Tuesday, 12 December 2017

New VIDEO: Faze ft Harrysong – Business Man

New VIDEO: Faze ft Harrysong – Business Man


New VIDEO: Faze ft Harrysong – Business Man


DOWNLOAD

Tabia 6 za kufuata kupata ngozi laini bila madoa/beauty habits to get glowing skin


1.TUMIA ANTIOXIDANT SERUM.
Sio kila mtu ana bahati ya kupata ngozi laini na nyororo bila kuifanyia kazi. Kwa wengine it a must to work hard ili kupata that perfect skin you have always wanted.

So Ladies you have to change your beauty routine, unatakiwa uanze asubuhi yako in a healthy way. Jinsi unavyoanza siku yako itaonesha kwenye uso wako.

Antioxidants kama vile Vitamin C&E hulinda ngozi yako ili isi dehydrate na pia zile aging radicals zitalindwa from UV-ray pollution na bad dietary habits(kula vibaya). Paka antioxidant serum baada tu ya kutoka kuoga, subiri dakika chache then paka moisturizer yako.

2.KULA PROTEIN YA KUTOSHA.
Kula breakfast ambayo ipo high in protein, husisha mayai, karanga, yogurt nk. Hivi husaidia kujenga collagen ambayo ndio kitu kikubwa ambacho hukusaidia ngozi yako isizeeke mapema. Ngozi yako haitokuwa na mikunjo wala kutepeta. Watu ambao hula protein for breakfast hula kidogo for the rest of the day, na pia protein husaidia kukuza nywele zako.

3.TUMIA SPF.

SPF ni lazima. Kila mmoja weto anapaswa kutumia SPF, hata kama wewe ni mweusi. Na kama hutumii kisa tu unaona kuwa makeup yako na moisturizer yako ina SPF, hiyo haitoshi. Paka SPF usoni, kwenye shingo, juu ya macho, kwenye lips, nyuma ya mikono, yani paka sehemu zote ambazo huwahi kuanza kuzeeka.

 4. HYDRATE! KUNYWA MAJI YA KUTOSHA.
Maji ni part kubwa sana ya urembo wa kila mtu. Kila asubuhi baada tu ya kuamka chukua maji ya uvuguvugu kamulia ndimu nusu kisha kunywa. Hii itasaidia kujenga more collagen..na ku-replenish ngozi yako.
5. MOVE YOUR BODY! EXERCISE
Si lazima kufanya yale mazoezi ya kufa mtu, No. Lakini ni lazima angalau uufanyishe mwili wako kazi kidogo. Unaweza hata ukaanza tu na mazoezi ya dakika 10-15 kila siku hadi utakapozoea.

Unaweza ukachagua kufanya Yoga. Kwa kifupi ni fanya kitu chochote ili kufanya heart rate yako ipande asubuhi, kunyoosha viungo vyako, ku-sweat kidogo. Lakini kama unajiweza si mbaya kufanya mazoeze haswa.

Mazoezi yatakupa nguvu for the rest of the day, pumps your blood na kukupa a glow kwa uso wako.
6. KUNYWA GREEN TEA
Yes Loves, green tea sio kwa ajili ya kukufanya upungue tu, bali husaidia pia ngozi yako. Ina-slowdown ageing process ya ngozi yako na kuifanya ionekane bado nzuri.


Tumia matunda haya ili kuboresha Ngozi yako



Wakati mwingine ili uweze kuboresha mwonekanao wa ngozi yako si lazima utumie makemikali yenye viambatano vyenye sumu ili uweze kufanya hivyo, bali inahitajika uweze kutumia matunda ambayo yana msada mkuubwa wa kuweza kufanya ngozi yako ing`are.

1.   Parachichi.
Tunda hili limekuwa maarufu sana kwa kutengenezewa juisi lakini huenda watu  hawalipendi kwa sababu kwa kutokuwa na sukari katika radha yake. Tunda hili lina vitamin kibao, ambapo pia huongeza mafuta mwilini kwa wale walitumialo mara kwa mara, wanashauriwa kula au kunywa juisi ya parachichi wakati wowote endapo kama huna matatazo yeyote yananahusiana na kuzidi kwa mafauta mwilini. Pia tunda hili huongeza uzito endapo utalitumia mara kwa mara.

