Thursday, 25 January 2018

Rais wa Simba Fc alazwa Muhimbili


MWENDESHA Mashtaka Mwandamizi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa ,(Takukuru) , Leonard Swai ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva amelazwa Hospital ya Taifa ya Muhimbili akisumbuliwa na Figo.

Aveva ambaye ni mshtakiwa wa kwanza mshtakiwa mwingine katika kesi ya uhujumu uchumi anashtakiwa pamoja na Makamu rais wa klabu ya Simba, Godfrey Nyange 'Kaburu' ambaye alikuwepo mahakamani hapo

Wakili Swai amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Amedai, walishachukua maelezo ya mshtakiwa wa pili na kwamba wanaangalia jinsi ya kupata maelezo ya mshtakiwa wa kwanza ambaye kwa sasa ni mgonjwa.Baada ya kueleza hayo Hakimu Nongwa ameaihirisha kesi hiyo hadi February 8,2018 kwaajili ya kutajwa.

Aveva na Kaburu wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha Dola za kimarekani 300,000.


Mwanafunzi atuhumiwa kwa kumnyonga mpenzi wake Gesti




Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) aliyetambulika kwa jina la Mwita Marwa kwenye miaka (30) anatuhumiwa kufanya mauaji kwa kumnyonga mpaka kufa mpenzi wake Kibua Adam (39) mkoani Morogoro.

Akiongea na www.eatv.tv Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mpaka sasa jeshi la polisi linaendelea kumtafuta mtuhumiwa.

"Mpaka sasa zipo tetesi tu za hapa na pale hatuwezi kujua sababu kubwa iliyopelekea kijana huyo kufanya jambo hilo, kwani yeye alimchukua huyo mwanamke akampeleka guest na kunyonga huko mpaka akafa" alisema Matei

Kamanda Matei anadai jeshi la polisi walipopata taarifa za kunyongwa mwanamke huyo alifika katika guest hiyo na kuukuta mwili wa mwanamke huyo na kuondoka nao, lakini mpaka sasa mwanafunzi ambaye anatuhumiwa kufanya mauaji hayo hajapatikana na jeshi la polisi linaendelea kumtafuta.

Sugu, mwenzake wamkataa hakimu wakidai hawana imani naye


Mbunge wa Mbeya Mjini 'Sugu' na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga wamemkataa Hakimu Mkazi Mfawidhi, Michael Mteite wakidai hawana imani naye katika mwenendo wa kesi hiyo.

Sugu na Masonga wanashtakiwa kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli wanayodaiwa kuitoa Desemba 30,2017.

Washtakiwa leo Alhamisi Januari 25,2018 asubuhi wamefika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya kwa ajili ya kuanza kutoa ushahidi baada ya upande wa Jamhuri kukamilisha na kufunga ushahidi wao.

Upande wa Jamhuri umewasilisha mashahidi watano mahakamani na vielelezo viwili ikiwamo sauti iliyorekodiwa.

Baada ya utaratibu wa kimahakama kukamilika ili kuanza ushahidi, wakili Boniface Mwabukusi anayewawakilisha Sugu na Masonga alimuomba hakimu Mteite akisema wateja wake wana jambo la kuieleza Mahakama.

Hakimu alipowaruhusu kuzungumza, Sugu ambaye ni mshtakiwa wa kwanza katika kesi hiyo, amesema kutoka ndani ya nafsi yake ameitafakari kesi na mwenendo wake na kufikia uamuzi wa kumkataa hakimu kwa kuwa hana imani naye kwa sababu tatu.

Amesema, “Naomba niitaarifu Mahakama hii kwamba nimetafakari mwenendo wa kesi hii, mimi mshtakiwa wa kwanza Joseph Mbilinyi naona nikukatae wewe hakimu kutokana na mambo yafuatayo: kwanza; sijawahi kuona hakimu yuko biased (wenye upendeleo) kama ulivyo wewe, ulivyoninyima dhamana bila sababu za kisheria na Katiba.”

