Tanzania\'s leading online News Edition (The National Newspaper). Get access to the most current and latest authoritative news on local issues, politics, events, celebrations, editorial, columnists, features, people and business.
Wednesday, 25 October 2017
Tuesday, 24 October 2017
Kenya: Watu 3 waenda mahakamani kusitisha uchaguzi
Mahakama ya juu nchini Kenya itatoa uamuzi wa muda wa mwisho kuamua iwapo marejeleo ya uchaguzi wa urais yanaweza kufanyika siku ya Alhamisi.
Mahakama hiyo itasikiza ombi la dharura siku ya Jumatano kuhakikisha kuwa uchaguzi huo unafutiliwa mbali siku moja kablka ya kufanyika kwa uchaguzi huo.
Hatua hiyo inajiri baada bya mahakama hiyo kufanya uamuzi wa kihistoria ilipofutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa urais na kutaka uchaguzi huo kurejelewa.
Sasa inatakiwa kuingilia kati kwa mara nynegine na itaamua , ikiwa imesalia chini ya saa 24 kabla ya uchgauzi huo kufanyika kuhusu iwapo uchaguzoi huo unafaa kuendelea.
Kuna utata kati ya sheria za uchaguzi, katiba na vile mahakama ilivyofafanua sheria hizo.
Kiongozi mkuu wa upinzani Raila Odinga ametumia mojawapo ya uamuzi wa mahakama kujiondoa katika uchaguzi huo akiutaja kuwa usio huru na haki na hautatoa maono ya Wakenya.
Rais aliyepo sasa Uhuru Kenyatta amesema kuwa uchaguzi huo ni sharti ufanyike, huku akiwa na muswada wa uchaguzi katika meza yake unaotarajiwa kutiwa saini
Mahakama ya juu imekubali kusikiliza ombi hilo la muda wa lala salama ambalo linahoji iwapo tume ya uchaguzi na mwenyekiti wake wataweza kufanya uchaguzi ulio huru na haki siku ya Alhamisi.
Inataka uchaguzi huo kubadilishwa na uchaguzi mpya hatua ambayo huenda ikaongeza muda wa uchaguzi huo kwa kipindi cha mwezi mmoja .
Wapiga kura watatu wameelekea katika mahakama ya juu wakitaka kusimamisha uchaguzi huo wa Alhamisi.
Bwana Khalef Khalifa , Samuel Mohochi na Gacheke Gachuhi wanadai kwamba tume ya uchaguzi imegawanyika na haiwezi kufanya uchaguzi ulio huru na haki.
Wanadai kwamba makamishna wa IEBC wanahudumu kwa upendeleo na mwenyekiti wa tume hiyo Wafula Chebukati amekiri hadharani kwamba hawezi kusimamia uchaguzi ulio huru na wa haki.
Walalamishi hao watatu ,wanaowakilishwa na Harun Ndubi pia wanataka mahakama kuamua kuhusu hatua ya Raila Odinga kujiondoa katika uchaguzi huo.
Wanavyoelewa ni kwamba hatua ya Raila Odinga kujiondoa katika uchaguzi huo inamaanisha kwamba uchaguzi huo unafutiliwa mbali.
Wanahoji kwamba ilani ya gazeti rasm la serikali lililotangaza uchaguzi huo imepitwa na wakati kufuatia hatua hiyo ya Odinga.
Wanadai kwamba tume ya IEBC huenda isiweze kusimamia uchaguzi huo kama ilivyoagizwa na mahakama ya juu kutokana na maadalizi hafifu.
Kuna hatari kwamba uchaguzi huo huenda usifanyike katika idadi kubwa ya kaunti hatua itakayoweka hatma na maisha ya Wakenya katika matatizo.
Watatu hao wameagizwa kuwakabidhi wahusika agizo la kesi hiyo kufikia saa kumi na mbili jioni.
Wakati wa kuchapishwa kwa taarifa hii wakili wa rais Uhuru Kenyatta Tom Macharia na wale wanaowakilisha IEBC walikuwa washakabidhiwa agizi hilo.
IEBC na wengine wanatarajiwa kujibu kufikia kesho saa mbili alfjiri .
Kusikizwa kwa kesi hiyo kunatarajiwa kuanza saa nne ya alfajiri siku ya Jumatano.
Wakitoa uamuzi wao manmo tarehe mosi Septemba, majaji sita wa mahakama ya juu waliunga mkono ombi lililowasilishwa na Raila Odinga kwa majaji 4-2 aliyedai kwamba mfumo wa kielektroniki ulidukuliwa na kuingiliwa kwa lengo la kumsaidia rais Uhuru Kenyatta.
Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi wa kura hiyo kwa asilimia 54.
Majaji hao walisema: Tume ya uchaguzi ilishindwa ama hata kukataa kufanya uchaguzi wa urais katika hali ambayo inalingana na katiba .
Hatahivyo mahakama hiyo haikumlaumu rais Kenyatta ama hata chama chake.
Kenyatta alisema kuwa anajutia kwamba watu sita wameamua wataenda dhidi ya matakwa ya raia lakini hatopinga uamuzi huo. Kenya: Watu 3 waenda mahakamani kusitisha uchaguzi
Mahakama hiyo itasikiza ombi la dharura siku ya Jumatano kuhakikisha kuwa uchaguzi huo unafutiliwa mbali siku moja kablka ya kufanyika kwa uchaguzi huo.
Hatua hiyo inajiri baada bya mahakama hiyo kufanya uamuzi wa kihistoria ilipofutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa urais na kutaka uchaguzi huo kurejelewa.
Sasa inatakiwa kuingilia kati kwa mara nynegine na itaamua , ikiwa imesalia chini ya saa 24 kabla ya uchgauzi huo kufanyika kuhusu iwapo uchaguzoi huo unafaa kuendelea.
Kuna utata kati ya sheria za uchaguzi, katiba na vile mahakama ilivyofafanua sheria hizo.
