Tuesday, 12 December 2017

Jerusalem umekuwa mji mkuu wa Israel kwa miaka 3000 - Netanyahu



Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema kuwa wapalestina ni lazima wakubali kuwa Jurusalem ndio mji mkuu wa Israel ili amani iweze kupatikana.

Netanyahu alisema Jerusalem umekuwa mji mkuu wa Israel kwa miaka 3,000 na haujakuwa mji mku wa watu wengine.

Aliongea huku maandamano yakiendelea kwenye ulimwengu wa kiislamu kufuatia hatua ya Marekani kuutambua Jurusalem kuwa mji mkuu wa Israel.

Ghasia zilizuka karibu na ubalozi wa Marekani nchini Lebanon na kwingineno siku ya Jumapili.

Jerusalem kwenyewe, mpalestina mmoja alikamatwa kwa kumdunga kisu na kumjeruhiwa vibaya afisa wa usalama wa Israel karibu na kituo kimoja cha basi.

Akiongea mjini Paris baada ya mazungumzo na rais wa Ufaransa Emmauel Macron, Bw Netanyahu alisema kuwa jitihada za kuwanyima wayahudi mji wa wa Jerusalem ni kitu kibaya.

"Unaweza kusoma katika kitabu kizuri zaidi, kinaitwa Biblia, alisema. Unaweza kuyaskia katika historia ya jamii wa wayahudi kote duniani… Ni wapi tena kuna mji wa Israel, isipokuwa Jerusalem?



Kamanda alieiba matunda ya wapalestina asimamishwa kazi



Kamanda wa jeshi la Israel alieonekana  katika  operesheni ya kusambaratisha waandanaji el Halil Palestina akiiba matunda « aple » amesimamishwa kazi kwa muda.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya jeshi kuthibitisha tukio hilo.

Wauza  matunda  katika Ukingo wa Magharibi  walilazimika kuondoka katika vibanda vyoa wakikimbia ghasia ndipo kamanda huyo alionekana kuiba matunda.

Video  inayomuonesha kamanda huyo akiiba matunda imezagaa katika mitandao ya kijamii.

Simba yaachana na Mrundi


Baada ya Simba kuhusishwa na kutaka kumsajili Mrundi, Nahimana Shassir anayeichezea Rayon Sport, dili hilo limekufa rasmi baada ya Kocha Msaidizi wa Simba, Masoud Djuma kusema hawatamsajili.

Djuma ambaye ni raia wa Burundi, alipendekeza kusajiliwa kwa mchezaji huyo, lakini baada ya kumuangalia zaidi, amejiridhisha kwamba hata akija hatakuwa na msaada wowote.

Djuma amesema: “Nilipendekeza asajiliwe lakini mpaka sasa tumesitisha dili hilo kwa sababu ameshuka kiwango, nimemuangalia kwenye michuano ya Chalenji nimeona hajaisaidia chochote timu yake, hivyo hatutamsajili tena.

“Hatuwezi kumsajili mchezaji wakati uwezo wake ni mdogo kuliko wale waliopo ndani ya kikosi chetu cha sasa.”


Hata Kama Mambo Yanakwenda Vibaya, Fanya Hivi



Ni rahisi sana kuwa na hasira, kukatishwa tamaa na hata msongo wa mawazo. Hiki ni kiu ambacho kila mtu anaweza akawa nacho kwenye maisha yake.

Nikiwa na maana kila mtu akikasirishwa, anaweza akakasirika sana au mtu akikatishwa tamaa anaweza akakata tamaa pia sana.

Lakini yote hiyo haiwezi kusaidia kitu. Busara na ukomavu wako wa kimaisha unakuja pale hasa unapokwenda kinyume na mambo hayo.

Ni kweli unaweza ukawa umekasirishwa na ukatamani upige mtu sana, sasa je, kwani ni lazima ifike mahali ukakakasirika kwa kiasi hicho?

