Tuesday, 12 December 2017

TANGAZA BIASHARA YAKO NA WINOKEMEDIA360



Tangaza Biashara yako nasi ili uweze kufikia malengo uliyo jiwekea katika Biashara yako, WINOKEMEDIA360 inauwezo mkubwa sana wa kuitangaza Biashara yako yoyote ile.

Kama vile
Maduka / Bidhaa
Makampuni na Mashirika
Shule / Vyuo
Viwanja / Mashamba
Nyumba / Apartment
Hotel / Restaurant
Mikutano / Sherehe


Bei zetu ni nafuu sana mawasiliano nasi 0675762540 Au 0688108760 Kwa Namba Ya Whatsapp.

MSANDO AMUANDIKIA MAKONDA "Tumewahi kupingana, kutofautiana, kubishana"

MSANDO AMUANDIKIA MAKONDA "Tumewahi kupingana, kutofautiana, kubishana"

Nassari atembelea waliopigwa kwenye Udiwani

Nassari atembelea waliopigwa kwenye Udiwani


Majibu ya Roma na Aslay baada ya Stamina kuvuta jiko

Majibu ya Roma na Aslay baada ya Stamina kuvuta jiko

Steve Nyerere atangaza kuwania tena Ubunge Kinondoni

Steve Nyerere atangaza kuwania tena Ubunge Kinondoni


Alichoongea Thobias Mwisiga baada ya kuukosa Uwenyekiti UVCCM

Alichoongea Thobias Mwisiga baada ya kuukosa Uwenyekiti UVCCM


Kauli ya Waziri Mwijage juu ya wanaohama vyama vyao


MAGAZETI LIVE: Siri nzito Babu Seya, Aliyesamehewa na Magufuli, alifutiwa kifo na Nyerere


Audio | Tunda Man – Toto | Mp3 Download

Audio | Tunda Man – Toto | Mp3 Download
Audio | Tunda Man – Toto | Mp3 Download

Shamsa Ford ampa somo Shilole kuhusu ndoa


 STAA wa Filamu nchini, Shamsa Ford amefungukia uamuzi wa msanii mwenzake wa Muziki, Zuwena Mohammed maarufu kama Shilole kwa kuamua kufunga ndoa tena ya Kidini na mpenzi wake, Uchebe ndoa iliyoshuhudiwa hivi karibuni na kutikisa kwenye mitandao na vyombo vya habari huku ikiwaacha midomo wazi kwa wale walidhani kuwa angerudiana na mpenzi wake wa zamani, Nuh Mziwanda.

Shamsa ambaye pia alifunga ndoa mwaka huu na mpenzi wake, Chidi Mapenzi ametumia ukurasa wake wa Instagram kumsihi Shilole atulie, aweke umaarufu pembeni, aitunze ndoa yake na hatimaye atafaidi matunda ya ndoa iliyo bora.

Shamsa ameandika;
“Hongera sana mamy. Umefanya maamuzi sahihi ya kumpendeza Mwenyezi Mungu.Cha muhimu uwe mke bora wa Kitanzania kwa mumeo na ustar uweke pembeni.

“Mumuweke Mungu mbele, uvumilivu na kuheshimiana inshaallah mtazikana.Karibu kwenye Chama mama….Sasa nyie mnao subili matajiri wawaoe wakati hao matajiri wana wake zao wameanza nao moja mtasubili sana mpaka uso uote sugu.Uzuri na Ustar una mwisho wake. Iitafika muda hata inzi hakusogelei……HONGERA MAMA @shilolekiuno_badgirlshishi,” ameadika Shamsa.






Zanzibar: Bei mpya ya mafuta kwa mwezi wa Disemba kuanzia Kesho



MAMLAKA ya udhibiti wa huduma za nishati na maji Zanzibar (ZURA) imetoa taarifa juu ya bei mpya ya mafuta itakayoanza kutumika rasmi kuanzia kesho Jumanne tarehe 12-12-2017. Akizungumza na waandishi wa habari huko ofisini kwake Maisara, Kaimu Mkurugenzi masuala ya wateja, Mussa Ramadhani Haji  alisema kuwa bei hizo Zura imepanga kufuatia mambo yafuatayo;-

Wastani wa mwenendo wa mabadiliko ya bei za mafuta Duniani (Platts Quatations) katika mwezi wa Novemba 2017 , kwa lengo la kupata kianzio cha kufanyia mabadiliko ya bei za mafuta kwa mwezi wa Disemba 2017.