Kiongozi mkuu wa upinzani Raila Odinga ametumia mojawapo ya uamuzi wa mahakama kujiondoa katika uchaguzi huo akiutaja kuwa usio huru na haki na hautatoa maono ya Wakenya.
Rais aliyepo sasa Uhuru Kenyatta amesema kuwa uchaguzi huo ni sharti ufanyike, huku akiwa na muswada wa uchaguzi katika meza yake unaotarajiwa kutiwa saini
Mahakama ya juu imekubali kusikiliza ombi hilo la muda wa lala salama ambalo linahoji iwapo tume ya uchaguzi na mwenyekiti wake wataweza kufanya uchaguzi ulio huru na haki siku ya Alhamisi.
Inataka uchaguzi huo kubadilishwa na uchaguzi mpya hatua ambayo huenda ikaongeza muda wa uchaguzi huo kwa kipindi cha mwezi mmoja .
Wapiga kura watatu wameelekea katika mahakama ya juu wakitaka kusimamisha uchaguzi huo wa Alhamisi.
Bwana Khalef Khalifa , Samuel Mohochi na Gacheke Gachuhi wanadai kwamba tume ya uchaguzi imegawanyika na haiwezi kufanya uchaguzi ulio huru na haki.
Wanadai kwamba makamishna wa IEBC wanahudumu kwa upendeleo na mwenyekiti wa tume hiyo Wafula Chebukati amekiri hadharani kwamba hawezi kusimamia uchaguzi ulio huru na wa haki.
Walalamishi hao watatu ,wanaowakilishwa na Harun Ndubi pia wanataka mahakama kuamua kuhusu hatua ya Raila Odinga kujiondoa katika uchaguzi huo.
Wanavyoelewa ni kwamba hatua ya Raila Odinga kujiondoa katika uchaguzi huo inamaanisha kwamba uchaguzi huo unafutiliwa mbali.
Wanahoji kwamba ilani ya gazeti rasm la serikali lililotangaza uchaguzi huo imepitwa na wakati kufuatia hatua hiyo ya Odinga.
Wanadai kwamba tume ya IEBC huenda isiweze kusimamia uchaguzi huo kama ilivyoagizwa na mahakama ya juu kutokana na maadalizi hafifu.
Kuna hatari kwamba uchaguzi huo huenda usifanyike katika idadi kubwa ya kaunti hatua itakayoweka hatma na maisha ya Wakenya katika matatizo.
Watatu hao wameagizwa kuwakabidhi wahusika agizo la kesi hiyo kufikia saa kumi na mbili jioni.
Wakati wa kuchapishwa kwa taarifa hii wakili wa rais Uhuru Kenyatta Tom Macharia na wale wanaowakilisha IEBC walikuwa washakabidhiwa agizi hilo.
IEBC na wengine wanatarajiwa kujibu kufikia kesho saa mbili alfjiri .
Kusikizwa kwa kesi hiyo kunatarajiwa kuanza saa nne ya alfajiri siku ya Jumatano.
Wakitoa uamuzi wao manmo tarehe mosi Septemba, majaji sita wa mahakama ya juu waliunga mkono ombi lililowasilishwa na Raila Odinga kwa majaji 4-2 aliyedai kwamba mfumo wa kielektroniki ulidukuliwa na kuingiliwa kwa lengo la kumsaidia rais Uhuru Kenyatta.
Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi wa kura hiyo kwa asilimia 54.
Majaji hao walisema: Tume ya uchaguzi ilishindwa ama hata kukataa kufanya uchaguzi wa urais katika hali ambayo inalingana na katiba .
Hatahivyo mahakama hiyo haikumlaumu rais Kenyatta ama hata chama chake.
Kenyatta alisema kuwa anajutia kwamba watu sita wameamua wataenda dhidi ya matakwa ya raia lakini hatopinga uamuzi huo. Kenya: Watu 3 waenda mahakamani kusitisha uchaguzi
Darasa: Azungumzia ujio wake mpya,,,
Msanii wa muziki wa Bongo Flava, Darassa amezungumzia ujio wake mpya.
Rapper huyo ambaye mara mwisho alisikika na ngoma ‘Hasara Roho’ ameiambia Dj Show ya Radio One yupo katika maandalizi ya kufanya hivyo ila kwa sasa asingependa kulizungumzia sana kwani yeye siku zote siyo muongeaji zaidi ya kazi.
“Kwenye single mpya watu wananijua mimi siyo mtu wa kuongea ongea kama sina kitu cha kuongea mara nyingi huwa nakuja kuongea nikiwa na kitu, kwa sasa naandaa project ambazo naamini nitakuja kufunga nazo mwaka watu wakae tayari tunakuja tuko poa kabisa” amesema Darassa.
Mwishoni mwa mwaka jana Darassa alifunga mwaka na ngoma Muziki ambayo alimshirikisha Ben Pol ambayo inatajwa kuwa ndio ngoma pekee kuwa hit ya kutisha kutoka kipindi hicho hadi mwaka huu.
Rapper huyo ambaye mara mwisho alisikika na ngoma ‘Hasara Roho’ ameiambia Dj Show ya Radio One yupo katika maandalizi ya kufanya hivyo ila kwa sasa asingependa kulizungumzia sana kwani yeye siku zote siyo muongeaji zaidi ya kazi.
“Kwenye single mpya watu wananijua mimi siyo mtu wa kuongea ongea kama sina kitu cha kuongea mara nyingi huwa nakuja kuongea nikiwa na kitu, kwa sasa naandaa project ambazo naamini nitakuja kufunga nazo mwaka watu wakae tayari tunakuja tuko poa kabisa” amesema Darassa.
Mwishoni mwa mwaka jana Darassa alifunga mwaka na ngoma Muziki ambayo alimshirikisha Ben Pol ambayo inatajwa kuwa ndio ngoma pekee kuwa hit ya kutisha kutoka kipindi hicho hadi mwaka huu.