Ni kweli unaweza ukawa umekatishwa tamaa, lakini kwa wewe haina haja kuendelea kufanya mambo ambayo yanakukatisha tamaa zaidi.

Unachotakiwa kufanya au kujifunza ni kuweza kugeuza mambo ya hovyo na yakawa bora zaidi hata kama imetokea hali ya kukasirishwa au kukatishwa tamaa.

Kufanya hali mbaya ambayo tayari naweza kusema umeshapewa na ikawa ni nzuri, huo ni ukomavu wa hali ya juu utakaokufanya uishi vizuri sana duniani.

Mtu amekuuzi sana na wewe huhitaji kuendelea kufoka au kuumia zaidi. Unatakiwa kutuliza akili yako na kufanya mambo ili yawe mazuri.

Kufanya mambo yawe mazuri hasa pale yanapokuwa yameharibika ni kitu ambacho unatakiwa ujifunze nacho sana karibu kila siku.

Kila siku na kila wakati endelea kuweka juhudi za kuwa mtu chanya, mpaka maisha yako yalete utofauti mkubwa na kwa wengine.

Ni watu wachache sana ambao wako tayari kubadilisha hali mbaya ya msongo wa mawazo walionayo, kukatishwa tamaa na kukasirishwa kuwa nzuri.

Wengi wakikasirishwa na wengine hukasirika na kukasirisha zaidi. Hivyo, unatakiwa usiwe miongoni mwao. Unatakiwa uwe mtu wa kubadilisha hali.

Kufanya hali yoyote iwe bora ni zoezi ambalo unaweza ukalifanya karibu kila siku kwenye maisha yako pale ambapo unakuwa unaona mambo hayajakwenda sawa.

Unatakiwa uelewe hili, pale mambo yako yanapokwenda hovyo, fanya mambo hayo yawe bora. Jitahidi kubadili hali hiyo kwa busara na ikawa bora.

Matunzo Ya Kuku Wanaotaga



Hapa tunaangalia majogoo na mitetea yenye umri wa kuanzia miezi minne na kuendelea.

Matunzo mengi wanayopewa ni sawa na ya kuku wanaokua (tafadhali rejea kwenye somo la matunzo ya kuku wanaokua).

Matunzo mengine ya ziada:-
1. Watenge majogoo na matetea kwa idadi inayofaa.

Kama unafuga huria, jogoo mmoja kwa mitetea 6.

Kama unafuga kwenye vyumba, jogoo mmoja kwa mitetea 4-5.

2. Wape chakula cha ‘layers’ chenye virutubisho vya kutosha.

3. Endelea kuchanja Newcastle kila baada ya wiki 10.

 4. Endelea kuwapa dawa ya minyoo kila baada ya wiki 10.

5. Walishe majani na mboga mboga kwa wingi, ili mayai watakayotaga yawe na kiini cha njano.

6. Kuwa makini sana na sehemu ya kifua na eneo la chini la mitetea, ambapo ndipo mayai yanapohifadhiwa kwa ndani. Kuku akigongwa au akijigonga eneo hilo,  yai linaweza kupasuka kwa ndani, na tetea huyo atanyong'onyea, na baada ya siku kadhaa atakufa.

7. Okota mayai mara nyingi iwezekanavyo, ili kuzuia kuku kula mayai au wasiyavunje au kuyawekea ufa.

8. Kuku wanapoanza kutaga nunua daftari ya kutunza kumbukumbu za mayai yanayotagwa kila siku. Hii itakusaidia kujua siku wanapopunguza kutaga, ili kutafuta chanzo, na kama ni ugonjwa, watibiwe haraka.

Kila la kheri katika ufugaji wako, na endelea kuwa pamoja nasi katika masomo mengine ya ufugaji wa kuku.

Kama Unafikiri Mafanikio Utayapata Kwa Njia Hii, Sahau



Kujenga nidhamu binafsi na kuishi maisha unayoyataka wewe sio kitu rahisi kinachotokea tu mara moja.

