aliteuliwa kugombea na kamati ya utendaji ya wilaya.
Alisema wakati anateuliwa uongozi wilaya na mkoa ulikuwa haujawasiliana na makao makuu kujua msimamo juu ya uchaguzi huo.
Jimbo la Singida Kaskazini liko wazi baada ya aliyekuwa mbunge kwa tiketi ya CCM, Lazaro Nyalandu kujivua uanachama wa chama hicho hivyo kupoteza nyadhifa zote ukiwamo ubunge. Alijiunga na Chadema.
Uchaguzi pia unafanyika katika majimbo ya Longido ambako matokeo ya uchaguzi wa ubunge ya mwaka 2015 yalibatilishwa na Mahakama; na Songea Mjini ambako aliyekuwa mbunge kwa tiketi ya CCM, Leonidas Gama alifariki dunia.

Wasanii wanaovaa Nusu Uchi Waanza kushughulikiwa Na Serikali



Waziri wa Habari, Utamaduni, sanaa na Michezo, Dkt Harrison Mwakyembe amesema wizara imeanza kutekeleza agizo la Rais Magufuli juu ya baadhi ya wasanii ambao wanadaiwa kuwa chanzo cha kuporomoka kwa maadili ya kitanzania.
Waziri Mwakyembe ametoa taarifa hiyo alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari na kusema kwamba kitendo cha Rasi Magufuli kusema suala hilo, kimewapa nguvu ya kuzidi kupambana na wasanii, ambapo hapo awali walikuwa wakiwagusa huwajia juu na kulalamika.
"Pale tunapoona kuna ukiukwaji, tufumbe macho tusijali malalamiko yanavyokuja kutolewa, maana ukiwagusa wasanii walikuwa wanakuja juu sana, lakini tunashukuru mkuu wa nchi kulisemea hilo, basi na sisi tumeongezewa nguvu basi hatutaachia suala hilo kuendelea kuharibu vizazi vyetu", amesema Waziri Mwakyembe.
Hivi karibuni Rais Magufuli alizitaka mamlaka husika kuwachukulia hatua wasanii wanaovaa nusu utupu kwenye kazi zao za sanaa ambazo zingine huonyeshwa kwenye television, ambazo amedai hazina maadili na zinadhalilisha utamaduni wetu na kuharibu kizazi kijacho.

Baada ya Askofu Kakobe kuikashifu Serikali , CCM yamjibu



Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema Askofu Zakaria Kakobe wa Kanisa la FGBF lililopo Mwenge jijini Dar es Salaam amekosa hekima na busara kwa kugeuza madhabahu ya kanisa kuwa jukwaa la kisiasa na kuanza kukashifu viongozi wa serikali akiwemo Rais Dkt John Pombe Magufuli.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Dar es Salaam, Frank Kamugisha alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ikiwa ni siku moja baada ya Aksofu Kakobe kukosoa namna serikali inavyotenda mambo yake, akisisitiza kwamba Tanzania si nchi ya chama kimoja kama ambavyo viongozi wanataka kuigeuza na hivyo kuwataka viongozi wa serikali waanze kutubu.
Kamugisha amesema kuwa, wao kama viongozi wa CCM hawaweza wakakaa kimya wanapoona chama kinachafuliwa na viongozi wake ambao wanafanya kazi kwa niaba ya watanzania wakikashifiwa.
Aidha, alisema kuwa, siasa ni kwa ajili ya wanasiasa, na kama kiongozi wa dini ana jambo lolote analotaka kuzungumzia, kuna busara za kutumia na sio kutumia kanisa kusema hayo.

Marekani Yawawekea kikwazo wataalamu Wa kutengeneza Makombola korea Kaskazini




Marekani imewawekea vikwazo maafisa wawili wa Korea Kaskazini ambao inasema kuwa wamechangia kuundwa makombora ya nchi hiyo.
Wizara ya fedha nchini Marekani iliwataja Kim Jong-sik na Ri Pyong-chol na kusema kwua wote walikuwa viongozi wakuu katika mpango wa makombora ya masafa marefu wa Korea Kaskazini.
Baraza la ulianzi la Umoja wa Mataifa liliiwekea vikwazo vipya Korea Kaskazini siku ya Ijumaa kujibu majaribio yake ya makombora ya masafa marefu, Korea Kaskazini ilisema kwa hatua hiyo ni kama ya vita.
Vikwazo hivyo vipya vya Marekani vitazuia shughuli zozote za wanaume hao wawili zinazofanywa nchini Marekani, na hata kutwaliwa kwa mali yao yaliyo nchini Marekani.