Giggs Asema anazitamani Everton na Leicester City
Kocha msaidizi wa zamani wa Manchester United Ryan Giggs amesema anatamani kuchukua mikoba ya makocha Ronald Koeman na Craig Shakespeare katika klabu za Everton na Leicester City.
Giggs ambaye alikuwa msaidizi wa Louis Van Gaal ndani ya Manchester United ameweka wazi nia yake hiyo wkaati akifanya mahoajiano na Sky Sports kuhusiana na uelekeo wake kwenye kufundisha soka.
“Hizi ni klabu zinazonivutia kuzifundisha kutoakana na aina yake ya uchezaji na zina wachezaji ambao wana viwango bora”, amesma Giggs
Hata hivyo Giggs amegoma kuweka wazi endapo atatuma maombi kwa uongozi wa timu hizo ili kumpatia nafasi hiyo ya kuongoza benchi la ufundi.
Leicester City ilimfuta kazi kocha Craig Shakespeare wiki iliyopita kabla ya jana Everton kumfuta kazi Ronald Koeman. Giggs amekuwa nje ya masuala ya ukocha kwa kazi ya juu tangu alipoondoka Manchester United mwaka 2016 baada ya mkuu wake Van Gaal kuondolewa.
Giggs ambaye alikuwa msaidizi wa Louis Van Gaal ndani ya Manchester United ameweka wazi nia yake hiyo wkaati akifanya mahoajiano na Sky Sports kuhusiana na uelekeo wake kwenye kufundisha soka.
“Hizi ni klabu zinazonivutia kuzifundisha kutoakana na aina yake ya uchezaji na zina wachezaji ambao wana viwango bora”, amesma Giggs
Hata hivyo Giggs amegoma kuweka wazi endapo atatuma maombi kwa uongozi wa timu hizo ili kumpatia nafasi hiyo ya kuongoza benchi la ufundi.
Leicester City ilimfuta kazi kocha Craig Shakespeare wiki iliyopita kabla ya jana Everton kumfuta kazi Ronald Koeman. Giggs amekuwa nje ya masuala ya ukocha kwa kazi ya juu tangu alipoondoka Manchester United mwaka 2016 baada ya mkuu wake Van Gaal kuondolewa.
Serikali kuboresha shule 85 za kata...
Serikali imetoa takribani Shilingi Bilioni 21 kwa ajili ya kuboresha shule 85 za Kata hapa nchini ili ziwe na Kidato cha Tano na Sita hali itakayoongeza ubora wa kiwango cha elimu na kuimarishwa kwa miundombinu.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mhe. Selemani Jafo wakati wa kipindi cha TUNATEKELEZA kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) siku za Jumatatu na Alhamisi.
Akifafanua Waziri Jafo amesema kuwa dhamira ya Serikalini katika kuboresha sekta ya elimu ambapo kila mwezi imekuwa ikitoa takribani Bilioni 23 zinazotumika kugharimia elimu bure hali inayochochea kuongezeka kwa wanafunzi wanaojiunga katika shule za msingi na Sekondari .
“Tumejenga madarasa mengi na vyoo vingi ili kuendana na kasi ya udahili wa wanafunzi na pia tutahakikisha kuwa kuna kuwa na uwiano katika mgawanyo wa walimu katika maeneo mbalimbali hapa nchini. Aliongeza kuwa Serikali katika kuboresha huduma za Afya imeshapeleka fedha katika vituo 172 kote nchini ili kuboresha huduma zinazotolewa na pia watumishi katika sekta hiyo wataajiriwa kwa kuzingatia mahitaji kutokana na nafasi zilizoachwa wazi baada ya zoezi la ukaguzi wa vyeti feki.
Aidha Waziri Jafo aliwataka Viongozi wote katika Mikoa na Halmashauri kusimamia vizuri miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali katika maeneo yao ili thamani halisi ya fedha zilizowekezwa ionekane. “Nawasihi watanzania walipe kodi kwa kuwa fedha zinazotokana na kodi ndizo zinazotumika kutekeleza miradi ya maendeleo na ni matumaini yangu kuwa maelekezo niliyotoa kwa wakurugenzi kuhusu ukusanyaji wa mapato yatazingatiwa na watasimamia kazi hiyo vyema na kubuni vyanzo vipya vya mapato”Alisisitiza Jafo.
Aidha Waziri Jafo amewataka watumishi wa Wizara hiyo kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwa kuwa hadi sasa watumishi zaidi ya 300 wameshachukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu kwa kushindwa kutimiza wajibu wao.
Kwa upande wa sekta ya Viwanda amebainisha kuwa wamejipanga vyema kutekeleza dhana ya ujenzi wa uchumi wa viwanda kwa kutenga maeneo maalum ya uwekezaji katika Halamashauri na Mikoa.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mhe. Selemani Jafo wakati wa kipindi cha TUNATEKELEZA kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) siku za Jumatatu na Alhamisi.
Akifafanua Waziri Jafo amesema kuwa dhamira ya Serikalini katika kuboresha sekta ya elimu ambapo kila mwezi imekuwa ikitoa takribani Bilioni 23 zinazotumika kugharimia elimu bure hali inayochochea kuongezeka kwa wanafunzi wanaojiunga katika shule za msingi na Sekondari .
“Tumejenga madarasa mengi na vyoo vingi ili kuendana na kasi ya udahili wa wanafunzi na pia tutahakikisha kuwa kuna kuwa na uwiano katika mgawanyo wa walimu katika maeneo mbalimbali hapa nchini. Aliongeza kuwa Serikali katika kuboresha huduma za Afya imeshapeleka fedha katika vituo 172 kote nchini ili kuboresha huduma zinazotolewa na pia watumishi katika sekta hiyo wataajiriwa kwa kuzingatia mahitaji kutokana na nafasi zilizoachwa wazi baada ya zoezi la ukaguzi wa vyeti feki.