2.   Apple.
Hili ni tunda maarufu sana duniani lihusishwalo na wapendanao, lakini tunda hili pamoja na kupema umaarufu mkubwa duniani na kuwa na vitamin na madini kibao, pia lina kazi sana katika kukupa muonekano mzuri wa ngoz  ya mwili wako. Tunda hili husaidia kuboresha mzunguko wa damu pamoja na kuhifadhi ngozi isipoteze uhalisia wake.

3.   Ndizi.
Hili pia ni tunda lenye jina kubwa kwa watu wengi wanaojali ulaji wa wa matunda, kwani ni tamu na lenya radha safi. Tunda hili husaidia kulainisha ngozi ya uso iliyokauka, kwa mfano utakuta kuna baadhi ya mafuta au rosheni zimechorwa ndizi. Kula ndizi ili urekebishe ngozi ya uso wako pamoja na kuupa uwezo mzuri wa umeng`enyaji chakula.

4.   Papai.
Ni tunda sahihi kabisa kati kukupa ngozi yenye mafauta, kurudishia au kuziba majeraha ya mwili. Papai pia hung`arisha ngozi rangi ya ngozi yako, yote haya hufanyika enzyme inayotokana na papai ambayo huitwa papain. Enadapo kama utaka kutumia papai katika ngozi yako, basi chukua asali changanya na papai liloiva nap aka usoni kwako kwa dakika kumi kisha safisha kisha utona kitakachotokea katika uso wako, utaonekana na kama ngozi ya mtoto wa siku moja.

Asante na endelea kutembelea Muungwana blog kila wakati.

Madhara Ya Kuangalia Video Za Ngono (Porn) Na Namna Ya Kuacha



Kuangalia video za ngono sio jambo jipya kwa jamii yetu, kimsingi ni watu wachache sana wanaweza kujizuia kujichua au kupiga punyeto baada ya kuangalia video za ngono.

Bahati mbaya tabia ya kuangalia video hizi watu wengi huipata wakiwa wadogo sana na usipokua makini tabia hii itakufanya vibaya sana kisaikolojia.

Tabia ya kujichua sasa iko wazi kwa jinsia zote yaani wanawake na wanaume japokua imekua ikiathiri zaidi wanaume sababu ya maumbile yao.

Japo wengi hufanya kwa siri na kuficha ili wasijulikane na wengine. Vijana wengi wamekuwa wakiangalia video hizo wakiwa wamejificha wenyewe chumbani, na hasa nyakati za usiku.

Kuangalia video za ngono kuna madhara mbalimbali ya kiafya na kisaikolojia. Haya hapa ni baadhi ya madhara unayoweza kuyapata kama utaangalia sana video za ngono.
Kuishiwa hamu ya tendo la ndoa na nguvu za kiume

Kuangalia sana video za ngono hukufanya ushindwe kusisimuliwa na mwanamke au mwanaume wa kawaida, video za ngono zina wanawake na wanaume wazuri sana ambao wako vile sababu ya kufanyiwa upasuaji mbalimbali wa kuongeza makalio na matiti, hata wanaume hufanyiwa upasuaji wa kuongeza uume hivyo mwanamke anayeangalia atatamani uume mkubwa kama ule au mwanaume anayeangalia atatamani mwanamke kama yule ambaye katika mazingira ya kawaida hayupo.

Sasa wanaume wanao angalia video za ngono hawawezi kusisimka au kuamsha uume hata mwanamke wa kawaida akipita uchi na hii huweza kuathiri sana mahusiano yao na kuonekana hawana nguvu za kiume kwani wao hutegemea video hizo kuamsha uume.

Kujichua au kupiga punyeto sana
Video za ngono zina wanawake na wanaume tofauti, kila video nzuri unayoangalia utaenda kujichua huku ukimuwaza wanaume au mwanamke husika. Hii itakufanya ujichue hata mara kumi kwa siku kama unaziangalia mara kwa mara. Kuishiwa nguvu za kiume, kusahau sana, kushindwa kumpa mwanamke mimba, kuchoka sana na kufika kileleni haraka wakati wa tendo la ndoa ni moja ya madhara makuu ya punyeto.

