Friday, 13 October 2017

Ndege ya Uturuki yatua Kwa dharula pwani ya kenya

Ndege ya Uturuki yatua kwa ghafla katika uwanja wa ndege wa Moi mjini Mombasa Kenya
Ndege moja ya kampuni ya ndege ya Uturuki Turkish Airlines iliokuwa ikibeba abiria 121 na wafanyikazi sita ilitua kwa dharura nchini Kenya siku ya Ijumaa alfajiri baada ya mojawapo ya injini zake kuingiwa na ndege, kulingana na polisi.
Ndege hiyo aina ya TK673 ilikuwa ikiondoka katika mji huo wa pwani ya Kenya ikielekea Istanbul wakati ndege huyo alipoingia katika injini yake mwendo wa saa 10 alfajiri .
Ilibidi ndege hiyo izunguke katika anga ya mombasa kwa takriban saa moja ili kumaliza mafuta yake kabla ya kutua kwa dharura.
Hakuna mtu aliyejeruhiwa.
Ndege hiyo ilichunguzwa na mafundi kabla ya kuondoka.

Marekani na Israel zajiondoa katika UNESCO

Marekani na Israel zimetangaza kujiondoa kutoka shirika la elimu sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO zikidai Israel inabaguliwa.
Wizara ya mambo ya kigeni ilisema kuwa itabuni ujumbe wa waangalizi kwenye shirika hilo lenye makao yake nchini Ufaransa kuchukua mahala pa uwakilishi wake.
Mkuu wa Unesco Irina Bokova, amesema amesikitishwa lakini hajashangazwa.
Tangu wakati wa kampeni zake Trump alikuwa akitoa matamshi ya kuubeza Umoja wa mataifa na pia kulalamika kwamba Marekani ndio inayochangia fedha nyingi zaidi, hivyo kukariri kwamba atapunguza mchango wake.
Mwaka 2011 Marekani ilifuta bajeti yake kwa Unesco kupinga hatua yake ya kuwapa Wapalestina uanachama kamili.
Marekani hutoa asilimia 22 ya bajeti ya kawaida ya Umoja wa Mataifa na asilimia 28 kwa shughuli za amani za Umoja wa Mataifa.
Unesco iko katika mikakati ya kumteua kiongozi mpya huku mawaziri wa zamani wa Qatari na Ufaransa, Hamad bin Abdulaziz al-Kawari na Audrey Azoulay wakiwa mstari wa mbele katika ushindani huo wa ni nani atachukua mahala pake bi Bokova

ACACIA waendelea kulia na makinikia..wadai yanawatia hasara

Ikitarajia kuchapisha hesabu zake za fedha kwa robo ya tatu ya mwaka, kampuni ya Acacia inaendelea kuugulia maumivu ya zuio la kutosafirisha mchanga wa madini.
Kwenye taarifa yake ya awali iliyotolewa jana kwa wadau wake na jamii kwa ujumla, kampuni hiyo imeeleza kuimarika kwa uzalishaji lakini ikabainisha kupungua kwa mapato kutokana na zuio hilo lililoanza mapema Machi.
“Mauzo yalikuwa madogo kutokana na zuio la kusafirisha makinikia yanayozalishwa kwenye migodi ya Bulyanhulu na Buzwagi nchini Tanzania,” inasema taarifa hiyo fupi.
Machi, Serikali ilizuia usafirishaji wa mchanga wa madini na Rais John Magufuli akaunda kamati mbili za kuchunguza uchimbaji, usafirishaji na biashara nzima ya dhahabu ambazo zilibaini udanganyifu unaofanywa hivyo kulinyima Taifa mapato linayostahili.
Licha ya zuio hilo, Serikali ilifanya mabadiliko kwenye sheria za madini ili kuongeza usimamizi wa uzalishaji, udhibiti wa mapato na ushiriki wa Watanzania katika umiliki wa kampuni zenye vibali vya uchimbaji nchini.
Kwa robo nzima ya mwaka, kampuni hiyo inayomilikiwa na Barrick Gold Corporation kwa asilimia 63.9 imezalisha wakia 191,203 na kuuza wakia 132,787. Pamoja na takwimu hizo, changamoto za upatikanaji wa vibali na kupunguzwa kwa uzalishaji kwenye baadhi ya migodi yake kumeathiri kiasi cha dhahabu iliyopatikana.
Vibali viliathiri uzalishaji wa Mgodi wa North Mara ambao umetoa wakia 72,011 ndani ya miezi mitatu ya Julai, Agosti na Septemba wakati Mgodi wa Bulyanhulu ukizalisha wakia 50,094 kutokana na kupunguza operesheni zake.
“Uzalishaji umezidi matarajio katika Mgodi wa Buzwagi uliochangiwa na ubora dhahabu iliyopatikana. Tulizalisha wakia 69,097,” inasomeka taarifa hiyo.
Kuanzia Julai 31, mazungumzo baina ya Serikali na Barrick yanaendelea kutafuta muafaka wa zuio hilo pamoja na kuongeza faida kwa kila upande. Miongoni mwa yanayojadiliwa kwenye mazungumzo hayo ni faini ya Dola 190 bilioni za Marekani (zaidi ya Sh424 trilioni) ambayo Acacia imeandikiwa na Mamlaka ya Mapato (TRA) ikiwa ni kodi iliyokwepwa pamoja na riba yake.
Tangu kuanza kutekelezwa kwa zuio hilo, bei ya hisa za kampuni hiyo iliyoorodheshwa Soko la Hisa London (LSE) na Dar es Salaam (DSE) imeshuka kutoka Sh12,000 mpaka Sh5,000 kila moja.

Audio | chin beez Ft kaligraph jones _ Kababayee Remix | Mp3 Download

Bovya hapa kudownload.....
https://cloudup.com/files/iJSBNBKQTq0/download

Audio | Lee1 Ft Side kichwa – Sina Raha | Mp3 Downloa

Audio | Lee1 Ft Side kichwa – Sina Raha | Mp3 Download

Bovya hapa kidownload....
https://cloudup.com/files/iXQeCKcdRvn/download

Audio | Chidinma_Live and Die In Africa | mp3 Download

https://cloudup.com/files/iu6P0VNDJ8v/download

Audio | One Six X Jaco Beats _ Wacha Moonbeam | Mp3 Download

https://cloudup.com/files/iFdx2XBiDTs/download

Monday, 9 October 2017