Aidha Waziri Jafo aliwataka Viongozi wote katika Mikoa na Halmashauri kusimamia vizuri miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali katika maeneo yao ili thamani halisi ya fedha zilizowekezwa ionekane. “Nawasihi watanzania walipe kodi kwa kuwa fedha zinazotokana na kodi ndizo zinazotumika kutekeleza miradi ya maendeleo na ni matumaini yangu kuwa maelekezo niliyotoa kwa wakurugenzi kuhusu ukusanyaji wa mapato yatazingatiwa na watasimamia kazi hiyo vyema na kubuni vyanzo vipya vya mapato”Alisisitiza Jafo.
Aidha Waziri Jafo amewataka watumishi wa Wizara hiyo kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwa kuwa hadi sasa watumishi zaidi ya 300 wameshachukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu kwa kushindwa kutimiza wajibu wao.
Kwa upande wa sekta ya Viwanda amebainisha kuwa wamejipanga vyema kutekeleza dhana ya ujenzi wa uchumi wa viwanda kwa kutenga maeneo maalum ya uwekezaji katika Halamashauri na Mikoa.
Abilia Waanzisha Vurugu Uwanja wa ndege,,,, ,,,,
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia(FFU) leo wamelazimika kuingilia kati kutuliza vurugu zilizoazishwa na abiria 75 waliokosa usafiri wa ndege ya kampuni ya FastJet kutoka Mwanza kwenda Dar es Salaam kutokana na hitilafu za kiufundi.
Abiria hao waliokaa uwanjani hapo kwa zaidi ya saa nne kuanzia saa 3:00 asubuhi walipotakiwa kusafiri hadi saa 7:00 mchana, walianzisha vurugu kushinikiza kupatiwa usafiri.
Wakizungumza na Mwananchi uwanjani hapo kwa nyakati tofauti, abiria Rukia Mohamed, Juma Kisombi na Mamad Mohamed wamesema walilazimika kuushinikiza uongozi wa kampuni hiyo kuwapa maelezo ya kutosha baada ya ahadi ya kutakiwa kusubiri kidogo kutotekelezwa kwa zaidi ya saa tatu waliyosubiri uwanjani hapo.
“Nimefika Jumapili iliyopita na leo, nilitakiwa kurejea jijini Dar es Salaam na nilifika uwanjani kwa muda uliotakiwa lakini hadi sasa hakuna ndege na uongozi hautoi maelezo ya kueleweka,” alilalamika Rukia.
Akizungumzia kadhia hiyo, Meneja wa FastJet Mkoa wa Mwanza, Ezekiel Manyiga amesema ndege iliyotakiwa kusafirisha abiria hao haikufika kutoka jijini Dar es Salaam kutokana na kupata hitilafu ya kiufundi.
“Hata abiria waliotakiwa kusafiri kutoka Dar es Salaam kuja Mwanza hawajafika hadi sasa; tunafanya kila lililo ndani ya uwezo wetu kutatua tatizo hili,” amesema Manyiga
Ilipofika saa 7:00 mchana jana, uongozi wa kampuni hiyo ulifikia uamuzi wa kuwarejeshea nauli abiria waliokuwa tayari kupokea fedha zao ili kutafuta usafiri mwingine pamoja na Sh30, 000 ya kujikimu kwa kila abiria aliyekosa usafiri.
“Watakaokuwa tayari kusubiri ndege yetu watalazimika kusafiri kesho (Jumatano) kwa sababu ndege tayari imejaa,” amesema Manyigan
Abiria hao waliokaa uwanjani hapo kwa zaidi ya saa nne kuanzia saa 3:00 asubuhi walipotakiwa kusafiri hadi saa 7:00 mchana, walianzisha vurugu kushinikiza kupatiwa usafiri.
Wakizungumza na Mwananchi uwanjani hapo kwa nyakati tofauti, abiria Rukia Mohamed, Juma Kisombi na Mamad Mohamed wamesema walilazimika kuushinikiza uongozi wa kampuni hiyo kuwapa maelezo ya kutosha baada ya ahadi ya kutakiwa kusubiri kidogo kutotekelezwa kwa zaidi ya saa tatu waliyosubiri uwanjani hapo.
“Nimefika Jumapili iliyopita na leo, nilitakiwa kurejea jijini Dar es Salaam na nilifika uwanjani kwa muda uliotakiwa lakini hadi sasa hakuna ndege na uongozi hautoi maelezo ya kueleweka,” alilalamika Rukia.
Akizungumzia kadhia hiyo, Meneja wa FastJet Mkoa wa Mwanza, Ezekiel Manyiga amesema ndege iliyotakiwa kusafirisha abiria hao haikufika kutoka jijini Dar es Salaam kutokana na kupata hitilafu ya kiufundi.
“Hata abiria waliotakiwa kusafiri kutoka Dar es Salaam kuja Mwanza hawajafika hadi sasa; tunafanya kila lililo ndani ya uwezo wetu kutatua tatizo hili,” amesema Manyiga
Ilipofika saa 7:00 mchana jana, uongozi wa kampuni hiyo ulifikia uamuzi wa kuwarejeshea nauli abiria waliokuwa tayari kupokea fedha zao ili kutafuta usafiri mwingine pamoja na Sh30, 000 ya kujikimu kwa kila abiria aliyekosa usafiri.
“Watakaokuwa tayari kusubiri ndege yetu watalazimika kusafiri kesho (Jumatano) kwa sababu ndege tayari imejaa,” amesema Manyigan
Ofisa wa TRA Afikishwa Mahakamani
Dar es Salaam. Ofisa Msaidizi wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Jennifer Mushi amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashtaka mawili ikiwamo la kukutwa akimiliki magari 19, mali isiyolingana na kipato chake halali.
Jennifer ameshtakiwa chini ya kifungu cha 27(1) (a) na (b) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007.