Kushindwa kudumu kwenye mahusiano
Kuangalia video za ngono hukufanya uwaze kujiridhisha mwenyewe tu na hata mwenza wako akitaka kulala na wewe unakua hutaki tena. Lakini hata kwa vijana ambao hawako kwenye mahusiano hujikuta wanakua waoga sana kuwafuata wanawake au wasione sababu ya kua kwenye mahusiano. Vile vile wanaume hushindwa kuwaridhisha wenza wao na wanawake kusingizia kuchoka kila siku.

Kuanza kufanya ngono ambazo sio za kawaida
Hivi karibuni idadi kubwa ya wanawake wamekua wakijihusisha sana na mapenzi ya kinyume na maumbile. Hii imesababishwa sana na kuangalia video za ngono na kuona ni kitu cha kawaida wakati kina madhara mengi. Wanawake waliozoea kuingiliwa nyuma hata wakiolewa huendelea kufanywa na wanaume wa nje hasa kama waume waliowaoa hawajawahi kujihusisha na tabia hiyo. Aina zingine za ngono ambazo zinababishwa na tabia ya kuangalia video hizi ni ushoga, usagaji, au mwanamke kulala na wanaume zaidi ya mmoja au mwanaume kulala na wanawake zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja.

Inawezekana wewe unayesoma hapa tayari hii tabia inakuumiza sana kwa sasa na umeshindwa kuiacha, kuna mambo ya msingi unaweza kufanya ili uweze kuacha kuangalia video hizi..

Ondoa zana zote za kuangalia video hizi
Kama una tarakilishi (computer) au simu futa video zote, futa tovuti (website) zote za video ambazo unazitumia kuangalia. Kuna watu wamo kwenye makundi ya WhatsApp ya kutumiana video za ngono, ondoka kabisa huko kwani unajiharibu.

Anza kufanya mazoezi
Ni mazoezi pekee yanayoweza kumfanya mtu aweze kuachana na tabia zote ambazo sio za kawaida ambazo alikua anazifanya kipindi cha nyuma. Unapofanya mazoezi utatumia nguvu nyingi na mwili wako utachoka na kupata usingizi. Vilevile ufanyaji wa mazoezi hukuepusha na kukaa bila shughuli yoyote.

Jijengee tabia ya kukaa na marafiki zako muda mrefu au kufanya shughuli nyingine zitakazokuweka ‘busy’

Kama una tabia ya kuangalia video hizi basi, fanya mpango uwe unafanya mambo mengine muda ambao umekua ukiangalia hizi video, ikiwemo kusoma vitabu au kuongea na watu. Hii itakusaidia kusahau video hizo na kuacha kabisa.

Pata ushauri wa kitaalamu na matibabu
Unaweza kumuona mtaalamu wa ushauri wa kisaikolojia ili kukusaidia ushauri wa namna ya kufanya ili kuepukana na tabia hiyo. Kama umeshapata madhara kiafya, basi waone wataalamu wa afya hasa masuala ya uzazi ili wakushauri namna ya kulitibu tatizo lako.

Jenga mahusiano ya karibu na mpenzi wako
Hii itakusaidia kumuwaza yeye zaidi ya video za ngono na pia pale unapopata hamu ya kufanya mapenzi basi hutoogopa kumwambia ili mfanye. Kuwa karibu na mpenzi wako kutakujengea ujasiri na kuyakuza mahusiano yenu.

New Action Movies 2017 | New Adventure movies 2017 English Subtitles

New Action Movies 2017 | New Adventure movies 2017 English Subtitles


Master Thief 2017 NEWEST ADVENTURE Movies Crime ACTION Full Length Movies

Master Thief 2017 NEWEST ADVENTURE Movies Crime ACTION Full Length Movies

Kwanini Jumuiya ya Wazazi Bungeni aingie 1, hii nitaifuta, tutaenda pasupasu - JPM

Kwanini Jumuiya ya Wazazi Bungeni aingie 1, hii nitaifuta, tutaenda pasupasu - JPM


Tuzo za Mwajiri bora mwaka 2017

Tuzo za Mwajiri bora mwaka 2017


Takukuru yaendelea na uchunguzi dhidi ya Manyara



Dar es Salaam. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru), imesema inaendelea na uchunguzi wa tuhuma dhidi ya mkuu wa mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti.