“Pili, jana nimeshuhudia kielelezo cha tape recorder kikitokea mikononi mwa wakili wa serikali ambacho wakili wangu (Mwabukusi) alikikana na ukamshambulia sana wakili wangu kwamba wakati anakitoa yeye (wakili) alikuwa ametoka wakati mimi nilikuwa hapa sikuona. Sasa kitendo kile naona wewe hakimu una interest (masilahi) dhidi yangu,” amesema.

Sugu amesema, “Lakini pia jana ulikiri kwamba katika kesi hii unapata mateso, hivyo mimi ni Mkristo, sasa ili nisikupe tabu na mateso naomba nikukatae na apangiwe hakimu mwingine atakayeendesha kesi hii kwa uhuru na haki.”

Amesema kwa sababu hizo anaomba amkatae hakimu huyo.

Baada ya ombi hilo la Sugu, hakimu Mteite alimpa nafasi Masonga ambaye pia alimkataa akitoa msimamo unaofanana na wa Sugu.

Katika sababu zake, Masonga amesema, “Mheshimiwa jana ulipotoa uamuzi wa kupokea vielelezo kutoka kwa upande wa Jamhuri, wa tape recorder na register mheshimiwa hakimu ulieleza Mahakama yako kwamba unaruhusiwa kisheria wakati upande wa Jamhuri ulikubali ushahidi upokewe kama Id (utambulisho) lakini register ipokewe kama  kidhibiti. Lakini bado uamuzi wako ulikuja tofauti na upande wa Jamhuri.”

Amesema, “Ulipofanya uamuzi wakati tulipokuomba dhamana, ulisema unakubaliana na hoja za pande zote mbili (utetezi na Jamhuri). Na Jamhuri walisema kwa ajili ya usalama wetu (washtakiwa), wanaomba tusipewe dhamana. Na wewe katika uamuzi wako umezingatia hoja zao lakini umezingatia zetu kwa sababu ni haki yetu kisheria na kikatiba. Na uamuzi wako ulisema unazuia dhamana kwa sababu unataka kesi hii iendee haraka, bila kujadili hoja zilizoletwa mbele yako.”

Hakimu Mteite amesema amezingatia hoja hizo na atatoa uamuzi baada ya saa moja.

KIVURUGE WA TANDALE -01



SAA saba na dakika zake mchana, tumbo la Ashrafu lilikuwa likiunguruma kwa kusakamwa na njaa kali, aliamua kutoka ofisini kwao ndani ya Jengo la Al- Haramain, Mtaa wa Shaurimoyo jijini Dar na kuamua kushuka kwa kuzikanyaga ngazi moja baada ya nyingine.

Kazi yake ya ufundi wa kompyuta na vifaa vya kielektroniki ilimfanya kuwa kijana maarufu sana na hii ilitokana na uwezo mkubwa aliokuwa nao kwenye kazi yake kiasi cha makampuni mengi kugombea kumwajiri lakini mwenyewe akawa hataki. Kwake aliona ni bora ajiajiri lakini kama kuna kampuni inahitaji huduma yake, inamfuata na wanafikia makubaliano kisha kazi inafanyika.

Baada ya kushuka ngazi kwa tabu hatimaye alijisogeza taratibu hadi mgahawani ambapo palijulikana kwa jina maarufu la Kwa Makofia. Hapo alikutana na umati mkubwa hivyo kushindwa kabisa kuagiza chakula alichokuwa akihitaji hivyo aliamua kuhamia kwenye mgahawa wa jirani yake, kabla hajachukua uamuzi wa kuondoka Kwa Makofia, macho yake yalikutana na kitu kilichomfanya ashtuke kidogo.

Mrembo matata mwenye mvuto wa kipekee, mweupe aliyepanda juu, mwenye macho kama anasikia usingizi, alikuwa amekaa kama anayesubiria huduma! “Dah, huyu ni mtu wa kawaida au ni malaika ameshuka kupunga upepo duniani?” Ashrafu alijikuta akiropoka ingawa ni kwa sauti ndogo na ya chini kabisa na hakuna aliyemsikia hata kwa herufi moja. “Nafanyaje jamani kuhusu huyu msichana mzuri hivi?