Akisoma hati ya mashtaka hayo leo Jumanne, Wakili wa Serikali Mkuu, Vitalis Peter mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi alidai kuwa mshtakiwa huyo kati ya Machi 21, 2016 na Juni 30, 2016 jijini Dar es Salaam akiwa mwajiriwa wa TRA kama Ofisa Forodha Msaidizi alikutwa akimiliki magari 19.
Aliyataja magari hayo kuwa ni Toyota RAV4, Toyota RAV4, Toyota Dyna Truck, Toyota Vitz, Suzuki Carry, Toyota Ipsum, Toyota Wish, Toyota Mark II, Toyota Wish na Toyota Mark X.
Mengine ni Toyota Regiusage, Toyota Estima, Toyota Alex, Toyota Noah, Toyota Crown, Toyota Hiace, Toyota Estima, Toyota Passo na Suzuki Carry yote yakiwa na thamani ya Sh 197,601,207 mali ambayo hailingani na kipato chake halali.
Wakili huyo alidai kuwa mshtakiwa huyo kati ya Machi 21 ,2012 na Machi 30, 2016 Dar es Salaam akiwa mwajiriwa wa TRA kama ofisa forodha msaidizi alikutwa akiishi maisha ya kifahari yenye thamani ya Sh 333,255,556.24 fedha ambayo hailingani na kipato chake halali.
Baada ya kusomewa mashtaka hayo mshtakiwa huyo alikana na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.
Wakili wa mshtakiwa huyo, Elisaria Mosha aliiomba Mahakama kumpatia dhamana mteja wake ya masharti nafuu.
Hakimu Shaidi, alimtaka mshtakiwa huyo kuwa na mdhamini mmoja anayeaminika ambaye atasaini bondi ya Sh 20 milioni.
Mshtakiwa huyo alikamilisha masharti hayo ya dhamana na kuachiwa huru.
Kesi imeahirishwa hadi Novemba 7, 2017 kwa ajili ya mshtakiwa huyo kusomewa maelezo ya awali (PH).
Jennifer ameshtakiwa chini ya kifungu cha 27(1) (a) na (b) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007.
Akisoma hati ya mashtaka hayo leo Jumanne, Wakili wa Serikali Mkuu, Vitalis Peter mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi alidai kuwa mshtakiwa huyo kati ya Machi 21, 2016 na Juni 30, 2016 jijini Dar es Salaam akiwa mwajiriwa wa TRA kama Ofisa Forodha Msaidizi alikutwa akimiliki magari 19.
Aliyataja magari hayo kuwa ni Toyota RAV4, Toyota RAV4, Toyota Dyna Truck, Toyota Vitz, Suzuki Carry, Toyota Ipsum, Toyota Wish, Toyota Mark II, Toyota Wish na Toyota Mark X.
Mengine ni Toyota Regiusage, Toyota Estima, Toyota Alex, Toyota Noah, Toyota Crown, Toyota Hiace, Toyota Estima, Toyota Passo na Suzuki Carry yote yakiwa na thamani ya Sh 197,601,207 mali ambayo hailingani na kipato chake halali.
Wakili huyo alidai kuwa mshtakiwa huyo kati ya Machi 21 ,2012 na Machi 30, 2016 Dar es Salaam akiwa mwajiriwa wa TRA kama ofisa forodha msaidizi alikutwa akiishi maisha ya kifahari yenye thamani ya Sh 333,255,556.24 fedha ambayo hailingani na kipato chake halali.
Baada ya kusomewa mashtaka hayo mshtakiwa huyo alikana na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.
Wakili wa mshtakiwa huyo, Elisaria Mosha aliiomba Mahakama kumpatia dhamana mteja wake ya masharti nafuu.
Hakimu Shaidi, alimtaka mshtakiwa huyo kuwa na mdhamini mmoja anayeaminika ambaye atasaini bondi ya Sh 20 milioni.
Mshtakiwa huyo alikamilisha masharti hayo ya dhamana na kuachiwa huru.
Kesi imeahirishwa hadi Novemba 7, 2017 kwa ajili ya mshtakiwa huyo kusomewa maelezo ya awali (PH).
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Aingilia Kati Ugomvi wa FFU na Wananchi wa Ukonga Dar
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema amewapiga marufuku askari wa kikosi cha FFU na kusema hataki kuwaona wakisumbua wananchi katika eneo la Ukonga Dar es Salaam na kutaka waliohusika wachukuliwe hatua kwa kitendo walichofanya kuwapiga wananchi.
Sophia Mjema amesema hayo alipowatembelea wananchi hao ambao wamelalamika kufanyiwa fujo na kupigwa na askari hao kwa siku mbili kutokana na askari mmoja kuuwawa na watu wasiojulikana.
Mkuu wa Wilaya anasema kuwa askari hao walipaswa kufanya uchunguzi kujua ni watu gani walihusika kufanya mauaji ya askari huyo na si kwenda kufanya fujo na kuwapiga wananchi pasipokuwa na sababu.
"Kama kuna askari alipatikana ameshafariki utaratibu ulikuwa uchunguzi ufanyike ili waweze kujiridhisha baada ya hapo wale ambao wangetambulika ndiyo wangechukuliwa hatua lakini kwa hili halikubaliki, kwa hiyo nasema hivi askari wote waliohusika kufanya fujo na vurugu wachukuliwe hatua za kinidhamu na huku barabarani sitaki kuona FFU yoyote anasumbua wananchi" alisema Mjema
Aidha Mkuu wa Wilaya huyo ametaka wananchi ambao wameumizwa na askari hao kwa vipigo kwa siku mbili mfululizo waweze kujiorodhesha kwa majina ili wapatiwe matibabu na kusema wale ambao wamepoteza mali zao utaratibu utafanyika kuona nini kifanyike
Sophia Mjema amesema hayo alipowatembelea wananchi hao ambao wamelalamika kufanyiwa fujo na kupigwa na askari hao kwa siku mbili kutokana na askari mmoja kuuwawa na watu wasiojulikana.