Mkurugenzi mkuu wa Takukuru, Valentino Mlowola aliliambia gazeti hili jana kuwa uchunguzi unaendelea baada ya kukamilika hatua nyingine zitafuata.

Mnyeti ambaye kabla ya kutuhumiwa kutoa rushwa alikuwa ni mkuu wa wilaya ya Arumeru, anadaiwa kunaswa katika mkanda wa video na sauti kupitia mtandao wa kiuchunguzi uliokuwa umetegwa na mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari.

Oktoba mosi, Nassari na Godbless Lema (mbunge wa Arusha Mjini) walipeleka ushahidi ambao unawatuhumu madiwani 10, kuhama katika chama hicho kwa kupewa rushwa huku wakiomba Rais John Magufuli kuchukua hatua ili kukomesha vitendo hivyo.

Nassari alisema katika ushahidi wao, ambao wameuonyesha kwa wanahabari wakidai madiwani waliojizulu wamepokea rushwa ya fedha, ajira, posho za vikao vyote vilivyobaki na kiinua mgongo cha udiwani miaka mitano na kulipiwa mkopo wa benki.

Kuhusu matumaini ya kukamilika kwa uchunguzi huo, Mlowola alisema: “Muda wa sheria kwa uchunguzi unaendelea tukikamilisha hatua nyingine zitafuata.”

Hata hivyo, kwa nyakati tofauti viongozi hao walikana tuhuma hizo, katibu tawala wa wilaya ya
Arumeru, Timoth Mzava ambaye alionekaa katika video hiyo, alisema ameufuatilia ushahidi unaozungumzwa na wabunge hao na kubaini kuwa ni wa kuungaunga na hauna ukweli wowote.



Arumeru, Timoth Mzava ambaye alionekaa katika video hiyo, alisema ameufuatilia ushahidi unaozungumzwa na wabunge hao na kubaini kuwa ni wa kuungaunga na hauna ukweli wowote.

Huyu ndie mshindi wa tuzo ya mchezaji bora Afrika



Mohamed Salah wa Misri amechaguliwa kuwa mshindi wa Tuzo ya BBC kwa Mwanakandanda Bora wa Afrika Mwaka 2017.

Nyota huyu wa Liverpool alipata kura nyingi zaidi ya Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon, Naby Keïta wa Guinea, Sadio Mané wa Senegal na mchezaji wa Nigeria Victor Moses.

"Nimefurahi sana kupata tuzo hii," mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 aliiambia BBC Sport.

"Huwa ni hisia ya kipekee unaposhinda kitu. Unahisi ulikuwa na mwaka mzuri sana. Kwa hivyo nina furaha sana. Ningependa kushinda tena mwaka ujao!"

Salah, aliyefunga mabao mengi zaidi ligi kuu England, akiwa na mabao 13, amekuwa na mwaka wenye mafanikio.

Mapema 2017 alikuwa nyota wa Misri walipochukua nafasi ya pili katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika.

Baadaye mwakani, mshambuliaji huyu aliye na kasi alichangia katika magoli yote yaliyowasaidia Mafirauni kufuzu kushiriki michuano ya Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza tangu 1990 - aliwasaidia wenzake kufunga mabao mawili, naye akafunga mabao matano, moja ikiwa penalti kati yao na Congo iliyowawezesha kufuzu kwa fainali hizo za Urusi.

"Ninataka kuwa mwanakandanda bora zaidi wa Misri kwa hivyo mimi hutia bidii," anasema kijana huyu ambaye amekuwa raia wa tatu wa Misri kupata tuzo hii tangu 2008.

"Mimi hufuata njia yangu na ninataka watu wote Misri kufuata njia yangu"

Mchezo wake kwenye klabu yake umekuwa mzuri sana, sawa na ule wa nchi yake.

Nchini Italia, alifunga mabao 15 na kusaidia ufungaji wa mengine 11 na kuisaidia Roma kumaliza katika nafasi ya pili kwenye Serie A, nafasi yao bora zaidi kwenye ligi katika miaka saba, kabla ya kujiunga na Liverpool na kufunga bao mara 13 katika mechi zao 16 za kwanza kwenye ligi.