Naanzaje kumuacha tena amekaa mwenyewe katika mazingira kama haya? Sasa sijui yuko na mwenzake na ametoka kidogo tu au yuko mwenyewe na mbona leo nimekosa kabisa ujasiri ambao nimekuwa nao kwa siku zote?” Ashrafu alijiwazia moyoni huku akiondoka eneo hilo na kujisogeza kwenye mgahawa wa jirani na hapo. Alifika na kuagiza chakula ambapo alichagua moja ya viti vilivyokuwemo ndani na kukaa huku mawazo yake yakibaki kwa msichana aliyekutana naye pale Kwa Makofia.

Katika hali ya kushangaza, wakati anawaza juu ya mwanamke huyo, alishangaa kumuona msichana yule akiingia mgahawani hapo na kukaa kwenye moja ya viti na kisha kuagiza chakula.

Ni hapo ndipo Ashrafu alishindwa kuvumilia na kuamua kutumia ujasiri wake wa asili ambao humuwezesha kumvaa mtu yeyote kwa wakati wowote na kumwambia chochote kwa mazingira yoyote. “Dada, samahani kidogo,” Ashrafu aliita kwa nidhamu zote na kuonesha heshima ambayo hata yeye mwenyewe aliishangaa imetoka wapi. “Mimi…?” Msichana wa watu aliitika kwa mshangao na macho ya kuuliza kama ni yeye aliyekuwa akiitwa. “Yeah…” Ashrafu aliitikia na kumpa ishara ya mkono msichana yule ambaye alionesha kusita… akatingisha bega lake kuonesha kukataa wito wake. “Samahani nakuomba au ni vibaya kukuita? Kataa neno usikatae wito,” Ashrafu alichombeza.
“Samahani kaka! Samahani lakini, mimi kwa watu ambao siwafahamu siwezi hata kuwasogelea…” alisema yule msichana na kuagiza chakula. Ashrafu alishusha pumzi chini…lile tumbo lake lililokuwa likiunguruma safari hii aliona limezidi mara mbili yake. “Hata mimi nikuombe samahani! Naomba nikae hapo karibu na wewe!” Ashrafu alirusha karata nyingine tena huku akimtolea jicho la aibu. Yule msichana alikubaliana na Ashrafu, ilikuwa furaha kubwa kwake kama siyo ushindi kutokana na mazungumzo ambayo alipanga kuyaendesha kwa muda ambao watakuwa wanasubiri chakula, aliamini kabisa hadi zoezi la kula linamalizika, atakuwa ameshaibuka kidedea. “Siwezi kumkosa huyu mtoto, kwanza anaonekana laini na mwepesi kama maharage ya Mbeya,” Ashrafu aliwaza huku akimtazama usoni msichana yule. “Samahani tena kwa usumbufu…” “Bila samahani kaka…” “Naitwa Ashrafu kwa kirefu, sijui wewe mrembo unaitwa nani?” “Kwa nini unaniita mrembo jamani?” Aliuliza yule msichana huku akijiangalia kiunoni hadi miguuni. “Si kama hivi ulivyo mzuri na mrembo au huoni?” “Aaah, kawaida bwana na huwa sipendi kabisa mtu akiniita mrembo…” “Okey, samahani kwa hilo.”
“Wala usijali. “Unaitwa nani?” “Naitwa Nancy, ni mwenyeji wa Morogoro eneo la Kilombero.” Ashrafu aliendelea kumtolea macho na masikio akiwa haamini kama maneno yale yanatoka kwa yule msichana. “Mi mwenyewe mkazi wa Morogoro!” “Weee! Sehemu gani?” Nancy alishangaa, alionekana kubadilika sura na kuwa ya tabasamu mara baada ya kuambiwa kuwa wanatoka mkoa mmoja kumbe ulikuwa uongo wa Ashrafu ili kumnasa. “Mi natokea Morogoro mjini kabisa eneo moja hivi linaitwa Kihonda, unapajua?”