Kujitoa na kufanya yale yanayotakiwa kufanyika ili kuweza kutimiza ndoto zako, halikadhalika hicho nacho si kitu rahisi.

Kuweza kutimiza ahadi zako na kuwa na mawazo zingativu juu ya ndoto zako pia nacho hicho si kitu rahisi kuweza kukufanikisha kama unavyofikiri.

Kupanga mipango yako na kufanyia kazi ili iweze kutoa mafanikio pia hicho sio kitu rahisi, kuna ugumu fulani unaojitokeza.

Ukiangalia katika maisha karibu kila kitu ambacho unataka kukifanya na kweli kikatoa mafanikio, kina ugumu wa aina fulani hivi.

Ukiona kuna jambo ukilifanya ni mteremko sana kwako na halihitaji wewe  kujibidiisha sana, ujue hapo kufanikiwa si rahisi sana pia.

Utaona mpaka hapo mafanikio yanahitaji nguvu na kujitoa sana kila wakati  na kila siku ili uweze kuyafikia.

Lakini ikiwa utaamua kuyaendea mafanikio kwa mkono wako mlegevu au kwa jinsi unavyotaka wewe kufanikiwa kwako itakuwa ni shida.

Hapa sina shaka unapata picha kamili kwamba hakuna kitu rahisi katika hii dunia. Kila kitu kina ugumu wake katika kukipata.

Ukiona mtu anakwambia mafanikio ni rahisi au wewe mwenyewe unaona mafanikio ya mwingine yamepatikana kama kwa urahisi vile, sio kweli.

Ipo namna yule mtu ambaye labda unamuona kafanikiwa kiurahisi kapigana na kuweza kufanikiwa kwa mafanikio yale.

Lakini ukiwa na ndoto za kufanikiwa huku umelala, na bila kijibiidisha vya kutosha andika utaumia hutaweza kufanikiwa popote.

Amua kwenye maisha yako kutenga muda wa kutafuta mafanikio yako, kubali kupigika kiakili, kimwili lakini usikubali ukashindwa kufanikiwa.

Unajua dunia tunayoishi ina kila kitu cha kukupa mafanikio. Kinachosababisha ukose mafanikio ni juhudi na nguvu zako tu na sio kitu kingine.

Kama unataka mali na pesa hizo zipo, lakini sio rahisi kuzipata, unatakiwa uweke juhudi na kufanya kazi kwa nguvu zote na kuachana na mchezo mchezo.

Kama utacheza na huku unasema unatafuta mafanikio makubwa, nikwambie tu ukweli huo ni uongo, ambao tena labda unajidanganya wewe na kuwadanganya na wengine pia.

Elewa hauna kitu ambacho cha kimafanikio ni rajisi katika maisha yako, ipo nguvu ambayo unatakiwa kuitumia ili kupata kitu chochote kile.

Chochote kile ambacho kinakupa mafanikio au chochote kile ambacho kinabadili tabia au hali yako na kuwa bora si rahisi sana kukipata.

Kama unafikiri mafanikio utayapata kwa njia ya urahisi, sahau. Unatakiwa kuweka juhudi kwa nguvu zako zote.


Mbinu Bora Ya Kuishi Ndani Ya Bajeti Yako


Hivi falsafa juu ya matumizi ya  bajeti ambayo ipo  ndani ya uwezo wako ikoje? Hili ni swali la muhimu sana ambalo kila mmoja wetu anatakiwa kujiuliza kataka maisha yake ya kila siku.

Nasema hivi kwa sababu moja kati ya tabia ya watu wengi huwa wanaishi nje ya bajeti ambayo wanakuwa wamepanga.

Yote hii hutoka na sababu kubwa moja, sababu hiyo ni pale mtu ambapo amepata fedha nyingi kwa wakati mmoja. Kitendo hicho ndicho ambacho humfanya mtu kuweza kuishi nje ya bajeti yake ya kila siku.

