Monday, 27 November 2017

Audio | Fabreezy – Sina Team | Mp3 Download

Audio | Fabreezy – Sina Team | Mp3 Download

Fabreezy - Sina Team

Audio | Fabreezy – Sina Team | Mp3 Download


                                                DOWNLOAD HERE

Audio | Dully Sykes – Bombardier(Instrumental) | Mp3 Download

Audio | Dully Sykes – Bombardier(Instrumental) | Mp3 Download

Dully Sykes – Bombardier(Instrumental)

Audio | Dully Sykes – Bombardier(Instrumental) | Mp3 Download


                                              DOWNLOAD HERE

Video | Walter Chilambo – Kuna Jambo | Mp4 Download

Video | Walter Chilambo – Kuna Jambo | Mp4 Download

Walter Chilambo - Kuna Jambo

Video | Walter Chilambo – Kuna Jambo | Mp4 Download




                                                 DOWNLOAD HERE

Video | Saida Karoli – Omulilo | Mp4 Download

Video | Saida Karoli – Omulilo | Mp4 Download


Saida Karoli - Omulilo

Video | Saida Karoli – Omulilo | Mp4 Download






                                                       DOWNLOAD

Gospel Audio Walter Chilambo – Kuna Jambo.| Mp3 Download

Gospel Audio Walter Chilambo – Kuna Jambo.| Mp3 Download


Gospel Audio Walter Chilambo – Kuna Jambo.| Mp3 Download


                                                 DOWNLOAD HERE

Audio | AT. – Homa.| Mp3 Download

Audio | AT. – Homa.| Mp3 Download


Audio | AT. – Homa.| Mp3 Download



                                                      DOWNLOAD HERE

Sunday, 26 November 2017

Rais Magufuli aishukuru Serikali ya watu wa China kwa msaada wao




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, ameishukuru serikali ya watu wa China kwa msaada wao walioutoa kwa wananchi wa Tanzania wa kuwapatia matibabu bure, akisema jambo hilo ni upedo usio elezeka.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo alipoenda kutembelea meli yenye madaktari bingwa kutoka China ambayo imetia nanga kwenye bandari ya Dar es salaam, na kutoa huduma za vipimo na matibabu kwa wakazi wa Dar es salaam bila gharama yoyote.

"Tunapenda kusema shukrani kwa dhati kwa serikali ya China kuamua kuituma meli na madaktari kuja Tanzania, tunafurahi kwa huduma zao, wameokoa maisha ya watanzania zaidi ya elfu 6,400, huu ni upendo wa pekee unaogusa, ndio maana leo nimeshindwa kuvumilia nimeona bora nije nishukuru, nimeguswa mno na ndugu zetu wachina, yapo mataifa mengine matajiri, yenye mali nyingi lakini hayajaguswa", amesema Rais Magufuli.

Sambamba na hayo Rais Magufuli amewakabidhi madaktari hao barua maalum kwenda kwa raisi wa nchi yao Xi Jinping pamoja na kinyago kama zawadi kwake, kumshukuru kwa mchango wake na ukarimu wake kwa watanzania masikini.

Pia Rasi Magufuli amewatakia safari njema madaktari hao na kuwaomba kurudi tena wakati mwengine, na kuwataka kukaa kwa muda mrefu zaidi ili waweze kutoa huduma kwa watanzania wengi hata watakaotoka mikoani.


Mawakala wa vyama wazuiwa kuingia vyumba vya kupiga kura



Manyara. Mawakala wa vyama vya CCM, Chadema na ACT Wazalendo kwenye Kata ya Makiba wilayani Arumeru wamezuiwa kuingia katika vyumba vya uchaguzi kwa madai ya kukosa vibali.

Kata hiyo ina jumla ya vituo 14 na hadi hivi sasa upigaji kura unaendelea bila kuwepo kwa mawakala hao 42 wa vyama hivyo.