“Ndiyo, sasa mara nyingi huwa nafikia kwa Shangazi sehemu moja inaitwa Mji Mpya nakaa siku mbili tatu ndiyo naelekea Kilombero.” Wakati wanaendelea na mazungumzo ya kufahamiana, mhudumu alileta vyakula kulingana na maagizo ya kila mmoja wao, ambapo kwa pamoja waliamua kutumia meza moja kula. “Hujaniambia lakini kuhusu kazi yako,” Nancy alianza kuchokoza. “Ah, mi mzugaji tu mjini hapa, nabangaiza ilimradi siku ziende. Nakaa mtaa wa tatu kutoka hapa,” Ashrafu alidanganya kwa mara nyingine hali iliyomfanya Nancy ashtuke. “Mh! Hongera, kama kweli unafanya kazi hizo na unaonekana mtanashati hivyo!”

“Asante sana na wewe je?” “Mimi nafanya kazi katika kampuni ya kuuza vifaa vya solar kutoka China, pale karibu na ‘round about’ alimuelekeza Ashrafu kwa kumnyooshea mkono. “Naishi Mikocheni, niko mwenyewe na maisha yanasonga kwa kweli,” alisema Nancy huku akimtazama Ashrafu kwa macho yaliyojaa aibu za kikekike. Kwa ilivyoonesha, Nancy alikuwa mzungumzaji sana maana ndani ya muda mfupi tu, alishayatawala mazungumzo na mbinu kali alizozitumia Ashrafu, zilimfanya ajikute akimzoea haraka utafikiri wamefahamiana miaka kadhaa iliyopita. Walimaliza kula. Nancy akamwambia alikuwa na safari ya kuelekea Posta kufuatilia hundi ya malipo kwenye kampuni moja waliyofanya nayo biashara.

“Okey, basi nakuomba tubadilishane mawasiliano ili tuendelee kuwa karibu zaidi,” Ashrafu alitupa ndoano kimtego kwa Nancy. “Namba za simu tena? Hapana huwa sitoi namba za simu, utanisamehe kwa hilo,” Nancy alisema huku akiinuka, akachukua mkoba wake mdogo na kuanza kutembea kimadaha, akaenda mpaka kaunta na kulipa bili yake, akamgeukia Ashrafu ambaye bado alikuwa amekaa palepale akiendelea kuusifu uumbaji wa Maulana kwa kiumbe yule. Alimpungia mkono kichokozi huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wake, akatoka zake na kumuacha Ashrafu akiwa bado ameganda palepale kama barafu.


“Ndege mjanja hunasa kwenye tundu bovu,” alijisemea huku tabasamu hafifu likichanua kwenye uso wake, akashusha pumzi ndefu na kuinuka kuelekea kaunta kulipa. Je, nini kitafuata? Usikose kufuatilia kwenye Gazeti la Risasi Mchanganyiko siku ya Jumatano. KUTOKA KWA MWANDISHI: Nimeamua kusitisha simulizi ya Bosi wa Kibamia iliyoanza Jumatano iliyopita kweye Gazeti la Risasi Mchanganyiko, hii ni kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wangu. Poleni kwa usumbufu wasomaji wangu na sasa tuungane kwenye simulizi hii mpya itakayokuacha na funzo kubwa la maisha.

Instrumental | Olamide – Science Student (BEAT) | Mp3 Download

Instrumental | Olamide – Science Student (BEAT) | Mp3 Download

Instrumental | Olamide – Science Student (BEAT) | Mp3 Download

DOWNLOAD INSTRUMENTAL

Audio | Mr Paul ft. Sharon Searle – Turn Me On | Mp3 Downlaod

Audio | Mr Paul ft. Sharon Searle – Turn Me On | Mp3 Downlaod

Audio | Mr Paul ft. Sharon Searle – Turn Me On | Mp3 Downlaod

DOWNLOAD Mp3

New VIDEO: Stella Mwangi – KUCHIZI

New VIDEO: Stella Mwangi – KUCHIZI
New VIDEO: Stella Mwangi – KUCHIZI

Iyobo azungumzia ishu ya Aunt kumnyima penzi




DANSA maarufu Bongo, Moses Iyobo, amesema kuwa kuandika kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram kuwa amenyimwa penzi na mzazi mwenzie Aunt Ezekiel hajaona kama kuna tatizo ingawa aliandika kama utani.