Kwa mfano mtu akipokea mshahara hawezi kuishi maisha ambayo alikuwa ameyazoea ukifananisha na alipokuwa hana pesa, unakuta matumizi yanakuwa mengi kuliko pesa aliyonayo. Wapo wengine mara baada ya kutumia pesa yote hujikuta wanaingia kwenye madeni yasiyo ya msingi.

Achilia mbali madeni, wapo baadhi ya watu pindi wapatapo pesa utakuta wananua vitu vingi hata ambavyo hawakupanga kununua, tatizo hili lipo kwa watu wengi sana, siwezi ita tu ni tatizo bali ni ugonjwa wa matumizi ya pesa.

Niliwahi soma kitabu kimoja cha kanuni ya pesa, ndani ya kitabu hicho mwandishi anasema ya kwamba ukimpa mtu maskini pesa basi ndani ya sekunde kadhaa basi jiandae kujua tabia za mtu huyo, hii ni kwasababu ni mtu ambaye mara zote huongozwa na pesa, basi kila kilichopo mbele yake anataka kukimiliki yeye.

Lakini pesa hiyo ukimpa mtu ambaye anaelewa ni nini maana ya pesa,  basi  pesa hiyo huweza kufanya kitendo cha uwekezaji, ili pesa hiyo iweze kujizalisha yenyewe hapo baadae. Kwa nukta hiyo jaribu kutafakari  hivi pesa ambayo huwa unaipata mikononi mwako   unajiona upo kundi gani kati ya hayo niliyoyaeleza?

Kama utaona ya kwamba upo kundi ambalo umekuwa ni mtumiaji mzuri kuliko kuwa mwekezaji basi tambua lipo tatizo kubwa ndani yako, ambalo linakufanya uishi nje ya mstari wa bajeti yako, Hivyo unatakiwa kujua ni kwa namna gani unatakiwa kuishi ndani mstari bajeti yako kwa kuzingatia jambo hili.

Jambo Kwanza kabisa hakikisha pesa isikupelekeshe hasa pale unapoipata ila wewe ndiyo unatakiwa kuipelekesha pesa, kwa kuzingatia ya kwamba pindi utakapo ipa nafasi pesa ikuendeshe  basi tambua fika lolote linaweza kutokea ndani yako.

Lakini pia kwa  kuwa wanasema pesa ina makelele sana hasa pale unapoipata hivyo hakikisha pale unapoipata pesa unaishi kwenye pajeti yako ambayo umeizoa, kwani pindi utapopandisha bajeti yako eti kwa sababu umeipata pesa basi tambua ya kwamba  utaunganaa na wale wanaosema vyuma vimekaza.

Hivyo  pesa isiongeze matumizi yako ya kila siku eti kwa sababu umepata pesa, hivyo kila wakati jifunze kuishi ndani ya bajeti yako.



Rafiki Wa Karibu Wa Kukupa Mafanikio Ni Huyu Hapa



Kama unataka kusonga mbele na kuwa na mafanikio makubwa zaidi, mshirika wa kwanza ambaye unatakiwa kushirikiana naye bila kumwacha hadi akakupa mafanikio hayo ni muda wako ulionao.
Ufanye muda uwe rafiki yako wa karibu sana ili ukupatie mafanikio. Usipoteze muda wako kwa mambo ya hovyo, fanya vitu vyako kwa umakini na mpangilio mkubwa, kila unapotumia muda wako.

Inawezekana maisha yako umekuwa ukiyaona hayafai hasa kwa kuona hujatimiza karibu kila kitu. Hiyo inaweza ikawa ni sawa, lakini wakati na nafasi ya kubadili mambo hayo na kuwa mazuri unayo tena.

Muda ukiutumia vizuri unaweza kukupa uwezo wa kukamilisha mambo ambayo kwa kawaida yalionekana ni magumu kuweza kuyatimiza. Kipi unachokitaka ambacho kitashindikana kwa sababu ya muda.