Video | Mr Flavour Ft Zoro – Ijele | Mp4 Download

Video | Mr Flavour Ft Zoro – Ijele | Mp4 Download

Video | Mr Flavour Ft Zoro – Ijele | Mp4 Download

DOWNLOAD


Audio | Isha Mashauzi – Thamani Ya Mama | Mp3 Download

Audio | Isha Mashauzi – Thamani Ya Mama | Mp3 Download

Audio | Isha Mashauzi – Thamani Ya Mama | Mp3 Download

DOWNLOAD

Audio | Moni Centrozone Ft Country Boy – Mwaaah.| Mp3 Download

Audio | Moni Centrozone Ft Country Boy – Mwaaah.| Mp3 Download

Audio | Moni Centrozone Ft Country Boy – Mwaaah.| Mp3 Download

DOWNLOAD

Tuesday, 26 December 2017

Video | Kiss Daniel _ No Do | Mp4 Download

Video | Kiss Daniel _ No Do | Mp4 Download



DOWNLOAD

Nyumba ya Rais Yachomwa moto



Nyumba ya Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila imechomwa moto katika shambulizi linaloshukiwa kufanywa na waasi, ambapo askari mmoja aliuawa
Tukio hilo limetokea Desemba 25, 2017, ambapo taarifa zinasema kuwa waasi wa kundi lijulikanalo Mai Mai walijaribu kuiba mali kutoka makazi hayo ya rais yaliyoko eneo la Musienene, katika jimbo la Kivu ya Kaskazini.
Wakati wa tukio Rais Kabila hakuwa kwenye nyumba hiyo ambayo iko kijijini maili 1,680 Mashariki mwa mji wa Kinshasa, huku kundi la Mai Mai na kundi la waasi wa ADF wakiwa washukiwa wa kwanza juu ya tukio hilo.
Hivi karibuni Rais Kabila amekuwa akipingwa na wanasiasa mbali mbali kwa kitendo chake cha kutaka kugombea nafasi ya urais kwa muhula mwengi

Aliyemlawiti Mtoto Tarime Matatani



Jeshi la Polisi Mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya, linamshikilia Said Selemani 30-40 mkazi wa Mtaa wa Kebasa Halmashauri ya Mji Tarime mkoani Mara kwa tuhuma za kulawiti mtoto wa miaka minne.
Kamanda mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya, Henery Mwaibambe, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema mtuhumiwa amefunguliwa shtaka kituoni hapo namba TAR/IR/5034/2017 na kuwa atafikishwa mahakamani baada ya
upelelezi kukamilika.
Aidha, Kamanda huyo aliongeza kuwa mtuhumiwa huyo anatarajia kupelekwa mahakamani kesho ili kujibu shtaka linalomkabili kwa kuongeza kuwa mtuhumiwa huyo pia amatuhumiwa kumsababishia maumivu makali mtoto huyo.
Akizungumzia tukio hilo nyumbani kwake, mama mzazi wa mtoto huyo (jina limehifadhiwa), amesema tukio hilo lilibainika Disemba 14, 2017 wakati mtoto aliposhindwa kula na kuanza kuharisha mara kwa mara.
“Kugundua kuwa mtoto wangu ameathirika na kitendo hicho ni baada ya kuwa ameshindwa kula huku akiwa anaharisha mara kwa mara, kitendo ambacho kilinishtua moyo wangu na mtoto hakuwa na dalili ya kuugua ikabidi nianze kufanya ufuatiliaji wa kina ili kujua kilichompata,” alisema.
Ameongeza kuwa tukio hilo amelipokea kwa masikitiko makubwa na kuwa hakuwa na habari kuwa mwanaye wa miaka minne anaweza kutendewa kitendo cha kinyama kiasi hicho na mtuhumiwa ambaye ni mpangaji mwenzake.
Akizidi kufafanua, amesema kuwa baada ya kugundua mwanaye amekuwa akilawitiwa mara nyingi kwa nyakati tofauti, alichukua hatua za kwenda kwa wataalamu ili kuchukuliwa vipimo kwa ajili ya kijiridhisha.
“Hatua nilizochukua baada ya kugundulika kuwa mwanangu alikuwa ameathirika kwa muda mrefu ni kwenda kituoni polisi ili kutoa taarifa kwa hatua zaidi kuchukuliwa dhidi ya mtuhumiwa,”alisema mama huyo..
”Baada ya kwenda polisi ilibidi twende hospitalini kwa uchunguzi ambapo daktari alisema hakuona dalili zozote ila nikasema kuwa haiwezekani kuna mchezo unafanywa, andipo niliomba kwenda Bugando kwa uchunguzi zaidi ambapo polisi walitoa askari wa kwenda kujiridhisha,” aliongeza.
Alibainisha wakati wakiwa Bugando, daktari aliyemfanyia vipimo alisema mtoto huyo amelewitiwa mara nyingi zaidi ya mwaka mmoja.