Mkuu wa Wilaya anasema kuwa askari hao walipaswa kufanya uchunguzi kujua ni watu gani walihusika kufanya mauaji ya askari huyo na si kwenda kufanya fujo na kuwapiga wananchi pasipokuwa na sababu.
"Kama kuna askari alipatikana ameshafariki utaratibu ulikuwa uchunguzi ufanyike ili waweze kujiridhisha baada ya hapo wale ambao wangetambulika ndiyo wangechukuliwa hatua lakini kwa hili halikubaliki, kwa hiyo nasema hivi askari wote waliohusika kufanya fujo na vurugu wachukuliwe hatua za kinidhamu na huku barabarani sitaki kuona FFU yoyote anasumbua wananchi" alisema Mjema
Aidha Mkuu wa Wilaya huyo ametaka wananchi ambao wameumizwa na askari hao kwa vipigo kwa siku mbili mfululizo waweze kujiorodhesha kwa majina ili wapatiwe matibabu na kusema wale ambao wamepoteza mali zao utaratibu utafanyika kuona nini kifanyike
Askari Akatwa sikio Na kuuawa Dsm
Kwamujibu wa kamanda wa Polisi kanda maalumu ya Dar es salaam SACP Lazaro Mambosasa, ameeleza kuwa Jeshi la Polisi Kanda Maalum DSM mnamo tarehe 21/10/2017 majira ya saa 06:O0hrs huko maeneo ya kambi ya polisi kikosi cha kutuliza ghasia Ukonga Makao makuu mkoa wa kipolisi Ilala, askari wakiwa kazini walikuta mwili wa marehemu X-G 475 PC CHARLES YANGA ukiwa pembeni mwa uzio wa kambi hiyo akiwa ameanguka chini huku pikipiki yake aliyokuwa akiendesha ikiwasha taa za tahadhari(hazards light), mwili huo ulikutwa ukiwa na majeraha kwenye paji la uso na sikio moja likiwa limekatwa kabisa.
TAZA
TAZA
Umoja wa Mataifa wataka Wapinzani waliokamatwa waachiwe...
Umoja wa mataifa umetoa wito ya kuachiwa mara moja kwa watu 30, wa chama kikuu cha upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kutoka korokoroni.
Wanachama wa vyama vikuu viwili vya Union for Democracy na wenzao wa Social Progress, walikamatwa siku ya Jumapili katika mji wa Lubumbashi, ulioko Kusini mashariki mwa nchi hiyo, baada ya polisi kuvunja mkutano waliokuwa nao.
Utawala wa Rais, Joseph Kabila, umepiga marufuku mkutano wa aina yoyote wa kisiasa, pamoja na maandamano ya upinzani, tangu muda wake wa kuhudumu kama Rais kisheri, ulipomalizika mwaka mmoja uliopita.
Rais Joseph Kabila amesalia mamlakani hata baada ya muhula wake kuhudumu kumalizika mwaka mmoja uliopita
Tume ya uchaguzi nchini humo, imesema kuwa, haitakuwa rahisi kuandaa uchaguzi mkuu wa Urais, kabla ya mwezi Aprili mwaka ujao wa 2019.
Chama kingine cha upinzani- Union for the Congolese Nation, kimesema kwamba, kitajiondoa katika serikali ya ugawanaji mamlaka, kuhusiana na kucheleweshwa kwa uchaguzi mkuu.
Maandamano ya mara kwa mara ya upinzani nchini humo umekabiliwa vikali na utawala wa Rais Joseph Kabila.
Wanachama wa vyama vikuu viwili vya Union for Democracy na wenzao wa Social Progress, walikamatwa siku ya Jumapili katika mji wa Lubumbashi, ulioko Kusini mashariki mwa nchi hiyo, baada ya polisi kuvunja mkutano waliokuwa nao.
Utawala wa Rais, Joseph Kabila, umepiga marufuku mkutano wa aina yoyote wa kisiasa, pamoja na maandamano ya upinzani, tangu muda wake wa kuhudumu kama Rais kisheri, ulipomalizika mwaka mmoja uliopita.
Rais Joseph Kabila amesalia mamlakani hata baada ya muhula wake kuhudumu kumalizika mwaka mmoja uliopita
Tume ya uchaguzi nchini humo, imesema kuwa, haitakuwa rahisi kuandaa uchaguzi mkuu wa Urais, kabla ya mwezi Aprili mwaka ujao wa 2019.
Chama kingine cha upinzani- Union for the Congolese Nation, kimesema kwamba, kitajiondoa katika serikali ya ugawanaji mamlaka, kuhusiana na kucheleweshwa kwa uchaguzi mkuu.
Maandamano ya mara kwa mara ya upinzani nchini humo umekabiliwa vikali na utawala wa Rais Joseph Kabila.
Ronaldo Anyakua tuzo FIFA
England. Cristiano Ronaldo ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa dunia wa Fifa 2017 baada ya kuwapiku wachezaji Lionel Messi na Neymar katika kipengele hicho.
Tuzo hizo zimetolewa Oktoba 23 ambapo mchezaji huyo aliyeambatana na mpenzi wake na mwanae amewashukuru waliompigia kura kwa kuweza kushinda pamoja na mashabiki na wachezaji wenzake.
“Nashukuru wote mlionipigia kura kwa kunifanya nishinde tuzo hii,” amesema Ronaldo.
Mbali na tuzo hiyo Ronaldo ametajwa katika kikosi bora cha mwaka 2017 ambacho kimewajumuisha Messi na Neymar na nyota wengine akiwemo Sergio Ramos, Toni Kroos, Andres Iniesta, na Dani Alves.
Tuzo ya mchezaji bora wa kike wa Fifa 2017 ilienda kwa Lieke Martens ambaye hakuudhuria katika utoaji wa tuzo kutokana na kujiandaa na kujiandaa na mechi ya kufuzu kombe la dunia la wanawake.