"Ningependa kuwashukuru wenzangu wa timu ya Liverpool na pia nilikuwa na msimu mzuri na Roma, kwa hivyo lazima niwashukuru wenzangu huko na wale pia wa timu ya taifa," alisema Salah.

"Tangu nije hapa, nilitaka kujia bidii sana na kuonyesha kila mtu uchezaji wangu. Nilitaka kurudi Ligi ya Premia tangu nilipoondoka, kwa hivyo nina furaha sana."

Salah amerejea Ligi ya Premia kwa kishindi msimu huu, tofauti sana na alipokuwa kwenye ligi hiyo mara ya kwanza akiwa na Chelsea kati ya 2014-15.

"Anastahiki," anasema meneja wa Liverpool Jurgen Klopp, aliyemkabidhi mchezaji huyo tuzo yenyewe katika uwanja wa mazoezi wa klabu hiyo wa Melwood.

"Kwa kweli mimi ni mtu mwenye bahati sana. Nilikuwa na fursa ya kufanya kazi na wachezaji wachache wa kipekee, wazuri, na nina furaha kwamba sasa nina Mo.

"Jambo zuri ni kwamba yeye bado mdogo wa umri, anaweza kuimarika sana, ana uwezo mwingi ambao bado tunaweza kuufanyia kazi, na hivyo ndivyo inafaa kuwa. Ni furaha sana kwangu, kusema kweli, kufanya kazi naye."

Salah sasa ameongeza jina lake kwenye orodha ya wachezaji hodari kutoka Afrika, kama vile Abedi Pele, George Weah, Jay-Jay Okocha na Didier Drogba, ambao wamewahi kushinda Tuzo ya BBC kwa Mwanakandanda Bora wa Afrika wa mwaka.

"Nina furaha isiyo na kifani kuwa kama wao katika kushinda tuzo hii," amesema raia huyo wa Misri, ambaye amewafuata raia wenzake Mohamed Barakat (2005) na Aboutreika (2008) katika kushinda taji hilo.

Washindi wa awali wa Tuzo ya BBC kwa Mwanakandanda Bora wa Afrika wa Mwaka:

2016: Riyad Mahrez (Leicester City & Algeria)

2015: Yaya Toure (Manchester City & Ivory Coast)

2014: Yacine Brahimi (Porto & Algeria)

2013: Yaya Toure (Manchester City & Ivory Coast)

2012: Chris Katongo (Henan Construction & Zambia)

2011: Andre Ayew (Marseille & Ghana)

2010: Asamoah Gyan (Sunderland & Ghana)

2009: Didier Drogba (Chelsea & Ivory Coast)

2008: Mohamed Aboutrika (Al Ahly & Misri)

2007: Emmanuel Adebayor (Arsenal & Togo)

2006: Michael Essien (Chelsea & Ghana)

2005: Mohamed Barakat (Al Ahly & Misri)

2004: Jay-Jay Okocha (Bolton & Nigeria)

2003: Jay-Jay Okocha (Bolton & Nigeria)

2002: El Hadji Diouf (Liverpool & Senegal)

2001: Sammy Kuffour (Bayern Munich & Ghana)

2000: Patrick Mboma (Parma & Cameroon)

Atiwa mbaroni kwa kubaka watoto wanne



JESHI la Polisi Mkoa wa Kusini Unguja, linamshikilia kijana wa miaka 30 kwa tuhuma za kuwabaka watoto wanne, wawili wa familia moja.

Tukio hilo limeripotiwa Desemba 8, mwaka huu, huko Muyuni A, Mkoa wa kusini Unguja na mtuhumiwa huyo anadiwa kuwabaka na kuwalawiti watoto hao ambao ni chini ya umri wa miaka 18.

Kamanda wa Polisi mkoa huo, Makarani Khamis, alisema hapo awali mtuhumiwa  huyo alidaiwa kuwabaka watoto saba, lakini baada ya uchunguzi wa daktari ulibainika kuwa ni watoto wanne ndio walioharibiwa na watatu wakiwa salama.

Alisema mtuhumiwa huyo ambaye ni fundi seremala alidaiwa kuwafanyia matukio hayo watoto hao kwa siku na nyakati tofauti.

Alisema mtuhumiwa yupo ndani kwa hatua za kiupelelezi na zitapokamilika atafikishwa katika vyombo vingine vya kisheria kwa hatua zaidi.