Akizungumza na gazeti hili, Iyobo alisema kuwa yeye na Aunt ni watu ambao wanataniana sana japokuwa tayari ni wazazi kwa hiyo hata alipoandika juzikati Instagram, alikuwa kwenye kuendeleza utani japo mashabiki wao wameipokea vibaya.

“Unajua watu wanashindwa kuelewa lakini mimi na mama Cookie (Aunt) tunataniana sana kwa hiyo hata kuandika vile ni kumtania tu sasa watu hawakuelewa naona wametoa povu kweli,” alisema Iyobo.

Iyobo alikomenti kwenye video aliyoposti Aunt ikimuonesha akitembea akisindikiza na ujumbe wa neno ‘fresh’:

“Umeninyima penzi halafu uposti fresh?” alikomenti Iyobo.

Chuchu afunguka ishu ya kumtoboa sikio mtoto wake



MUIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Chuchu Hans amefungukia madai ya kumtoboa sikio mtoto wao wa kiume Jaden mwenye umri wa mwaka mmoja akidai kuwa suala hilo limepokelewa ndivyo sivyo.

Akizungumza na gazeti la Global publishers, Chuchu alisema kuwa hakumtoboa kabisa sikio bali baba yake (muigizaji Vincent Kigosi ‘Ray’) ndiye aliyemvalisha kihereni cha kubandika na siyo kumtoboa moja kwa moja.

“Watu hawajatuelewa jamani hatuwezi kumtoboa sikio mtoto kwenye umri alionao tena wa kiume bali baba yake alimvalisha hereni ya kubandika tu, wasituzungumzie vibaya bwana,” alisema Chuchu.




Kadja Nito kwenye bifu zito na Mama yake


MREMBO wa Bongo Fleva, Natasha Lisimo ‘Kadja Nito’ ambaye aliingia kwenye bifu zito na mama yake baada ya kubadili dini na kuwa Mkristo na kumsamehe kipindi alipokuwa mahututi akijifungua, amemtibua tena mzazi wake huyo kutokana na kukomaa kwenye dini hiyo.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, kitendo cha mama yake Kadja kumsamehe alipokuwa mahututi leba, aliamini baada ya kurejea kwenye hali yake ya kawaida huenda angemtii na kurudi kwenye Uislamu lakini ndiyo kwanza, dini ya Kikristo imemkolea na sasa anajianika waziwazi hadi mitandaoni, jambo linalomchefua mzazi wake huyo.

Kutokana na ishu hiyo Kadja alipoulizwa alisema; “Kuna vitu sipendi kuviongelea sana kwa sasa, hususan mambo yangu na mama yangu ni masuala ya kifamilia, kama mnaona najianika kwenye Ukristo na nilibadili dini nikawa huko, sioni kama kuna haja ya kuzungumzia hilo kwa kina.


Watumishi wa Idara ya Uhamiaji wapewa siku tatu kuhama mjini



o

IDARA ya Uhamiaji katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imetoa siku tatu kwa watumishi wake walioripoti Dodoma kuhamia katika nyumba zake zilizopo eneo la Iyumbu, nje kidogo ya Manispaa ya Dodoma, badala ya kung’ang’ania kuishi katikati ya mji.

Nyumba hizo 63 zenye thamani ya Sh. bilioni 3.8 zimekabidhiwa jana kwa Idara hiyo na Shirika la Nyumba (NHC).

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Kamishna wa Fedha wa Idara hiyo, Peter Chogero, kwa niaba ya Kamshina Mkuu alisema serikali imeshanunua nyumba kwa ajili ya watumishi hao hivyo hakuna sababu ya wao kuendelea kuishi katikati ya mji wa Dodoma.