Mgombea udiwani wa CCM katika kata hiyo Samson Laizer amethibitisha Mwananchi Leo Jumapili kuwa mawakala wake kuzuiwa kuingia kwenye vituo vya kupiga kura.

Vilevile wakala wa Chadema wa Kituo cha Kanisani A,  Adam Woisso amesema japokuwa alikuwa na barua ya utambulisho wa chama hicho na barua ya uthibitisho ya Tume ya Taifa ya  Uchaguzi(NEC) lakini alizuiwa kuingia ndani.

Kwa upande wake wakala wa ACT Wazalendo, Said Yusuf amesema alizuiwa kuingia kwa sababu ya kukosa barua kutoka NEC.

Mgombea udiwani wa ACT Wazalendo, Ernest Maturo amesema hizo ni mbinu za kuhakikisha mgombea udiwani anayetakiwa kushinda na tume anashinda nafasi hiyo.

Familia ya Ndikumana yafanya maamuzi haya juu ya mtoto Krish Ndikumana



Familia ya marehemu Ndikumana ambaye alikuwa mume wa muigizaji wa filamu Tanzania, Irene Uwoya, imesema iko tayari kumsaidia mtoto wao aliyeachwa na marehemu Hamadi Ndikumana, Krish Ndikumana, ili kuweza kufikia ndoto yake ya kuwa mcheza soka maarufu

Akizungumza na Big Chawa kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, mdogo wa marehemehu Hamadi Ndukaman, Laddy Ndikumana, amesema wao kama familia wako tayari kuhakikisha ndoto hiyo inatimia, kwani kipaji cha soka kipo kwa familia yao nzima.

"Tutajaribu kumsaidia kwa sababu kama familia nzima ni wanasoka, na hiyo ni kipaji ambacho yuko nacho tayari, tutamsaidia kufikia malengo yake", alisikika Laddy Ndikumana akimwambia Big Chawa.
Marehemu Ndikumana ameacha watoto wawili akiwezo Krish ambaye amezaa na muigizaji Irene Uwoya, na aliwahi kusikika akisema nataka kuwa mcheza soka maarufu kama baba yake.

Yanga yamsajili kimya kimya straika Mkomola



STRAIKA wa timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 20 'Ngorongoro Heroes', Yohana Mkomola, amesaini mkataba wa miaka miwili kwa ajili ya kuichezea Yanga, kuanzia mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara.

Mkomola ambaye ni tegemeo ndani ya Ngorongoro Heroes, alijiunga na Etoile Du Sahel  mwezi Agosti, klabu iliyomchukua kwa makubaliano maalumu ya kumlea kwa sababu alikuwa na miaka chini ya 18 na baada ya hapo, wangemsajili jumla.

Hata hivyo, licha ya tetesi hizo kujulikana, uongozi wa Yanga na Mkomola mwenyewe, wamegoma kuthibitisha na wakidai kama suala hilo lipo, litajulikana tu.

Huo utakuwa usajili wa pili wa Yanga, awali walimsajili Mcongo Fiston 'Festo' Kayembe Kanku kwa mkataba wa miaka mwili.

Hizi ndio sababu za Dk Shika kualikwa Kahama




Kahama. Mkurugenzi wa Chuo cha Tiba ya Binadamu Kahama, Yona Bakungile amesema alimualika Dk Louis Shika kwenye mahafali ya kwanza ya wanachuo wake kwa sababu ya ahadi zake za shaka za ununuzi wa nyumba, alizoshinda kwenye mnada zitasaidia kutangaza chuo hicho.

Novemba 9, Kampuni ya Udalali ya Yono kwa niaba ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), iliendesha mnada wa nyumba mbili za Lugumi zilizopo Mbweni JKT na moja ya Upanga jijini Dar es Salaam ambazo zote Dk Shika alifikia bei ya kuzinunua kwa Sh3.2 bilioni lakini alishindwa kulipa asilimia 25 ya mwanzo.

Akizungumza na Mwananchi mjini Kahama juzi, Bakungile alisema aliona atumie nafasi hiyo kumwita Dk Shika Kahama na hiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kwenda wilayani humo.