Ukumbi ulilipuka kwa shangwe wakati linatangazwa goli bora la mwaka ‘Puskas’ ambapo katika magoli 10 bora mashabiki walisikika wakimtaja nyota wa Arsenal, Olivier Giroud ambaye alitangazwa kama mshindi.
Wengine walioshinda tuzo za Fifa 2017 ni Zinedine Zidane (Kocha bora kwa waume), Sarina Wiegman (kocha bora kwa wanawake) Gianluigi Buffon (Kipa bora), Mashabiki wa Celtic (Kikundi bora), Francis Kone (Mchezo wa kiungwana).
Tuzo hizo zimetolewa Oktoba 23 ambapo mchezaji huyo aliyeambatana na mpenzi wake na mwanae amewashukuru waliompigia kura kwa kuweza kushinda pamoja na mashabiki na wachezaji wenzake.
“Nashukuru wote mlionipigia kura kwa kunifanya nishinde tuzo hii,” amesema Ronaldo.
Mbali na tuzo hiyo Ronaldo ametajwa katika kikosi bora cha mwaka 2017 ambacho kimewajumuisha Messi na Neymar na nyota wengine akiwemo Sergio Ramos, Toni Kroos, Andres Iniesta, na Dani Alves.
Tuzo ya mchezaji bora wa kike wa Fifa 2017 ilienda kwa Lieke Martens ambaye hakuudhuria katika utoaji wa tuzo kutokana na kujiandaa na kujiandaa na mechi ya kufuzu kombe la dunia la wanawake.
Ukumbi ulilipuka kwa shangwe wakati linatangazwa goli bora la mwaka ‘Puskas’ ambapo katika magoli 10 bora mashabiki walisikika wakimtaja nyota wa Arsenal, Olivier Giroud ambaye alitangazwa kama mshindi.
Wengine walioshinda tuzo za Fifa 2017 ni Zinedine Zidane (Kocha bora kwa waume), Sarina Wiegman (kocha bora kwa wanawake) Gianluigi Buffon (Kipa bora), Mashabiki wa Celtic (Kikundi bora), Francis Kone (Mchezo wa kiungwana).
Mawaziri Na Wabunge Kuanza Kupewa Tuzo
Kamati ya utawala ya shindano la tuzo za utekelezaji maendeleo kwa kasi ya juu kwa Wabunge na Mawaziri (THSDA) imezindua shindano la kutoa tuzo kwa Wabunge na Mawaziri watakaofanya vizuri katika kutekeleza majukumu ya kuwaletea Wananchi maendeleo.
Hayo yamesemwa Jijini Dar es Salaam na Katibu wa Kamati hiyo Bw. Wilson Maage alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, juu ya uzinduzi wa shindano hilo ambalo litafanyika kwa muda wa miezi miwili.
“Tuzo hizo zimetokana na kuwepo wazo bunifu (intellectual property) ambalo azma yake ni kuhamasisha utekelezaji wa shughuli za huduma na maendeleo kwa wananchi wa Tanzania na kupima kasi ya utekelezaji wa shughuli hizo kwa viongozi wa ngazi mbalimbali katika sekta na taasisi za kiserikali hapa nchini,” alifafanua Maage.
Aliendelea kusema kuwa, vigezo vitakavyotumiwa katika kuteua viongozi hao ambao ni wabunge pamoja na Mawaziri ni pamoja na kuwa mtetezi wa Wananchi wake bila uoga akiwa ndani au nje ya Bunge, mtendaji bora wa maendeleo yenye kuonekana, sifa ya kutoa hoja zenye tija kwa kutumia lugha ya staha bila matusi, sifa ya utekelezaji wa haraka apatapo matatizo ya Wananchi wake pamoja na sifa ya kutetea demokrasia, uhuru na kutetea wanyonge.
“Faida za shindano la tuzo hizi ni kwamba zinaweka Wananchi karibu na viongozi, kuchochea utekelezaji huduma na maendeleo kwa kasi ya juu, utawla bora na uwajibikaji wa viongozi kwa Wananchi, uhusiano mzuri kati ya serikali na Wananchi na kuimarisha furaha, utulivu na amani,” alieleza Maage.
Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa Kamati hiyo, Herman Mnenuka alisema kuwa Wananchi ndiyo nguzo kuu ya kupata kiongozi atakayepata tuzo hiyo kwani wao ndio watakaopendekeza majina ya wabunge pamoja na mawaziri wanaofaa kuwania tuzo hiyo.
Katika tuzo hiyo, hatua ya kwanza, wananchi wanapaswa kupendekeza wabunge 15 kwa kila kigezo shindanishi, pia Wananchi watawateua Mawaziri 5 kwa kila kipengele shindanishi kwaajili ya kuingia kwenye ushindani wa tuzo hiyo na wabunge watano na Mawaziri watatu watakaopata kura nyingi kwa njia ya ujumbe mfupi (SMS) kutoka kwa wananchi wataingia katika fainali ya king’anyiro kuwania tuzo hiyo.
Aidha aliongeza kuwa, katika hatua nyingine, wananchi kupitia simu watawachuja washiriki waliofika hatua ya fainali kwa kutuma SMS na mbunge pamoja na waziri atakayepata kura nyingi ndiye atakaye kuwa mshindi katika kilele cha tuzo hiyo kitakachofanyika tarehe 23 Desemba Mwaka huu.
“Niwaombe wananchi washiriki kikamilifu ili kuweza kupata kiongozi anayejishughulisha na anayechapa kazi kupitia tuzo hii na mwisho wa kilele tutapata mshindi wa kila kipengele kilichowekwa ambacho kina tija muhimu katika taifa kupitia waheshimiwa wabunge na mawaziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alieleza Mnenuka.
