Thursday, 25 January 2018

Vijana waigao tamaduni za wageni wawatia Aibu wa zanzibari


Kamati ya utamaduni  ya wilaya ya  Magharib B wachoshwa na Kadhia ya wanaojitia pamba za masikio kudharau utamaduni wao wa asili na kufuata tamaduni zakigeni wawataka wabadilike venginevyo Serikali ya Wilaya iondoe muhali na hali na kuwatia hatiani.
Hayo yamebainika kufuatia baadhi ya vijana kujiingiza katika dimbwi zito la kuiga tamaduni za kigeni ambapo kilio cha baadhi ya Wananchi wakisema.”Vijana tunakunasihini tukimuona mtu hajavaa nguo rasmin lazima ule mtu tumwite, tumuhoji na ipo haja hata yakufungiwa kuwa asifanye lile jambo kwasababu wanatupotosha mila zetu na silka za kizanzibari”
Nae Katibu mtendaji wa baraza la sanaa Zanzibar Omar Abdallah Adam amewataka wananchi kufuata tamaduni na silka zilizomo nchini.
“Vijana kwakeli wameingia katika dibwi ambalo mi silipendi nami ninawaonea huruma sana kwasababu wao ni nguvu kazi ta Taifa, kwamijibu wa tamaduni zetu Silka zetu na desturi zetu tuwe karibu na wazee wetu kuskiliza wanachokisema na wanachokitaka vile wanavyotufahamisha. Sasa bilisi huyu sijui katokea wapi”
Kwaupande wake Afisa mipango kutoka Magharib B Zawadi Daniel Yussuf Amewasisitiza vijana kuwa makini katika kuendeleza utamaduni wao ili kizazi kijacho kiwe na mwenendo mwema.

Lowassa uso kwa uso na Membe msibani



Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje katika Serikali ya Awamu ya Nne, Bernard Membe wamekutaka katika msiba wa mama wa Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.

Membe na Lowassa wamekutana leo Alhamisi Januari 25,2018 nyumbani kwa Askofu Gwajima, Salasala wilayani Kinondoni.

Wawili hao walijitosa katika kura ya maoni ya CCM kuwania kupitishwa na chama hicho tawala kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Katika mchakato huo jina la Lowassa lilikatwa mapema, huku Membe akiwa miongoni mwa wagombea watano waliopitishwa na Kamati Kuu ya CCM. Walishindwa na John Magufuli aliyepeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi huo na kuibuka na ushindi.

Ruth Basondole, mama mzazi wa Askofu Gwajima amefariki dunia akiwa na miaka 84

LIVE:Takribani Bilion 660 zimetolewa na Serikali kuboresha Jiji la Dar es salaam


Waziri Mwigulu asimamisha zoezi la utoaji wa hati za kusafiria (Passport)

Waziri Mwigulu asimamisha zoezi la utoaji wa hati za kusafiria (Passport

Tundu Lissu afunguka kutolewa risasi nyingine mwilini


Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akifanya mazoezi akiwa hospitalini nchini Ubelgiji. Picha na Maktaba

 Siku 35 baada ya Tundu Lissu kusema mwili wake bado una risasi moja baada ya kutolewa nyingine 15, jana mbunge huyo wa Singida Mashariki (Chadema) amelieleza Mwananchi kuwa madaktari wamemtoa kipande cha risasi kilichokuwa mwilini mwake.

Hata hivyo, mwanasheria huyo mkuu wa Chadema, ambaye alishambuliwa kwa zaidi ya risasi 30 akiwa ndani ya gari lililokuwa nje ya makazi yake mjini Dodoma Septemba 7 mwaka jana, alisema chuma hicho ni tofauti na risasi iliyonayo mwilini, ambayo alielezwa na madaktari wa Hospitali ya Nairobi, Kenya kuwa iko sehemu mbaya, lakini isipotolewa haiwezi kumdhuru.

“Leo (jana) madaktari wamenitoa kipande cha chuma katika sehemu ya makalio ambacho nilipokuwa Nairobi (Kenya) madaktari walikiona lakini kilikuwa ndani ya nyama wakashindwa kukitoa,” alisema Lissu kwa njia ya simu kutoka Ubelgiji ambako alipelekwa Januari 7 kwa ajili ya tiba ya mazoezi.

“Kipande hiki kilisogea na wamekitoa. Ni tofauti na ile risasi ambayo iko mwilini mwangu.”