Je, unataka kuandika kitabu? andika mistari michache kila siku, muda utafika kitabu chako kitakamilika. Je, unataka kujenga biashara yako? anza na biashara yoyote hata kama ni ndogo sana na ikuze kidogo kidogo, muda ukifika itakuwa kubwa sana.

Chochote unachotaka kukifanikisha kwako inawezekana, hata iwe unataka kuongea lugha mpya? jifunze maneno machache kila siku na wakati utafika utafanya kwa ufasaha na kujikuta mzungumzaji tayari.

Kama nilivyotangulia kusema, karibu kitu chochote unachokitaka, kipo ndani ya uwezo wako na unayo nafasi kubwa ya kukifikia ikiwa utaamua kutenga muda wako kufanya jambo hilo na kulifanikisha.

Rafiki wa karibu yako, rafiki ambaye anaweza kukupa mafanikio makubwa sana  ni muda wako. Unatakiwa ukae chini na kujiuliza maswali ya msingi, je muda wako unautumia vizuri au hovyo hovyo.

Kama unatumia muda wako hovyo, utakuwa kwenye wakati mgumu sana wa kuweza kubadili hali ya maisha yako na hadi kuwa nzuri. Kumbuka hata ukiwa na hali mbaya vipi, lakini ukiweka juhudi na kujipa muda utafanikiwa.

Hakuna ambaye ameachwa mtupu, kama matumizi ya muda wake ni sahihi. Kama ulikuwa hujaanza kutunza muda wako kwa ajili ya mafanikio, anza leo. Fanya mambo ya kukua mafanikio hata kama ni madogo sana, baada ya miaka michache utafanikiwa.

Monday, 11 December 2017

Mo kusaini Miaka miwili Simba SC



KLABU ya Yanga imeshindwa kumpa kiungo Mohamed Ibrahim ‘Mo Ibra’ kile anachotaka, hivyo leo Jumatatu mchezaji huyo anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili na klabu yake ya Simba.

Akizungumza na Championi Jumatatu, Meneja wa Mo, Jamal Kisongo amesema kuwa mteja wake huyo anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili na Simba baada ya kushindwana na Yanga ambao nao walikuwa wanamtaka huku Msimbazi wao wakitimiza makubaliano waliyokuwa wanataka.

Alisema walifanya mazungumzo na Yanga lakini kuna baadhi ya vitu kwenye mkataba hawakuridhika navyo na walipozu-ngumza na Simba wakakubali kurekebisha baadhi ya vipengele kwenye ule mkataba wa awali hivyo rasmi mteja wake anabaki Simba na leo atasaini kandarasi baada ya ile ya awali kumalizika.

“Kesho (leo) natarajiwa kwenda kusaini mkataba mpya wa miaka mawili na mchezaji Mohammed pale Simba baada ya ule wa awali kumalizika, hivyo tunaongeza mwingine.
“Yanga nao walionyesha kumhitaji lakini kuna vitu walishindwa kukamilisha na tulipozungumza na Simba wamekubali kurekebisha baadhi ya vipengele, hivyo atabaki huko,” alisema Kisongo.





Kamishna Magereza awapa neno waliopata msamaha wa Rais


Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Juma Malewa amewataka wafungwa waliotolewa kwa msamaha wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli siku ya uhuru, waheshimu mamlaka iliyowatoa na waende wakawe raia wema huko waendako.

Kamishna Malewa amesema anaamini kuwa wafugwa hao walioachiliwa huru kwa msamaha huo wameshajifunza na kujirekebisha na kuwaomba raia wawapokee na kuwatengenezea mazingira ya kuwaingiza katika kazi ili na wao waende sambamba nao.

"Kwa wafungwa waliobaki gerezani wao nao waishi kwa amani, wafanye kazi warekebishike, kwahiyo kwa sasa hata wale wafungwa wa vifungo virefu ambao tulikuwa hatuwatumii huko nyuma kwa kuogopa mambo mbalimbali lakini sasa hivi watakuwa wamejifunza katika hili kwamba ukiishi gerezani ukirekebishika mheshimiwa Rais yupo atatumia mamlaka yake kama alivyopewa na atawasamehe kama alivyowasamehe wengine", amesema Kamishna Malewa.