Aidha aliongeza kuwa, Wananchi watapendekeza majina kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu kupitia namba 15555 kwa mitandao ya Tigo, Airtel, Vodacom, Halotel Smart na Zantel na kila SMS itatozwa gharama ya shilingi 500 vilevile kutakuwa na vipindi vya radio runinga na magazeti ili kuwakumbusha mwenendo na hatua za shindano la tuzo za THSDA hadi siku ya kilele.
Hizi ni tuzo za kwanza kuandaliwa hapa nchini na kamati hiyo ambazo zitafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa rasilimali fedha.
Hayo yamesemwa Jijini Dar es Salaam na Katibu wa Kamati hiyo Bw. Wilson Maage alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, juu ya uzinduzi wa shindano hilo ambalo litafanyika kwa muda wa miezi miwili.
“Tuzo hizo zimetokana na kuwepo wazo bunifu (intellectual property) ambalo azma yake ni kuhamasisha utekelezaji wa shughuli za huduma na maendeleo kwa wananchi wa Tanzania na kupima kasi ya utekelezaji wa shughuli hizo kwa viongozi wa ngazi mbalimbali katika sekta na taasisi za kiserikali hapa nchini,” alifafanua Maage.
Aliendelea kusema kuwa, vigezo vitakavyotumiwa katika kuteua viongozi hao ambao ni wabunge pamoja na Mawaziri ni pamoja na kuwa mtetezi wa Wananchi wake bila uoga akiwa ndani au nje ya Bunge, mtendaji bora wa maendeleo yenye kuonekana, sifa ya kutoa hoja zenye tija kwa kutumia lugha ya staha bila matusi, sifa ya utekelezaji wa haraka apatapo matatizo ya Wananchi wake pamoja na sifa ya kutetea demokrasia, uhuru na kutetea wanyonge.
“Faida za shindano la tuzo hizi ni kwamba zinaweka Wananchi karibu na viongozi, kuchochea utekelezaji huduma na maendeleo kwa kasi ya juu, utawla bora na uwajibikaji wa viongozi kwa Wananchi, uhusiano mzuri kati ya serikali na Wananchi na kuimarisha furaha, utulivu na amani,” alieleza Maage.
Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa Kamati hiyo, Herman Mnenuka alisema kuwa Wananchi ndiyo nguzo kuu ya kupata kiongozi atakayepata tuzo hiyo kwani wao ndio watakaopendekeza majina ya wabunge pamoja na mawaziri wanaofaa kuwania tuzo hiyo.
Katika tuzo hiyo, hatua ya kwanza, wananchi wanapaswa kupendekeza wabunge 15 kwa kila kigezo shindanishi, pia Wananchi watawateua Mawaziri 5 kwa kila kipengele shindanishi kwaajili ya kuingia kwenye ushindani wa tuzo hiyo na wabunge watano na Mawaziri watatu watakaopata kura nyingi kwa njia ya ujumbe mfupi (SMS) kutoka kwa wananchi wataingia katika fainali ya king’anyiro kuwania tuzo hiyo.
Aidha aliongeza kuwa, katika hatua nyingine, wananchi kupitia simu watawachuja washiriki waliofika hatua ya fainali kwa kutuma SMS na mbunge pamoja na waziri atakayepata kura nyingi ndiye atakaye kuwa mshindi katika kilele cha tuzo hiyo kitakachofanyika tarehe 23 Desemba Mwaka huu.
“Niwaombe wananchi washiriki kikamilifu ili kuweza kupata kiongozi anayejishughulisha na anayechapa kazi kupitia tuzo hii na mwisho wa kilele tutapata mshindi wa kila kipengele kilichowekwa ambacho kina tija muhimu katika taifa kupitia waheshimiwa wabunge na mawaziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alieleza Mnenuka.
Aidha aliongeza kuwa, Wananchi watapendekeza majina kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu kupitia namba 15555 kwa mitandao ya Tigo, Airtel, Vodacom, Halotel Smart na Zantel na kila SMS itatozwa gharama ya shilingi 500 vilevile kutakuwa na vipindi vya radio runinga na magazeti ili kuwakumbusha mwenendo na hatua za shindano la tuzo za THSDA hadi siku ya kilele.
Hizi ni tuzo za kwanza kuandaliwa hapa nchini na kamati hiyo ambazo zitafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa rasilimali fedha.
Kizimbani kwa kutishia kumuua Diwani,,
WATU nane wakazi wa Ntyuka Manispaa ya Dodoma, wamefikishwa katika Mahakama ya Mwanzo ya Chamwino kwa tuhuma za kutishia kumuua kwa maneno Diwani wa Kata ya Ntyuka, Theobale Emmanuel.
Waliofikishwa kizimbani na kusomewa shtaka hilo ni Edward Lamoli, Edward Lauli, Petro Mjelwa, Yona Andrea, Lucas Mombo, Stephen Karashani, Zabron Leganga na Mussa Majana.
Kesi hiyo namba 234 ya mwaka 2017 inasikilizwa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo ya Chamwino, Zawadi Ndudumizi.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo Ntyuka kinyume cha kifungu cha 89 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 ambacho kilifanyiwa marejeo mwaka 2002.
Hata hivyo, Washtakiwa wako nje kwa dhamana na kesi hiyo itasikilizwa tena Oktoba 24 mwaka huu.
Waliofikishwa kizimbani na kusomewa shtaka hilo ni Edward Lamoli, Edward Lauli, Petro Mjelwa, Yona Andrea, Lucas Mombo, Stephen Karashani, Zabron Leganga na Mussa Majana.
Kesi hiyo namba 234 ya mwaka 2017 inasikilizwa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo ya Chamwino, Zawadi Ndudumizi.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo Ntyuka kinyume cha kifungu cha 89 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 ambacho kilifanyiwa marejeo mwaka 2002.
Hata hivyo, Washtakiwa wako nje kwa dhamana na kesi hiyo itasikilizwa tena Oktoba 24 mwaka huu.
Subscribe to:
Comments (Atom)