Akieleza kiundani kuhusu hali yake, Lissu alisema anaendelea vizuri.

“Huu mkono wa kushoto ambao ulikuwa na tatizo, wameunyoosha na kuufanyia mazoezi kweli kweli na huu mguu wa kulia ambao ndio wenye tatizo, unaendelea vyema,” alisema.

“Huku ni mazoezi tu. Kwa siku nafanya mazoezi kwa saa nne, Naingia saa 3:00 asubuhi hadi saa 4:00 asubuhi, narudi tena saa 5:00 asubuhi hadi saa 6:00 mchana. Mwisho naingia mazoezini saa 8:00 mchana hadi saa 10:00 jioni. Hiyo ndiyo ratiba yangu kwa siku.”

Alisema katika mazoezi hayo anatumia magongo maalumu pamoja na kiti cha magurudumu.

“Mfano, huu mguu wa kulia natakiwa kuukanyagia kwa kilo 20 hadi 25 katika mzani na mimi nina kama kilo 90. Ninapoukanyagia ninaulizwa kama unauma, ikiwa sijasikia maumivu ina maana sijafanya kitu, kwa hiyo ni kazi kwelikweli,” alisema.

Kuhusu muda ambao anatakiwa kufanya mazoezi hayo mpaka atakaporejea katika hali yake ya kawaida, Lissu alisema bado hajajua.

“Ah bwana we, hapa madaktari wamegoma kunieleza hilo, lakini wameangalia katika maungio ya goti la mguu wa kulia kuna mfupa haujaunga vizuri, ni lini utaunga hilo sijajua,” alisema.

Mara baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu ambao hadi sasa hawajajulikana, Lissu alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma kwa matibabu ya awali kabla ya kuhamishiwa Hospitali ya Nairobi nchini Kenya siku hiyo usiku.

Desemba 21 mwaka jana wakati akihojiwa na kituo cha televisheni cha Azam, Lissu alisema madaktari wa Nairobi walimueleza kuwa risasi iliyokuwa imesalia mwili haina madhara.

Alisema risasi saba zilitolewa na madaktari hao, jambo lililomaanisha kuwa risasi nyingine nane, zilitolewa na madaktari wa Tanzania, saa chache baada ya kushambuliwa alipofikishwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.   



Dk Kigwangalla kutaja majina wanaotuhumiwa kwa ujangili



Dar es Salaam. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla anatarajiwa kutaja hadharani majina ya watu wanaotuhumiwa kwa ujangili nchini.

Kupitia akaunti yake ya Twitter, Dk Kigwangalla amesema atazungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Januari 25,2018 mjini Dodoma kuelezea mambo yanayohusu wizara hiyo.

“Pia nitaweka hadharani watu mbalimbali wanaotuhumiwa kwa ujangili nchini,” ameandika Dk Kigwangalla.

Amesema tangu alipoteuliwa na Rais John Magufuli Oktoba 7,2017 kushika wadhifa huo, alijua kuna mambo mawili ambayo ni changamoto katika wizara hiyo.

 “Nilipoteuliwa nilijua kuna mawili, kujiunga na mtandao wa uovu ili nifaidike binafsi au kuukataa mtandao huu; nilijua kabisa mshahara wa dhambi ni mauti, na kwamba dhuluma haijawahi shinda vita dhidi ya haki, na wala uongo haujawahi shinda vita dhidi ya ukweli,” ameandika Dk Kigwangalla.

Nafasi za kazi leo Jan 25

Tausi Mdegela afunguka kuolewa Mke wa pili


Msanii wa filamu wa Tanzania mwenye muonekano wa kipekee na kipenzi cha watoto, Tausi Mdegela, ameutaarifu umma kuwa anatarajia kuolewa kuwa mke halali wa mpenzi wake wa siku nyingi ambaye ni msanii wa muziki wa taarabu, Prince Amigo.

Akizungumza na mwandishi wa www.eatv.tv Tausi amesema suala la ndoa ni mipango lakini ni jambo ambalo lipo, kwani tayari wamekuwa kwa muda mrefu kwenye mahusiano na mpenzi wake huyo ambaye ni mwanamuziki wa taarab, ambaye tayari ana mke wa kwanza.