Aliitaka jamii isiwe mbali na watoto wao kutokana na matukio ya udhalilishaji wanaofanyiwa watoto siku hadi siku.

Aidha, aliwashauri wazazi na walezi kufuatilia nyendo za watoto wao na kuhakikisha wanawaogesha badala ya kuwaacha waoge wenyewe ili kama ana majeraha aweze kugundua mapema.

Watoto hao walitambuliwa kuwa wanafanyiwa vitendo hivyo baada ya mmoja ya wazazi wa watoto hao kumgundua mwanawe akiwa anaharufu mbaya na alipomuhoji ndipo alipomtaja mtuhumiwa huyo.

Baada ya kumuhoji mtoto wake alimtaja mtuhumiwa huyo na kuwataja watoto wenzake ambao wamekuwa wakifanywa na mtuhumiwa huyo na kuwapa Sh. 5,000.

Sheha wa Shehia ya Muyuni ‘A’ Maulid Hassan Zidi, alisema baada ya kutokea tukio hilo kuna wananchi wengine zaidi ya saba wanalalamika watoto wao wameharibiwa na mtu huyo, lakini hakuna aliye kwenda kuripoti.

Aliitaka jamii kuripoti matukio hayo yanapotokea badala ya kulalamika mitaani kwani kufanya hivyo kunachangia watendaji wa makosa hayo kuendelea kuyafanya.Sheha huyo alisema katika shehia yake hilo ni tukio la kwanza kutokea ndani ya mwaka huu, lakini huko nyuma kuna matukio kama hayo yalitokea na watuhumiwa wapo mitaani ndio kinachowafanya wananchi kushindwa kuripoti matukio hayo.

Mbowe ameitaka Serikali kutoa tamko kuhusu Azory


Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ameitaka Serikali kutoa tamko kuhusu aliko mwandishi wa habari wa kujitegemea wa kampuni ya Mwananchi Communications Ltd, Azory Gwanda.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam kwa niaba ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Mbowe alisema kitendo cha Serikali kukaa kimya kinaleta wasiwasi kwa ndugu na jamii ya wanahabari.

“Sasa ni wiki ya tatu tangu Azory ametoweka nyumbani kwake, lakini Serikali haijatoa tamko lolote, hatuelewi nini kimemtokea,” alisema.

Azory (42), anayefanya kazi za uandishi wa habari Kibiti na Rufiji mkoani Pwani ametimiza siku 22 tangu atoweke kwa kuchukuliwa na watu wasiojulikana Novemba 21.

Mbowe alisema kumekuwa na matukio ya kutisha kama watu kupotea na maiti kuokotwa zikiwa zimefungwa kwenye mifuko hali ambayo inawatia wasiwasi wananchi.

“Tunaomba vyombo vya dola kuhakikisha uchunguzi wa kina unafanyika ili kufahamu aliko mwandishi huyo,” alisema.

Mbali ya wito huo, mwenyekiti wa Baraza Kuu la CUF, Julius Mtatiro alisema kufungia vyombo vya habari kwa sababu vimekosea kuandika takwimu si halali.

Alisema makosa ya takwimu yanatakiwa kusahihishwa lakini si kukifungia chombo cha habari kwa kuwa madhara yake ni watu kukosa ajira hata ambao hawakuhusika moja kwa moja na makosa yaliyofanywa.


Dully Sykse atokwa povu kisa Bombardier



Mkongwe wa Bongo Fleva nchini, Dully Sykse.

ETI kisa Bombardier! Mkongwe wa Bongo Fleva nchini, Dully Sykse ametoa povu ikiwemo kutangaza vita na wasanii wa kizazi kipya kwa sababu ya kushindwa kumsapoti kwenye wimbo wake mpya.

Dully Sykes ambaye ameachia wimbo mpya wa Bombardier, alisema wasanii wa sasa ambao wengi ni wapya wana roho mbaya na yeye yuko tayari kupambana nao.

“Wasanii wa sasa wana roho mbaya, hawasapotiani kama wasanii wa zamani, ndiyo maana Bombadier yangu hawajanisaidia kuitangaz, hiyo inaonesha muziki ni vita na mimi niko tayari kupambana nao,” alisema Dully