Kamishna Malewa pia amemuelezea Nguza Viking (Babu Seya )  na kusema kuwa alikuwa mfungwa mwenye nidhamu sana na alipewa cheo kikubwa gerezani yaani Unyampara mwaka mmoja tu alivyoingia gerezani.

9 Desemba mwaka huu siku ya uhuru kwa mujibu ya ibara ya 45 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Rais John Pombe Magufuli alitoa msamaha kwa  wafungwa 61 waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa na wawili Nguza Viking (Babu Seya ) na Johnson Nguza (Papii Kocha ) waliohukumiwa kifungo cha maisha jela.










Kauli ya Roma baada ya Stamina kumvalisha pete mpenzi wake



kumuomba asihishie hapo amuoe kabisa mpenzi  wake huyo.

Kupitia ukurasa wake wa instagram msanii mwenzake ambae wanafanya naye kazi kwa karibu hivi sasa Roma mkatoliki amemtahadharisha kwa kumwambia " Congratulation My Brother @staminashorwebwenzi On Your #Engagement .Im Proud Of You Son....Sasa #Umuoe Sio Uishie Kwenye #Pete Tu!!Nisaidieni #Kumuwish Mdogo Wangu Marafiki!!"

Kheri James ashinda uenyekiti UVCCM



WAZIRI wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi, ambaye pia ni mjumbe wa Baraza la Wadhamini la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa (UVCCM), leo amemtangaza Kheri James kuwa Mwenyekiti mpya atakayeongoza kwa miaka mitano.

Kheri ametangazwa mshindi baada ya kupata Kura 319 kati ya kura 583 zilizopigwa akiwashinda wenzake 6 aliokuwa akichuana nao kuwania nafasi hiyo. Nafasi ya Makamu Mwenyekiti imechukuliwa na Tabia Mwita.

Mkutano wa Uchaguzi wa UVCCM umefanyika mjini Dodoma kwenye ukumbi wa Chuo Cah Mipango. Mbali na wajumbe wa idara hiyo ya vijana wengine walioshuhudia kutangazwa kwa Kheri ni Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana.

Mkutano huo wa uchaguzi wa UVCCM ulifunguliwa jana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt. John Pombe Magufuli na unafungwa leo na Rais wa Zanziobar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein.

Wagombea na Kura walizopata.
1. Kheri James 319
2. Tobias Mwesiga 127
3. Simon Kipala 67
4. Kamana Juma 27
5. Juma Mwaipaja 19
6. Seif Mtoro 16
7. Mganwa Nzota 1

Watoto sita wapelekwa Israel kwaajili ya Matibabu



Watoto sita wenye umri wa kuanzia mwaka mmoja hadi  miaka kumi na tatu wamepelekwa nchini Israel kwa ajili ya matibabu ya moyo.

Watoto hao wamepelekwa chini ya ushirikiano wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s  Heart – SACH) ya nchini Israel. Safari hiyo ya matibabu imejumuisha wauguzi pamoja na wazazi wa watoto ambao kwa pamoja wameondoka nchini Disemba 10 mwaka huu.

Baada ya matibabu ya watoto kukamilika, Maafisa Wauguzi wawili watabaki kwa ajili ya kuhudhuria mafunzo ya mwaka mmoja ya jinsi ya kuwahudumia wagonjwa waliopo katika wodi ya uangalizi maalum (ICU) na chumba cha upasuaji.

Aidha kundi hilo limekuwa ni kundi la tano la watoto kwenda kutibiwa magonjwa ya moyo nchini Israel tangu mwaka 2015 ambapo Taasisi ya Moyo ilianza ushirikiano  na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart –SACH) ya kuwapeleka wagonjwa nchini humo. Hadi sasa watoto 46 wameshatibiwa nchini humo na wanaendelea vizuri.