“Ndoa ni mipango mtuombee Mungu tufike mbali, ni muda mrefu tumeanza tunaishi pamoja, ila Amigo ana mke mkubwa, kwa hiyo mimi nasubiria kuwa mke mdogo, hapa akiongezeka watatu ndio itakuwa mtihani, wawili tushatosha wengi wa nini, hapo ndo tutapigana sasa, na tukigundua kuna wa tatu hapo ndio litakuwa lingine, na mke mkubwa kashakubali”, amesema Tausi.

Tausi ameendelea kwa kusema kwamba yeye hajali maneno ya watu wanayosema kuhusu mahusiano yake hayo, kwani anachoangalia ni maisha yake na sio watu wanasema nini.


Daktari wa timu ya Olimpiki ahukumiwa kifungo


Larry Nasser daktari wa zamani wa timu ya Olympiki ya Marekani

Aliyekuwa daktari wa timu ya Olimpiki Larry Nasser amehukumiwa kwenda jela miaka 175 baada ya kukutwa na makosa ya ukatili wa kingono dhidi wananawake na wana michezo.

Katika kesi hiyo mashahidi 160 wamewasilisha ushahidi wao huku Nasser mwenyewe alikiri makosa kumi.

Alikuwa tayari akitumikia kifungo cha miaka 60 kutokana na kukutwa na hatia ya kumiliki picha ngono za watoto kinyume cha sheria.

Jaji Rosemary Aquilina ameiambia mahakama kuwa amejisikia fahari na furaha kubwa kutoa adhabu hiyo kutokana na kitendo alichofanya Nasser na kwamba anataka iwe fundisho kwa wengine.

'Nataka ukae jela maisha yako yote'. Hata hivyo baada ya hukumu hiyo mmoja wa waathirika amesisitiza kuwa washirika wa daktari huyo wanapaswa kushitakiwa pia.

Muda mfupi baada ya kutolewa hukumu hiyo, mkuu wa chuo kikuu cha jimbo la Michigan (MSU) alikokuwa anafanya kazi Nassar kati ya mwaka 1997 na 2016, amejiuzulu.

Bi Simon alikana taarifa kuwa MSU ilifahamu kuhusu tuhuma hizo za unyanyasaji lakini kilishindwa kuchukua hatua.

Katika taarifa yake alisema: "kwa waathiriwa, samahani yangu haiwezi kutosha, kuwa daktari aliyeaminika, aliyefahamika alikuwa ni mtu muovu kwa kweli, aliyewadhulumu kwa kutumia kigezo cha kuwatibu."

"Ushahidi wa wahanga wa unayanyasaji wa Nassar ni wa kusikitisha, kuvunja moyo na binafsi unaonitia kichefu chefu," aliongeza.

Takriban wasichana 140 wamewasilisha kesi dhidi ya Nassar, taasisi ya USA Gymnastics na chuo kikuu cha MSU, wakidai kuwa taasisi hizo mbili zilipokea tuhuma za unyanyasaji wa kingono dhidi ya daktarihuyo miaka kadhaa ya nyuma.

Taasisi hiyo ya michezo na chuo hicho zimekana kuwa kulikuwa na chochote cha kufichwa.

Hukumu ya Larry Naser inafuatia wiki ya ushuhuda kutoka kwa wanawake takribani mia moja na sitini, wakiwemo washindi wa medali ya dhahabu ya olympiki Biles, Aly Raisman, Gabby Douglas na McKayla Maroney

Arsene Wenger afunguka kuhusu Sanchez


Meneja wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amesema kwa sasa mambo ya usajili wa Alexis Sanchez yameshapita ndani ya timu hiyo.

Sanchez amekamilisha dili lake la kujiunga na Manchester United huku likimuhusisha Henrikh Mkhitaryan kuhamia Emirates mwanzoni mwa wiki hii.

Kufuatia ushindi dhidi ya Chelsea katika michuano ya Carabao Cup hapo jana siku ya Jumatano Wenger akizungumza na vyombo vya habari juu ya uhamisho wa Sanchez amesema kuwa “Tumepoteza mchezaji bora lakini kama timu kunahaja ya kuendelea nayale muhimu ili kutopoteza muelekeo wetu,” amesema Wenger.

“Kwa sasa tunafahamu tunapaswa kuendelea mbele sote kwa pamoja kujipatia muda.”

Kikosi cha Wenger kimefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya michuano ya Carabao Cup na kutarajiwa kucheza na Manchester City baada ya kuifunga timu ya Chelsea hatua ya nusu fainali.