“Uhamiaji imenunua nyumba 63 eneo la Iyumbu ambazo zimejengwa na NHC, tutashangaa kuona watumishi wengine waendelee kuishi mjini wakati nyumba zao zipo hapa Iyumbu,” alisema.

Alitoa siku tatu kuanzia jana kila mtumishi aliyepangwa kuhamia kwenye nyumba hizo awe ameingia kwa kuwa hakuna sababu ya kung’ang’ania kuishi nje ya nyumba hizo wakati zimelipiwa na serikali.

Chongero alisema kabla ya manunuzi ya nyumba hizo, Idara hiyo ilikuwa na nyumba 10 mjini Dodoma ambazo hazikuweza kutosheleza watumishi wote, ikiwamo waliohamia kutoka Makao Makuu Dar es Salaam.

Alibainisha waliamua kuongeza idadi ya nyumba ili kila mtumishi wa Uhamiaji aishi kwenye nyumba ya serikali na kwamba wanatarajia kuongeza nyingine 40.

Naye, Meneja Masoko wa NHC, Itandula Gambalagi alisema ujenzi wa nyumba za Uhamiaji ulianza Desemba, 2016 katika eneo lenye ukubwa wa ekari 234 na ni moja ya sehemu ya mji uliopangiliwa kitaalamu kwa kuzingatia sheria na kanuni za mipango miji.

Alisema nyumba zilizokabidhiwa Uhamiaji ni sehemu ya nyumba 150 zilizojengwa katika mradi wa Iyumbu na tayari nyumba zilizobaki zote zimepata wanunuzi.

Gambalagi alisema nyumba hizo zina miundombinu yote inayotakiwa.

Kwa upande wake, mthamini wa mali za serikali, Joseph Maliti aliagiza Uhamiaji kuingiza nyumba hizo katika daftari la mali za serikali mara moja, ikiwa ni pamoja na thamani kwa kila nyumba.

Maduka 95 ya kubadilisha Fedha yasitisha Biashara


MADUKA 95 kati ya 297 ya kubadilishia fedha yaliyokuwepo nchini kufikia katikati ya mwaka jana, yamesitisha biashara katika zoezi la uandikishwaji na utoaji upya wa leseni.

Kwa mujibu wa taarifa ya ufafanuzi kwa Nipashe iliyotolewa na Mkurugenzi wa Uzimamizi wa Mabenki wa Benki Kuu (BoT), Kened Nyoni, maduka 64 hayakuomba leseni kama ilivyotakiwa kisheria Juni, mwaka jana.

Kwa mujibu wa ufafanuzi huo wa juzi, maduka 233 yaliwasilisha nyaraka muhimu kwa ajili ya maombi ya leseni na 64 yaliruhusiwa kuendelea na biashara, huku 31 yakiamua kufunga, na 138 BoT inafanya mapitio ya taarifa zake.

"Kati ya maduka 297 yaliyotakiwa kuomba upya leseni zao, maduka 64 hayakuwasilisha nyaraka yoyote... baada ya kupitia nyaraka za maduka 233, maduka 31 yaliamua kufunga biashara," alibainisha.

Taarifa ya BoT Juni, mwaka jana, ilionyesha kuwa maduka hayo yamepewa miezi mitatu kukamilisha usajili mpya kwa lengo la kuboresha usimamizi na kuweka mfumo wa kisasa utakaoleta tija katika mabadiliko ya uchumi.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, BoT iliongeza mtaji wa maduka hayo kutoka Sh. milioni 100 hadi Sh. milioni 300 kwa yale ya daraja A.

Aidha, BoT ilipandisha mtaji kutoka Sh. milioni 250 hadi Sh. bilioni moja kwa maduka ya daraja B na kuongeza amana zisizo na faida kutoka dola za Marekani 50,000 hadi 100,000 (sawa na Sh. milioni 112 hadi Sh. milioni 224).