Baada ya kuulizwa na Mwananchi kwanini alitumia gharama kubwa kumsafirisha kwa ndege Dk Shika huku akijua wazi kwamba Dar es Salaam alishinda mnada na hakuwa na fedha za kulipa, Bakungile alidai kushindwa kulipa kwa fedha za mnada ndilo jambo lililompa umaarufu.

“Najua wazi Dk Shika alishindwa kulipa Sh900 milioni kwenye mnada wa nyumba za Lugumi hivyo katika chuo changu ameahidi kutoa kila mwaka Dola 1 milioni za Marekani (sawa na Sh2.2 bilioni) ambazo akishindwa kuzilipa ataendelea kutangazwa kwamba ameshindwa kulipa hiyo itakuwa fursa ya chuo changu kuendelea kutangazwa,” alisema Bakungile.

Alhamisi iliyopita Dk Shika aliingia mjini Kahama akiwa mgeni mwalikwa wa chuo hicho na baada ya kupewa nafasi ya kuzungumza alitoa ahadi hiyo ya fedha akisema ataziwasilisha baada ya miamala ya kuhamisha fedha zake kutoka Urusi itakapokamilika.

Hata hivyo, baadhi ya watu walisema ‘bilionea’ huyo hapaswi kupewa heshima hiyo na badala yake anapaswa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria kwa kuvuruga mnada.

Kiongozi wa ACT Wazalendo atiwa mbaroni



Misungwi. Wakati upigaji kura katika Kata ya Kijima wilayani Misungwi likiendelea vema, mratibu wa shughuli za kampeni za ACT Wazalendo katika kata hiyo, John Mbozu anashikiliwa polisi kwa tuhuma za kupiga picha eneo la kituo cha kupiga kura bila kibali.

Mbozu ambaye pia ni Katibu wa Mambo ya Nje wa ACT Wazalendo amepelekwa kituo cha Polisi cha Misasi kwa mahojiano zaidi.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Eliud Mwaiteleke amesema hadi kufikia saa 4:00 asubuhi leo Jumapili Novemba 26, hakuna tukio lolote lililoripotiwa kukwamisha upigaji kura zaidi ya hilo la mtu mmoja kukamatwa akipiga picha kituo cha kupiga kura bila kibali maalum kutoka ofisini kwake.

Wakazi wa Kata ya Misasi wanapiga kura leo Jumapili kumchagua diwani kutokana na kifo cha aliyekuwa diwani wa kata hiyo, Kwabi Pandoji (CCM).

Mwananchi:

Mgombea wa Chadema afunguka kilichosababisha akamatwe



Morogoro. Mgombea udiwani kwa tiketi ya Chadema katika Kata ya Sofi wilayani Malinyi mkoani Morogoro, Riko Venance ambaye aliwekwa chini ya ulinzi kwa takribani saa moja amesema polisi walifanya hivyo baada ya kuhoji sababu za mwananchi mmoja kuzuiliwa kupiga kura.

Alizungumza na Mwananchi leo Jumapili baada ya kuachiwa amesema alipofika katika kituo cha kupigia kura cha Shule ya Msingi Mission alipata malalamiko toka kwa mmoja wa wapiga kura aliyejulikana kwa jina moja la Akwilina kwamba amezuiliwa kupiga kura.

“Nilikuwa nahoji kwa nini Akwilina azuiliwe kupiga kura na ndipo nilipoambiwa nasababisha vurugu na kuwekwa chini ya ulinzi," amesema Venance.

Amesema mpiga kura huyo alipoulizwa jina alisema anaitwa Akwilino wakati kwenye kadi imeandikwa Akwilina na hapo ndipo utata ulipoanzia, hata hivyo baadaye aliruhusiwa kupiga kura.

Mgombea huyo ambaye anaendelea kutembelea vituo tayari ameshatembelea vituo 10 kati ya vituo 21 vya kupigia kura vilivyopo katika kata hiyo.