Pia thamani ya shillingi ya  Tanzania , gharama za usafiri , Bima na’ Premium ‘hadi Zanzibar  . Kodi za serikali  na kiwango cha faida kwa wauzaji wa jumla na rejareja.

Alisema bei za rejereja ya mafuta ya Petroli kwa mwezi wa Disemba, 2017 imepanda kwa shillingi (100) kwa lita kutoka shilling 2,130 Mwezi wa Novemba , 2017 hadi shilling 2,230 kwa lita katika mwezi wa Disemba , 2017 sawa na ongezeko la asilimia 4.5%.

Pia alisema bei ya rejereja ya mafuta ya Dizeli kwa Mwezi wa Disemba , 2017 imeshuka kwa shilling (90) kwa lita kutoka shilling 2,280 kwa lita katika mwezi Novemba hadi shilling 2,190 kwa lita katika mwezi wa Disemba, 2017 sawa na  asilimia 4%.

Aidha alisema bei ya reja reja ya mafuta ya Taa kwa mwezi wa Disemb 2017 imepanda kwa shilling (80)  kwa lita kutoka shillingi 1.539 kwa lita katika mwezi wa Novemba , 2017 hadi shilling 1,619 katika mwezi wa Disemba , 2017 sawa na ongezeko la asilimia 4.9%

Vilevile bei ya reja reja ya mafuta ya Banka kwa mwezi waDisemba,  2017 imeshuka kwa shilling (90) kwa lita kutoka shillingi 2,122 kwa lita katika mwezi wa Novemba, 2017 hadi shilling 2,032 katika mwezi wa Disemba , 2017 sawa na ongezeko la asilimia 4.4%.

Handeni: Wauzaji wa nyama wagoma kufungua maduka ya kuuzia bidhaa hiyo.



Wauzaji wa nyama pamoja na wachinjaji wanaofanya shughuli zao kwenye machinjio yaliopo wilayani Handeni mkoani Tanga wameendesha mgomo wa kutokuchinja na kuuza nyama mpaka pale viongozi wa halmashauri watakaposikiliza kero zao na kuzitatua ikiwemo ya kulazimiswa kutumia gari maalum la kusambaza nyama hali ambayo wamesema kuwa hawakushirikiswa ipasavyo kwenye swala hilo.

Kamera ya ITV imefika machinjio ya wilaya na kukuta yakiwa meupe bila kuwepo dalili ya kupatikana huduma hiyo na ilifanikiwa kuongea na mwenyekiti wao na hapa anaelezea sababu.

Hata hivyo mkurugenzi wa halmashauri ya mji alifika machinjioni hapo na kukiri kuwa kweli ushirikishwaji haukufanyika huku wafanya biashara hao wakimkataa daktari wa machinchio hayo mbele ya mkurugenzi.

Rais wa Korea Kaskazini ampinga Trump kuhusu Jerusalem



Rais wa Korea-Kaskazini Kim Jong Un amesema kuwa uamuzi wa Trump kutangaza kuutambua mji wa Jerusalem kama mji mkuu wa Israel hauna maana yeyote.

Mpango wa Marekani kuamisha ubalozi wake Tel Aviv na kuhamia Jerusalem ni jambo la kukemewa.

Kim Jong Un anapinga uamuzi wa Trump kuhusu jiji la Jerusalem.

Rais wa Korea-Kaskazini amesema kwa kejeli kuwa iwapo kuna taifa linaitwa Israel basi mji wake mkuu uwe Jerusalem.

Kwa mujibu wa kituo cha habari cha Ufaransa cha AFP ni kwamba  msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Korea-Kaskazini amesema kuwa Marekani i natishia amani na utulivu  ulimwenguni .

Ujumbe wake ulimalizia kwa kusema kuwa  Korea-Kaskazini ipo bega kwa bega na wapalestina  na waarabu wanaopigania haki yao.