Aidha, Benki Kuu katika masharti yake kwa biashara hiyo ya kubadilisha fedha za kigeni ilizuia wenye hisa, wakurugenzi, mmoja wa mameneja au mfanyakazi kuwa kwenye duka zaidi ya moja.

Maduka yote yalitakiwa kufunga kamera maalum za ulinzi za CCTV, masharti hayo yalitaka, "ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua zote muhimu za ulinzi na usalama kama zilivyoanishwa kwenye kanuni za mwaka 2015".

Aidha, wamiliki wa maduka hayo kwenye usajili wanatakiwa kutoa taarifa zao binafsi, ikiwamo chanzo cha mapato yaliyowezesha kuwepo kwa duka husika, na kueleza kwa undani kila kilichojazwa kwenye fomu mahali kilipo kwa kuwa kitafuatiliwa kwa kina.

Nyoni alisema Januari 2, mwaka huu, BoT ilitoa notisi kwa wafanyabiashara ambao hawajakamilisha nyaraka za usajili na walioshindwa kufikia vigezo vilivyotakiwa.

"Kwa kuzingatia kuwa maombi mengine yaliletwa dakika za mwisho (kelekea Desemba 31, mwaka jana), tumeongeza siku 30 kwa ajili ya mapitio kwa ambao hawakuwa wamekamilisha nyaraka za mwisho wafanye hivyo kuruhusu leseni kutolewa Januari 31, mwaka huu," alifafanua.

Alisema kwa kipindi cha kusubiri leseni maduka yaliyo kwenye utaratibu wa kupata leseni yanaruhusiwa kuendelea na kazi za kila siku.

MWAKA 1992Maduka ya kubadilishia fedha za kigeni yana historia fupi nchini kutokana na kuanzishwa na Sheria ya Fedha za Kigeni ya mwaka 1992 ambayo inampa Gavana wa BoT mamlaka ya kuanzisha maduka ya kuuza na kununua fedha za kigeni na pia mamlaka ya kutunga kanuni, taratibu, miongozo na maelekezo ya kusimamia maduka hayo.

Kanuni za kwanza zilitungwa na Gavana mwaka 1999, lakini kwa kuwa maduka hayo hayakuwa mengi hakukuwa na masharti magumu mpaka mabadiliko ya kanuni ya mwaka 2015 ambayo yalichangiwa pamoja na mengine, serikali kutambulisha mfumo mpya wa ukusanyaji kodi kwa kupitia mashine za kodi za kielektroniki (EFD).

Ndipo likaja tangazo la Juni 30, mwaka jana kwenye gazeti la serikali ambalo lilitata mchakato huo wa usajili upya kumalizika Septemba kabla ya kuongezwa muda mara mbili mpaka Januari 31, mwaka huu.

Habari zinadai masharti mapya ya Serikali yanatokana na BoT, kwa kushirikiana na vyombo vingine, kubaini maduka mengi yalikuwa yanaficha mitaji halisi.

Imeelezwa vitabu vya mahesabu vya maduka mengi vilionyesha mitaji ambayo siyo halisi, na baadhi kudai kupata hasara kila mwaka.

Mzee Majuto amelazwa Muhimbili



Mchekeshaji Amri Athuman aka Mzee Majuto Jumatano hii amelazwa katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar es saalam kwa mujibu wa taarifa ya Afisa Habari wa Chama Cha Waigizaji Mkoa wa Kinondoni.

Akiongea na Bongo5 Alhamisi hii Asifa Habari huyo, Masoud kaftany, amesema muigizaji huyo alipelekwa hospitali hapo siku ya jana baada ya kuzidiwa.

“Ni kweli Mzee Majuto anaumwa na sasa hivi tupo naye hapa Muhimbili anaendelea na matibabu,” alisema Masoud kaftany. Kusema anaumwa nini ni mapema zaidi lakini baadae tutatoa taarifa rasmi baada ya kupokea taarifa ya madaktari,”

Afisa huyo amekiomba Chama cha Waigizaji, wadau wa filamu Tanzania na wa Tanzania wote wamuombee muigizaji aweze kupona haraka

Source: Bongo 5