Saturday 28 October 2017

Ruby: Siwezi kupotea kwenye mziki kisa kuzaa

Ruby: Siwezi kupotea kwenye mziki kisa kuzaa

MWANADADA kutoka kiwanda cha muziki wa Bongo Fleva, Hellen George ‘Ruby’ amefunguka kuwa hawezi kupotea kimuziki kisa kuzaa.

Ruby aliiambia Mikito Nusunusu kuwa, anatamani sana kuitwa mama na haofii kuwa atapotea kimuziki kama inavyotokea kwa wasanii wengine kwa sababu amejipanga kikamilifu.

“Natamani sana kuitwa mama kwa kweli na ikitokea muda wowote nitamshukuru Mungu na nitazaa maana sina kipingamizi, siwezi kupotea kimuziki maana mtoto ni moja ya baraka pia,” alisema Ruby.

No comments:

Post a Comment