Monday, 4 December 2017

NINE TAILED FOX 13 BY DJ MOO FAYAA

NINE TAILED FOX 13 BY DJ MOO FAYAA

NINE TAILED FOX 12 BY DJ MOO FAYAA

NINE TAILED FOX 12 BY DJ MOO FAYAA


NINE TAILED FOX 11 BY DJ MOO FAYAA

NINE TAILED FOX 11 BY DJ MOO FAYAA

NINE TAILED FOX 10 BY DJ MOO FAYAA

NINE TAILED FOX 10 BY DJ MOO FAYAA


NINE TAILED FOX 09 BY DJ MOO FAYAA

NINE TAILED FOX 09 BY DJ MOO FAYAA

NINE TAILED FOX 08 BY DJ MOO FAYAA

NINE TAILED FOX 08 BY DJ MOO FAYAA


NINE TAILED FOX 07 BY DJ MOO FAYAA

NINE TAILED FOX 06 BY DJ MOO FAYAA

NINE TAILED FOX 06 BY DJ MOO FAYAA


NINE TAILED FOX 05 BY DJ MOO FAYAA

NINE TAILED FOX 05 BY DJ MOO FAYAA


Rais Magufuli kuzindua kampeni ya Uzalendo na Utaifa


Kampeni ya Uzalendo na Utaifa ‘Nchi Yangu Kwanza’ itazinduliwa Ijumaa hii Disemba 8 2017 kupitia ‘Usiku Wa Kitendawili’ mjini Dodoma ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na msanii wa muziki wa asili nchini, Mrisho Mpoto kupitia Kikundi cha Sanaa cha Mpoto Theatre Gallery na wadau wa sanaa za Ubunifu ndio wataouratibu usiku huo wa Kitendawili.

Usiku wa Kitendawili ulianzishwa baada ya msanii wa muziki wa asili nchini, Mrisho Mpoto kuachia wimbo ‘Kitendawili’ na baadaye kufikiria kuanzisha usiku wa wimbo huo na kuanzisha mjadala kuhusu uzalendo.


Akiongea na wadau wa sanaa katika Maandalizi ya Kampeni hiyo ya Kitaifa itayokuwa ikifanyika kila mwaka sambamba na maadhimisho ya kifo cha Baba wa Taifa, Hayati Julis Kambarage Nyerere, Mrisho Mpoto amesema kampeni hiyo ina lengo la kurejesha hali ya Uzalendo na Utaifa katika kutatua changamoto zilizojitokeza na zitakazojitokeza ndani ya Taifa letu.

Alisema mambo ambayo yatayozingatiwa katika kampeni hiyo ni pamoja na kudhubiti na hatimaye kukomesha kabisa mmomonyoko wa maadili kwa viongozi wa Umma, kuongezeka kwa tuhuma za rushwa, kuibuka ufisadi, ubadhilifu wa mali za Umma pamoja kuongeza hari ya kufanya kazi na Uzalendo.

“Usiku wa Kitendawili utatumika kama jukwaa la kuwaleta pamoja watanzania pamoja na viongozi wao ili kukumbushana kuhusu wajibu na kujadili mustakabali wa Taifa. Kutakuwa na vivutio mbalimbali pamoja na wimbo maalumu kutoka kwa wasanii maalumu Mwaka Huu,” alisema Mpoto.

Aliongeza,”Tumekuja kuunadi Uzalendo na Utaifa ‘Nchi Yangu Kwanza’ kwasababu tunaamini Uzalendo na Utaifa lazima uwepo ili kufanikisha maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kisiasa ili kuunga mkono juhudi za Raisi Dkt.