Mwalimu afikishwa Mahakamani baada ya kumuua mtoto wake kwa panga



 Mwalimu wa sekondari Stephen Wachira Wangara mwenye umri wa miaka 43, amefikishwa Mahakamani kwa kosa la kumuua mtoto wake wa miezi 7 kwa kumchinja na panga nchini Kenya.

 Mashahidi watano wa tukio hilo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Jimbo la Kirinyaga, Maina Muriuki wamemweleza Jaji Lucy Gitari wa Mahakama Kuu ya Kerugoya, jinsi mtuhumiwa alivyoua mtoto wake,

Maina ameieleza Mahakama kuwa mwili wa mtoto huyo ulikuwa umewekwa ndani ya gunia ukiwa na damu, nje ya nyumba ya Wangara na pembeni ya mwili huo kuliwa na panga ambalo lilitumiwa kumuua mtoto huyo.

Shahidi mwingine Joseph Muriithi amesema wakati wa tukio hilo alikuwa shambani kwa Wangara akifanya kibarua na alimwona mtuhumiwa akiwa na madoa ya damu na muda mfupi baadaye alisikia kelele kutoka kwenye nyumba ya mwalimu huyo.

Mahakama imeahirisha kesi hiyo hadi March 1, 2018, ambapo itasikilizwa tena.

Wangara ambaye ni mtuhumiwa ni baba mwenye watoto wawili na mwalimu katika shule ya Sekondari ya Gituya

Wanaohusika na uteswaji wa Vijana kukamatwa


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt Mwigulu Nchemba ameagiza kutafutwa na kukamatwa mara moja kwa watu wote wanaohusika na uteswaji wa vijana wanaopelekwa nje ya nchi kutafuta ajira.

Dkt. Mwigulu amesema hayo leo wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari baada ya kupata taarifa ya mateso wanayopata baadhi ya wananchi wa Tanzania wanaokwenda kufanya kazi tofauti tofauti nje ya nchi na kusema wameshafanya mawasiliano na Wizara zote zinazohusika na wameshakubaliana kila mmoja kuchukua hatua kulingana na wizara yake.

"Wale watu wanaoweka rehani vijana wetu, wamekuwa wakikimbia hapa na pale na ambao bado hawajakamatwa mpaka sasa waendelee kusakwa wote na wafikishwe katika mkono wa sheria ili sheria iweze kufuata mkondo wake kwa vitendo hivyo vya kinyama na kuwapeleka vijana wetu katika vitendo vya kinyama na kusababisha majonzi kwa familia husika",alisema Dkt. Mwigulu.

Pamoja na hayo na Waziri Nchemba amesema matatizo wanayoyapata vijana hao kwa kisingizio cha kupatiwa kazi nje ya nchi mpaka sasa yamekuwa makubwa mno.

"Tumeona vijana wakiwa wamefungwa miguu vichwa chini na mikono yote huku wakitandikwa viboko kwa madai ya kwamba miongoni mwao kuna aliyewapeleka kuwapa kazi nzuri ya kufanya lakini kwa bahati mbaya wakifika huko wanawekwa rehani kwamba hawataondolewa pale walipo mpaka wale waliowapeleka wakiwa wameshamaliza kupeleka fedha za dawa za kulevya", alisisitiza Waziri Mwigulu Nchemba.

Rais wa Simba Fc alazwa Muhimbili


MWENDESHA Mashtaka Mwandamizi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa ,(Takukuru) , Leonard Swai ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva amelazwa Hospital ya Taifa ya Muhimbili akisumbuliwa na Figo.

Aveva ambaye ni mshtakiwa wa kwanza mshtakiwa mwingine katika kesi ya uhujumu uchumi anashtakiwa pamoja na Makamu rais wa klabu ya Simba, Godfrey Nyange 'Kaburu' ambaye alikuwepo mahakamani hapo

Wakili Swai amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Amedai, walishachukua maelezo ya mshtakiwa wa pili na kwamba wanaangalia jinsi ya kupata maelezo ya mshtakiwa wa kwanza ambaye kwa sasa ni mgonjwa.Baada ya kueleza hayo Hakimu Nongwa ameaihirisha kesi hiyo hadi February 8,2018 kwaajili ya kutajwa.

Aveva na Kaburu wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha Dola za kimarekani 300,000.