John Pombe Magufuli za kujenga Taifa lenye Uzalendo, Utu, Weledi na Uadilifu uliotukuka. Mimi ni mzalendo ndio maana hata kwenye hizi harakati nipo toka nimetoa wimbo wangu wa kwanza, ukiangalia nyimbo zangu zote ni za kuonganisha jamiii 120 za watanzani,”

 “Naamini kwenye kufanya kazi ambayo itawafanya watanzania pamoja na kizazi kijacho kitambue kuna watu ambao walifanya kazi kubwa kwenye hili taifa, kuacha alama ambazo haziwezi kufutika katika maisha ya historia ya nchi hii, kwa sababu hivi vyote ambavyo vinaenda kufanywa ni kufufua upya na kuiweka pamoja mitazamo ya watanzania ili kujenga Taifa la Wazalendo na Wachapakazi kuiga nyayo zilizoachwa na hayati Baba wa Taifa,” alifafanua zaidi.

Mpoto amesema lengo kuu la maadhimisho hayo kuambatana na maadhimisho ya kifo cha Baba wa Taifa kuanzia mwaka 2018 ni kutumia jukwaa hilo kufikisha ujumbe wa umuhimu wa kujenga na kuendeleza Utaifa.

Alisema baada ya uzinduzi wa kampeni hiyo wiki hii huko Dodoma, itafanyika kwenye mikoa yote nchini na itasimamiwa na Kamati za Utamaduni chini ya Uwenyekiti wa Mkuu wa Mkoa na  Wilaya.

Ndoa yampapresha Shilole



WAKATI akisubiri kufunga ndoa na mchumba wake, Uchebe Ashraf siku chache zijazo, staa wa muziki Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ yu gonjwagonjwa, Ijumaa Wikienda limedokezwa.

Chanzo makini ambacho ni mtu wa karibu wa wawili hao kilieleza kuwa, ndoa hiyo inampa presha Shilole kwani alizidiwa hivi karibuni na kwenda kulazwa hospitali licha ya kwamba kwa sasa anaendelea vizuri tofauti na awali.

“Unajua Shilole anatarajia kufunga ndoa na Uchebe hivi karibuni, kwa hiyo ana presha ya ndoa na ukizingatia na watu walivyozusha kuwa amerudiana na mpenzi wake wa zamani, Nuh Mziwanda ndiyo wakamchanganya kabisa,” kilidai chanzo hicho.

Ili kuujua ukweli wa habari hizo, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Shilole baada ya kuona picha alizosambaza mchumba wake Uchebe zikimuonesha mwanamama huyo akiwa amelazwa hospitalini ambapo alikiri kuzidiwa lakini akasema presha ya ndoa bali ni malaria.

“Jamani nililazwa hospitali kwa Dokta Mvungi kwa sababu nina malaria kali. Nilikuwa hoi, nikawekewa dripu, lakini kwa sasa ninaendelea vizuri na nimetoka hospitali,” alisema Shilole kwa sauti ya unyonge.

TBA yakiri mabweni ya UDSM kuwa na nyufa




Mkurugenzi wa Wakala wa Majengo nchini Mhandisi Elius A. Mwakalinga, amekiri picha zinazosambaa mitandaoni zikionyesha majengo mapya ya mabweni ya UDSM yana nyufa ni za majengo hayo, huku akisema ni kitu cha kawaida kwa majengo makubwa.

Akizungumza na mwandishi wa East Africa Television, Mwakalinga amesema kutokea kwa nyufa hizo ni moja ya hatua za 'expansion joint' ambazo hutumiwa kwenye ujenzi wa majengo, lakini majengo hayo yamekidhi vigezo vyote na vipimo wakati wa ujenzi wake.

"Kila design tunayofanya ya majengo sasa hivi tunatumia expansion joint, majengo mengi makubwa huwa inatumia hiyo, hivyo ni common na sio creck kubwa sana kama inavoonekana kwenye picha, nilienda ile jana usiku kukagua tukakuta hiyo hali, ni process za majengo ili yaweze kusatle, hivyo watu wawe na amani kabisa wala wasiwe na hofu", amesema Bwana Mwakalinga.

Mwakalinga ameendelea kwa kusema kwamba watu wanaosambaza picha hizo bila kutaka ufafanuzi kutoka kwake wanafanya makosa kwani wanawatia watu hofu kwa jambo la kawaida kwenye hatua za ujenzi, huku wakilaumu kitu ambacho hawana uhakika nacho.




Nafasi za kazi leo Dec 4